Pre GE2025 CCM mnataka hayati Magufuli agombee 2025?

Pre GE2025 CCM mnataka hayati Magufuli agombee 2025?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hoja siyo kutajwa, Bali ni kwa nini Kuna harakati kubwa Sana zinazofanana na Kampeni??

Kuna nini nyuma ya Pazia??
Hizo kampeni anazifanya mama yako au nani?
Huwezi futa legacy ya JPM kwa kumfananisha na huyu mama yenu anayeongozwa kwa Remote!
Magufuli alikuwa Rais sahihi wa kuisafisha nchi hii.
 
Hapana,

Wewe ndiye umejibana na kutoelewa muktadha na kulazimisha ushirikina.

Mimi siamini ushirikina. Ushirikina ni ujinga mtupu.

Lakini, hilo halinizuii kuelewa kwamba, ukimtaja Magufuli tu, kumbukumbu yake inaendelea kuishi kwenye mawazo.

Anakuwa si mtu aliyesahaulika kama babu wa babu wa babu wa babu wa babu yako ambaye hata jina humjui.

Sasa hapo ushirikina unaingiaje?
Uko sawa mkuu

Lakini kwa nini ni yeye tu aendelee kukumbukwa
 
Tuliosoma falsafa na historia tumekutana na hoja kwamba mtu hafariki mpaka siku mtu wa mwisho anapoacha kumuwaza.

Yani ukimfikiria, ukimkumbuka, ukimtaja, anaendelea kuishi katika mawazo yako.

Labda wanataka Magufuli aendelee kuishi katika mawazo ya watu.

"No one is finally dead until the ripples they cause in the world die away, until the clock wound up winds down, until the wine she made has finished its ferment, until the crop they planted is harvested. The span of someone’s life is only the core of their actual existence."

Terry Pratchett, Reaper Man (Discworld, #11; Death, #2)
Thanks for this piece of info
 
Ngurukia umeionaje, umeielewaje na kama umeikubali umeikubali vipi hiyo nukuu?
Inatafakarisha mno. Wengi tunaamini ukomo wa maisha yetu ni kifo. Lakini kiuhalisia kifo ni ukomo wa uhai (physical existance) ila uwepo wetu unaendelea katika mambo mengi mno.

Mathalan mimi simjui babu wa babu yangu lakini fact kwamba mimi nipo (nimezaliwa) ni wazi alama ya kuwa alikuwepo haitofutika, hata ikiwa si kimatamshi ila kinadharia ipo.

Uwepo wetu una mwanzo tu, hauna mwisho.
 
Kama anafaa au hafai, ni lazima watu wakumbuke.

Ili, kama anafaa, kwa kadiri anavyofaa, mazuri yake yadumishwe, na kama hafai, kwa kadiri asivyofaa, mabaya yake yaepukwe.

Pinga hoja, usipinge mtu kuzungumziwa. Kama wanachakachua historia, weka sawa. Lakini usiseme kwa nini mnamuongelea Magufuli mtu kashafariki. Mtu akifariki si mwisho wa kuongelewa. Kuna wengine wanaona ndiyo mwanzo wa kuongelewa, kwa sababu kumuongelea mtu maisha yake kabla hajayamaliza anaweza kubadilika, akifariki ndiyo hawezi kubadilika.

Kwa nini unaona watu kukumbusha historia ni jambo baya as long as kinachokumbushwa ni kweli?

Rais Mwinyi ametuachia somo kwamba maisha ya mtu ni hadithi, ishi ili hadithi yako iwe nzuri watu wakihadithia ulivyoishi, usiache aibu.

Sasa watu wakisimulia hadithi za mtu tatizo liko wapi?

Umeshindwa kufikiri kidhahania kwamba hayo mazuri ya huyo mtu yanaweza kuwapa darasa wengine la kuyafuata, au kama mabaya, yanaweza kutoa darasa la kuyaepuka?

Unataka mtu akifa asizungumziwe tena?

Rais aliyeongoza mamilioni ya watu akifa asizungumziwe tena?

Unaelewa kuna simulizi wa Wafalme waliokufa maelfu ya miaka, wa Kirumi, Kiyunani, Mafarao wa Misri, mpaka leo watu wanazisimulia kujifunza kutokana na maisha yao?

Watu wanaandika habari za Caesar, Augustus, Nero, Caligula, Alexander the Great, Darius, Rameses, Ptolemy, Genghis Khan, Napoleon, Washington, Hitler, Martin Luther King Jr., Kennedy.

Mpaka leo.

Wewe unashangaa habari za Magufuli kafariki juzi hapo? Hata watu hawajamuandikia biographies za maana za kuchambua maisha yake.

If anything Tanzania hatujamuongelea vya kutosha Magufuli. Hatujamuongelea kwa kina kuchambua mazuri na mabaya yake, tuepuke mabaya yake yasijirudie na mazuri yake tuyaenzi na kuyaendeleza.
Ujumbe mzuri sana

Naiscreenshot hii reply yako mkuu
 
Hawa watu wasiompenda Magufuli wanaoumizwa anapoongelewa Magufuli mimi nawashangaa sana.

Kwanza sielewi wanaumizwa na kipi. Wanaona wivu Magufuli akiongelewa?

Pili, kama kweli hawampendi Magufuli, presumably na CCM, mimi ningetegemea wafurahie wana CCM kumuongelea Magufuli ambaye amefariki (kwa sababu hawezi kugombea kwenye uchaguzi) na wao waitumie fursa hiyo kumnadi mgombea wao.

Sasa, badala ya wao kumnadi mgombea wao, na wao wanajiunga kumuanzishia uzi Magufuli.

Hapo ndipo swali lako linakuwa na uzito.

Mtu anaponda watu kumuongelea Magufuli. Badala ya yeye kuanzisha uzi wake atuambie habari za mgombea wake, anaunga tela kuanzisha uzi wa kumuongelea Magufuli.

This is a contradiction.
🤔🤔🤔🤔🤔
So thoughtful
 
Ni kama sielewi CCM inataka nani awe mgombea wao ngazi ya Urais kwenye uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Kati ya Hayati John magufuli na Wana CCM wengine walioko hai.

Kwenye mitandao ya kijamii hivi Sasa ni kama limezuka Kundi kubwa Sana la wana CCM linalofanya jitihada za kuhakikisha kuwa kila siku kunakuwa na habari za Hayati Pombe John Magufuli mitandaoni.

Ni kama vile wanatushawishi tuone ubora wake na achaguliwe kwenye uchaguzi ujao.

Magufuli alishafariki, Sasa hizo harakati za mitandaoni kumnadi lengo lake ni nini hasa!!??
Akili kubwa hapo wanatumia kumpoteza mama

Sent from my SM-A146P using JamiiForums mobile app
 
Hata kama niivyo, ndiyo wengine wadiriki kusema kuwa DAB au Tapeli gwajiboy wanafaa kuongoza nchi?? Tumefikia huko??
Shida yote hii inasababishwa na huyo alieko amekua mbayuwayu hatulii kiotani hivyo anasababisha wafuasi wake kukosa habari ya kuandika[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Ni kama sielewi CCM inataka nani awe mgombea wao ngazi ya Urais kwenye uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Kati ya Hayati John magufuli na Wana CCM wengine walioko hai.

Kwenye mitandao ya kijamii hivi Sasa ni kama limezuka Kundi kubwa Sana la wana CCM linalofanya jitihada za kuhakikisha kuwa kila siku kunakuwa na habari za Hayati Pombe John Magufuli mitandaoni.

Ni kama vile wanatushawishi tuone ubora wake na achaguliwe kwenye uchaguzi ujao.

Magufuli alishafariki, Sasa hizo harakati za mitandaoni kumnadi lengo lake ni nini hasa!!??
Lengo ni kura za kanda ya ziwa wala hawana lolote
 
Au wewe unawaelewa???

Maana mapichapicha ya video Sasa imekuwa kama dozi!!

Mara wanatengeneza mabango ya kumsifia kila siku hadi sielewi...

Sioni wakifanya harakati kama hizo Kwa Samia Suhulu Hassan ambaye ndiyo wanategemea awe mgombea wao 2025.
Huyo samia ndiyo nani tena wengine atumjui au ni yule aliye nunua pichu za halili dubai kwa mamilioni ya shilingi pamoja na saa 6 ambazo kila moja ni mil zaidi ya mil 100
 
Back
Top Bottom