CCM mtaogopa siasa za wazi hadi lini?

Hali ni mbaya, huu uzi ambao wanaoshabikia CCM ni 1/20. Whereas 1paskali20jfmembers!!lakini uchaguzi ukipgw ccm 80% win over!!..
 

CCM sio chama bora, bali ni bora chama. Ukiona chama kina miaka karibia 60, lakini uwepo wake madarakani unategemea mbeleko ya vyombo vya dola tu, ujue hicho sio chama. Hadi sasa kiko madarakani sio kwasababu ya uwezo wake kisiasa, bali sababu za kihistoria, woga wa wananchi na mafungamano yake na vyombo vya dola.

Hivyo unavyoita vikao, sijui taratibu na vikao ni kwakuwa bado iko madarakani. Lakini hakuna uwezekano CCM ikabaki hai pindi ikipoteza dola, kwasababu haina msingi imara wa kisiasa, bali inategemea mbeleko ya vyombo vya dola tu. CCM naifananisha na KANU ya Kenya. KANU ilikuwa imara tu ilipokuwa madarakani, baada ya kupoteza madaraka ilipotea hadi leo haijaamka. Hiki ndio kitakachoikumba CCM wiki ya kwanza baada ya kutoka madarakani.
 
Hakuna chama nchi hii chenye uwezo wa kushindana na CCM kihoja au kiajenda popote pale,CCM Ni chama Kiongozi,Ni chama kilichobeba matumaini ya watanzania,NI CHAMA chenye uchungu na maisha ya watanzania,Ni chama chenye ajenda na Sera zinazogusa maisha ya watanzania,Ni chama kilichojipambanua kwa matendo katika kuwatumikia watanzania wanyonge wasio na sauti,Ni chama kilicho msitari wa mbele katika kuwatetea na kuwasemea watanzania,Ni chama ambacho wakati wote kipo upande wa watanzania ,Ni chama ambacho kinapinga kwa matendo aina yoyote ya dhuruma na unyanyasaji,Ni chama ambacho Ni Mfano Wa kuigwa Barani Afrika
 

Kwahuu umasikini uliopo unachoongea hapa unaonekana kituko.
 
Mkuu Tindo , vifu vingine huhitaji elimu ya chuo kikuu kuvibaini, unatumia tuu logical progression ya reality. Tanzania tunafanya sensa kila miaka 10, sensa ya 2010 tulikuwa milioni 50 eligible voters walikukuwa milioni 30, tukaandikisha wapiga kura milioni 20 waliojitokeza kupiga kura ni milioni 8', JK akachaguliwa kwa kura milioni 5!.

Tusiandikie mate wakati wino upo, tender kwenye data

14. Voting statistics

Tanzania: 2010 Presidential election results
Updated January 2010

The United Republic of Tanzania elections for parliament and the presidency were held on 31 October 2010.


Voting statistics
Registered Voters 20 137 303
Total votes 8 626 283
% Turnout 42.84
Valid votes 8 398 394
Spoilt votes 227 889
% Spoilt votes 2.64

Table source
Commonwealth 2010, 31.

Results
Candidate Party Votes % Vote
Jakaya Kikwete Chama Cha Mapinduzi (CCM) 5 276 827 62.83
WP Slaa Chama Cha Demokiasia na Maendeleo (CHADEMA) 2 271 941 27.05
Ibrahim Lipumba Civic United Front (CUF) 695 667 8.28
Peter Mziray Kuga Progressive Party of Tanzania (PPT-MAENDELEO) 96 933 1.15
Rungwe Hashim Spunda National Convention for Construction and Reform (NCCR-Mageuzi) 26 388 0.31
Muttamwega Bhatt Mgaywa Tanzania Labour Party (TLP) 17 462 0.21
Yahmi Nassoro Dovutwa United People's Democratic Party (UPDP) 13 176 0.16
Total
8 398 394 99.99

Table source
Commonwealth 2010, 31.

References
COMMONWEALTH 2010 Report of the Commonwealth Observer Group: Tanzania General Elections 31 October 2010
Angalia niliwashauri nini hawa jamaa zangu Elections 2015 - Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni ...

Tuje uchaguzi wa 2015
Total15,193,862100.00
Valid votes15,193,86297.42
Invalid/blank votes402,2482.58
Total votes15,596,110100.00
Registered voters/turnout23,161,44067.34
Source: NEC

Tulikuwa watu milioni 50, eligible voters ni milioni 30 waliojandikisha ni milioni 25 waliojitokeza kupiga kura ni milioni 23,

Njoo uchaguzi wa 2020
Registered voters/turnout
Total14,830,195100.00
Valid votes14,830,19598.27
Invalid/blank votes261,7551.73
Total votes15,091,950100.00

Tulikuwa milioni 55 eligible voters ni milioni 35, wakajiandikisa watu milioni 29 wakajitokeza kupiga kura watu milioni 15 CCM ikashinda kwa kura milioni 9.

Hivyo kwa kuitumia logical progression uchaguzi wa 2025 sasa tutakuwa milioni 65, eligible voters ni milioni 40, watajiakisha milioni 35, CCM itashinda kwa kura milioni 15.

Hizi ni numbers, dataz na statistics!, numbers don't lie!.
P
 
Kuna kitu kinaitwa "is" na "ought", is ni kile kilichopo na ought ni kile kilipaswa kiwe.

Ukifanya mashindano yoyote, wale bora ni top ten, kuna wa kwanza kwenye hao top ten atashika number 1, na wa mwisho kwenye top ten atashika number 10.

Ukifanya top ten ya walioshindwa kwenye hao wa mwisho nao wana top ten yao, kwenye kundi hilo pia kuna wa kwanza wao!.

Hivyo kwenye siasa za Tanzania, top party ni CCM, hakina mpinzani wala mshindani ndicho the best we have and it's the one and only!.

Hilo la CCM kuwa kama KANU au UNIP ya Zambia au MPC ya Malawi, CCM wameona kilichotokea, ndio maana hata Museveni anajua kitakachotokea akishindwa hivyo CCM inahakikisha kamwe haishindwi hivyo inatumia CCM kutumia Hooks & Crooks Kushinda Chaguzi, Inajua Ikishindwa Ndio Itakufa Jumla, Itakubali? na itatawala milele na milele, kubali kataa, unless otherwise!.
The best thing kwa Watanzania ni kuukubali ukweli huu Kupata maendeleo ya kweli, Watanzania ni lazima tujifunze kuukubali ukweli!. Hili la CCM kutawala milele ni kweli!.
P
 

Achana na data za kupika tafadhali. Tumia akili. Watu 61m, inawezekana vipi watu wazima wakawa wengi kuliko watoto? Idadi yetu watanzania iko kwa mfumo wa Msonge, watoto wako chini watu wazima wako juu. Sasa unaposema hivi unamaanisha watoto nchi hii ni wachache kuliko watu wazima!

Uchaguzi wa 2020 wanasema wapiga waliandikishwa 29m+, tukasema ni uongo wa wazi, haiwezekani watu wazima kuwa sawa na watoto. Na kama kweli waliandikishwa watu 29m+, maana yake ni kila watu wawili hapa nchini, mtu mmoja alijiandikisha kupiga kura. Je ni kweli kwenye familia yako kama mko 6, watatu walijiandikisha kupiga kura? Huu sio kwamba ni uongo tu, bali ni ujinga wa kitoto.
 

Kushinda uchaguzi by hooks and croocks haimaanishi hicho ni chama bora. Huenda neno ubora limepoteza maana yake siku hizi.
 
Tunarudi kule kule kwenye "is" and "ought", sisi waandishi ni kama watoto ndani ya familia.

Wewe ni mtu wa kawaida, a working class umepanga chumba kimoja kuanza maisha na mkeo chocolate color toka kijijini. Kila siku unaamka na kutoka kila asubuhi, kwenda kutafuta mkate, mke wako ni mashaalah, amejaaliwa, ni house wife, anashinda nyumbani, siku mambo ni mabaya, anashinda njaa mpaka kurudi na kuna siku unarudi tupu mnapiga pasi ndefu mnalalia maji!.

Next door anapanga kijana galacha shababi, six pack, mweupe wa point 5 kama Hemed PHD, anapanga ubazi mzima self contained!.

Licha ya wewe kukabiliwa na hali ngumu ya uchumi, mkeo ni mja mzito, na kuna siku kibao unamshindisha njaa, lakini ujauzito umemkubali, ananawiri na kupendeza!.

Siku ya siku ya kufungua, amekuzalia kidume, copyright na neighbor next door ila huyo ni mtoto wako hata kama ni copyright na galacha wa next door!.

Hali hiyo ndio hali yetu sisi waandishi wa habari wa Tanzania, unafuata ulichoelezwa na mamlaka, waliojandikisha ni milioni 29, waliojitokeza kupiga kura ni milioni 15!. You take it as it is, there is no way ya kuthibitisha otherwise.

Serikali ni kama mama kwenye jamii, Mama yako akikuambia huyu ndio baba yako, wewe kama mtoto mtiifu kwanza unatakiwa kumuamini mama, na pili kumheshimu huyo baba, hata kama umefanana copyright na baba wa jirani chumba cha pili!.

Serikali imesema imeandikisha wapiga kura milioni 29 kwenye BVR, majina yapo, picha zao zipo na biometrics data zao zipo, who M I ku doubt?.

Ungekuwa wewe ni media ungefanya nini?.
P
 

Nimekuelewa bro, ww ni media ambaye hata taarifa za upotoshaji unapaswa kuzisambaza ili mradi zinatoka serikalini. Je unatarajia na mimi au wengine wanaojitambua tuamini huo upotoshaji, kisa umeletwa na serekali? Unategemea tutaacha kutumia akili zetu kwenye mambo yaliyo wazi hivi?
 
Mmmh! Nakutabiria 2025 unapewa uDC...sema Amen.
 
Serikali ndio Mama, ukiambiwa na mama yako huyu ndio baba yako, would you doubt her kwasababu wewe umefanana na neighbor next door?.

Serikali nilisema imeandikisha watu milioni 29, then ni watu milioni 29!.
P
 
Ccm wamewafanyia nn, hivi mke mwenza akizuiwa na mwenziwe asilale na mume wake atafanyaje, chadema na act mjibu maana mnaaibisha nchi na kuitangaza vibaya
 
Serikali ndio Mama, ukiambiwa na mama yako huyu ndio baba yako, would you doubt her kwasababu wewe umefanana na neighbor next door?.

Serikali nilisema imeandikisha watu milioni 29, then ni watu milioni 29!.
P

Mama yako hata akae uchi mbele yako kwa kulazimisha huyu ndio baba yako, kama sio, sio tu. Labda uwe zwazwa, au huna namna ya kuishi, zaidi ya kumtegemea yeye ndio utakubali ili usife njaa. Lakini ukweli unabaki palepale kuwa sio baba yako fullstop.
 
Mama yako hata akae uchi mbele yako kwa kulazimisha huyu ndio baba yako, kama sio, sio tu. Labda uwe zwazwa, au huna namna ya kuishi, zaidi ya kumtegemea yeye ndio utakubali ili usife njaa. Lakini ukweli unabaki palepale kuwa sio baba yako fullstop.
Huo labda ni ubishi wa kizungu, anayemjua baba yako ni Mama yako, huwezi kumbishia!. Ndio maana wenzetu Waislamu wanazika kwa jina la mama.
P
 
Huo labda ni ubishi wa kizungu, anayemjua baba yako ni Mama yako, huwezi kumbishia!. Ndio maana wenzetu Waislamu wanazika kwa jina la mama.
P

Mtu kuwa mama yako haimaanishi anateka ufahamu wako. Haitoshi yeye kukuambia kuwa ni baba yako, na ndio ikawa hitimisho. Ukiwa huna ujanja nje ya maelekezo yake utakubali ili usife njaa, huku ukiwa unamchora.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…