CCM mtaogopa siasa za wazi hadi lini?

CCM mtaogopa siasa za wazi hadi lini?

CCM ni chama kina mifumo yake ya uendeshaji na maamuzi ya kichama yatatokana na vikao, ila pia viongozi wa CCM wanaweza kuamua maamuzi binafsi bila vikao kama uamuzi wa katiba sio kipaumbele changu ni uamuzi binafsi wa kiongozi ambao haukutokana na vikao, ilani ya CCM ya 2015 -2020 ilikuwa na katiba mpya, ila ilani ya 2020- 2025 issues ya katiba iliondolewa, ndio maana nimewashauri watu, kama ilani ya 2020 ilikuwa na Katiba, JPM akasema katiba sio kipaumbele chake na hatukumshinikiza, hii ilani ya sasa ya CCM haina issue ya katiba hivyo tusimshinikize Samia kuhusu katiba mpya.
P
Ndiyo maana nasema kinacho fanyika ndani ya CCM ni utashi wa anayekuwa madarakani,katiba ya JMT na ya CCM zote zimeyumba,athari za utashi wa mtu badala ya nguvu ya organs inaweza kulitumbukiza taifa kwenye nyakati nguvu
 
Achana na data za kupika tafadhali. Tumia akili. Watu 61m, inawezekana vipi watu wazima wakawa wengi kuliko watoto? Idadi yetu watanzania iko kwa mfumo wa Msonge, watoto wako chini watu wazima wako juu. Sasa unaposema hivi unamaanisha watoto nchi hii ni wachache kuliko watu wazima!

Uchaguzi wa 2020 wanasema wapiga waliandikishwa 29m+, tukasema ni uongo wa wazi, haiwezekani watu wazima kuwa sawa na watoto. Na kama kweli waliandikishwa watu 29m+, maana yake ni kila watu wawili hapa nchini, mtu mmoja alijiandikisha kupiga kura. Je ni kweli kwenye familia yako kama mko 6, watatu walijiandikisha kupiga kura? Huu sio kwamba ni uongo tu, bali ni ujinga wa kitoto.
Cooked data
 
Kushinda uchaguzi by hooks and croocks haimaanishi hicho ni chama bora. Huenda neno ubora limepoteza maana yake siku hizi
Ubora wa ungepimwa kwa kushinda chaguzi kweli CCM ingekuwa bora sana,angalia aina ya chaguzi zetu huenda ndiyo chaguzi chafuzi mbaya sana kutokea duniani,votes za voters hazi determine mshindi,waliokaa mbele ya voters wasimamizi wa chaguzi ndiyo wanaamua nani kashinda bila kuzingatia idadi ya kura.

Na kwa kuwa refari wao ni vyombo vya usalama imesababisha kupoteza uhalali wa kuwa chama cha siasa.

Ndani yake anayesema malkia yuko uchi hata kama kweli yuko uchi atashughulikiwa ipasavyo kumuondoa kwenye motion.
 
Wanaopaswa kuwa chama cha mfano ni CDM kwa kuwa wamejifunza siasa za kisasa toka magharibi - ajabu ukipima uendeshaji wa CDM umekuwa wa kimwinyi - ukimgusa Mwenyekiti unatimuliwa @ Zitto, Mabrouk, Wangwe, Sumaye, Lowassa nk
 
Wanaopaswa kuwa chama cha mfano ni CDM kwa kuwa wamejifunza siasa za kisasa toka magharibi - ajabu ukipima uendeshaji wa CDM umekuwa wa kimwinyi - ukimgusa Mwenyekiti unatimuliwa @ Zitto, Mabrouk, Wangwe, Sumaye, Lowassa nk
No comparison kwenye mada hii,CDM hajatajwa humu ila kama unataka tufanye comparison lete mada tuichambua
 
Back
Top Bottom