Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,434
SEHEMU YA KWANZA
Hatimaye kiini macho cha muungano kinakaribia kukiumbua chama chetu kikongwe cha CCM. Kwa miaka 50 sasa, ccm iliwafanyia wananchi mchezo wa mazingaombwe and managed to get away with it. Lakini kama ambavyo nimekuwa nikisema over and over again, it reaches a to point when:
The "trick" nayozungumzia hapa ni suala zima la mfumo wa muungano wa serikali mbili (sera rasmi ya ccm), mfumo ambao umetawaliwa zaidi na kiini macho (illusion) kuliko ukweli au uhalisia wa mambo. Kwa mujibu wa dictionary, an illusion is:
Kitendo cha Chama Cha Mapinduzi kudanganya umma kwa miaka karibia 50 kwamba mfumo wa muungano uliopo ni mfumo wa serikali mbili, is deceiving the people kwani for 50 years, the party has been busy producing a false impression before the people that the Government of Tanganyika doesn't exist while in reality, it has been in existence since 1964.
Kada wa CCM na Mwanasiasa Mkongwe kutoka Zanzibar ambae pia historia inamweka kama mmoja wa wajumbe thelathini wa Revolutionary Council (1964), Mzee Hassan Nassor Moyo alinukuliwa na Mwandishi wa Gazeti la ----- toleo la Oktoba 3-9, 2013 akisema maneno yafuatayo:
Huu ndio uhalisia wa mambo, uhalisia ambao viongozi wa CCM wameamua kujitoa mhanga kuugeuza kuwa "kiini macho" (illusion) kwa miaka 50 ya muungano. Tulitarajia viongozi vijana ndani ya ccm kama kina Nape Nnauye ndio wawe mstari wa mbele kukirekebisha chama katika kosa lake hili ambalo kimsingi, huko tuendako ndio litakuwa ni sanda katika jeneza la ccm kama chama tawala nchini Tanzania. Nape Nnauye amefika hapo alipo kutokana na umahiri wake wa kusimamia haki, uwazi, na ukweli lakini kumbe ilikuwa ni danganya toto kwani lilipokuja suala la kusimamia haki ya msingi kabisa ya watanganyika, ikizingatiwa kwamba haki yetu kikatiba imeshaporwa na katiba ya zanzibar (2010), nape na viongozi wenzake ndani ya chama wameshindwa kusimamia haki yetu ya msingi na ya kikatiba. Badala yake, tumemsikia nape na wenzake wakitoa maneno ya kejeli na mara nyingine matusi kwa wananchi (hata wazee wao) wanaotetea haki ya Tanganyika katika muungano wetu.
Kama vile ccm imeshindwa kabisa kusoma alama za nyakati na kuamua kufa na tai yake shingoni, wiki chache kuelekea bunge la Katiba, CCM kupitia Nape ilikuja na tamko la CCM (NEC) ambalo lilisisitiza kwamba chama kinaelekea bungeni kwenda kupigania msimamo na sera yake ya serikali mbili ndani ya muungano. Swali kwamba ccm iliwashirikisha vipi watanzania (let alone wanachama wa ccm) kabla ya kufikia uamuzi mkubwa kama huu, ni swali ambalo limekosa wa kulijibu ipasavyo. Wanaojitahidi kulivaa swali hili huwa wanaishia kuisingizia historia. Wanasahau kwamba historia kamwe haiwezi singiziwa, na hili litazidi kuwa dhahiri huko tuendako.
Baada ya chama kuingia kwenye bunge la katiba na msimamo wake wa serikali mbili licha ya rais kuhimiza vyama kuacha tabia ya kuweka mbele itikadi za vyama na badala yake maslahi ya taifa, zimeenea taarifa kwamba ccm sasa imekuja na waraka wa rasimu ya katiba mbadala, habari ambazo bado hazijakanushwa na ccm hadi sasa. Cha ajabu ni kwamba ndani ya waraka huo, inadaiwa kwamba chama kinapendekeza uwepo wa baraza la wawakilishi la "Tanzania bara" kwa ajili ya kushughulikia masuala ya bara tu. Hii ni ajabu kwani rasimu ya katiba (2013 na hata mkataba wa muungano (1964) hakuna pahala inataja "Tanzania Bara", hivyo kutuacha na swali la msingi kabisa kwamba je, Zanziba iliungana na Tanzania Bara?
Haya ndio mazingaombwe ya ccm ambayo ni dhahiri yanaelekea ukingoni kwani kuna kila dalili sasa kwamba "our great magician is running out of tricks"; swali linalofuatia ni je,
*How many more tricks could CCM have in the hat?
Mzee Mwanakijiji alijadili vizuri suala hili katika mjadala wetu mwingine.
Kilichodhahiri ni kwamba mashabiki wengi sana tayari wameshatoka kwenye ukumbi huu wa mazingaombwe baada ya kuanza kumshtukia mwanamazingaombwe na hata wale ambao bado wapo ndani ya ukumbi, wengi wao hawapo tena kushangilia yanayojitokeza jukwaani bali wanajadili yalio nje ya jukwaa.
Wanachojadili wengi ni jinsi gani ccm baada ya kutambua kwamba umma utaiumbua 2015, imefikia hatua ya kufanya vituko ndani ya bunge la katiba, kinyume kabisa na matarajio ya wengi ambao walitegemea ccm itaenda kutetea sera yake ya muungano wa serikali mbili kwa hoja. Moja ya vituko hivi ni kile cha ccm aidha kwa kujua au kutokujua, kuunga mkono mfumo wa serikali tatu kwa kupendekeza baraza la wawakilishi la Tanzania Bara pekee, lakini hapo hapo chama kikisema kwamba hakita yumba na msimamo wake wa serikali mbili (mfano rejea kauli ya waziri mkuu pinda hivi karibuni). Katika hili, nadhani mzee hassan nassor moyo alilizungumzia vizuri katika mahojiano yake na gazeti la ----- mwaka jana aliposema hivi:
Maneno haya ya mzee Moyo yanazidi kuelezea uhalisia wa mambo, kwani iwapo ni kweli wana ccm kwenye bunge la katiba sasa wamefikia hatua ya kupendekeza uwepo wa baraza la wawakilishi la kushughulikia masuala ya "Tanzania Bara", basi kweli kuna haja ya kuwapima akili kwani kwa maana hii, uelewa wao ni kwamba Zanzibar iliungana na Tanzania Bara na sio Tanganyika.
----- pia linamnukuu Mzee Moyo Katika kongamano la kamati ya maridhiano lililofanyika hoteli ya bwawani mwaka jana (2013, akisema:
Wajumbe wa kongamano wakajibu "matatuuuuuu!"
Mzee moyo akauliza:
Lakini kama tunakumbuka vyema, vituko vya ccm vilivyoashiria kilometa za mwisho za safari ya mazingaombwe vilianzia pale wazanzibari walipofanya mambo makuu mawili muhimu:
1. Kujipatia Katiba yao (2010)inayoitambua Zanzibar kama "moja ya nchi zinazounda JMT". Hii ni tofauti na Katiba yake ya awali ambayo iliitambua zanzibar kama "sehemu ya jamhuri ya muungano wa Tanzania".
Tume ya katiba chini ya jaji warioba pia inaakisi hili katika utangulizi wa rasimu iliyopo mbele ya wajumbe wa katiba dodoma leo.
2. Serikali ya CCM ilipopeleka muswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba kwa wazanzibari, ndugu zetu wazanzibari kama iliyo jadi yao kuipigania Tanganyika kama njia yao ya kufanikisha zanzibar kutambulika kama dola kamili, waliuchana na kuuchoma moto muswada ule kwani ulizuia suala la muungano kuwa sehemu ya mjadala kama vile muungano ni suala ordained from God na sio suala linalojengwa na kulindwa na watu/wananchi. Isingekuwa busara za waziri sitta ambae ndiye aliyeiwakilisha serikali katika halfa ile, pengine leo tungekuwa tunaongea mengine.
Itaendelea...
Cc Nguruvi3, Nape Nnauye JokaKuu Jasusi happyfeet, Bongolander, Mag3 Candid Scope MTAZAMO Kimbunga Mkandara Pasco, Zinedine, Zakumi, gfsonwin Kobello, zumbekuu, Kichuguu JingalaFalsafa ZeMarcopolo Ritz, Mzee Mwanakijiji, zomba MwanaDiwani, EMT, AshaDii, ukwelikitugani, TIMING, na wengine wote niliowasahau;
Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Hatimaye kiini macho cha muungano kinakaribia kukiumbua chama chetu kikongwe cha CCM. Kwa miaka 50 sasa, ccm iliwafanyia wananchi mchezo wa mazingaombwe and managed to get away with it. Lakini kama ambavyo nimekuwa nikisema over and over again, it reaches a to point when:
Even a magician runs out of tricks
The "trick" nayozungumzia hapa ni suala zima la mfumo wa muungano wa serikali mbili (sera rasmi ya ccm), mfumo ambao umetawaliwa zaidi na kiini macho (illusion) kuliko ukweli au uhalisia wa mambo. Kwa mujibu wa dictionary, an illusion is:
something that deceives by producing a false or misleading impression of reality
Kitendo cha Chama Cha Mapinduzi kudanganya umma kwa miaka karibia 50 kwamba mfumo wa muungano uliopo ni mfumo wa serikali mbili, is deceiving the people kwani for 50 years, the party has been busy producing a false impression before the people that the Government of Tanganyika doesn't exist while in reality, it has been in existence since 1964.
Kada wa CCM na Mwanasiasa Mkongwe kutoka Zanzibar ambae pia historia inamweka kama mmoja wa wajumbe thelathini wa Revolutionary Council (1964), Mzee Hassan Nassor Moyo alinukuliwa na Mwandishi wa Gazeti la ----- toleo la Oktoba 3-9, 2013 akisema maneno yafuatayo:
Tuna serikali ya mapinduzi Zanzibar na serikali ya Tanganyika ambayo ipo katika serikali ya jamhuri ya muungano. Kwahiyo ni serikali tatu tokea huko nyuma. Sasa ukiniambia unataka serikali mbili, nakuachia wewe mwenyewe uendelee na ujinga wako
Huu ndio uhalisia wa mambo, uhalisia ambao viongozi wa CCM wameamua kujitoa mhanga kuugeuza kuwa "kiini macho" (illusion) kwa miaka 50 ya muungano. Tulitarajia viongozi vijana ndani ya ccm kama kina Nape Nnauye ndio wawe mstari wa mbele kukirekebisha chama katika kosa lake hili ambalo kimsingi, huko tuendako ndio litakuwa ni sanda katika jeneza la ccm kama chama tawala nchini Tanzania. Nape Nnauye amefika hapo alipo kutokana na umahiri wake wa kusimamia haki, uwazi, na ukweli lakini kumbe ilikuwa ni danganya toto kwani lilipokuja suala la kusimamia haki ya msingi kabisa ya watanganyika, ikizingatiwa kwamba haki yetu kikatiba imeshaporwa na katiba ya zanzibar (2010), nape na viongozi wenzake ndani ya chama wameshindwa kusimamia haki yetu ya msingi na ya kikatiba. Badala yake, tumemsikia nape na wenzake wakitoa maneno ya kejeli na mara nyingine matusi kwa wananchi (hata wazee wao) wanaotetea haki ya Tanganyika katika muungano wetu.
Kama vile ccm imeshindwa kabisa kusoma alama za nyakati na kuamua kufa na tai yake shingoni, wiki chache kuelekea bunge la Katiba, CCM kupitia Nape ilikuja na tamko la CCM (NEC) ambalo lilisisitiza kwamba chama kinaelekea bungeni kwenda kupigania msimamo na sera yake ya serikali mbili ndani ya muungano. Swali kwamba ccm iliwashirikisha vipi watanzania (let alone wanachama wa ccm) kabla ya kufikia uamuzi mkubwa kama huu, ni swali ambalo limekosa wa kulijibu ipasavyo. Wanaojitahidi kulivaa swali hili huwa wanaishia kuisingizia historia. Wanasahau kwamba historia kamwe haiwezi singiziwa, na hili litazidi kuwa dhahiri huko tuendako.
Baada ya chama kuingia kwenye bunge la katiba na msimamo wake wa serikali mbili licha ya rais kuhimiza vyama kuacha tabia ya kuweka mbele itikadi za vyama na badala yake maslahi ya taifa, zimeenea taarifa kwamba ccm sasa imekuja na waraka wa rasimu ya katiba mbadala, habari ambazo bado hazijakanushwa na ccm hadi sasa. Cha ajabu ni kwamba ndani ya waraka huo, inadaiwa kwamba chama kinapendekeza uwepo wa baraza la wawakilishi la "Tanzania bara" kwa ajili ya kushughulikia masuala ya bara tu. Hii ni ajabu kwani rasimu ya katiba (2013 na hata mkataba wa muungano (1964) hakuna pahala inataja "Tanzania Bara", hivyo kutuacha na swali la msingi kabisa kwamba je, Zanziba iliungana na Tanzania Bara?
Haya ndio mazingaombwe ya ccm ambayo ni dhahiri yanaelekea ukingoni kwani kuna kila dalili sasa kwamba "our great magician is running out of tricks"; swali linalofuatia ni je,
*How many more tricks could CCM have in the hat?
Mzee Mwanakijiji alijadili vizuri suala hili katika mjadala wetu mwingine.
Kilichodhahiri ni kwamba mashabiki wengi sana tayari wameshatoka kwenye ukumbi huu wa mazingaombwe baada ya kuanza kumshtukia mwanamazingaombwe na hata wale ambao bado wapo ndani ya ukumbi, wengi wao hawapo tena kushangilia yanayojitokeza jukwaani bali wanajadili yalio nje ya jukwaa.
Wanachojadili wengi ni jinsi gani ccm baada ya kutambua kwamba umma utaiumbua 2015, imefikia hatua ya kufanya vituko ndani ya bunge la katiba, kinyume kabisa na matarajio ya wengi ambao walitegemea ccm itaenda kutetea sera yake ya muungano wa serikali mbili kwa hoja. Moja ya vituko hivi ni kile cha ccm aidha kwa kujua au kutokujua, kuunga mkono mfumo wa serikali tatu kwa kupendekeza baraza la wawakilishi la Tanzania Bara pekee, lakini hapo hapo chama kikisema kwamba hakita yumba na msimamo wake wa serikali mbili (mfano rejea kauli ya waziri mkuu pinda hivi karibuni). Katika hili, nadhani mzee hassan nassor moyo alilizungumzia vizuri katika mahojiano yake na gazeti la ----- mwaka jana aliposema hivi:
...anayesema hivyo Tanzania bara imeungana na zanzibar huyo inabidi apelekwe hospitali ya wagonjwa wa akili kabisa kabisa. Maana ni kitu cha wazi kinachoonyesha kwaba nchi mbili ndizo zilizofanya jamhuri ya muungano, sasa wewe leo unatuambia Tanzania Bara imeungana na Zanzibar? Ulipata wapi habari hiyo? Wewe si bora tukupeleke hospitali ya Milembe kwa Tanganyika na Kidongo chekunda unguja? Ndio maana yake. Tujue kwamba ni nchi mbili: Tanganyika na zanzibar ndizo ziliungana
Maneno haya ya mzee Moyo yanazidi kuelezea uhalisia wa mambo, kwani iwapo ni kweli wana ccm kwenye bunge la katiba sasa wamefikia hatua ya kupendekeza uwepo wa baraza la wawakilishi la kushughulikia masuala ya "Tanzania Bara", basi kweli kuna haja ya kuwapima akili kwani kwa maana hii, uelewa wao ni kwamba Zanzibar iliungana na Tanzania Bara na sio Tanganyika.
----- pia linamnukuu Mzee Moyo Katika kongamano la kamati ya maridhiano lililofanyika hoteli ya bwawani mwaka jana (2013, akisema:
...sasa kwa utaratibu au kutoa mfano mzuri ni kwamba wewe umekwenda sokoni, umenunua machungwa matatu, moja ukaliweka kwenye mkoba mmoja na mawili ukayatia kwenye mkoba wa pili, utakuwa na machungwa mangapi?
Wajumbe wa kongamano wakajibu "matatuuuuuu!"
Mzee moyo akauliza:
sasa leo tunaambiwa tuna machungwa mawili kisa tu tumetia kwenye mikoba miwili?
Lakini kama tunakumbuka vyema, vituko vya ccm vilivyoashiria kilometa za mwisho za safari ya mazingaombwe vilianzia pale wazanzibari walipofanya mambo makuu mawili muhimu:
1. Kujipatia Katiba yao (2010)inayoitambua Zanzibar kama "moja ya nchi zinazounda JMT". Hii ni tofauti na Katiba yake ya awali ambayo iliitambua zanzibar kama "sehemu ya jamhuri ya muungano wa Tanzania".
Tume ya katiba chini ya jaji warioba pia inaakisi hili katika utangulizi wa rasimu iliyopo mbele ya wajumbe wa katiba dodoma leo.
2. Serikali ya CCM ilipopeleka muswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba kwa wazanzibari, ndugu zetu wazanzibari kama iliyo jadi yao kuipigania Tanganyika kama njia yao ya kufanikisha zanzibar kutambulika kama dola kamili, waliuchana na kuuchoma moto muswada ule kwani ulizuia suala la muungano kuwa sehemu ya mjadala kama vile muungano ni suala ordained from God na sio suala linalojengwa na kulindwa na watu/wananchi. Isingekuwa busara za waziri sitta ambae ndiye aliyeiwakilisha serikali katika halfa ile, pengine leo tungekuwa tunaongea mengine.
Itaendelea...
Cc Nguruvi3, Nape Nnauye JokaKuu Jasusi happyfeet, Bongolander, Mag3 Candid Scope MTAZAMO Kimbunga Mkandara Pasco, Zinedine, Zakumi, gfsonwin Kobello, zumbekuu, Kichuguu JingalaFalsafa ZeMarcopolo Ritz, Mzee Mwanakijiji, zomba MwanaDiwani, EMT, AshaDii, ukwelikitugani, TIMING, na wengine wote niliowasahau;
Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Last edited by a moderator: