Vyanzo vyangu vya uhakika vinanieleza kwamba kauli ya
Nape Nnauye hivi karibuni kwamba NEC imeazimia kwamba CCM inaenda na msimamo mmoja kwenye bunge la katiba kupigania sera ya ccm ya serikali mbili ni taarifa zisizo sahihi. Kwa mujibu wa chanzo changu, kikao kile kilimalizika huku wajumbe wakiwa wamegawanyika kuhusiana na msimamo wa chama juu ya mfumo wa muungano. Inasemekana kwamba wapo waliojenga hoja kwamba sera ya ccm haitakelezeki hivyo kuna haja ya serikali tatu na hoja hii kupokewa kwa nguvu sana ndani ya kikao, lakini pia wapo wachache walioendelea na msimamo wa serikali mbili ingawa makada hawa hawakuweza kufafanua wala kutetea kwanini serikali mbili ndio mfumo unaofaa. Iwapo walishindwa kusimamia hoja yao ndani ya chama, ni vigumu kuelewa wataisimamia vipi kwenye bunge la katiba. Ndio maana nimekuwa nikijadili sana kwamba kuna uwezekano wa makada wa ccm kumtumia mwalimu vibaya katika hoja zao pamoja na kuwatishia watanzania juu ya athari za serikali tatu kwa mujibu wa hoja zao za kutunga.
Kimsingi, sasa ni wazi kwamba ccm imebadilisha msimamo wake juu ya mfumo wa muungano, lakini inajisikia aibu kuja hadharani kuweka hilo wazi. Matokeo yake ni nape kuja hadharani kusema kwamba chama chake bado kinaamini katika muunda wa serikali mbili huku akielezea jinsi gani anaamini kero za muungano zitapata ufumbuzi.
Nguruvi3 amejadili vyema jinsi gani such a belief na ndoto za alinacha kwani iwapo kero hizi zimeshindwa kupata ufumbuzi kwa miaka 50, tena chini ya ccm ya wakati ule ambayo ili command legitimacy kubwa sana mbele ya umma, tena kwa hiyai ya wananchi, iweje leo ccm ya kina nape ambayo kila kada ni msemaji wa chama, ccm iwe na uwezo wa kutatua kero za muungano? Tutazijadili kero hizi punde ili kupima hoja ya nape lakini kwa sasa ebu tuchambue zaidi ukinyonga wa ccm katika suala hili la mfumo wa muungano, hoja ya msingi ikiwa ni kwamba tamati ya mazingaombwe ya mfumo wa serikali mbili imeanza kuwa dhahiri kama mabandiko yangu ya awali yalivyoweka wazi.
Swali linalofuatia ni je, kwanini ccm imebadili msimamo wake wa awali?
Jibu ni kwamba, kama nilivyojadili awali, legitimacy ya CCM kutawala nchi haijawahi kuwa ni Katiba ya nchi as source of legitimacy bali mambo mengine (azimio la arusha na ujamaa, historia ya TANU kutetea haki za wanyonge ndani na nje ya nchi, na charisma ya baba wa taifa, Mwalimu Nyerere). Kama nilivyofafanua awali, all the three sources of legitimacy have now been eroded, mostly kwa sababu ya internal factors - ccm yenyewe kuliko external factors. Sasa CCM wamezinduka usingizini na kubaini kwamba bila ya uangalifu, msimamo wao sio tu utavunja muungano bali pia utakipotezea ushindi chama 2015.
CCM sasa imegundua kwamba msimamo wake kisera regardless how much msimamo huu unapakwa "make up" na kufanyiwa "face lift", ukweli kwamba serikali mbili hazitekelezeki ni ukweli usiokwepeka, and again kuendelea kulazimisha "face lift" kisera huku msimamo ukiwa ni serikali mbili mwisho wake ni kuvunja muungano.
Kinachojadiliwa kwamba ni nyaraka ya ccm ambayo imebeba mawazo mbadala ya rasimu ya pili ya katiba, inasemekana content yake kubwa ni matokeo ya waraka kutoka idara ya siasa na uhusiano wa kimataifa ya CCM ambayo ipo chini ya Dr. Migiro. Katika waraka huu ambao aliuwasilisha kwenye NEC iliyomaliza kikao chake hivi karibuni, kikao ambacho
Nape Nnauye anatueleza kwamba chama kiliondoka na msimamo mmoja wa kusimamia serikali mbili, inasemekana kwamba mapendekezo ya migiro katika kikao kile cha NEC yalithibitisha kwamba kuendelea na mfumo wa serikali mbili ni kuchongea jeneza muungano baina ya Tanganyika na Zanzibar. Jina la Tanganyika inasemekana linatajwa wazi wazi ndani ya vikao vya chama na wajumbe lakini wasemaji wa chama wakija hadharani, inatajwa "Tanzania Bara".
Msimamo huu wa migiro unatufanya tujiulize maswali kadhaa:
1. Was it a coincidence kwa Rais kumteua kuwa waziri wa sheria ba katiba?
2. Je, sasa tunapata idea juu ya kwanini Kikwete aliwaonya wana ccm kujiandaa kisaikolojia na ujio wa serikali tatu?
3. The fact kwamba haya yanaendelea huku kiongozi mkuu wa shughuli za serikali ambae pia ni mwenyekiti wa wabunge wa CCM Mizengo Pinda anasema haitambui Tanganyika, je maana yake ni kwamba ccm ipo tayari to settle na serikali tatu ilimradi ile ya tatu isiitwe Tanganyika?
Hapo juu niliahidi kurejea kujadili kero za muungano, kero ambazo Nape Nnauye katueleza kwamba ni changamoto ambazo zitafanyiwa kazi. Katika hili,
Nguruvi3 ameuliza maa 17, mara 20, je ccm ina mwarubaini wakati huu baada ya kukosa tiba ya ugonjwa husika kwa miaka 50? Is there a medical break through that ccm is about to reveal? Its obvious kwamba jibu ni hapana, unless tushauriane kuwa wavumilivu kusubiri press conference ya Nape kwamba sasa chanjo ya kero za muungano imepatikana.
Naungana na
Nguruvi3 na wengine kwamba kero za muungano haziwezi kupatiwa ufumbuzi chini ya serikali mbili. Tuangalie mambo ambayo nape anayaita changamoto za muungano na ana amini yatapatiwa ufumbuzi chini ya serikali mbili.
*kwanza ni suala la rais wa znz kuondolewa kuwa makamo wa rais wa JMT. Kama tunakumbuka vyema, miaka ya sitini, mwalimu alielezea umma kwamba mfumo wetu tumeiga ule wa unitary system wa UK. Mfumo huu ulifanikiwa kwasababu ya mfumo wa chama kimoja, ndio maana baada ya ujio wa vyama vingi, kuendelea na muungano wa "unitary" kungepelekea hali ya znz kuwa na ais wa chama kimoja na bara kuwa na rais wa chama kingine. Ndio maana akateuliwa jaji bomani kuja na solution ambae baadae akaja na wazo la mgombea mwenza kwa kuiga "federal structure" ya USA. Tukumbuke kwamba mkataba wa muungano (1964) ulilenga shirikisho (federalism) na kama ungefuatwa tangia mwanzo, kero za muungano zingekuwa chache sana, bearing in mind kwamba in any union, there's no absolute stability, but relative stability; ukweli huu upo USA, Australia, UK, Switzerland etc.
*pili (kero nyingine) ni ukweli kwamba chini ya serikali mbili, tutalazimika kuwa na mambo mengi ya muungano, suala ambalo litazidi kuimeza zanzibar. Tukumbuke kwamba for 50 years, the "union question" has always been the "zanzibar question". Katika hili, jaji warioba pia amelijadili kwa sura ya "koti la muungano" ambalo limevaliwa na Tanganyika.
*tatu, lenye uhusiano na hilo hapo juu la pili ni kwamba, chini ya serikali mbili, ni vigumu kutenganisha mamlaka ya serikali ya JMT kwa masuala ya muungano na mamlaka ya serikali hiyo hiyo kwa masuala yasio ya muungano. Jaji warioba alifafanua sana tatizo hili wakati wa halfa ya kuwasilisha rasimu ya pili ya katiba, na pia
Nguruvi3 na wadau wengine humu wamelifafanua vizuri suala hili. Kimsingi, mfumo wa serikali mbili unaopigiwa debe na ccm unafukia madudu mengi sana yanayohusiana na mgawanyiko wa mapato na matumizi juu ya uendeshaji wa serikali ya muungano, na hii ni moja ya kero kubwa sana ambazo sasa watanganyika wameamua kuivalia njuga. Serikali mbili haiwezi kutatua kero hii bali serikali tatu kama nilivyowahi jadili kwa kina elsewhere, vinginevyo ikishindikana, kama asemavyo
Nguruvi3, na pia job ndugai kaanza kutumia maneno haya haya, tupasue jahazi na kila mtu abebe mbao zake. CCM inajaribu to repair meli inayovuja, tena ikiwa katikati ya bahari. Its nonsense, its a non starter.
*tatizo lingine ambalo haliwezi kupatiwa ufumbuzi na serikali mbili ni the obvious one - katiba ya znz (2010) pamoja na yaliyomo mle, mambo ambayo znz haiwezi kurudi tena nyuma juu yake. CCM inajaribu kupigania katiba ya sasa ya JMT inayotambulisha Tanzania kama nchi moja wakati zanzibar kimsingi kama anavyosema
Nguruvi3, imeshauvunja muungano uliopo. Katiba ya znz inaitambua znz kama moja ya nchi mbili zinazounda JMT.
Itaendelea.
Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums