CCM Na Bunge La Katiba: Mazingaombwe yanayoelekea ukingoni

CCM Na Bunge La Katiba: Mazingaombwe yanayoelekea ukingoni

Tuna tabia ya kuyazunguka matatizo badala ya kuya-address na kusonga mbele. As it stands, Muungano huu una matatizo makubwa. Lakini badala ya kuyatatua tunayazingukia kwa hoja za serikali tatu, serikali mbili na mabunge matatu, huku Rais wa Tanzania akidai kuwa Zanzibar ni nchi kwa ndani lakini nusu nchi kwa nje.

Kama Zanzibar ingekuwa nchi kwa ndani lakini nusu nchi kwa nje, basi kwenye ile kesi ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar dhidi ya Machano Khamis Ali na wengine 17, Makakama Kuu isingeamua kuwa treason is a "Union matter and not a matter exclusively for the Revolutionary Government of Zanzibar" simply kwa sababu treason inakuwa committed internally and not externally. Na sasa katiba ya Zanzibar inasema wazi kwenye Ibara wa kwanza kuwa "Zanzibar ni Nchi [emphasis added] which may suggest that treason can now be committed against Zanzibar.

Solution pekee ya hiki kiini macho cha Muungano ni referendum ambapo wananchi wa pande zote wataamua wenyewe na bila kushurutishwa kama wanautaka au hawautaki muungano na kama bado wanautaka, wangependa kuwa na muungano wa aina gani. Kama wakisema hawautaki Muungano, then that should be it. Their wishes should be respected. Wengine wanadai kuwa referendum itaweka "bad precedent". This is probably because wananchi hawajazoeshwa kujiamulia mambo yao wenyewe. We seem to trust politicians with their rhetoric promises kutuamulia mambo.

The right of peoples to determine themselves (the right to self-determination) iliishia siku ile tulipojipatia uhuru. Baada ya hapo, haki hiyo ilibadilika na kuwa the "right of politicians to determine themselves". Hiki ndicho kinachoendelea sasa hivi huko Dodoma kwenye "Bunge la Katiba" ambalo limejaa wanasiasa wanaodai kuwa wanawawakilisha wananchi ambao hawakuwachagua kwa ajili ya kuwatengenezea katiba mpya.

Mkuu naona una hoja ya msingi juu ya wananchi kuamua hatima yao. Lakini kwa wananchi hawa ambao bado maamuzi yao yanakuwa influenced na vyama bado siasa zitaamua hatima. Na katika muktadha huo si sahihi vyama vinavyopigania idadi tofauti za serikali kutojibainisha vinataka nini hasa, ndio maana nikasema walau CCM anaelewa kama chama anataka nini na kwa mfumo upi, ila vyama vingine vinalilia serikali tatu ila mfumo ambao wanaupigania hasa haujulikani.
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Mkuu naona una hoja ya msingi juu ya wananchi kuamua hatima yao. Lakini kwa wananchi hawa ambao bado maamuzi yao yanakuwa influenced na vyama bado siasa zitaamua hatima. Na katika muktadha huo si sahihi vyama vinavyopigania idadi tofauti za serikali kutojibainisha vinataka nini hasa, ndio maana nikasema walau CCM anaelewa kama chama anataka nini na kwa mfumo upi, ila vyama vingine vinalilia serikali tatu ila mfumo ambao wanaupigania hasa haujulikani.

Lakini maoni ya chama fulani do not necessarily represent the views of the people. Ifike sehemu wananchi wapewe mamlaka yao ya kujiamulia mambo yao wenyewe. Tume ya Warioba si inadai kuwa ilichofanya ni kukusanya maoni ya wananchi? Kama ni hivyo, maoni ya hao wananchi yalikuwaje kuhusiana na muungano?

Tume hiyo pia ilikusanya pia maoni ya chama cha CCM kama institution? Maoni ya chama hicho yalikuwaje? Yaliwekwa kwenye Rasimu ya Katiba? Kama hayakuwekwa kwenye hiyo Rasimu labda ndiyo maana CCM imeamuwa kuyapeka maoni yake moja kwa moja kwenye Bunge la Katiba? If that is the case, then maoni ya hicho chama yanaweza ku-override maoni yaliyotolewa na wananchi juu ya serikali tatu? Nimeuliza haya maswali as if I believe (in fact I don't) that rasimu ya Katiba, hasa katika suala la serikali tatu, inabeba maoni ya Watanzania.

Kuhusiana na vyama vingine na aina ya muungano au serikali wanaoitaka, naweza kukubaliana wewe. They have not been straight on this issue. Mfano kwenye thread yangu ya https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/524852-chadema-serikali-tatu-na-serikali-ya-majimbo.html nilihoji kuwa CHADEMA wanataka kuwe na serikali tatu. Wakati huo huo wanataka kuwe serikali ya majimbo. Kwa maana hiyo, kutakuwa na Rais wa Muungano na wakuu wawili wa serikali za Bara na Zanzibar. Pia kutakuwepo na gavana katika kila jimbo ambao watakuwa na mamlaka kamili kwenye majimbo yao.

Ukiondoa suala la gharama ambalo kwa demokrasia ni vyema kuzipitia kiutawala hii imekaa sawa? Utawala wa majimbo chini ya serikali tatu unawezekana? Dhana kuu ya sera ya serikali ya majimbo ni kuhamisha madaraka ya maamuzi kutoka kwa watu wachachewalioko juu na kuyarejesha mikononi mwa wananchi walio chini.

Kama ni hivyo, hizo serikali mbili za Bara na Zanzibar zitakazokuwa zinaongozwa na wakuu wawili zitakuwa zinafanya nini? Madaraka ya wakuu wa serikali hizo mbili hayatagongana na madaraka ya magavana wa majimbo? Kama serikali moja chini ya utawala wa majimbo haiwezekani, solution ni kuwa na utawala wa majimbo chini ya serikali tatu? Ukiangalia hapo, hata vyama vya upinzani vinalizungukia tatizo la Muungano badala ya kuli-address directly. Lakini kwa sababu mara nyingi hapa hoja huwa zinajadiliwa kivyama zaidi, ni wachache ambao wamejaribu kufikiria long-term implications ya miundo ya serikali kama hii.
 
Kwa nini Jakaya alishindwa kumdhibiti Amani Karume kama Mwalimu alivyofanya kwa Aboud Jumbe? Ni Jakaya huyuhuyu na wanamtandao wake ndio waliosaidia Amani Karume kuwa Rais kule Zanzibar!

Kwanini alitakiwa amdhibiti?
Kwani kafanya uhalifu gani?
 
Tunapozungumzia serikali moja, tunazungumzia nchi moja, hivyo hapo kutakuwa hakuna tena, mtu anayeitwa Mzanzibari, hapo wote ni Watanzania, tukifika huko, ni wengi wape!, hata kama Wanzibari wote hawataki serikali moja, wabara wote tukitaka serikali moja, na kama tuko wengi, then ni serikali moja Wazanzibari watake wasitake!.
Pasco.

Hahahahahahahahahaaaaa!
 
W. J. Malecela,
Usomi hauonyeshwi kwa dhana za mavazi, vitabu, kujisifia na vyinginevyo, kinachomtambulisha mtu usomi ni jinsi wanavyoweza kujenga hoja katika jamii kiuchambuzi bila kuwa palpet wa upande fulani bali kuwa na mizani yenye kupima mambo kwa werevu kama afanyavyo mwanachama asiyeona shida kujipambanua kama mwana CCM mwanaJF Mchambuzi wengi tunavyomfahamu.

Dhana mbaya ni pale mtu unapoamua kwa akili yako timamu kuuza utu wako na uhuru wa mawazo yako kwa ajili ya kuhemekea nafasi ya kisiasa, hicho ndicho kinachowaharibu wengi na ipo siku watajutia walilotenda maana huwa limewapotezea muda na zaidi kujikuta umepwaya katika mtazamo wa kisomi katika jamii ya wasomi na wapenda maendeleo. Pengine wengine hufanya hivyo ili kutia vifusi mashimo waliyochimba siku za nyuma, lakini kama mashimo ulifanya kwa nia njema kukinga maji yasimomonyoe udongo nini udhalilishe utu wako kwa kuhemekea?

Hapa hakuna siri kwamba kila mtu anamwelekeo wake katika itikadi, wengine itikadi zimekuwa ndio ilani ya maisha yao ya kila siku na baadhi wenye kuchambua mambo kwa werevu wanaangalia mbali masilahi ya kitaifa iwe kiuchumi, kisiasa, kiutamaduni nk, maana kuendekeza itikadi ni maisha ya kisiasa zaidi ambayo si usomi bali kile moyo ukipenda na pengine shinikizo la maisha kutafuta unafuu katika kuyaweka maisha sawa kwa njia ya mkato.

Tunaweza kujiuliza kwa nini sasa hivi bunge la Katiba inaelekea mbinu za CCM kuteka mwada na kuingiza mbadala unaelekea kupiga ngumi ukutani? Wakati ukuta, kumlazimisha punda kwenda kisimani rahisi lakini hiari ya kunywa maji ni yake vinginevyo usishangae kupigwa na teke la punda uliyemwongoza kwenda kisimani kiulaini. Dhahiri wajumbe kadhaa wametaharuki wale ambao wanaangalia masilahi ya taifa na familia zao ndio imefikia hadi kutetea kura za siri badala ya zile za kuropoka tu kama asiye na akili timamu kwa kufuata mkumbo tu wa woga.

Nimeongelea hili mara kadhaa kuingia darasani, kuhitimu chuo nk si kujihakikishia kuelimia pamoja na kwamba hiyo ni njia kuu ya kuelimika, hilo latokana na watu ambao huwezi kuamini wanapojitangaza kwa uhitimu wao wa elimu na pengine kujionyesha kwa mavazi ya graduation huku kinachowatoka mdomoni hakiendani na taswira ya nje wanayoonyesha usomi wao, kumbe ni wasomi wasioelimika. Hilo limesababisha tuwe na wenye PHD fake ili mradi heshima ya elimu ni kupata vyeo kwa njia nyepesi ya kutundika vyeti ukutani.

Kinachosikitisha zaidi watu ambao wametembea na kuweza kuona dhana bora za uongozi unaofuata sheria, nidhamu, na utendaji uliotukuku huku uwajibikaji ukiwa njia pekee kuwaogopesha wazembe, tumekuja kuwa ndio wakingia kifua walio kinyume cha mfumo huo mzuri wa uwajibikaji vyamani, serikalini, nk. Pale mtu unapoona tu rangi ya bluu basi kukingia kifua Chadema, ukiona nyekundu huna budi kwa nguvu zote kutetea CUF, pale inapokuwapo kijani na Njano basi unakuwa golikipa wewe hata kama umepewa kipenga cha kuwa mwamuzi. Nini kama si utumwa wa kileo katika kizazi hiki?
 
- Kaka unanikumbusha sana maneno ya Jana kuna Mbunge mmoja wa bunge la Katiba alisema "kuna watu humu bungeni wandhani wao tu ndio wanajua na kwamba wao tu ndio wamesoma wengine wote hatujui kitu, ukweli ni kwamba Uingereza haina wala haijawahi kuwa na Katiba", I mean the way you writte ni kama vile wengine wote humu JF ni wajinga wajinga flani hivi ni wewe tu ndio mwenye akili humu ndani na waht you say ndio final truth, ukweli ni kwamba una hasira sana na CCM na kwa muda mrefu sana lakini mpaka leo hakuna utabiri wowote uliowahi kuutoa ukawa kweli, umetabiria mabaya CCM kwa muda mrefu sana lakini never happened hata mara moja na here you are as usual na mahasira yako na mautabiri ya waganga wa kienyeji,

- I mean kaka Nassoro Moyo ndiye peke yake aliyebaki kati ya walioanzisha Muungano? Kama alikuwa na tatizo na Muungano kwa nini hakusema Muasisi wake Mwalimu alipokuwa hai? Nassoro Moyo ana nafasi gani ya uzito wa kisiasa Visiwani sasa hivi? He is nobody, sasa kuandika post based on what Nassoro Moyo said baada ya kuukubali Muungano kwa robo tatu ya maisha yake na kujaribu kuubeza now unasema huyo ndio anatakiwa kuwa the final say ya Muungano uwepo au usiwepo? Really?

- Kwenye Criminology nilifundishwa mtu anayejiamini na kujua anachokisema huwa hataji majina ya wengine kwenye hoja zake, sasa wewe tizama watu wote uliowataja na kuwatumia copy ya hii post yako I mean una wasi wasi wa nini kama unajua na kuamini ulichoandika ni sawa sawa, why Mwanakiijiji hivi ni kweli unaamini Mwanakijiji hataki Muungano kama wewe?,

- Eti CCM ilikuwa inawadanganya wananchi kwa miaka 50? na wewe ulikuwa wapi miaka yote hiyo kuwaelimisha wananchi kwamba CCM inawadanganya? I mean wanaodai Serikali tatu wanatumia akili zao ila wale wote wanaodai Serikali mbili wametumwa na CCM? Really kweli an academician unaweza kusimama na kundika low arguments kama hizi?

- Kaka mimi ni muumini wa Serikali Mbili tu, siamini in Serikali tatu kwa sababu kwanza Dunia nzima hakuna Taifa lenye Serikali Tatu, pili Muungano uliua Serikali za Tanganyika na Zanzibar na kuunda Serikali ya Tanzania ndiyo ninayoitaka na kuiamini na ndio ninaisimamia na nitaisimamia mpaka mwisho, sijatumwa na CCM na wala wewe siamini kuwa umetumwa na WApinzani, jamani acheni kujipa madaraka ya kuwakilisha wananchi na huku hamjachaguliwa kuwawakilishia mawazo yao, kila mwananchi wa Tanzania ana haki ya kutoa mawazo yake, wewe mawazo yako ni kuvunja Muungano that is all ungetoa hoja on that line badala ya kujipachika madaraka ambayo ya kuwaongelea wananchi kwa hoja weak kama ulizotoa, kwa kutumia maneno ya Kiongozi ambaye wala hana nafasi yoyote kubwa kwenye siasa za Taifa wapo wanaomzidi wengi sana na bado hawawezi kuongelea wananchi wengine,

- Kaka nasikia kutapika sana ninapoona unakichafua CCM kwa kujifanya na wewe ni CCM na huku unajua wazi kwamba wewe sio CCM ila ni muumini wa kuona CCM inavurugika kitu ambacho hakitakuja kutokea, umetoa utabiri wako wa waganga wa kienyeji kwa muda mrefu sana kuhusu matatizo ndani ya CCM lakini ndio kwanza CCM ipo vizuri na imeshinda Viti 23 vya Udiwani na huku unaowatetea wamepata viti 3 pamoja na helikopta zote walizotumia, kaka si wanasema shetani akiwa mzee anakuwa malaika maana toka uanze na utabiri wako against CCM haujawahi kutoa hata mara moja badilika kaka!!

Le Mutuz
Katika hoja zako zote sijaona mahali ulipojibu hoja za Mchambuzi hata kwa bahati mbaya.
Le Mutuz, Mzee Malecela alikuwa muumini wa serikali 3 na ilikuwa itokee akiwa PM.
Huyu ni CCM damu.Vipi huoni kuna jambo la kumuuuliza akusaidie kufafanunua?

Pili, Naso Moyo ndiye mwenyekiti wa kamati ya maridhiano. Kamati hiyo ina wajumbe katika tume ya Warioba kwa siri na kwa wazi. Mmoja wao ni mtanagazaji Maarufu wa BBC.

Wajumbe wa bunge la katiba wamechaguliwa kwa influence ya Moyo na wenzake.
Makundi yote hayo yanapokea maagizo kutoka kwa Moyo.

Ni ngumu kusema mtu huyu hana influence wakati tunaona infuluence yake. Hata kama hana ukweli utabaki kuwa Nasor Moyo ni mjumbe wa baraza la kwanza la mpinduzi, ni mjumbe aliyekaa Motel Agip na Akina Banduka akiandika katiba unayoitumia wewe ya CCM.

Hivyo Moyo siyo sawa na wewe unayetumia nembo ya familia, Moyo ana legacy yake na kauli zake ni muafaka kufanyiwa reference.

Tatu, kuwataja watu ni njia nzuri sana ya kuwaeleza kuwa hata kama watajificha historia itawatambua tu.
Nape anapotoa hoja za NEC za uongo huongea kama Nape na katibu mwenezi.
Kuna siri gani.Nani asiyejua kuwa Nape ni mmoja wa wanaoandika rasimu mabadala na Andrea! Kusema hayo ni kujiamini kwasababu ndio ukweli na nashauri watu waendelee kuwataja watu kwa majina ili historia iandikwe vema.

Nne,CCM imewalagahi watu kwa miaka 50 kuwa muungano ni imara. Leo CCM hiyo hiyo inasema kuna kero za muungano, tena inaandika waraka mbadala wa rasimu. Ni CCM hiyo iliyokuwa madarakani miaka 50 imeshindwa kuja na dawa ya tatizo leo tunaambiwa wameagiza Dawa kutoka Apollo India na nyingine zinatengenezwa gongola mboto na akina Andrea, huo kama si ulaghai na uhuni sijui ni kitu gani.

Tunakuuliza utufahamishe hivi nini kilishindikana miaka 50 unadhani sasa kimepatiwa ufumbuzi.

Kwa umri wako na fursa ya maisha uliyopata inabidi ujiulize kama unalitendelea taifa hili haki.
Ushindi wa udiwani siyo ushindi wa nchi, hapa tunatafuta ushindi wa nchi.

Ushindi wa nchi haupatikani kwa waraka wa Andrea ambaye alikana kuandikwa katiba mpya akiwa mwanasheria. Ni Andrea huyo ameliingiza taifa katika hasara leo unataka tuamini ana uwezo wa kutusaidia kuandika lolote la maana.

Nakusihi urudi ukamuulizae mzee wako atakueleza kwa kina nini Watanganyika wanataka na kwanini.

Siasa za vyama hazisaidii nchi, nchi kwanza magwanda na magamba baadaye. Utaweza kuvua gamba au gwanda , huwezi kuvua nchi. Hapo ndipo mwenye akili timamu na inayofanya kazi atasimamia.
Siasa za vitongoji katika suala la katiba ni maji taka the least to say
 
.
Le Mutuz, Mzee Malecela alikuwa muumini wa serikali 3 na ilikuwa itokee akiwa PM.
Huyu ni CCM damu.Vipi huoni kuna jambo la kumuuuliza akusaidie kufafanunua?

Ukisema haya anaanza kulalamika name calling n.k wakati yeye ni bingwa wa kutukana kina warioba. Pamoja na mapungufu yake Mwalimu, cha msingi ni kwamba alishatuambia kina nani ni wahuni.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Ukisema haya anaanza kulalamika name calling n.k wakati yeye ni bingwa wa kutukana kina warioba. Pamoja na mapungufu yake Mwalimu, cha msingi ni kwamba alishatuambia kina nani ni wahuni.


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Tena Mwalimu hakukataa hoja, alichokataa ni uhuni.
Kwamba watu wachache wajifungie na kuamua hatima ya nchi bila kuwauliza wananchi na bila kuuliza wanachama wa chama hatamu na pekee wakati huo. Ni uhuni huo huo CCM wanaotaka kuufanya sasa hivi.

Kwamba wananchi wameulizwa wakasema, CCM wanataka kurudia makosa yale yale aliyokataa mwalimu ya kikundi cha watu kuwa nchi. Na ''uhuni'' huo wa Malecela ndio wanaoutaka akina Nape na Andrea.
 
Ukisema haya anaanza kulalamika name calling n.k
wakati yeye ni bingwa wa kutukana kina warioba
Nakumbuka huyu Le Mutuz alimshutumu Warioba kwa kufanya jambo asilo tumwa.

Hakushutumu tume, alikwenda kwa Jaji Warioba na kumporomoshea matusi kama kwamba Warioba ndio tume na si jina la tume ni la Warioba.

Tume ya Warioba imeundwa kwa mujibu wa sheria, ikakusanya maoni ya wananchi na kisha kuyafikisha kule ilikotumwa.

Aliyeunda tume ni mwenyekiti wa CCM, kabla ya kumutuhum Warioba Le Mutuz alipaswa kumtuhumu Kikwete kwa kumpa Warioba hadidu rejea.

Le Mutuz amuulize Mzee Malecela, yeye alipoamua Tanganyika irudi alitumwa na nani?
CCM walikana kumtuma, vipi yeye amuone Warioba na si Mzee wake

Le Mutuz anasema CCM mwendo ni serikali 2, well, kama Mtanzania ana haki ya kutoa maoni yake.

Ingekuwa ni busara endapo angeanza kwa kusema 'Baba Malecela alikosea kuhusu serikali 3, kwa hali iliyopo serikali 2 ziendelee' hapo tungemwelewa.

Kinyume chake anakwenda kumzogozoa Mzee Warioba tena akiandika mitandaoni wakati Mzee Malecela yupo kiti cha pembeni akisoma gazeti.

Vipi kama angemuuliza mzee wake nini kilitokea na kinataofauti gani na kile akina Andrea wanachotaka kufanya?

Lakini si hivyo tu, Andrea anajulikana kwa msimamo kuwa katiba iliyopo ni safi. Kasema hayo akiwa Mwanasheria.

Ni Andrea aliyeiingiza nchi katika mikataba mibovu, ya aibu na inayolitia taifa hili aibu achilia mbali umasikini.

Akina Le Mutuz na Nape wanampa mtu huyo huyo fursa ya kuandika Mkataba wa wananchi kwa jina la rasimu mbadala.

Andrea hafai na hana moral authority ya kuandika lolote kuhusu taifa hili, eti aandike katiba mbadala!!

Name calling ipi anayoongelea Le mutuz wakati yeye ni bingwa tena kwa wazee waliomzidi umri?

Akina Le Mutuz, Nape na kundi lao walifanya mbinu za kupandikiza watu watoe maoni ya serikali 2.
Hilo limeshindikana sasa wana katiba mbadala.
Wanasema ni maoni ya CCM, hakuna anayejua ni CCM ipi wanayoongelea.

Halmshauri kuu iliisha kwa kugawanyika kati ya Wazalendo na wasaliti.
Hata kwa mantiki ni vipi NEC ya CCM ijadili kitu isichokijua? Hili si wazo la CCM ab initio.

Badala ya kumshambulia Warioba pengine wangemshambulia Kikwete alitangaza mchakato, akaunda tume huku akijua ni kinyume na 'maoni ya genge la CCM'

Serikali 2 ni hizo za mabunge 3, baraza la wawakilishi la Tanzania bara(nchi iliyogunduliwa hivi karibuni na genge la wahuni wa CCM', baraza la wawakilishi zanzibar, Bunge la JMT ambalo wabunge wa znz watakuwa wanatoka kutegemeana na shauri gani lipo mbele.

Halafu rasimu mbadala ya Nape na Andrea inasema Rais awe mmoja, yule wa Tanzania a.k.a Tanganyika na SMZ iwe na rais wake. Kama si vituko sijui tuite nini.

Waraka wa CCM ya Nape unasema, Makamu wa rais awe Rais wa SMZ hata kama Rais atatoka Znz.
Kwa maana nyingine ipo siku Watanganyika watatawaliwa na viongozi wa nchi jirani ya znz yenye katiba ya 2010. Huko ndiko akina Nape wanapotaka kulipeleka taifa.

Historia ipo wima kwa Nape, tungefurahi kama wengine watajitokeza zaidi ili siku moja wenye nchi watakapotoa hukumu mbele ya mahakama yoyote kuwe na fair trial.

 
In short ni kwamba wazanzibari (wananchi) hawautaki muungano na wamegundua njia rahisi ya kuuvunja ni kuirudisha serikali ya Tanganyika chini ya mwamvuli wa serikali tatu. Watanganyika wamekuwa kwenye mood ya "who cares" kwa muda mrefu na recently wamejikuta wakikerwa na manung'uniko yasiyoisha kuhusu muungano. They have just realized, kuwa there is nothing to loose serikali tatu, vunja muungano it's just ok.

All in all, yatasemwa, yatajadiliwa, watu watatishwa, watapongezwa, watalaaniwa, watasutwa lakini ukweli ni kuwa this is "The beginning of the end" Muungano ndio unakwenda huo.
 
In short ni kwamba wazanzibari (wananchi) hawautaki muungano na wamegundua njia rahisi ya kuuvunja ni kuirudisha serikali ya Tanganyika chini ya mwamvuli wa serikali tatu. Watanganyika wamekuwa kwenye mood ya "who cares" kwa muda mrefu na recently wamejikuta wakikerwa na manung'uniko yasiyoisha kuhusu muungano. They have just realized, kuwa there is nothing to loose serikali tatu, vunja muungano it's just ok.
All in all, yatasemwa, yatajadiliwa, watu watatishwa, watapongezwa, watalaaniwa, watasutwa lakini ukweli ni kuwa this is "The beginning of the end" Muungano ndio unakwenda huo.
Nyambala tunafahamu hilo na wala si kuwa hatujui nia yao.
Kama wamekusudia kuvunja muungano hilo tutawasaidia, tumewahi kuwapa mbinu ingawa hawataki kuzitumia, hatujui ni woga wa kuteremshwa mgongoni au uvivu wa kutembea.

Kama ulivyosema, Tanganyika wana lose nini. Sana sana wana gain kwasababu mambo 17 yaliyoondolewa katika muungano hayamgusi Mtanganyika hata kidogo.

Tumegundua janja ya wznz kuwa wanataka kuwepo na 'kishikizo' ili watumie Tanganyika kusitiri haja zao.Wanafahamu kijiografia, kijamii,kisiasa na kiuchumi hakuna Zanzibar imara bila Tanganyika.

Kwa mwendo utasikia wakisisitiza uwepo wa mkataba au kuwe na muungano wa mambo machache ili kulinda masilahi yao.

Kurejea kwa Tanganyika ni kuwa na upande wa pili ambao kama ilivyo SMZ utasimimia taratibu, sheria na mikakati yake bila kufungwa na utegemezi. Hadi hapo Mtanganyika hatakuwa ame lose.

Ukisoma rasimu ya Warioba ya pili imeeleza vema mambo yanayohusu muungano ambayo ukiacha katiba ni takribani 6.

Arguably wapo wanaosema bado mambo hayo yatakuwa mzigo kwa Tanganyika.
Ni kweli lakini yana namna yatakavyoshughulikiwa.

Mathalan, uwepo wa Tanganyika ina maana ni serikali itakayohitaji mapato na matumizi.
Itakuwa rahisi Tanganyika kusema tunaweka mezani sh 5 wenzetu mnaweka nini katika kikapu?tofauti na sasa ambapo Tanganyika inaweka sh 10 mezani na znz wanahisi ya herufi 3 za jina baasi

Hilo litakuwa na tofauti na sasa ambapo Tanganyika haina mtetezi katika muungano, wakati inatoa sana na kupokea 'hakuna' kutoka kwa mshirika.
Ironically mshirika mwenye serikali anapokea zaidi bila kuweka katika kikapu.
By any means Tanganyika haitapoteza pengine ita gain.

Yes tunafahamu hesabu zao lakini ni kuhakikishie ni mbovu na ni njema kwa upande wetu.
Ni bahati mbaya kikundi kidogo cha wzn kinaendesha kundi kubwa lisilojielewa, mbele ya safari wataelewa hii move yao ina ujira gani.

That being said and done, hakuna namna ambayo Tanganyika itakubali tena kuchukua lawama kwa gharama zake. Na hakuna utangamano tena hata kama muungano utakuwepo. Mznz ataangaliwa kama mzanzibar popote alipo Tanganyika. Hilo halina mjadala tena

Kama ulivyosema sasa hivi ni liwalo na liwe. Umemsikia Ndugai akisema mchana kweupe kuwa uwezekano wa kvunja jahazi tugawane mbao na misumari unaweza tokea. Kauli hiyo ni dalili ya namna Watanganyika walivyowachoka wznz.

Hatudhani kuwa Tanganyika inapaswa kuwa na koloni, wala hakuna justification yoyote kuwa Tanganyika inanyonya znz isipokuwa kwa wapuuzi na wajinga ambao elimu ni tatizo.
Kuendelea kuishi na znz ni kuendelea kulea matatizo. Wenzetu wanafikiria umeme wa meli na tv za rangi, wengine nafasi za ubalozi ! phweeh

Na wala hakuna uwezekano wa kuwa na serikali 1, hizo 2 zimeshindikana miaka 50 na hakuna jipya.

Yapo mambo mawili tu ya kufanya
1. Tanganyika irejee halafu hayo mambo 7 tuangalie yanachangiwaje.
Ule ujinga wa kugawana nafasi za ubalozi hauhitajiki wakati wa kujadili muungano.

Ule upuuzi wa kugawana madaraka haukubaliki.
Kitakachoamua nani ale nyama kubwa ni ukali wa kisu chake.

Wznz waje na utamaduni wa kufikiria gharama hata bila namba. I mean watamke neno gharama maana kwao hawajui hicho kitu, waache fomu za ubalozi mahotelini waje na namba mezani.

2. Lau kana haliwezekani, basi tupeane mkono wa heri, tuvunje jahazi tugawane mbao na misumari. Nasema mbao na misuamari kwasababu jahazi linajengwa na vitu hivyo a.k.a assets and liabilities.

Option ya mkataba wa aina yoyote haikubaliki. Hakuna mktaba wa maana utakaofanywa na znz na mkataba wowote maana yake ni kuwatia Watanganyika katika viatu ili wafunge mbeleko ya kumbeba mznz kwa nusu karne tena.
Haijambo laiti kungekuwa na utulivu, lakini ubebwe mgongoni halafu uvae manyanga na njuga ucheze msewe mgongo kwa mtu, hilo sasa basi, wznz tumechoka jamani tuacheni tupumue! miaka 50 na furushi la samadi kazi ati!

Masalaam
 
Mkuu Bobwe, call it what you may, chuki, udikiteta, au jina lolote,
Muungano utadumu!. Wale mnaodhani tofauti, mtaishia kujifia na vijiba vyenu vya roho!.
Pasco

Mkuu Pasco ni vyema tukijadili suala hili kwa upeo mpana badala ya kusema lolote liwalo Muungano Utadumu!!

Mimi nadhani Muungano wetu mtukufu unakaribia ukingoni. Serikali mbili zimeleta kero kwa Wazanzibar, kila siku wanasema kuna kero za Muungano. Wao wanataka serikali/dola yao (sovereign state).

Kwa mujibu wa sheria za kimataifa huwezi kupata dola ndani ya federation. Federal Government ndiyo imependekezwa na Tume ya Waryoba. Hivyo hata ikikubalika hii ya serikali tatu bado Wazanzibar wataendelea kuwa na kero kwa kuwa hawataweza kujiunga na mashirika ya Kimataifa na wala kupata kiti UN! Hivyo ndani ya Federation (serikali tatu) kero zitazidi na matokeo yake tutagawana jamvi.

Kwa vyovyote itakavyokuwa, siuoni muungano wenye afya baada ya katiba mpya.

 
Last edited by a moderator:
Nilikuwa natazama kipindi cha Skonga kwenye EATV, mazungumzo kati ya mtangazaji na mwanafunzi wa kidato cha pili yalikuwa kama ifuatavyo:

Mtangazaji:Tanganyika ilipata uhuru mwaka gani?

Mwanafunzi: Mwaka 1961.

Mtangazaji: Tanzania je?

Mwanafunzi: Tanzania haijawahi kupata uhuru.

Mtangazaji: kuna nchi inaitwa Tanganyika?

Mwanafunzi: ipo

Mtangazaji: Tanzania ni nchi gani?

Mwanafunzi: Tanzania ni muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Mtangazaji: Nani ni rais wa Tanzania?

Mwanafunzi: Kikwete.

Mtangazaji: Nani ni rais wa Tanganyika?

Mwanafunzi: Ali Hassan Mwinyi.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
They have unwritten constitution, we have written constitution......we all have.
 
They have unwritten constitution, we have written constitution......we all have.

Lowest Common Denominator is "Constitution".

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Mkuu Pasco ni vyema tukijadili suala hili kwa upeo mpana badala ya kusema lolote liwalo Muungano Utadumu!!

Mimi nadhani Muungano wetu mtukufu unakaribia ukingoni. Serikali mbili zimeleta kero kwa Wazanzibar, kila siku wanasema kuna kero za Muungano. Wao wanataka serikali/dola yao (sovereign state).

Kwa vyovyote itakavyokuwa, siuoni muungano wenye afya baada ya katiba mpya.


Katika hali ya kushangaza, muungano wa Tanganyika na Zanzibar umezaa watoto waitwao Tanzania Bara na Zanzibar. Huu ndio msingi wa tatizo.



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Pasco ni vyema tukijadili suala hili kwa upeo mpana badala ya kusema lolote liwalo Muungano Utadumu!!

Mimi nadhani Muungano wetu mtukufu unakaribia ukingoni. Serikali mbili zimeleta kero kwa Wazanzibar, kila siku wanasema kuna kero za Muungano. Wao wanataka serikali/dola yao (sovereign state).

Kwa mujibu wa sheria za kimataifa huwezi kupata dola ndani ya federation. Federal Government ndiyo imependekezwa na Tume ya Waryoba. Hivyo hata ikikubalika hii ya serikali tatu bado Wazanzibar wataendelea kuwa na kero kwa kuwa hawataweza kujiunga na mashirika ya Kimataifa na wala kupata kiti UN! Hivyo ndani ya Federation (serikali tatu) kero zitazidi na matokeo yake tutagawana jamvi.

Kwa vyovyote itakavyokuwa, siuoni muungano wenye afya baada ya katiba mpya.

@Kimbunga niseme kuwa muungano hautakuwa dhaifu baada ya katiba mpya, ni kwamba sasa hivi ni dhaifu zaidi na pengine baada ya katiba mpya itakuwa hitimisho tu.

Udhaifu ulianza na serikali ya CCM chini ya JK ilipoachia znz kuwa na mamlaka juu ya katiba ya JMT kwa mabadiliko ya mwaka 2010. Hapo ndipo udhaifu ulipoanzia.

Historia ipo wazi, Jumbe aliopoondolewa madarakani na CCM aliyoiasisi, sababu hazikuwa kudai serikali 3 tu bali ilikuwa ni kufanya mambo nyuma ya pazia(behind the curtain) thanks to Maalim Seif for leaking the info prematurely

Salimin alitaka kubadili katiba ya znz aongeze muda wa kutawala. Aliitwa Dodoma na hoja ikafa kwa kuzingatia kuwa katiba mama ya JMT hairusu jambo hilo.

JK akaachia Amani na wenzake wabadili katiba na iwe na mamlaka zaidi ya katiba ya JMT.
CCM hawakumuuliza mwenyekiti wao imekuwaje na kwanini.

Znz kubadili katiba yao haikuwa issue kubwa, issue ni katiba yao kuwa supreme ya katiba ya JMT.

Hilo lime wa upset Watanganyika na kujiuliza, je ni marudio yale yale ya G55? wanajiuliza hali hiyo itaendelea hadi lini na kwanini znz wapewe upper hand kiasi hicho.

CCM ya Nape hawaonekani kuelewa grievances za Watanganyika na wala historia kwa ujumla.
Wamekuja na mbadala uliozaa nchi mpya ya Tanzania bara.

Well, kama ipo Zanzibar ambayo inasimamia masilahi yao, Tanzania bara ambayo znz imo itasimamia masilahi ya nani? Huwezi kuwa na subset nayobadilika kuwa set kamili, hesabu hazikubali hivyo.

Hapo tunakwenda mbali na kusema kama Tanzania ipo basi lazima kuwe na mtetezi wa Tanganyika ambaye ni Tanganyika.

Tunakuja kwenye hoja kuwa wznz wanaihitaji Tanganyika for certain gain.
Kwa mfano, unaposema Znz wanataka kiti UN hilo halina tatizo.
Lakini basi huwezi kuwa na dola yenye kiti UN bila kuwa na ulinzi na usalama!!

Hutasikia wznz wakizungumzia ulinzi na usalama kwasababu wanaihitaji Tanganyika.
Na sababu kubwa ni gharama zitokanazo.

Kwakuelewa kuwa Tanganyika inabeba nusu ya znz na kwamba inaongeza social strain katika services muungano ukivunjika, znz inaitaka Tanganyika kwa mkataba.

Maana yake kuwe na mambo yanayoifaidsha znz yatakayounda JMT.
Wanataka kutumia jina Tanzania for their own benefits at the expense of Tanganyika.

Ndio maana tunasema ili kuondoa hali ya kutegemewa na si muungano lazima Tanganyika irudi.
Tanganyika ikirudi maana yake ni kuwa kutakuwa na level field ya majadiliano kukiwa na pande mbili kila moja ikisimamia masilahi yake.

Mfano, kwasasa wazanzibar wananufaika na fursa za kiuchumi, kiulinzi, usalama na kijamii kwa kutumia jina la Tanzania.

Ndiyo maana wameweza ku exploit Tanganyika kwa jina tu.
Mtanganyika hafaidiki na jambo lolote znz kwasababu siyo mzanzibar.

In other words identity ya Mtanganyika ndiyo Tanzania kwa faida ya mzanzibar na identity ya mzanzibar imebaki kuwa ya mzanzibar bila faida kwa Mtanganyika.

Kwa hiyo tunabaki na option mbili tu.
1. Serikali 3 ambazo 2 zitakuwa na mchango sawa kwa ya tatu.
2. Vunj jahazi tugawane mbao.

Katika option hizo,Tanganyika will not lose anything.

 
Ndugu wanabodi,

Leo hii nitazungumza yangu moyoni na kwa Uwazi pasipo kuuma maneno maana naona watu wengi tunapiga kelele pasipo hata kujua tunataka nini isipokuwa ni reaction tu baada ya kuona hali ni tete kama vile mfa maji. Tatizo kubwa la Wadanganyika wengi ni kutojua maana hivyo wanadai katiba mpya pasipo hata kuisoma wala kuijua katiba iliyopo inasema nini na ina makosa gani ambayo ndio sababu haswa ya kutakiwa katiba mpya.

Ni jambo la kushangaza sana tunapoitaka katiba mpya wakati hatujui katiba iliyopo imesema nini pinzani na hali halisi tuitakayo. na ndivyo hivyo hivyo katika swala la Muungano. Watu wengi wanadai serikali 1 (unitary state) au 3 (Federation) lakini hawajui huu muungano wa serikali mbili asili yake nini na kwa minajiri ipi umeundwa isipokuwa tu tumefika mahala tunasema koti likikubana sana unalivua! hii ndio sababu nayoiona mimi na hakuna jingine.
Mchambuzi, Ukimsoma vizuri Nassoro Moyo anaeleza kwa umakini Muungano wetu na jinsi ulivyotungwa kwa kuelezea machungwa matatu ktk vikapu viwili, ni muungano pekee ambao kwa kidhungu unaitwa POLITICAL UNION na imefanyika hivyo kwa sababu maalum. Na kama mliwahi kumsoma mwalimu Nyerere alisema wazi kabisa kwamba Afrika haiwezi kuungana moja kwa moja na kuunda nchi moja ni lazima tuanzae kwa stages akitofautiana na Nkurumah aloitaka Afrika moja. Na ili Muungano huu mdogo uweze kudumu mawazo yote haya tunayoyaziungumzia leo yaliwekwa ubaoni na wakachukua lilokuwa bora zaidi nalo ni serikali 2. na hakika inatimizia miaka 50 pasipo kuvunjika muungano kuvunjika wakati nchi zilizochukua mfumo wa serikali 3 zimevunjika zote.

Inasikitisha sana leo sisi tunafikiria kufanya mabadiliko ya muungano huo kwa sababu tu ya kero za wahaini ambao kisheria walitakiwa kutiwa ndani wasionekane kabisa. Tazameni yanayotokea huko Ukraine ambako wana Muungano wa ushirikiano wa kiuchumi kama ilivyo EU au EAC na sasa Russia inataka kuchukua hatua kutokana na makubaliano yalounda katiba yao ktk kuulinda muungano wao.

Na hata Ukizungumzia Marekani, UK au nchi zote ziloungana,swala la kuvunja muungano uliopo ni UHAINI na kutamka tu kuuvunja muungano huo ni kosa kubwa ambalo pengine kuhumu yake ni kifo. Na muungano hauwezi kuwa altered na unilateral decision of either party, states or the federal political body. Sasa unakuja Tanzania ambapo rais, mawaziri, wabunge na wanasiasa wote wameapa kabla ya kushika madaraka kuwa wataulinda Muungano wetu, leo wamekuwa na kiburi cha ku question hata Muungano wenyewe ili kuandika katiba mpya! Hivi kile kiapo walichochukua kilikuwa Usanii na inakuwaje bado wanapotaka mabaidiliko haya bado wamesima akama wabunge au wanachama wa CCM, CDM au CUF!

Binafsi yangu, naihitaji katiba mpya kwa sababu iliyopo haijitoshelezi. Ni katiba ilopitwa na wakati baada ya Tanzania kuodnoka ktk mfumo wa Kijamaa na kuingia Ubepari. Katiba mpya ilitakiwa toka mwaka 1993 ili kukidhi hali halisi ya dunia ya leo ktk maswala ya mawasiliano, Kiuchumi na Kijamii tofauti kabisa na kuliweka swala la Muungano ndani ya katiba hii.

Na hata hivyo Muungano unaweza tu kubadilishwa kwa kufanya referendum na sio vikao vya wanasiasa na wateule ambao wote sio wawakilishi wa wananchi wote ktk swala hilo. Hivyo kama kweli utaratibu wa kuvunja muungano inabidi ifanyike referendum kwa Wazanzibar na ifanyike pia kwa Tanganyika maana kwanza tunatofautiana sana kifikra. Zanzibar kulingana na CUF wao hawataki kuwa ktk muungano wowote iwe serikali 1, 2 au 3 wanachotaka ni Zanzibar yenye mamlaka kamili na kiti chake UN (Uhaini) na Bara nao kwa sababu tu ya madai ya kero za Wazanzibar wanataka muungano uwepo lakini iwe kwa serikali 3, jambo ambalo hayati mwalimu Nyerere alikwisha lizungumzia sana.

Hivyo basi ni Ujinga mkubwa kuendelea kuzungumzia muungano wakati nchi mbili zote wananchi wake wanataka muungano tofauti. Wazanzibar sio wajinga hawataweza kabisa kukubaliana na serikali 1 ama 3, kwa sababu wanajua wanafaidika na kuwepo kwa serikali 2, isipokuwa kutokana na mfumo wa utawala unaoendeshwa leo haifungamani na hali halisi ya mageuzi ktk mfumo wa kiuchumi tulochukua (ubepari) Wazanzibar wanaona ni kheri wajikate.

Nasi huku bara pia kwa sababu hizo hizo za kikatiba kuendelea kutukuza Ujamaa ktk hali ya Kibepari tunapendekeza serikali 3 ili kuondokana na kadhia ya koti hili linalotubana. Hivyo hapa kinachofanyika ni kukomoana, kama wewe waujua huu basi mimi naujua huu. hii sio busara wala hekima hata kidogo bali ni ujinga unaotokana na kutoelewa maana.

Mwisho nitasema tu ya kwamba katiba mpya haitapatikana nahata kama ikija patikana haitakuwa muarobaini wa matatizo ama kero zetu isipokuwa tutazidi kuwa ktk umaskini. Katiba mpya ingelenga tu mabadiliko ya kiuchumi ambapo wananchi wote tungeweza kuwa na mamlaka ya kuhodhi mali na ardhi (utajirisho), Uraia, serikali kusimamia tu nguzo za kiuchumi badala ya kufanya biashara, mfumo wa ukusanyaji wa kodi, na jinsi gani Zanzibar inaweza kufaidika na mikopo inayotoka nje kwa ajili ya ujenzi wa Tanzania.

Katiba ya nchi haitungwi na wanasiasa wala makundi ya watu wanaodai haki zao bali hutungwa na intellectuals. watu wenye elimu na uelewe, mental capacity ya kuelewa katiba ni msahafu/biblia ya jamii tunayoishi na sii tuitakayo. Katiba inayolinda maslahi ya wananchi wote pasipo ubaguzi na sii mapendekezo ya kila kundi la kijamii.. Na kwa jinsi tulivyoanza na makundi na sii wanataaluma nina hakika mwsho wake utakuwa mbaya sana - Kwa leo inatosha

Mtayakumbuka maneno yangu.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mkandara
Nakubaliana nawe kuhusu kura ya maoni na nipo katika rekodi kuanzia siku ya kwanza ya kutangazwa kuanza kwa mchakato.

Nilisema kuwa muungano ni sehemu kubwa sana ya mambo ya kiuchumi na kijamii na katiba mpya haiwezi kuandikwa bila kupata ridhaa ya wananchi endapo wanahitaji muungano.


Nilisema kura ya maoni ifanywe kwa znz ambao muungano kwao ni una ncha mbili, yakwanza ni mwiba na ya pili ni neema.

Tukaenda mbali na kuwachagiza kuhusu hilo.
Kwa uelewa finyu au woga au kukosa kujiamini wznz hawakuweza kushinikiza.

Waznz wakatumia muda wao mwingi sana kwenye mikutano ya kumtukana Nyerere baada ya hapo roho zinaridhika, wameikomboa nchi yao!!

Kwa upande wa pili, Tanganyika wamekuwa wavumilivu kwa muda mrefu.
Kitendo cha Mkandara kusema watangyika wanafanya 'knee jerk reaction' si kweli na ni kufumbia macho ukweli. Ni hivi Mkandara kama sisi ni taifa moja tunapaswa tuwe hivyo.


Znz na wznz wanakuwa Watanzania pale wanapohitaji mafao yao iwe kama serikali au mtu mmoja mmoja. Nje ya hapo ni wznz ambao asili yao ni Oman na Afrika wametokea kwa bahati mbaya.

Utakumbuka miaka ya 80 Watanganyika walikwenda znz kwa passport.
Baada ya Wabunge wa Tanganyika kuchachamaa iwepo passport ya kuingia bara,wznz wakaondoa hali hiyo wakijua fika ni loser katika mtinange huo.


Kibaya kilichoudhi watu ni pale wznz wanapokuja kukaa na kufanya maamuzi yanayohusu Tanganyika bila kuwa sehemu ya Tanganyika na wala kuithamini Tanganyika.

Imefika mahali ambapo Tanzania bara haiwezi kufanya maamuzi hadi BLW likubali.
Kwamba tunataka kuimarisha hali za watu wa singida kwa jambo ABCD basi ni lazima BLW liridhie. Hiyo ni nini kama si dharau, kiburi na uhuni.


Wakati wznz wakitaka maamuzi ya nchi ya Tanganyika yafanyike ndani ya BLW, wao wamekwenda mbali na kuivunja katiba ya JMT kwa kufanya mambo kadri wanavyotaka na si kadri tunavyotaka. Hiyo dharau, kiburi na ufedhuli umeamsha hisia kali kwa upande wa Tanganyika.

Ujeuri,kiburi na uhuni wa znz dhidi ya JMT unakuja na gharama kubwa.
Tanganyika ambayo basically ndiyo Tanzania, inasimamia muungano huu ambao znz haiutambui isipokuwa pale penye mafao tu kwa gharama za Mtanganyika


Wnz wametumia mwanya huo wa muungano kujiona wao ni bora na muhimu sana katika muungano wakati ukweli ni kuwa umuhimu wao haupo kwa kuzingatia kuwa nusu yao wanaishi Tanganyika wakiongeza strain katika social services.

Wznz wanatumia muungano kama silaha ya kudai kile kisicho chao kwa kujua kuwa watapewa pipi kila watakapolilia . Hapa unataka kusema kuna muungano kweli mkuu.

Pamoja na uvumilivu wa Watanganyika dhidi ya ndugu zao, kiburi cha wenzetu kimepelekea Mtanganyika kuwa mgeni na hata kuchukiwa na mznz kuliko raia mwingine wa ukanda huu.

Kitendo cha kuwachoma moto Watanganyika huwezi kukiweka katika mizani na kusema kuna muungano wa maana.

Ubaguzi kwa Mtanganyika ni sehemu ya utamaduni wa mznz kwa wazi kabisa.
Mkuu, unaposema Mtanganyika ana knee jerk reaction sikuelewi kabisa.

Nadhani Watanganyika wamevumilia kiasi kwamba sasa hakuna namna ya kuishi tena na wznz kwa muungano uliopo.


Tunaposema serikali 2 zimeshindwa tunamaana zimeshindwa.
Hakuna namna au dawa iliyobaki kutoka Apollo India au kwa mchina itakayoweza kutengeneza mfumo zaidi ya uliopo.

Tume 5 zilzioundwa zimeliona hilo na hakuna iliyokuja na mapendekezo tofauti na tume ya Warioa.


Serikali 1 haiwezekani kwa sababu ya Narcissisms ya kizanzibari. Kwamba wao wanadhani ni raia bora kuliko wanadamu wengine. Muungano wa serikali 1 unahitaji kutoa na znz haipo tayari.

Serikali 3 kwakweli ni kwa ajili ya kunusuru muungano japo kwa miongo kadhaa ijayo.
Mambo yamebaki 7 ambayo kimsingi ni 5.

Tanganyika ishughulike na mambo yake na znz iwe na yake. Hatuna sababu za kubeba mzigo wa gharama za muungano kwa kutishiwa nyau kila uchao. Japo haijambo anayetishia angekuwa na msuli, hapana! yupo mgongoni na Mkandara anashauri Watanganyika wakae kimya na mbeleko, wznz waendelee kucheza msewe migongoni mwetu! Yakhe tafadhali muungwana!

Kama hilo halitawezekana basi tukubaliane kutokubaliana na tupasue jahazi tugawane mbao.

Kinyume cha hivyo Mtanganyika atageuzwa kuwa Mtumwa na mznz kwa miaka mingine 50. Hatuwezi kushindwa kuchimba vyoo vya shule eti hadi watu 50 wanaowakilisha watu laki 5 waliobaki znz waamue. Ni upuuzi kwa BLW kuwa juu ya sheria zinazotawala watu milioni 40.

Na mwisho, hatunasababu za kulazimishana , njia ipo wazi kwa wznz kuondoka katika muungano.
Endapo watahitaji muungano, equation imebadilika, uwe muungano wa kiuchumi kwamba kila upande ufaidike na si upande mmoja kubeba zigo kwasababu za kisiasa.

 
Mkuu Mkandara
Nakubaliana nawe kuhusu kura ya maoni na nipo katika rekodi kuanzia siku ya kwanza ya kutangazwa kuanza kwa mchakato.

Nilisema kuwa muungano ni sehemu kubwa sana ya mambo ya kiuchumi na kijamii na katiba mpya haiwezi kuandikwa bila kupata ridhaa ya wananchi endapo wanahitaji muungano.


Nilisema kura ya maoni ifanywe kwa znz ambao muungano kwao ni una ncha mbili, yakwanza ni mwiba na ya pili ni neema.

Tukaenda mbali na kuwachagiza kuhusu hilo.
Kwa uelewa finyu au woga au kukosa kujiamini wznz hawakuweza kushinikiza.

Waznz wakatumia muda wao mwingi sana kwenye mikutano ya kumtukana Nyerere baada ya hapo roho zinaridhika, wameikomboa nchi yao!!

Kwa upande wa pili, Tanganyika wamekuwa wavumilivu kwa muda mrefu.
Kitendo cha Mkandara kusema watangyika wanafanya 'knee jerk reaction' si kweli na ni kufumbia macho ukweli. Ni hivi Mkandara kama sisi ni taifa moja tunapaswa tuwe hivyo.


Znz na wznz wanakuwa Watanzania pale wanapohitaji mafao yao iwe kama serikali au mtu mmoja mmoja. Nje ya hapo ni wznz ambao asili yao ni Oman na Afrika wametokea kwa bahati mbaya.

Utakumbuka miaka ya 80 Watanganyika walikwenda znz kwa passport.
Baada ya Wabunge wa Tanganyika kuchachamaa iwepo passport ya kuingia bara,wznz wakaondoa hali hiyo wakijua fika ni loser katika mtinange huo.


Kibaya kilichoudhi watu ni pale wznz wanapokuja kukaa na kufanya maamuzi yanayohusu Tanganyika bila kuwa sehemu ya Tanganyika na wala kuithamini Tanganyika.

Imefika mahali ambapo Tanzania bara haiwezi kufanya maamuzi hadi BLW likubali.
Kwamba tunataka kuimarisha hali za watu wa singida kwa jambo ABCD basi ni lazima BLW liridhie. Hiyo ni nini kama si dharau, kiburi na uhuni.


Wakati wznz wakitaka maamuzi ya nchi ya Tanganyika yafanyike ndani ya BLW, wao wamekwenda mbali na kuivunja katiba ya JMT kwa kufanya mambo kadri wanavyotaka na si kadri tunavyotaka. Hiyo dharau, kiburi na ufedhuli umeamsha hisia kali kwa upande wa Tanganyika.

Ujeuri,kiburi na uhuni wa znz dhidi ya JMT unakuja na gharama kubwa.
Tanganyika ambayo basically ndiyo Tanzania, inasimamia muungano huu ambao znz haiutambui isipokuwa pale penye mafao tu kwa gharama za Mtanganyika


Wnz wametumia mwanya huo wa muungano kujiona wao ni bora na muhimu sana katika muungano wakati ukweli ni kuwa umuhimu wao haupo kwa kuzingatia kuwa nusu yao wanaishi Tanganyika wakiongeza strain katika social services.

Wznz wanatumia muungano kama silaha ya kudai kile kisicho chao kwa kujua kuwa watapewa pipi kila watakapolilia . Hapa unataka kusema kuna muungano kweli mkuu.

Pamoja na uvumilivu wa Watanganyika dhidi ya ndugu zao, kiburi cha wenzetu kimepelekea Mtanganyika kuwa mgeni na hata kuchukiwa na mznz kuliko raia mwingine wa ukanda huu.

Kitendo cha kuwachoma moto Watanganyika huwezi kukiweka katika mizani na kusema kuna muungano wa maana.

Ubaguzi kwa Mtanganyika ni sehemu ya utamaduni wa mznz kwa wazi kabisa.
Mkuu, unaposema Mtanganyika ana knee jerk reaction sikuelewi kabisa.

Nadhani Watanganyika wamevumilia kiasi kwamba sasa hakuna namna ya kuishi tena na wznz kwa muungano uliopo.


Tunaposema serikali 2 zimeshindwa tunamaana zimeshindwa.
Hakuna namna au dawa iliyobaki kutoka Apollo India au kwa mchina itakayoweza kutengeneza mfumo zaidi ya uliopo.

Tume 5 zilzioundwa zimeliona hilo na hakuna iliyokuja na mapendekezo tofauti na tume ya Warioa.


Serikali 1 haiwezekani kwa sababu ya Narcissisms ya kizanzibari. Kwamba wao wanadhani ni raia bora kuliko wanadamu wengine. Muungano wa serikali 1 unahitaji kutoa na znz haipo tayari.

Serikali 3 kwakweli ni kwa ajili ya kunusuru muungano japo kwa miongo kadhaa ijayo.
Mambo yamebaki 7 ambayo kimsingi ni 5.

Tanganyika ishughulike na mambo yake na znz iwe na yake. Hatuna sababu za kubeba mzigo wa gharama za muungano kwa kutishiwa nyau kila uchao. Japo haijambo anayetishia angekuwa na msuli, hapana! yupo mgongoni na Mkandara anashauri Watanganyika wakae kimya na mbeleko, wznz waendelee kucheza msewe migongoni mwetu! Yakhe tafadhali muungwana!

Kama hilo halitawezekana basi tukubaliane kutokubaliana na tupasue jahazi tugawane mbao.

Kinyume cha hivyo Mtanganyika atageuzwa kuwa Mtumwa na mznz kwa miaka mingine 50. Hatuwezi kushindwa kuchimba vyoo vya shule eti hadi watu 50 wanaowakilisha watu laki 5 waliobaki znz waamue. Ni upuuzi kwa BLW kuwa juu ya sheria zinazotawala watu milioni 40.

Na mwisho, hatunasababu za kulazimishana , njia ipo wazi kwa wznz kuondoka katika muungano.
Endapo watahitaji muungano, equation imebadilika, uwe muungano wa kiuchumi kwamba kila upande ufaidike na si upande mmoja kubeba zigo kwasababu za kisiasa.

Maneno mazito sana haya mkuu wangu japo kweli tupu. Sasa unafikiri serikali 1,2 au 3 itaondoa vipi chuki hiyo maana navyokusoma Znz ni sawa na mke wa Mtanganyika kiasili. Ni asili yetu mume kugharamia huduma zote za matumizi nyumbani na pia uijali familia hiyo wakati mke hata kama anafanya kazi fedha yake ni yake na ujue bado hajaondoa ktk familia ya wazazi wake, utafikiri mama yake na baba yake wao walikuwa ndugu. Mke atachuma kwako na kujenga kwao kwa maana siku ndoa ikivunjika yeye hana urithi wa utajiri ama mali zako isipokuwa watoto wenu ndio warithi.. Hii ni mila yetu kwa makabila karibu yote.

Muungano wetu pia umejengwa kwa asili hiyo na tukisema leo tumechoka na mke anayewapenda wazazi wake kuliko mume na kusingizia kwamba hata mume pia ana wazazi wake lakini kaipenda na kugharamia familia hii zaidi, hivyo yabidi tutoe taraka, au separation au hu mtindo mpya wa kusema mke naye awe independent agharamie si ndio kuvunja ndoa huko?.. hiyo separation si ndoo mke atatuletea mume mwingine ndani maana umempa uhuru kamili kwa hiari yako!

Mkuu haya ndio maisha tulokuwa nayo sisi wanaume wote wa Kitanzania, tunajua fika kwamba ndoa zetu mwanamme ndiye huingia gharama zote kubwa, hupoteza wazazi kwa kuanza mji wake lakini mwanamke bado hubakia na familia mbili na kwao (kwa wazazi)ndiko juu zaidi. sijui kama umenielewa!

Tanganyika ya mwalimu nyerere walifikiria yote haya ya serikali 1 au 3 na wakaona ubaya wake na tukakubali kubeba majukumu hayo kama waume wa Kitanzania ktk ndoa. Ni asili ilotufikisha hapa - Miafrika ndivyo tulivyo!

Sasa haya ya mke (ZnZ) kuanza kupiga makelele kwa sababu tumenunua gari kwa jina letu japo ni lake, sijui tunajenga nyumba kwa jina letu japoa anaishi humo, na kudai anataka uhuru wake wakati tunajua fika hawezi kugharamia ujenzi wa nyumba hii iwe ktk serikai 1 ama 3 isipokuwa atajenga kwao, hayo ya serikali 3 ni maisha ya Ulaya ambako mke huweka pato lake mezani na likapangiwa matumizi sawa na mume, mnanunua vitu kwa majina yote mawili -TUTAWEZA! maana tusifikirie tu ya kwamba maadam Ulaya wana serikali 1 au 3 ktk muungano basi nasi tunaweza ishi maisha hayo hayo huku kwetu Afrika. Mila, Tamaduni na mazingira hayaruhusu utaachwa na kila mwanamke maana kila mwanamke ataweka madai kama ya Zanzibar na ndio maana miungano yote ya nchi za Kiafrika inakufa kwa kuiga ya Ulaya! UPO?
 
Back
Top Bottom