CCM Na Bunge La Katiba: Mazingaombwe yanayoelekea ukingoni

CCM Na Bunge La Katiba: Mazingaombwe yanayoelekea ukingoni

wakuu nguruvi3 na mchambuzi kwanza nashukuru sana kwa elimu pana ambayo mnaitoa hapa jukwaan juu ya mustakabal mzima wa katiba na muungano wa tanganyika na zanzibar,hoja ni nzito sana na zina eleweka kwa mwenye kupima mambo na uhalisia wake,mi nadhan mambo ya msingi ambayo ccm ilipaswa kuhoji kwanza ni juu ya katiba ya smz,je kweli imeimeza na kuivunja katiba ya jmt?kama ndivyo ni wazi wenzetu wanataka taifa lao tena likiwa na mamlaka kamili,sasa kwa muktasar huo ni wazi serekal mbili kama wanavyodai kina nape au moja haziwezekani,suluhu ni serekal 3 ili kulinda muungano japo kwa hayo mambo 7.
 
Tunapozungumzia serikali moja, tunazungumzia nchi moja, hivyo hapo kutakuwa hakuna tena, mtu anayeitwa Mzanzibari, hapo wote ni Watanzania, tukifika huko, ni wengi wape!, hata kama Wanzibari wote hawataki serikali moja, wabara wote tukitaka serikali moja, na kama tuko wengi, then ni serikali moja Wazanzibari watake wasitake!.
Pasco.[/QUOTE mkuu Pasco umeyasoma haya maneno ya mwalimu Nyerere mwaka 1968 kama alivoandika Mchambuzi? Iwapo umma wa zanzibar bila ya ushawishi kutoka nje na kwa sababu zao wenyewe wataona kuwa muungano una hasara kwa uhai wao, sitowapiga mabomu kuwalazimisha. Muungano utakuwa hauna tena sababu ya kuendelea kuwepo iwapo washirika wake wataamua kuukana"

 
Last edited by a moderator:
Tunashukuru sana Mchambuzi kwa uchambuzi wako Murua, uko wazi kabisa na hakuna cha kuongeza kabisa. Cha msingi ni hivi, kosa kubwa sana litafanyika ni kutoamua kuwa na serikali tatu. Tofauti na uamuzi huu ni kutuletea mgogoro ambao mwisho wake unaweza kusababisha umwagaji damu. Zanzibar wanasubiria kwa hamu kuwa na nchi yao na si mkoa!!! Kama baadhi yao wanavyonanga!!
 
Kwa nini Jakaya alishindwa kumdhibiti Amani Karume kama Mwalimu alivyofanya kwa Aboud Jumbe? Ni Jakaya huyuhuyu na wanamtandao wake ndio waliosaidia Amani Karume kuwa Rais kule Zanzibar!

WildCard,

Issue hapa si kumdhibiti mtu fulani au kikundi fulani. Tunachotaka kijadiliwe hapa ni MAONI YA WATANZANIA KUHUSU MUSTAKABALI WA MUUNGANO wao uwe wa namna gani! Tume ya Warioba imezunguka nchi nzima imeongea na Wananchi wametoa maoni yao kwamba zaidi ya 60% wanaona Muungano wa Serikali 3 ndiyo unaofaa. Hawakuishia hapo kwa kutaka tu serikali 3 baali walikwenda hatua moja mbele zaidi na kwa kutoa sababu za kwanini iwe Serikali 3.

Tunajua sababu zilizotolewa na Watanzania zina mashiko. Tume wameliona hili kwa kurejea pia Tume nyingine zilizowahi kuundwa huko nyuma kuhusiana na Mambo ya Muungano; Tume ya Nyalali na Jaji Kissanga zote ziliainisha matatizo ya Muungano uliopo kwenye Serikali 2. Kuna KERO za Muungano ambazo zimedumu kwa miaka 50 tangu enzi za uhai wa Waanzilishi wa Muungano wenyewe: Mwl. JK Nyerere na Sheikh Abeid Amani Karume.

Kero za Muungano siyo ngeni. Mwalimu alikuwa anazijua fika na Sheikh Karume alikuwa anazifahamu fika. Walichokuwa wanafanya Mwalimu Nyerere na Sheikh Karume ni mchezo wa MBUNI wa kuficha kichwa kwenye mchanga anapoona moto unakuja. Huu ni ujinga wa mbuni ambao Mwalimu na Sheikh waliuendeleza.

Kuthibitisha hili ni pale ilipoanza kuibuka vuguvugu la kina Sheikh Abdou Jumbe na kina Njelu Kasaka na The G55 wakitaka kuwa na madaraka kamili kwenye Serikali ya Zanzibar kwa upande mmoja na Serikali ya Tanganyika kwa upande mmoja. Makundi haya mawili yalikuwa na HOJA za msingi na zilizo wazi lakini Nyerere na CCM yake wakatumia MABAVU kuiminya hoja hii!!! Mwl. alikuwa anahoji kibabe kwamba MOJA na MOJA ni MBILI haziwezi kuwa TATU. Kimahesabu au kinamba ni inaweza kuwa sahihi lakini unapokuja kwenye uhalisia wa kuunganisha NCHI na NCHI swala la kupata MBILI halina mashiko. Lakini pia kuna Hesabu za Kijitali kuwa MOJA na MOJA ni sawa na MOJA na siyo 2!

Kama unatuambia umeunganisha nchi 2 Tanganyika na Zanzibar tunataka tusikie kila nchi ikitajwa kwenye Muungano au Shirikisho hilo. Kama Zanzibar imeendelea kubaki mpaka leo hii kwa miaka 50 iweje jina la Tanganyika lilipotezwa kiaina???Zanzibar hawahawa ndiyo wamefikia hatua ya kuvunja Katiba kwa kujitangazia Serikali yao,Bendera, Wimbo wa Taifa na mipaka yake. Walichofanya Zanzibar ni kuvunja Muungano kwa kujitangazia serikali yao kamili kama Sovereingty state.Kwa maana hiyo basi Wazanzibar walishachoswa na kero za Muungano. Kwa mantiki hiyo basi swala la Muungano kwa Wazanzibar halipo.Hii ndiyo tunasema CCM ya sasa haiwezi kutulazimisha kuendelea na mfumo ambao umekataliwa na hauna tija kwa Watanzania.

Ufumbuzi wa mgogoro huu wa kutaka tuwe na Muundo gani wa Serikali uko wazi na tayari ulishaamuriwa na Watanzania wenyewe wakati wakitoa maoni yao kwenye TUME YA WARIOBA yaani Serikali TATU. Kuna kichekesho ambacho nakiona kwa Viongozi wa CCM ambao tunaweza kuwaita Wahafidhina(Conservative) ambao wanang'ang'ania Muundo wa Serikali MBILI kwa kisingizio cha WAASISI wa Muungano waliagiza Serikali 2! Huu ni upuuzi. Naamini Nyerere(RIP) angelikuwepo leo na akaingia kwenye Ukumbi wa Bunge la Katiba lazima angekubaliana na Muundo wa Serikali 3!!!Unashangaa??

Mwalimu JK Nyerere kama MUASISI wa Taifa hili mwaka 1992 alikubali mfumo wa vyama vingi.Mwalimu tofauti na viongozi wengi wa CCM wa sasa alikuwa na kipawa cha uongozi na alikuwa anaelewa kabisa kile kinachotakiwa kufanywa kwa wakti husika. Ndiyo maana Mwalimu alikubali kutoka mfumo wa Chama KIMOJA kwenda VYAMA VINGI! Alisoma ALAMA ZA NYAKATI na akaona kuwa kwa wakti huo mfumo wa Vyama vingi ulikuwa hauepukiki!!!

Tunawataka CCM wajifunze toka kwa MUASISI wa Tanzania Mwalimu JK Nyerere wa kukubali MABADILIKO kwa kusoma ALAMA ZA NYAKATI. Kwamba kwa sasa umefika wakti kuwa na Serikali 3 ili kuondokana na kero za Muungano. Ni puuzi na ujinga kuendelea kung'ang'ania serikali 2 ilhali zimeonyesha kushindwa kwa miaka yote hii 50! Ilikuwepo USSR(Union of Soviet Socialist Republics) ikagawanyika vipande vipande kila Taifa kivyake seuze itakuwa URT(United Repulic of Tanzania)?? CCM waache mzaha. Hii kudai eti ni msimamo na sera ya Chama ni uwendawazimu. Hii Katiba inayotengenezwa si ya Viongozi wa CCM wala Wanachama wa CCM ambao katika nchi hii hawazidi hata Milioni 6. CCM wajue kuwa kuna Watanzania zaidi ya Milioni 45 wanaotaka Katiba bora itakayowapeleka for another 50-100 years.

Wasalaam.
 
- Kaka unanikumbusha sana maneno ya Jana kuna Mbunge mmoja wa bunge la Katiba alisema "kuna watu humu bungeni wandhani wao tu ndio wanajua na kwamba wao tu ndio wamesoma wengine wote hatujui kitu, ukweli ni kwamba Uingereza haina wala haijawahi kuwa na Katiba", I mean the way you writte ni kama vile wengine wote humu JF ni wajinga wajinga flani hivi ni wewe tu ndio mwenye akili humu ndani na waht you say ndio final truth, ukweli ni kwamba una hasira sana na CCM na kwa muda mrefu sana lakini mpaka leo hakuna utabiri wowote uliowahi kuutoa ukawa kweli, umetabiria mabaya CCM kwa muda mrefu sana lakini never happened hata mara moja na here you are as usual na mahasira yako na mautabiri ya waganga wa kienyeji,

- I mean kaka Nassoro Moyo ndiye peke yake aliyebaki kati ya walioanzisha Muungano? Kama alikuwa na tatizo na Muungano kwa nini hakusema Muasisi wake Mwalimu alipokuwa hai? Nassoro Moyo ana nafasi gani ya uzito wa kisiasa Visiwani sasa hivi? He is nobody, sasa kuandika post based on what Nassoro Moyo said baada ya kuukubali Muungano kwa robo tatu ya maisha yake na kujaribu kuubeza now unasema huyo ndio anatakiwa kuwa the final say ya Muungano uwepo au usiwepo? Really?

- Kwenye Criminology nilifundishwa mtu anayejiamini na kujua anachokisema huwa hataji majina ya wengine kwenye hoja zake, sasa wewe tizama watu wote uliowataja na kuwatumia copy ya hii post yako I mean una wasi wasi wa nini kama unajua na kuamini ulichoandika ni sawa sawa, why Mwanakiijiji hivi ni kweli unaamini Mwanakijiji hataki Muungano kama wewe?,

- Eti CCM ilikuwa inawadanganya wananchi kwa miaka 50? na wewe ulikuwa wapi miaka yote hiyo kuwaelimisha wananchi kwamba CCM inawadanganya? I mean wanaodai Serikali tatu wanatumia akili zao ila wale wote wanaodai Serikali mbili wametumwa na CCM? Really kweli an academician unaweza kusimama na kundika low arguments kama hizi?

- Kaka mimi ni muumini wa Serikali Mbili tu, siamini in Serikali tatu kwa sababu kwanza Dunia nzima hakuna Taifa lenye Serikali Tatu, pili Muungano uliua Serikali za Tanganyika na Zanzibar na kuunda Serikali ya Tanzania ndiyo ninayoitaka na kuiamini na ndio ninaisimamia na nitaisimamia mpaka mwisho, sijatumwa na CCM na wala wewe siamini kuwa umetumwa na WApinzani, jamani acheni kujipa madaraka ya kuwakilisha wananchi na huku hamjachaguliwa kuwawakilishia mawazo yao, kila mwananchi wa Tanzania ana haki ya kutoa mawazo yake, wewe mawazo yako ni kuvunja Muungano that is all ungetoa hoja on that line badala ya kujipachika madaraka ambayo ya kuwaongelea wananchi kwa hoja weak kama ulizotoa, kwa kutumia maneno ya Kiongozi ambaye wala hana nafasi yoyote kubwa kwenye siasa za Taifa wapo wanaomzidi wengi sana na bado hawawezi kuongelea wananchi wengine,

- Kaka nasikia kutapika sana ninapoona unakichafua CCM kwa kujifanya na wewe ni CCM na huku unajua wazi kwamba wewe sio CCM ila ni muumini wa kuona CCM inavurugika kitu ambacho hakitakuja kutokea, umetoa utabiri wako wa waganga wa kienyeji kwa muda mrefu sana kuhusu matatizo ndani ya CCM lakini ndio kwanza CCM ipo vizuri na imeshinda Viti 23 vya Udiwani na huku unaowatetea wamepata viti 3 pamoja na helikopta zote walizotumia, kaka si wanasema shetani akiwa mzee anakuwa malaika maana toka uanze na utabiri wako against CCM haujawahi kutoa hata mara moja badilika kaka!!

Le Mutuz

Karibu katika mjadala. Hoja kuhusu uanachama wangu wa CCM nilishakujibu kwenye mjadala wetu mwingine, ule wako wa juzi uliouanzisha kumshambulia Lowassa.

Hoja yako nyingine inayahoji nilikuwa wapi miako 50 iliyopita, leo ndio naona sera ya ccm ni tatizo ni kwamba - kwanza umri wangu ni mdogo sana kulinganisha na wako, sitashangaa kama umenipita kwa miaka karibia 20 kiumri, hivyo mimi bado ni mchanga katika kuelewa siasa za nchi hii, hasa our political history, na katika uelewa wangu kadri siku zinavyozidi kwenda mbele, mtazamo wangu ndio huu ambao nimekuwa nauwasilisha, yote nikilenga kuachana na unafiki na badala yake kukosoa chama kwa mambo ambayo inayalinda kwa sababu za kijinga. Lakini muhimu pia ni kwamba, awamu za nyuma, hasa ile ya mwalimu, wananchi wengi walikuwa na imani na ccm na serikali yake na kuipa uhalali kwa vyanzo nje ya Katiba ya nchi, na hili nimejadili kwa kirefu awali (azimio la arusha, historia na mafanikio ya TANU kutetea wanyonge ndani na nje ya nchi, na uwepo wa nyerere as a charismatic leader). Haya ndio yaliipa ccm na serikali yake legitimacy, hence the union or zanzibar question na muundo wa muungano kwa ujumla kuweka kukaa under the carpet kwa muda. Leo hizi three sources of legitimacy hazipo tena, na njia pekee ya ccm kupata legitimacy sustainable na sio ya hila hila na ujanja ujana ni kwa kuhakikisha nchi inapata katiba inayotokana na matakwa ya wananchi, na vyama vyote including ccm kuheshimu katiba itakayopatikana kwa vitendo.

Hapo juu, hoja yako muhimu in my humble view ni ile kwamba United Kingdom doesn't have a written constitution, na naposema ina umuhimu ni kwa maana moja tu nayo ni kwamba, baadhi ya makada wa ccm wanajaribu kutetea muungano kwa hoja kwamba ni kitu almost like "ordained", na sio kwa mujibu wa matakwa ya binadamu/wananchi, matakwa yaliyokuwa expressed kwa mujibu wa written constitution iliyotokana na wananchi.

Ni hivi:

Ni kweli our former colonial ruler, the british hawana a written constitution. Taifa hili lina certain constitutional conventions ambazo zimeendelezwa historically kwa kipindi kirefu sana. Na hakuna mtawala yoyote wa uingereza ambae atathubutu kuzi breach hizi conventions. Kwa ufupi, hizi conventions derive their binding character kutoka kwenye political practice ya muda mrefu sanan hivyo zimepata historical legitimacy na sio legitimacy based on any legal document. Je, unataka kutuambia kwamba muungano wetu should be treated kwa mtindo huu wa uingereza? By the way, rais wa zanzibar, Dr. Shein ameshasema nakala ya mkataba wa muungano (1964) ipo ikulu ya znz, so hoja ya kufananisha unwritten constitution ya uingereza na suala la muungano goes straight to the trash bin. Nadhani unaelewa kwamba the legal foundation of our union ni mkataba wa muungano (1964.

Nirudi tena kwenye mfano wa Uingereza, taifa ambalo mwalimu alitueleza in the 1960s kwamba tumeiga our unitary union kutoka mfumo wao (bearing in mind kwamba baada ya mfumo wa chamma kimoja kufa, jaji bomano akapewa jukumu la kutafuta ufumbuzi kwani kwa unitary approach, ccm ingeshinda "bara" na cuf zanzibar uchaguzi wa 1995 and pengine chaguzi zilizofuatia). Jaji bomani akaja na wazo la mgombea mwenza kwa kuiga "federal system" ya USA. Mind you, we moved from unitary to federal elements za muungano (na mkataba wa muungano ambao ccm breached it from the get go had proposed a federal structure).

Kinadharia, bunge la uingereza linaweza kutunga sheria ambayo ita breach the constitutional conventions ambazo zipo katika taifa hilo kama nilivyojadili hapo juu. Kwa maana hii, bunge la uingereza isn't only a sovereign entity but also supreme.

Tuzidi kuingia kwenye hoja:
Now while uingereza haina a written constitution, makoloni yake yote yalipewa katiba iliyotoka lancaster hall london, katiba ambazo "zilikuwa enacted na bunge la uingereza"; kwa maana hii, katiba yetu ya kwanza siku ya uhuru ilipata its legal authority na validity kutoka kwa mkoloni. Kilichofuata baadae ni TANU na serikali yake kufanyia marekebisho katiba ile na kuipatia TANGANYIKA katiba yake mpya mwaka 1962. Tukiamua kufuatilia legal gene ya katiba yetu hata ya sasa, ujue tu kwamba haitatuchukua muda mrefu kubaini kwamba imetokana na an ordinary law iliyopitishwa na bunge la uingereza (in writting ingawa taifa husika lina unwritten constitution), tupo pamoja mpaka hapo?

Kwahiyo basi katiba ya sasa ya JMT (ambayo hata hivyo ccm imewaachia zanzibar waifutilie mbali), mizizi ya katiba hii ni written laws passed by bunge la uingereza. Nani alitunga katiba ya 1977? Bunge la katiba la chama kimoja, huku almost 55% ya wajumbe wake wakiwa sio wale kutoka majimboni bali kwenye dawati la rais ikulu. Nani alimpa rais wa jmt mamlaka ya kuteua bunge la katiba 1977? Ni mkataba wa muungano wa 1964, mkataba ambao inasemekana ulipitishwa na wabunge wa BLW na Tanganyika (kutoka vyama viwili vya tanu na asp pekee). Kumbuka, 1964 bado kulikuwa na mfumo wa vyama vingi kama vile vya zuberi mtemvu n.k. Kwahiyo kimsingi legal foundation ya muungano wetu kama anavyojadili shivji ni ule mkataba wa muungano (1964), na kwa vile mkataba huu ukaja chakachuliwa, matokeo yake ni kero za muungano kwa miaka 50 kero ambazo nape anatumabia sasa dawa itapatikana chini ya mfumo ule ule wa serikali mbili ndani ya muungano ambao umevunjwa na katiba ya ya znz (2010). Lakini kwa vile mnatanguliza matumbo kuliko ubongo, badala ya kuwekana vikao kujadili kwanini ccm imeruhusu hili, mnakaa kumjadili warioba.

Tanganyika yetu inarudi na sijui utajificha wapi uso wako utakaojaa aibu. Nasubiri kusikia mchango wako kwa hoja zangu bandiko #2 , #37 na #38 .



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Mkuu Bobwe, call it what you may, chuki, udikiteta, au jina lolote,
Muungano utadumu!. Wale mnaodhani tofauti, mtaishia kujifia na vijiba vyenu vya roho!.
Pasco
Its no longer there Pasco, that thing is gone! Utabakia nao kwenye makaratasi kama mkiulazimisha but in actual sense MUUNGANO HUU HAUPO!!!!! Jiandae kisaikolojia manake ww utaumia sana na unaweza ukafa kwa kihoro kwani unaonekana huna maandalizi yoyote
 
Tatizo lililopo ni kwamba tangia uhuru, tanu na baadae ccm imewekeza zaidi na inaendelea kuwekeza in controlling people, not controlling the territory. And that's how it has lost Tanganyika and gained personalities from both sides of the union, all vying to get into power to control even more people. Kumbe wenzetu wazanzibari wamegundua kwamba sio tu small is beautiful, bali pia less is more.

Cc Nguruvi3


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mambo mengi mtaongea ila ukweli utabaki kuwa ukweli huwezi kuwaunganisha waafrika, kwasabab moja kuu,viongozi wote afrika ni waroho wa madaraka.
 
Kwa mtazamo wangu naona tunahitaji kuwa pamoja ili kuwa na umoja,na tunahitaji umoja ili kushindana na mambo mengi ikiwa ni pamoja na uchumi, siasa, maadui nk.

Tuwe na serikali moja tu basi, hakuna cha Zanzibar wala Tanganyika. Kama Tanganyika ilishakufa basi na Zanzibar inabidi ife, tubakie na Tanzania. Unguja na Pemba iwe ni mikoa ndani ya Tanzania kama vile Iringa, Mbeya, Dodoma nk.
 
Baada ya chama kuingia kwenye bunge la katiba na msimamo wake wa serikali mbili licha ya rais kuhimiza vyama kuacha tabia ya kuweka mbele itikadi za vyama na badala yake maslahi ya taifa, zimeenea taarifa kwamba ccm sasa imekuja na waraka wa rasimu ya katiba mbadala, habari ambazo bado hazijakanushwa na ccm hadi sasa. Cha ajabu ni kwamba ndani ya waraka huo, inadaiwa kwamba chama kinapendekeza uwepo wa baraza la wawakilishi la "Tanzania bara" kwa ajili ya kushughulikia masuala ya bara tu.

Kwa kufupisha story, una maana kuwa pendekezo ni kuwa na serikali mbili na mabunge matatu?

If that is the case, then ni serikali (the executive) ipi itakuwa accountable kwa "Baraza la Wawakilishi wa Tanzania bara"?

Ni kiongozi yupi atakuwa na mamlaka ya kulivunja "Baraza la Wawakilishi wa Tanzania bara"?

Inaonekena kama vile hoja ya kuwa na serikali tatu inaingizwa kwenye katiba mpya kupitia "mlango wa wani" japokuwa funguo za kupitia "mlango wa mbele" zipo.

This proposal sounds very interesting. Kuna umuhimu wa kuona details zake ili kujua mgawanyo mzima wa madaraka, checks and balance, nk. utakuwaje kama hakutakuwa na "Serikali ya Tanzania Bara".
 
Wakati mwingine nafikiri pengine viongozi wengi na wana CCM wengi waliofanya kazi na Mwalimu Nyerere hawakuwahi kumwelewa kwanini muundo huu sasa aliona ndio utakaozaa Tanzania imara ili wasimamie hoja hizo sasa.

Kwanini CCM wanashindwa kutetea hoja ya serikali mbili hadi watumie viini macho kama anavyoita Mchambuzi katika issues ambazo zinahitaji kujenga hoja tu? Mbona Mwalimu aliweza kuvunja hoja za lile kundi la G55 kwa hoja na kundi kusambaratika bila vitisho wala ujanja ujanja? Lile kundi lilikuwa imara na waliamua kweli kujitosa lakini wakashindwa kupangua hoja makini za Mwalimu na kundi kufa kimya kimya.

CCM waache hizi mbinu zinazoleta dalili za kama wanataka kulazimisha mambo maana wataaibika, Wasisusiane chama bali wajenge hoja ili sisi wananchi tupime pengine wakaungwa mkono na kuheshimika tofauti na huu ujanja ujanja katika zama hizi za utandawazi.

Lakini pia msimamo wa CCM juu ya serikali mbili si dhambi wala uhaini ni kama Chadema wanavyoamini ktk serikali tatu lakini wananchi wasilazimishwe kile hivi vyama vinavyoamini bali wote wajenge hoja mwisho wananchi waamue maana kama ushindani utakuwa ule wa misimamo ya vyama hivi viwili vikubwa tu vipi sisi tunaoamini ktk serikali moja na hakuna taasisi kubwa inayotusemea?

Serikali mbili was transitional to one government, but let us agree the two government system was possible during mono party system, the change to Multiparty system has created more problems to this system.. CCM kwasasa inashindwa ifanyaje sasa Serikali moja haiwezekani kwasababu Zanzibar wao tayari wamekwisha kujitangaza kuwa taifa kamili, na CCM hawawezi kuwashawishi out ya huo msimamo, CCM wanachoweza ni kuendelea kuwa manipulate watanganyika na kiini macho cha muungano ili kufifisha vuguvugu la wananchi wa tanganyika ambao na wao sasa wanadai taifa huru la tanganyika. CCM wanalenga kuipa Zanzibar madaraka zaidi kwenye serikali ya Muungano ili kuwanyamazisha, ni kama hongo ili waweze kunyamaza na kutulia kwenye hiki kiini macho cha Muungano.
 
- Kaka unanikumbusha sana maneno ya Jana kuna Mbunge mmoja wa bunge la Katiba alisema "kuna watu humu bungeni wandhani wao tu ndio wanajua na kwamba wao tu ndio wamesoma wengine wote hatujui kitu, ukweli ni kwamba Uingereza haina wala haijawahi kuwa na Katiba",

Mkuu naomba nikusahihishe hasa hapo kwenye red na kujaribu kuondoa upotoshaji wa aina yoyote ile ukizingatia kuwa kuna wadogo zetu huwa wanapitia humu kujifunza.

Siyo kweli kuwa Uingereza haina katiba na kuwa hawajawahi kuwa na katiba. Uingereza ina katiba, tena one of the most old constitutions in the world. Tofauti ni kwamba katiba ya Uingereza haijaandikwa kwenye document kama zilivyo katiba za nchi nyingine.

Waingereza hawaja-codify katiba yao in a single document. Wamekuwa na mijadala whether they should codify their constitution lakini bado hawajafikia mwafaka.

Hata hivyo kumekuwa na series of statutes zilizopitiswa na bunge lao ambazo wanaziita "Constitutional Acts" kama vile sheria ya kujiunga na Muungano wa Ulaya (European Communities Act 1972), the Human Rights Act 1998 (incorporating the European Convention on Human Rights into the UK domestic law), na sheria iliyoanzisha the Supreme Court (Constitutional Reform Act 2005 inayotenganisha mahakama ya juu kabisa kutoka kwenye Bunge).

Huwa wanaziita ni "Constitutional Acts" kwa sababu zimeleta fundamental changes into the British Constitutional principles, kama Parliamentary Sovereignty aka the ability of Parliament to make and unmake law. Kwa mfano, Bunge la Uingereza haliwezi tena kutengeneza sheria ambazo zinaenda kinyume na sheria za Muungano wa Ulaya au Sheria ya Haki za Binadamu ya mwaka 1998.

Hivyo basi kama walikuwa hawana katiba, basi bunge lao lisingepitisha sheria kama Constitutional Reform Act 2005; otherwise wangekuwa wanafanya reform ya katiba ipi wakati unadai hawana na wala hawajawahi kuwa na katiba?

As it stands, Ungereza wana the so called "unwritten constitution". Nchi nyingine kama Tanzania, Marekani na Afrika Kusini wana the so called "written constitution". Kwa hiyo basi Uingereza kuwa na "unwritten constitution" haina maana kuwa haina katiba.

I mean the way you writte ni kama vile wengine wote humu JF ni wajinga wajinga flani hivi ni wewe tu ndio mwenye akili humu ndani na waht you say ndio final truth..

Mkuu hapa wala sina cha kuongeza maana hata mwanafunzi yoyote wa kidato cha sita anayesoma General Studies atakwambia confidently kuwa Uingereza ina katiba, sema tuu their constitution is unwritten.

Mwanafunzi huyo hatakubaliana kabisa na wewe kuwa Uingereza haina na wala haijawahi kuwa na katiba na kuna uwezekano nae akasema kuwa "the way you writte ni kama vile wengine wote humu JF ni wajinga wajinga flani hivi ni wewe tu ndio mwenye akili humu ndani na what you say ndio final truth..."

Weekend njema kaka.
 
Kwa kufupisha story, una maana kuwa pendekezo ni kuwa na serikali mbili na mabunge matatu?

If that is the case, then ni serikali (the executive) ipi itakuwa accountable kwa "Baraza la Wawakilishi wa Tanzania bara"?

Ni kiongozi yupi atakuwa na mamlaka ya kulivunja "Baraza la Wawakilishi wa Tanzania bara"?

Inaonekena kama vile hoja ya kuwa na serikali tatu inaingizwa kwenye katiba mpya kupitia "mlango wa wani" japokuwa funguo za kupitia "mlango wa mbele" zipo.

This proposal sounds very interesting. Kuna umuhimu wa kuona details zake ili kujua mgawanyo mzima wa madaraka, checks and balance, nk. utakuwaje kama hakutakuwa na "Serikali ya Tanzania Bara".
Mkuu huo waraka unashangaza sana. Wanasema kuwe na baraza la wawakilishi la Tanganyika, halafu kuwa na bunge la Muungano ambalo wakati wa kujadili mambo yasiyohusu Znz wabunge wa ZNZ wanatoka nje. Umeona? Kwamba kuna Baraza la wawakilishi Tanganyika, bunge la JMT ambalo pia litakuwa na sehemu ya Tanganyika.

Mkuu yaani wanataka serikali 3, wasichotaka kitokee ni rais wa JMT kukosa udhibiti na ZNZ.
Na hayo yote ni ili Rais huyo wa JMT aweza kuwapa vyeo kwa namna wanavyotaka.

Hii ndiyo rasimu mbadala ambayo imemuunganisa Nape Nnauye na Andrea
 
Kwa nchi masikini hii tunahitaji serikali moja. Ila kwasababu hakuna anayetaka kutatua tatizo serikali tatu ni njia ya kwenda solo gov.

Malalamiko ya Wazanzibar yananifanye nikumbuke ukoloni. Kama wazanzibar wanajiona hawako huru, wanaminywa, na wapo kwenye muungano kikoloni inabidi wapewe uhuru wao.

Muungano wa nchi mbili huwa unadumu kama pande zote mbili zinaridhiana na kukubali kuungana yaani watu, mali, ajira, ndoa, nk na kuwa nchi moja na serikali moja. Nchi nyingi zilizoungana ama kwa hiari ama kwa nguvu zilijitajihidi sana kumaliza utengano na kutengeneza serikali moja, amiri jeshi mmoja, dola moja ndio zilizodumu kwenye muungano.

Muungano wa kutengeneza madaraka hautamaliza kasheshe. Kinacholiliwa sasa ni muundo wa kugawana keki kwa kupeana madaraka na kumaliza kodi zetu kwa vyeo vya ajabu ajabu.
Ilivyo, CCM ya sasa ni ya kisanii haina dira, haina mikakati, haisomi historia, haijifunzi, iitikadi yake imabakia katika katiba na si vitendo, haina wazalendo tena bali imebakiwa na wachumia tumbo wachache ambao piga ua wanalazimika kufanya usaniii ili wasogeze muda na waendelee kula keki ya taifa japo hata kwa miaka michache ijayo huku wakijaribu kuwasogeza watoto wao na swaiba zao kuguguna keki yetu
 
Kwa kufupisha story, una maana kuwa pendekezo ni kuwa na serikali mbili na mabunge matatu?

If that is the case, then ni serikali (the executive) ipi itakuwa accountable kwa "Baraza la Wawakilishi wa Tanzania bara"?

Ni kiongozi yupi atakuwa na mamlaka ya kulivunja "Baraza la Wawakilishi wa Tanzania bara"?

Inaonekena kama vile hoja ya kuwa na serikali tatu inaingizwa kwenye katiba mpya kupitia "mlango wa wani" japokuwa funguo za kupitia "mlango wa mbele" zipo.

This proposal sounds very interesting. Kuna umuhimu wa kuona details zake ili kujua mgawanyo mzima wa madaraka, checks and balance, nk. utakuwaje kama hakutakuwa na "Serikali ya Tanzania Bara".

Tuliamua kuwa Chama Cha Mazingaombwe, au umesahau. Hata mimi nasubiri hizo details, vinginevyo kwa kila hali, you raise very important questions.




Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Mjadala ni mzuri na unaonesha jinsi mawazo yetu yalivyogawanyika juu ya hiki kizungumkuti cha Muungano.
Kwangu mimi ninao wasiwasi ambao siku zote umeambatana na mimi. Kwa wananchi wa kawaida serikali tatu ni kuelekea kwenye kuuvunja kabisa Muungano. Kama ifuatavyo:
Kwanza, Mfumo thabiti wa Muungano hata ndani ya serikali bado utaleta mkanganyiko. Hatari hapa ni kuamua tuwe na Tanganyika bila kuwa na makubaliano Tanganyika yenyewe itakuwa vipi. Kwa mfano Wazanzibar walifanya marekebisho ya kikatiba ikaonekana wamekiuka Katiba ya JMT. Mpaka leo watu wanapigania serikali ya Tanganyika si jambo baya lakini, hiyo Tanganyika inatakiwa kuongozwa kwa mfumo upi? Maake inawezekana mbele ya safari tukawa na katiba inayopingana na ya JMT je tutaitisha tena mchakato wa katiba mpya ya Muungano?
Pili, kuna utata wa mawazo ya jinsi hasa serikali ya Muungano inavyopaswa kuwa. Kuna kambi wanataka kama ilivyopendekezwa na Warioba, kuna wanaotaka mfumo unaopendekezwa wa Mkataba (ikumbukwe hawa ndio wengi Zanzibar) na kuna wanaopendekeza mfumo wa serikali tatu lakini zenye washirika wasiokuwa na hadhi ya kinchi (yaani washirika wawili waongozwe na magavana lakini Raisi awe mmoja) na pia kuna wanaopendekeza mfumo wa serikali ya Tanganyika yenye baraza la wawakilishi tofauti na lile la Muungano ila bila ya serikali kamili (hao msimamo wao bado haujawa rasmi). Wote hawa wanataka serikali tatu ila bila ya maridhiano ya serikali tatu za aina gani. Kiufupi naona kama hatujawa tayari kwani kuna mambo kadha wa kadha yanahitaji ufumbuzi.
 
Ilivyo, CCM ya sasa ni ya kisanii haina dira, haina mikakati, haisomi historia, haijifunzi, iitikadi yake imabakia katika katiba na si vitendo, haina wazalendo tena bali imebakiwa na wachumia tumbo wachache ambao piga ua wanalazimika kufanya usaniii ili wasogeze muda na waendelee kula keki ya taifa japo hata kwa miaka michache ijayo huku wakijaribu kuwasogeza watoto wao na swaiba zao kuguguna keki yetu

Mimi nadhani tunakosea tunapowasakama sana CCM katika hili wao kama chama wametoa maoni yao ya njia ya wanayotakiwa kufuata Muungano ni ipi na at least kwao ni sehemu ya dira yao kama chama. Ukiwasakama CCM kama chama ni vizuri pia ukatuambia vyama vingine vinasimamia wapi? Ikumbuke vinasema tu vinataka seriakali tatu ila bado mitizamo yao juu ya Muungano huo nao bado una matatizo.
 
Mkuu hapa wala sina cha kuongeza maana hata mwanafunzi yoyote wa kidato cha sita anayesoma General Studies atakwambia confidently kuwa Uingereza ina katiba, sema tuu their constitution is unwritten.

Mwanafunzi huyo hatakubaliana kabisa na wewe kuwa Uingereza haina na wala haijawahi kuwa na katiba na kuna uwezekano nae akasema kuwa "the way you writte ni kama vile wengine wote humu JF ni wajinga wajinga flani hivi ni wewe tu ndio mwenye akili humu ndani na what you say ndio final truth..."

Weekend njema kaka.


Mkuu EMT,

Katika moja ya kazi zake, professor shivji anajadili aina kuu ya wanasiasa ambao wapo ndani ya ccm kama ifuatavyo:

1. Jesters ambao kazi yao is to amuse and cheer up or charm their masters. If URT was a Kingdom na pale ikulu ingekuwa ni palace, wangekuwa ni wale wanaoratibu delivery ya maua ya kumumwagia mfalme kila akipita. Lakini kwa vile hatuna mfalme, their roles are so random na tumbo likitawala ubongo, wapo tayari hata kumwagia tindikali watu wanaopingana na their masters na agenda zao.

2. Kundi la pili analojadili professor shivji ni "demagogues". Hawa ni intellectual workers ambao they have an exceptional mental capacity to cojole and bamboozle, esp kwa kupitia prejudices and stereotypes zilizopo katika jamii. Wana ccm hawa hawana interest in arguing, hawana respect for logic or consistency, history or common human decency. Kazi yao kubwa ni kuja na slogans after slogans za chama ambazo wanazilazimisha kuwa ndio "absolute truth" na kwamba kila mtanzania lazima aziabudu na kuzuia zisiwe challenged kwenye jamii, kwenye mitandao etc. Hawa wana brand kila critic as an enemy. Kwa maneno ya shivji: "they would not see any independent merit in a political opponent but rather try to denigrate him or her by harping on biological (race, gender...) Or ideological or religious attributes".

3. Kundi la tati ni la "ideologues". Shivji anasema, "unlike demagogues, ideologues try to persuade by force of argument, consistency and coherence of their (world views). Their role is to rationalise the changing policies, strategies and even gimmicks of the rulers, who as we know, change like chameleons to stay in power. Ideologues are the people who would try to convince us that the rulers (or potential) rulers have a consistent direction. And even when politicians and political parties change direction and turn 180 degrees, their ideologues would try to assure us that it was only a change of tactics to keep up with changing times while the goals remained the same. Nape Nnauye falls into this category.

Ndugu yetu malecela hapo juu (aka field marshall es) amekuwa na tabia ya kushambulia sana wasomi au watu wanaokuja na hoja zinazoonyeshe uelewa, hasa wanao hoji status quo. Yeye ni mwanasiasa by all means, wa kundi gani kati ya hapo juu? You be the judge, but all I can say ni kwamba - let's admit kwamba watanzania wengi sasa ni wasomi (usomi sio lazima PhD, usomi ni pamoja na kuamua kujiendeleza kielimu kwa malengo ya kujipanua zaidi kiuelewa ili uweze kukabiliana na mazingira unayoishi whether ni kijamii, kisiasa, kiuchumi, kiutamaduni etc).

Ndugu yetu malecela amekuzwa katika utamaduni ambao politicians and ideologues have been thinking for us (jamii), na katika hali hii, sisi wasomi ambao kazi yetu ni kusaidia jamii to think for itself, it becomes a technical foul on them. Given the role ya wasomi in this context, ccm hawawezi kupenda maoni na mawazo ya wasomi.

Hapo juu ndugu malecela kanijadili kwamba kazi yangu na lengo langu ni kuona ccm ina angamia na ka ahidi kwamba hilo kamwe haliwezi tokea. Fine, lakini ndugu yetu huyu, kwa vile in my view he's more of a political jester, hawezi kuwa na muda wa kuchambua na kutofautisha baina ya constructive and destructive criticisms. Utofauti baina na destructive and constructive criticisms katika dunia ya huyu malecela is quite pedestrian - "what I don't like to hear or what my masters wouldn't like to hear is destructivve and what is in my favour or in my masters' favour, that is constructive."

Ni bahati mbaya sana hawa ndio wameteuliwa kuingia bunge la katiba kwenda kusimamia maslahi ya ccm ambayo sio tu yatakiangamiza chama bali pia muungano kama sio taifa. I remain to wonder kwanini hajateuliwa hata kupitia asasi zilizoundwa over night kwenda kuwa mjumbe wa bunge la katiba kwani kwa hoja zake humu za miaka nenda miaka rudi, alifaa sana kuingia mle kwenda kuitetea ccm. Given his experience kama dereva wa malori ya mizigo kwa muda mrefu new york, angalau basi angejipanga kwenda bungeni kupitia chama cha madereva wa malori Tanzania.
Candid Scope, Mag3, MTAZAMO



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Naiona Zanzibar huru ileee tartiiiiiiiiibu!
 
Mimi nadhani tunakosea tunapowasakama sana CCM katika hili wao kama chama wametoa maoni yao ya njia ya wanayotakiwa kufuata Muungano ni ipi na at least kwao ni sehemu ya dira yao kama chama. Ukiwasakama CCM kama chama ni vizuri pia ukatuambia vyama vingine vinasimamia wapi? Ikumbuke vinasema tu vinataka seriakali tatu ila bado mitizamo yao juu ya Muungano huo nao bado una matatizo.

Tuna tabia ya kuyazunguka matatizo badala ya kuya-address na kusonga mbele. As it stands, Muungano huu una matatizo makubwa. Lakini badala ya kuyatatua tunayazingukia kwa hoja za serikali tatu, serikali mbili na mabunge matatu, huku Rais wa Tanzania akidai kuwa Zanzibar ni nchi kwa ndani lakini nusu nchi kwa nje.

Kama Zanzibar ingekuwa nchi kwa ndani lakini nusu nchi kwa nje, basi kwenye ile kesi ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar dhidi ya Machano Khamis Ali na wengine 17, Makakama Kuu isingeamua kuwa treason is a "Union matter and not a matter exclusively for the Revolutionary Government of Zanzibar" simply kwa sababu treason inakuwa committed internally and not externally. Na sasa katiba ya Zanzibar inasema wazi kwenye Ibara wa kwanza kuwa "Zanzibar ni Nchi [emphasis added] which may suggest that treason can now be committed against Zanzibar.

Solution pekee ya hiki kiini macho cha Muungano ni referendum ambapo wananchi wa pande zote wataamua wenyewe na bila kushurutishwa kama wanautaka au hawautaki muungano na kama bado wanautaka, wangependa kuwa na muungano wa aina gani. Kama wakisema hawautaki Muungano, then that should be it. Their wishes should be respected.

Wengine wanadai kuwa referendum itaweka "bad precedent". This is probably because wananchi hawajazoeshwa kujiamulia mambo yao wenyewe. We seem to trust politicians with their rhetoric promises kutuamulia mambo. Politicians should guide the people rather than superimposing upon them their own political interests.

It seems to me that the right of peoples to determine themselves (the right to self-determination) iliishia siku ile tulipojipatia uhuru. Baada ya hapo, haki hiyo ilibadilika na kuwa the "right of politicians to determine themselves". Ndiyo maana wanasiasa wa Kiafrika wanapinga sana the right of the people to internal self-determination. Hiki ndicho kinachoendelea sasa hivi huko Dodoma kwenye "Bunge la Katiba" ambalo limejaa wanasiasa wanaodai kuwa wanawawakilisha wananchi ambao hata hawakuwachagua kwa ajili ya kuwatengenezea katiba mpya.
 
Back
Top Bottom