CCM na Chawa, CHADEMA na Makamanda - Nani yuko sahihi?

CCM na Chawa, CHADEMA na Makamanda - Nani yuko sahihi?

Kabende Msakila

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2020
Posts
1,809
Reaction score
1,692
WanaJF Salaam!

Nimeona leo kwenye mitandao ya kijamii issue ya uzinduzi wa Chawa wa Mama kwa upande wa CCM yangu;

Lakini upande wa CDM mara kadhaa majina ya kimkakati ya uendeshaji siasa nchini yanaitwa Makamanda, Operesheni Sangara nk.

Nachojiuliza ni kwa nini ndg zangu hawa wakubali kujiita Chawa wa Mama? Fasiri nyepesi ni ipi?

Mpaka sasa sijaamua kuwa kundi la chawa mpaka hapo nitakapopata uelewa juu ya dhana hii.

Msakila Kabende
Kakonko
 
Chawa wa mama ni wafuasi na mashabiki wa mama.

Hili jina chawa siyo sawa kwenye jamii, kwa kuwa chawa huambatana na watu wachafu. Pia chawa ni wadudu wasiotakiwa kuambatana na binadamu anayejielewa.

Tunawafundisha watoto na jamii kwa ujumla kuepuka uchafu ili wasisumbuliwe na chawa.

Tunaichanganya jamii.
 
Chawa wanafuata na kuishi katika uchafu. Jee wanataka kusema nini hao wajiitao "Chawa wa mama"?

Haya mambo ya hovyo na majina yake wanapohusisha na utawala wajue wana aibisha nchi yetu, kwani mama Samia nimchafu hadi aandamane na chawa wake?

Wahusika wafukuzie mbali hawa wajinga, huyo hata kama ni mwenyekiti wa Lichama la hovyo bado tuna mheshimu kama Rais wetu wote wa nchi.

JamiiForums2069581966.jpg


Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
 
Chawa ni parasitic creature ikimaanisha kwamba wana feed from another living organism.

Ukiangalia dhana ya chawa kama ilivyozagaa (msimu zagao) ni sawa kabisa na upambe/kuwa pamoja/Kuunga mkono siasa, itikadi, maono ya mama Samia Suluhu Hassan.

Ukiangalia kwenye context ya mdudu basi chawa ni mnyonyaji, anaishi kwenye uchafu na hafai. Tujue kutofautisha.
 
Hata marehemu Muhidin Guromo/Ngurumo wa msondo naye walimuita "kamanda", hii nakutoa hofu isikustue sana.

CCM imeweka misingi na mizizi mikubwa sana kwenye nchi hii.
 
Mtazamo wangu: Awali neno Chawa lilionekana kama "nitakua na Wewe popote ulipo"

Kutokana na kutokuwa na uwezo mzuri wa kufikiri na kuona mbali, watu hawa hawakufikiria kwamba IPO siku watu watauliza kazi na madhara hasa ya Chawa ni yapi!

Ni kama walipoanzisha Make Tanzania Great Again wakiiga kule America ya bwana Trump! Wasijue kwamba watanzania watafupisha na kuiita MATAGA ambayo kimsingi ilileta tafsiri basi na wao kuamua kulikataa jina la MATAGA mpaka likapotea kimya kimya. Ni nadra sana kumkuta kada na kumwita MATAGA akafurahia.

Kwa kuwa wenzetu wamekuwa wavivu wa kufikiri na kuchukua kila alisemalo mkubwa, kumbukeni Kuna wakati Mwenyekiti aliwahutubia UVCCM akawaambia waache uchawa haufai na wao wakauacha! Juzi wakati wa hitimisho la maridhiano Ile kauli ya mwenyekiti "Chawa wangu watakuvaa" ikawatoa Shimoni mithili ya panya na wakaamua kuirasimisha kabisa!

Hii kitu ikitumiwa vizuri na wapinzani wa ccm kupata political milage inawezekana kabisa hasa kwa kutumia maana halisi ya mdudu Chawa Pamoja a sifa na athari zake kwa binadamu!

Ni dhahiri kwamba itafanikisha kuonesha uhalisia wa maisha na muendelezo wa kujengeka kwa matabaka katika Jamii! Kwamba Chawa ndio wanaofaidi matunda ya nchi hii kwa kuinyonya huku watu wasafi wakiendelea kutaabika kwa ugumu wa maisha katika nyanja zote kiuchumi na kijamii!

Rais anabeba identity ya nchi! Hivyo anavyozidi kuwa na Chawa wengi na rate ya nchi kunyonywa inaongezeka. Rejea kula kwa urefu wa kamba, tunaitafsiri kwamba chawa wanyonge kadri wanavyo weza ila wasiumizane Matokeo yake ni nchi kudhoofika kiafya (kiuchumi na kijamii) huku Chawa wakizidi kuneemeka na kunenepa!

Ni jambo la kawaida mmeona sasa serikali (Rais) anakopa kwa Nia njema TU ya kufufua uchumi na kuboresha hali ya maisha ya watanzania kijamii (elimu, afya, maji, umeme) lakini wanaoteuliwa kusimamia fedha hizo ni waliojitanabaisha kuwa ni machawa hivyo huishia kuzitafuna na hatuoni hatua zote juu Yao (fumigation) na hivyo' deni la Taifa linakua na linaakisi kupanda kwa gahrama za maisha (mfumuko wa Bei) na kuumiza wasio machawa.

Ilikua ni Rai ya mheshimwa Mwenyekiti kukataa Katu Katu kuwa na Chawa ambao wanajirasimisha tena kupitia majengo ya umma na kuamua kuwa Rais wa watanzania wote na kuwateua watu kusimamia rasilimali za nchi hii kwa kujali uwezo wao na usafi wao badala ya machawa ambao hata inflation kwao ni karata pia ya kusifia!

Kuhusu Makamanda Hilo Sina wasi wasi nalo sana mana linaakisi hali halisi ya maisha ambayo inahitaji mapambano na mapambano yanahitaji Makamanda ambao wako Tayari kufia vitani Ili nchi ikombolewe. Tatizo linakuja kwenye practicability ya huo ukamanda! Inabaki kwenye keyboard au ni kwenda field au ni kutumia platforms mbali Mbali media na makongamano kuendeleza mapambano?
Kumbuka vita hii sio ya silaha ni vita ya hoja nzito zinazohitaji majibu na utekelezaji kwa wenye mamlaka!

Usisahau Michele kg 1= 3500
Nyama kg 1= 12000
Maharagwe kg 1= 4000
Vocha ya buku = 1200
Vyote hivi havitoki Russia Wala Ukraine

Dominika Njema
 
Hata marehemu Muhidin Guromo/Ngurumo wa msondo naye walimuita "kamanda", hii nakutoa hofu isikustue sana.

CCM imeweka misingi na mizizi mikubwa sana kwenye nchi hii.
Simply sema CCM sio chama Cha siasa ni chama dola kinachofanya siasa!
 
WanaJF Salaam!

Nimeona leo kwenye mitandao ya kijamii issue ya uzinduzi wa Chawa wa Mama kwa upande wa CCM yangu;

Lakini upande wa CDM mara kadhaa majina ya kimkakati ya uendeshaji siasa nchini yanaitwa Makamanda, Operesheni Sangara nk.

Nachojiuliza ni kwa nini ndg zangu hawa wakubali kujiita Chawa wa Mama? Fasiri nyepesi ni ipi?

Mpaka sasa sijaamua kuwa kundi la chawa mpaka hapo nitakapopata uelewa juu ya dhana hii.

Msakila Kabende
Kakonko
Kwani chawa anajitambua? Wewe ukubali usikubali wewe ni CHAWA.
 
Mtazamo wangu: Awali neno Chawa lilionekana kama "nitakua na Wewe popote ulipo"

Kutokana na kutokuwa na uwezo mzuri wa kufikiri na kuona mbali, watu hawa hawakufikiria kwamba IPO siku watu watauliza kazi na madhara hasa ya Chawa ni yapi!

Ni kama walipoanzisha Make Tanzania Great Again wakiiga kule America ya bwana Trump! Wasijue kwamba watanzania watafupisha na kuiita MATAGA ambayo kimsingi ilileta tafsiri basi na wao kuamua kulikataa jina la MATAGA mpaka likapotea kimya kimya. Ni nadra sana kumkuta kada na kumwita MATAGA akafurahia.

Kwa kuwa wenzetu wamekuwa wavivu wa kufikiri na kuchukua kila alisemalo mkubwa, kumbukeni Kuna wakati Mwenyekiti aliwahutubia UVCCM akawaambia waache uchawa haufai na wao wakauacha! Juzi wakati wa hitimisho la maridhiano Ile kauli ya mwenyekiti "Chawa wangu watakuvaa" ikawatoa Shimoni mithili ya panya na wakaamua kuirasimisha kabisa!

Hii kitu ikitumiwa vizuri na wapinzani wa ccm kupata political milage inawezekana kabisa hasa kwa kutumia maana halisi ya mdudu Chawa Pamoja a sifa na athari zake kwa binadamu!

Ni dhahiri kwamba itafanikisha kuonesha uhalisia wa maisha na muendelezo wa kujengeka kwa matabaka katika Jamii! Kwamba Chawa ndio wanaofaidi matunda ya nchi hii kwa kuinyonya huku watu wasafi wakiendelea kutaabika kwa ugumu wa maisha katika nyanja zote kiuchumi na kijamii!

Rais anabeba identity ya nchi! Hivyo anavyozidi kuwa na Chawa wengi na rate ya nchi kunyonywa inaongezeka. Rejea kula kwa urefu wa kamba, tunaitafsiri kwamba chawa wanyonge kadri wanavyo weza ila wasiumizane Matokeo yake ni nchi kudhoofika kiafya (kiuchumi na kijamii) huku Chawa wakizidi kuneemeka na kunenepa!

Ni jambo la kawaida mmeona sasa serikali (Rais) anakopa kwa Nia njema TU ya kufufua uchumi na kuboresha hali ya maisha ya watanzania kijamii (elimu, afya, maji, umeme) lakini wanaoteuliwa kusimamia fedha hizo ni waliojitanabaisha kuwa ni machawa hivyo huishia kuzitafuna na hatuoni hatua zote juu Yao (fumigation) na hivyo' deni la Taifa linakua na linaakisi kupanda kwa gahrama za maisha (mfumuko wa Bei) na kuumiza wasio machawa.

Ilikua ni Rai ya mheshimwa Mwenyekiti kukataa Katu Katu kuwa na Chawa ambao wanajirasimisha tena kupitia majengo ya umma na kuamua kuwa Rais wa watanzania wote na kuwateua watu kusimamia rasilimali za nchi hii kwa kujali uwezo wao na usafi wao badala ya machawa ambao hata inflation kwao ni karata pia ya kusifia!

Kuhusu Makamanda Hilo Sina wasi wasi nalo sana mana linaakisi hali halisi ya maisha ambayo inahitaji mapambano na mapambano yanahitaji Makamanda ambao wako Tayari kufia vitani Ili nchi ikombolewe. Tatizo linakuja kwenye practicability ya huo ukamanda! Inabaki kwenye keyboard au ni kwenda field au ni kutumia platforms mbali Mbali media na makongamano kuendeleza mapambano?
Kumbuka vita hii sio ya silaha ni vita ya hoja nzito zinazohitaji majibu na utekelezaji kwa wenye mamlaka!

Usisahau Michele kg 1= 3500
Nyama kg 1= 12000
Maharagwe kg 1= 4000
Vocha ya buku = 1200
Vyote hivi havitoki Russia Wala Ukraine

Dominika Njema
Good narration.
 
Yaani hilo jina ndani yake lina laana aiseee [emoji23][emoji23] .,..
Tena Laana kubwa yani Mzee Kinana na Mh Samia waliwaambia nendeni mkajenge hoja wenyewe wanatengeneza vihoha na viroja vya ajabu kabisa!

Serious mnajioganize kwenye nyumba ya serikali inatengwa fedha ya ukumbi, mapambo, maji, PA na gahrama za Mayor kwenda kuzindua kitu ambacho hata mbele za Mungu ni chukizo?

Kuhalalisha tabia ya kuishi kwa jasho la wengine kwa kujifananisha na Chawa? Serious!

We need mental liberation!

Akili za vijana wengi zimefungiwa kwenye chungu!

Sishangai watendaji wa serikali wakiboronga kwa maana wapo Chawa wa kuwatetea!
 
Back
Top Bottom