Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 17,005
- 20,425
CCM NA SERIKALI JIBUNI HOJA ZA POLEPOLE, MSIMZIME KIDOLA.
Na Yericko Nyerere
Kinga uliyonayo ni kwa muda tu, hakuna kinga ya kudumu, Hata Job Ndugai na wenzake kinga walizojiwekea kipindi walipokuwa kwenye dibwi la kuvunja haki za watu na kuvunja Katiba ya Tanzania, ina muda mfupi sana wataanza kutoa nachozi ya samaki soon. Hivi ndivyo wahenga husema, Kinga ya kirais aliyokuwa nayo Humphrey Polepole katika ule utawala dharimu imeisha, ni kinga hiyohiyo ndio alikuwa nayo Paul Makonda, Sabaya, Chalamila, Mnyeti, Odunga na wahuni wengine wengi.
Tulishaisikia na kuona milio ya maumivu ya Sabaya, huku Paul Makonda akianza kuwambwa kisawasawa na kuandaliwa makazi mapya Segerea. Naam miliyo ya maumivu ya Polepole tumeanza kuisikia vizuri sana, Bahati mbaya kwetu sisi milio hiyo sio migeni, Tulishalia sana, Tulishazika ndugu zetu wengu, Tulishafungwa jela sana na tulishafanyiwa madhila mengi, Polepole akiwa ni moja ya magenge makuu ya uhalifu huo nchini. Lakini tulishavuka viwango hivyo vya mateso, na Sasa tuna wajibu wa kumtetea yoyote anayeonewa.
Serikali inawajibu wa kujibu hoja za Polepole badala ya kutumia vyombo vyake vya dola kumnyamazisha, Hoja za Polepole ni nzito na zina maslahi kwa umma wa Watanzania, zijibiwe kwa hoja na sio vinginevyo. Uhuru wa Polepole usipokwe kwa njia zilezile tulizopitishwa sisi. Yale madhila yaishie kwetu, tuzuie yasiendelee kwa wengine. Polepole ajibibiwe.
Hoja ya Polepole kwamba hii ni Awamu ya Tano itakayokamilika 2025 na sio ya Sita ni hoja ya muhimu sana kwa umma, Kwasababu kwa muda mrefu serikali hii iliyojichagua kinguvu 2020 kukamilisha awamu ya tano ya miaka 10, imekuwa ikijitambulisha kwamba ni serikali ya awamu ya sita. Jambo ambalo kimantiki si kweli. Ni wajibu wa serikali itoke imjibu Polepole, badala yake inamjibu kwa kutumia machineries zilezile ilizotumia kwetu.
CCM na Serikali yake kwa miaka mingi ikishindwa kujibu hoja kinzani, imekuwa ikiagiza Vyombo vya "dola" kama Polisi, TRA, TCRA, Uhamiaji, TAKUKURU, MAHAKAMA nk, kuzima hoja za wapinzani, na kwa miaka mitano iliyopita vimetumika kwakiwango cha kutisha kuumiza Watanzania wengi sana hususani Wanachadema wengi hadi leo wako waliokufa (Alfonce Mawazo), wako walipotea (Ben Saanane na Azory), wako vilema (Lissu), wako walioko jela (Mbowe), na wako waliofilisiwa (Mbowe na wengine), wako wanaohangaika mahakamani kila siku (Wanachadema kila kona ya Tanzania. Msingi wa haya yote ni ccm na serikali yao kushindwa kujibu hoja zao.
Hatuna shida na Polepole kusulubiwa kwa mechanism zilezile zilizotusurubu sisi, Msulubuni Polepole kama Polepole kwa makosa mengine hata yake ya kijinga ya Vieitii, sio kwa hizi hoja zake, hoja zake jibuni kwa hoja, Hoja zake ni hoja zetu pia, Hoja zake zina maslahi kwa umma. Tunakemea na kuzitaka mamlaka zirudi kwenye mstari, Leo Polepole analilia uhuru wa kutoa maoni ambao yeye akiwa madarakani aliupora kwa wengine, Noo tunaka Polepole awe huru tena huru kabisa.
Ni Polepole huyu huyu na CCM yao walichota pesa ya Umma na wakaongoza genge la kupora uhuru wa Watu kuwa wanachama wa chama chochote wakipendacho, wakawatishia na kuwapatia pesa na ahadi lukiki za kimadaraka ili wahame vyama vyao walivyovipenda, ni Polepole huyu huyu alikuwa na lugha chafu sana kwa wanaccm wenzake waliokuwa na maoni tofauti ndani ya Chama kumbuka matusi yake ya nguoni kwa Paul Makonda alipoanza kuonyesha nia ya kugombea ubunge Kigamboni.
Hayo yote hayawezi kuwa sababu tuache kusikiliza na kujadili hoja zake, Tumpuuze Polepole, lakini tuzichukue hoja zake tuzichambue, tuzitake mamlaka ya dola na chama chake wazijibu hoja zake. Tutakuwa wajinga kama hatutaitaka serikali ijibu hoja za Polepole na badala yake tukaacha Polepole asulubiwa kama tulivyofanyiwa sisi, Kitendo cha kuitaka serikali ijibu na ikijibu, tutatukuwa tumefanikiwa kufunga njia ya mateso kwa Watanzania wengine kesho.
Tunaposimama kudai Katiba mpya tuna maana pana zaidi na moja ya mambo muhimu ni kama haya katiba itazuia vyombo vya dola kutumika kisiasa, Leo Mwenyekiti wetu amebambikiwa kesi ya Ugaidi kisa anadai katiba mpya, Hilo haliwezi kuwa mwisho wa madai ya umma kuhusu katiba mpya. Mwachieni Mbowe, jibuni hoja zake.
Na Yericko Nyerere
Kinga uliyonayo ni kwa muda tu, hakuna kinga ya kudumu, Hata Job Ndugai na wenzake kinga walizojiwekea kipindi walipokuwa kwenye dibwi la kuvunja haki za watu na kuvunja Katiba ya Tanzania, ina muda mfupi sana wataanza kutoa nachozi ya samaki soon. Hivi ndivyo wahenga husema, Kinga ya kirais aliyokuwa nayo Humphrey Polepole katika ule utawala dharimu imeisha, ni kinga hiyohiyo ndio alikuwa nayo Paul Makonda, Sabaya, Chalamila, Mnyeti, Odunga na wahuni wengine wengi.
Tulishaisikia na kuona milio ya maumivu ya Sabaya, huku Paul Makonda akianza kuwambwa kisawasawa na kuandaliwa makazi mapya Segerea. Naam miliyo ya maumivu ya Polepole tumeanza kuisikia vizuri sana, Bahati mbaya kwetu sisi milio hiyo sio migeni, Tulishalia sana, Tulishazika ndugu zetu wengu, Tulishafungwa jela sana na tulishafanyiwa madhila mengi, Polepole akiwa ni moja ya magenge makuu ya uhalifu huo nchini. Lakini tulishavuka viwango hivyo vya mateso, na Sasa tuna wajibu wa kumtetea yoyote anayeonewa.
Serikali inawajibu wa kujibu hoja za Polepole badala ya kutumia vyombo vyake vya dola kumnyamazisha, Hoja za Polepole ni nzito na zina maslahi kwa umma wa Watanzania, zijibiwe kwa hoja na sio vinginevyo. Uhuru wa Polepole usipokwe kwa njia zilezile tulizopitishwa sisi. Yale madhila yaishie kwetu, tuzuie yasiendelee kwa wengine. Polepole ajibibiwe.
Hoja ya Polepole kwamba hii ni Awamu ya Tano itakayokamilika 2025 na sio ya Sita ni hoja ya muhimu sana kwa umma, Kwasababu kwa muda mrefu serikali hii iliyojichagua kinguvu 2020 kukamilisha awamu ya tano ya miaka 10, imekuwa ikijitambulisha kwamba ni serikali ya awamu ya sita. Jambo ambalo kimantiki si kweli. Ni wajibu wa serikali itoke imjibu Polepole, badala yake inamjibu kwa kutumia machineries zilezile ilizotumia kwetu.
CCM na Serikali yake kwa miaka mingi ikishindwa kujibu hoja kinzani, imekuwa ikiagiza Vyombo vya "dola" kama Polisi, TRA, TCRA, Uhamiaji, TAKUKURU, MAHAKAMA nk, kuzima hoja za wapinzani, na kwa miaka mitano iliyopita vimetumika kwakiwango cha kutisha kuumiza Watanzania wengi sana hususani Wanachadema wengi hadi leo wako waliokufa (Alfonce Mawazo), wako walipotea (Ben Saanane na Azory), wako vilema (Lissu), wako walioko jela (Mbowe), na wako waliofilisiwa (Mbowe na wengine), wako wanaohangaika mahakamani kila siku (Wanachadema kila kona ya Tanzania. Msingi wa haya yote ni ccm na serikali yao kushindwa kujibu hoja zao.
Hatuna shida na Polepole kusulubiwa kwa mechanism zilezile zilizotusurubu sisi, Msulubuni Polepole kama Polepole kwa makosa mengine hata yake ya kijinga ya Vieitii, sio kwa hizi hoja zake, hoja zake jibuni kwa hoja, Hoja zake ni hoja zetu pia, Hoja zake zina maslahi kwa umma. Tunakemea na kuzitaka mamlaka zirudi kwenye mstari, Leo Polepole analilia uhuru wa kutoa maoni ambao yeye akiwa madarakani aliupora kwa wengine, Noo tunaka Polepole awe huru tena huru kabisa.
Ni Polepole huyu huyu na CCM yao walichota pesa ya Umma na wakaongoza genge la kupora uhuru wa Watu kuwa wanachama wa chama chochote wakipendacho, wakawatishia na kuwapatia pesa na ahadi lukiki za kimadaraka ili wahame vyama vyao walivyovipenda, ni Polepole huyu huyu alikuwa na lugha chafu sana kwa wanaccm wenzake waliokuwa na maoni tofauti ndani ya Chama kumbuka matusi yake ya nguoni kwa Paul Makonda alipoanza kuonyesha nia ya kugombea ubunge Kigamboni.
Hayo yote hayawezi kuwa sababu tuache kusikiliza na kujadili hoja zake, Tumpuuze Polepole, lakini tuzichukue hoja zake tuzichambue, tuzitake mamlaka ya dola na chama chake wazijibu hoja zake. Tutakuwa wajinga kama hatutaitaka serikali ijibu hoja za Polepole na badala yake tukaacha Polepole asulubiwa kama tulivyofanyiwa sisi, Kitendo cha kuitaka serikali ijibu na ikijibu, tutatukuwa tumefanikiwa kufunga njia ya mateso kwa Watanzania wengine kesho.
Tunaposimama kudai Katiba mpya tuna maana pana zaidi na moja ya mambo muhimu ni kama haya katiba itazuia vyombo vya dola kutumika kisiasa, Leo Mwenyekiti wetu amebambikiwa kesi ya Ugaidi kisa anadai katiba mpya, Hilo haliwezi kuwa mwisho wa madai ya umma kuhusu katiba mpya. Mwachieni Mbowe, jibuni hoja zake.