CCM na Serikali jibuni hoja za Humphrey Polepole, msimzime kidola

CCM na Serikali jibuni hoja za Humphrey Polepole, msimzime kidola

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2010
Posts
17,005
Reaction score
20,425
CCM NA SERIKALI JIBUNI HOJA ZA POLEPOLE, MSIMZIME KIDOLA.

Na Yericko Nyerere

Kinga uliyonayo ni kwa muda tu, hakuna kinga ya kudumu, Hata Job Ndugai na wenzake kinga walizojiwekea kipindi walipokuwa kwenye dibwi la kuvunja haki za watu na kuvunja Katiba ya Tanzania, ina muda mfupi sana wataanza kutoa nachozi ya samaki soon. Hivi ndivyo wahenga husema, Kinga ya kirais aliyokuwa nayo Humphrey Polepole katika ule utawala dharimu imeisha, ni kinga hiyohiyo ndio alikuwa nayo Paul Makonda, Sabaya, Chalamila, Mnyeti, Odunga na wahuni wengine wengi.

Tulishaisikia na kuona milio ya maumivu ya Sabaya, huku Paul Makonda akianza kuwambwa kisawasawa na kuandaliwa makazi mapya Segerea. Naam miliyo ya maumivu ya Polepole tumeanza kuisikia vizuri sana, Bahati mbaya kwetu sisi milio hiyo sio migeni, Tulishalia sana, Tulishazika ndugu zetu wengu, Tulishafungwa jela sana na tulishafanyiwa madhila mengi, Polepole akiwa ni moja ya magenge makuu ya uhalifu huo nchini. Lakini tulishavuka viwango hivyo vya mateso, na Sasa tuna wajibu wa kumtetea yoyote anayeonewa.

Serikali inawajibu wa kujibu hoja za Polepole badala ya kutumia vyombo vyake vya dola kumnyamazisha, Hoja za Polepole ni nzito na zina maslahi kwa umma wa Watanzania, zijibiwe kwa hoja na sio vinginevyo. Uhuru wa Polepole usipokwe kwa njia zilezile tulizopitishwa sisi. Yale madhila yaishie kwetu, tuzuie yasiendelee kwa wengine. Polepole ajibibiwe.

Hoja ya Polepole kwamba hii ni Awamu ya Tano itakayokamilika 2025 na sio ya Sita ni hoja ya muhimu sana kwa umma, Kwasababu kwa muda mrefu serikali hii iliyojichagua kinguvu 2020 kukamilisha awamu ya tano ya miaka 10, imekuwa ikijitambulisha kwamba ni serikali ya awamu ya sita. Jambo ambalo kimantiki si kweli. Ni wajibu wa serikali itoke imjibu Polepole, badala yake inamjibu kwa kutumia machineries zilezile ilizotumia kwetu.

CCM na Serikali yake kwa miaka mingi ikishindwa kujibu hoja kinzani, imekuwa ikiagiza Vyombo vya "dola" kama Polisi, TRA, TCRA, Uhamiaji, TAKUKURU, MAHAKAMA nk, kuzima hoja za wapinzani, na kwa miaka mitano iliyopita vimetumika kwakiwango cha kutisha kuumiza Watanzania wengi sana hususani Wanachadema wengi hadi leo wako waliokufa (Alfonce Mawazo), wako walipotea (Ben Saanane na Azory), wako vilema (Lissu), wako walioko jela (Mbowe), na wako waliofilisiwa (Mbowe na wengine), wako wanaohangaika mahakamani kila siku (Wanachadema kila kona ya Tanzania. Msingi wa haya yote ni ccm na serikali yao kushindwa kujibu hoja zao.

Hatuna shida na Polepole kusulubiwa kwa mechanism zilezile zilizotusurubu sisi, Msulubuni Polepole kama Polepole kwa makosa mengine hata yake ya kijinga ya Vieitii, sio kwa hizi hoja zake, hoja zake jibuni kwa hoja, Hoja zake ni hoja zetu pia, Hoja zake zina maslahi kwa umma. Tunakemea na kuzitaka mamlaka zirudi kwenye mstari, Leo Polepole analilia uhuru wa kutoa maoni ambao yeye akiwa madarakani aliupora kwa wengine, Noo tunaka Polepole awe huru tena huru kabisa.

Ni Polepole huyu huyu na CCM yao walichota pesa ya Umma na wakaongoza genge la kupora uhuru wa Watu kuwa wanachama wa chama chochote wakipendacho, wakawatishia na kuwapatia pesa na ahadi lukiki za kimadaraka ili wahame vyama vyao walivyovipenda, ni Polepole huyu huyu alikuwa na lugha chafu sana kwa wanaccm wenzake waliokuwa na maoni tofauti ndani ya Chama kumbuka matusi yake ya nguoni kwa Paul Makonda alipoanza kuonyesha nia ya kugombea ubunge Kigamboni.

Hayo yote hayawezi kuwa sababu tuache kusikiliza na kujadili hoja zake, Tumpuuze Polepole, lakini tuzichukue hoja zake tuzichambue, tuzitake mamlaka ya dola na chama chake wazijibu hoja zake. Tutakuwa wajinga kama hatutaitaka serikali ijibu hoja za Polepole na badala yake tukaacha Polepole asulubiwa kama tulivyofanyiwa sisi, Kitendo cha kuitaka serikali ijibu na ikijibu, tutatukuwa tumefanikiwa kufunga njia ya mateso kwa Watanzania wengine kesho.

Tunaposimama kudai Katiba mpya tuna maana pana zaidi na moja ya mambo muhimu ni kama haya katiba itazuia vyombo vya dola kutumika kisiasa, Leo Mwenyekiti wetu amebambikiwa kesi ya Ugaidi kisa anadai katiba mpya, Hilo haliwezi kuwa mwisho wa madai ya umma kuhusu katiba mpya. Mwachieni Mbowe, jibuni hoja zake.

FB_IMG_1639286718224.jpg

 
Kunatatzo kwenye engine ya gari, sasa ubaya wake Ni kuwa ili tufike, tunamaamzi 2, ama kuifumua engine yote, au kukodi Kali lituvute kutufikisha tunapokwenda, changamoto kubwa tulio nayo Ni kuwa fundi na drive, wanamawazo tofauti, wakati fundi anasema engine mbovu, dereva anasema hapana maana gari inawaka na kutembe kidg japo inatoa Moshi mwingi.

Abiria tupo tu hatujua, kila mtu anasema anavyojua, tutafika ila ama tutachelewa Sana au abiria wengi watakufa na njaa maana hawana akiba ya kutosha kuvumilia.

Stay tuned.
 
Karume alipofariki kulikuwa na uchaguzi? Jumbe alipojiuzuru kulikuwa na kura za wananchi?

Wapuuzi nyie dawa yenu imeshaiva, subirini kuinywa tu!
Hizo awamu nane zilichaguliwa na wananchi.

Hii tuliyonayo ni awamu ya tano iliyochaguliwa 2015 mhula wa kwanza, na baadaye 2020 mhula wa pili.

#kataawahuni
 
Shida ni kuwa polepole HAAMINIKI
Sitaki kuamini Kama mleta mada NI msahaulifu kiasi hichi.
Watu wanasema" KARMA IS REAL"
"unaijua vieitee wewe"?
CCM walivyoiba kura na mabegi ya kura feki yalivyokamatwa polepole alisema nini?.
Kuna wakati acha Mambo yapite.
Pole pole ni mchuma janga.
Aliingizwa CCM na MAGUFULI Sasa amekuwa YATIMA
 
CCM NA SERIKALI JIBUNI HOJA ZA POLEPOLE, MSIMZIME KIDOLA.

Na Yericko Nyerere

Kinga uliyonayo ni kwa muda tu, hakuna kinga ya kudumu, Hata Job Ndugai na wenzake kinga walizojiwekea kipindi walipokuwa kwenye dibwi la kuvunja haki za watu na kuvunja Katiba ya Tanzania, ina muda mfupi sana wataanza kutoa nachozi ya samaki soon.
Mimi naongezea, pamoja na polepole kuwa mhuni aliechangamka, akatu kwenye kaburi la SEIF (RIP) kijana alijitoa ufaham sana enzi zile, na bado wapo wengi wataokota makopo

Sasa wanaanza itatana viroboto wao kwa wao
 
Nyerere aliyetawala Tanzania kwa mihula minne ya jumla ya miaka 21 kwa kuchaguliwa na wananchi alitawala kwa awamu ngapi?
Awamu moja kwa idadi ya awamu alizochaguliwa.

However, baadaye katiba iliweka utaratibu wa ukomo wa mpaka mihula miwili (kila mhula miaka mitano) kwa kila awamu.

Hii tuliyopo ni awamu ya tano kwa maana uchaguzi uliopita Watanzania wengi tuliipa ridhaa awamu ya tano kumalizia mhula wa pili unaoisha 2025.

Akigombea 2025 na akashinda; Watanzania wengi tutakuwa tumempa ridhaa ya kuongoza awamu ya sita.
 
Iyo tafsiri ya Awamu umeitoa wapi?

ZANZIBAR kuna Awamu ya 8 saivi Polepole amewai kuwa hadi mwenezi wa CCM ulimsikia wapi akihoji hayo?

Mwambie Polepole kuna matokeo ya kumdharau Amiri Jeshi Mkuu.

Kama anataka kuyapata Safari hii atayapata!
Jana Polepole aliwaambia hoja haipigwi rungu, nadhani utakuwa hukumsikia, hoja za Polepole zijibiwe kwa hoja, sio kejeli au vitisho, huu wako ni ushamba.
 
Awamu moja kwa idadi ya awamu alizochaguliwa.

However, baadaye katiba iliweka utaratibu wa ukomo wa mpaka mihula miwili (kila mhula miaka mitano) kwa kila awamu...
Safi, umetengeneza foundation nzuri, Katiba iliyopo inaweka madarakani serikali husika, na Katiba hiyo hiyo inatoa maelezo nini kitatokea endapo Rais aliyepo madarakani ataondoka ofisini either kwa kufariki, kuugua, au vinginevyo.

Moreover, Katiba ikasema, kama Rais aliyepo madarakani hatamaliza muhula wake, ni yule atakayekuwa makamu wa Rais ndie atamalizia muda uliobaki, sasa hapa tunazungumza kisheria, sio habari za Zanzibar au popote pengine.

Ndipo unapoona hoja ya Polepole ilivyo na nguvu, huyu mtu anaonekana ameshachungulia mahala akapata majibu, na wala sio kusema tu CCM walijiwekea utaratibu wa kutoka awamu moja kwenda nyingine bila kuandikwa popote, wanasahau Katiba kama sheria mama inatoa majibu ya hayo yote.

Watake wasitake, Samia kisheria anamalizia muda uliobaki wa awamu ya tano, kama akitaka kugombea tena 2025 ndio ataianza awamu ya sita, hii ni sheria inavyosema sio kelele.
 
Safi, umetengeneza foundation nzuri, Katiba iliyopo inaweka madarakani serikali husika, na Katiba hiyo hiyo inatoa maelezo nini kitatokea endapo Rais aliyepo madarakani ataondoka ofisini either kwa kufariki, kuugua, au vinginevyo...
Unatokaje awamu ya tano kwenda ya sita bila kupewa ridhaa na Watanzania wengi?

Ilani anayoitekeleza ni ya awamu ya tano au ya sita?
 
Unatokaje awamu ya tano kwenda ya sita bila kupewa ridhaa na Watanzania wengi?

Ilani anayoitekeleza ni ya awamu ya tano au ya sita?
Haya ya ilani na mengineyo tusiyaegemee sana kwasababu Katiba yetu inampa Rais husika madaraka makubwa, anaweza akaitupa pembeni ilani ya mwenzake at any time akatengeneza yake japo alikuwa makamu wake wa Rais, naona hapa muhimu iangaliwe zaidi sheria inasema nini.
 
Unatokaje awamu ya tano kwenda ya sita bila kupewa ridhaa na Watanzania wengi?

Ilani anayoitekeleza ni ya awamu ya tano au ya sita?
Awamu yako ya Tano kulikuwa na ilani mbili tofauti za uchaguzi, ya mwaka 2015 na 2020.
 
Back
Top Bottom