CCM nambari wani

niwie radhi mkuu Erythrocyte nipe sababu 3 tu za wewe kukichukia Chama Cha Mapinduzi kinachoaminiwa na kupendwa na takriban 95% ya watanzania wote.

uongo wa takwimu zako ushahidi wake anao marehemu lewis makame , alishuhudia 2010 , tukija kwenye hili la sababu 3 za mimi kuichukia ccm , ukisoma vizuri uzi huu utagundua kwamba hakuna SABABU 3 TU PEKE YAKE , BALI KUNA MAMIA YA SABABU ZA KUYAPINGA MAGAMBA !
 
Last edited by a moderator:
kuna mzee hapo juu anatafuna mvinyo wa asili ( bila shaka ni chimpumu ) ambayo kila siku inampunguzia siku za kuishi , wao wanatafuna nyama choma na bia !
 

huu uzi umekaa kishabiki tu kweli yapo mambo machache CCM ilikosea . Lakini mazuri ya kujivunia yapo tena mengi sana legeza moyo wako
 
huu uzi umekaa kishabiki tu kweli yapo mambo machache CCM ilikosea . Lakini mazuri ya kujivunia yapo tena mengi sana legeza moyo wako

tuwekee hapa hayo mazuri tuyaone , hatulegezi moyo wala kamba , halafu huna haja ya kutia shaka mkuu , cdm ni watanganyika wenzio kwahiyo wakichukua nchi mwaka 2015 ( KAMA TUNAVYOTARAJIA ) Wewe utakuwa salama tu , LABDA KAMA NI MPIGA MAGUMASHI , MAANA KIUKWELI HAKUTAKUWA NA MSWALIE MTUME .
 
nimefanya random sampling

Mkuu hii random sampling sio sahihi. Umetumia makundi gani ktk jamii kufanyia utafiti huu?

Tafakari data nyepesi kwa akili ya kawaida; kundi la vijana na watoto chini ya miaka 18 linaunda asilimia ngapi ya Watz wote, ukitilia maanani kwamba kundi hili halina chama? Una maana kundi hili ndio hiyo 5% uliyobakiza? Kama tutachukulia kuwa hiyo ndio hali halisi, je, wanachama wa upinzani wanaunda asilimia ngapi?

Muhimu naona ktk nyuzi nyingi hapa JF mambo ya siasa hukaa kishabiki na kiupofu zaidi kuliko hali halisi. Tunatarajia wadau maarufu na wakubwa kutengeneza na kuonyesha njia badala ya kuyumbisha na kupotosha ukweli kama hivi. Ukweli na uadilifu ndio utakaotujengea Tz bora, leo na kesho!
 
usithubutu kumuamini kijana yeyote wa lumumba , ni wasakatonge .
 
ccm ndio mama yenu,amewazaa na kuwatunza toka nyerere mpaka sasa

Maneno yako yamekaa kichwa chini miguu juu! Unajua tofauti ya siasa za TANU na siasa za CCM? Jambo usilolijua litakusumbua.

Kusoma University bure na kusoma kwa mkopo kunafanana? Na je, kutibiwa hospitali moja na waziri kunafanana na wewe kutibiwa hospitali ya Temeke na waziri kutibiwa South Africa? Naona kama uko usingizini vile!
 


kipimo cha akili timamu si kuvaa nguo, kati 100% ya watanzania niliofanya nao mahojiano 95% wanatambua na kukubali mchango wa CCM ktk maendeleo ya taifa hili. Hawana imani na viongozi wa vyama vya upinzani na majibu utayapata 2015 :hail:
 
kipimo cha akili timamu si kuvaa nguo, kati 100% ya watanzania niliofanya nao mahojiano 95% wanatambua na kukubali mchango wa CCM ktk maendeleo ya taifa hili. Hawana imani na viongozi wa vyama vya upinzani na majibu utayapata 2015 :hail:

Tatizo lako umekaa kujihami kwamba kila anayetoa maoni yasiyoendana na msimamo wako basi ni mpinzani. Hizi ni fikra hafifu sana.

Unafikiri watu wana haja na CCM au Upinzani? Tunahitaji elimu nzuri, afya bora na huduma nyingine za kijamii zilizoboreshwa. Atawale yeyote, kama huwezi kupata mambo hayo haitafaa chochote.

Mfano, nilisoma darasa la 1-3 kwa ada ya shs 18/= kwa mwaka, na baada ya hapo nikaendelea hadi chuo kikuu BURE. Hiyo ni CCM? Soma maana na mantiki ya hoja kabla hujajibu. Usiwe kama askari wa siafu anayekaa meno wazi akisubiri kudaka chochote hata kipande cha kijiti akidhani ni adui!

Usijione kama una uchungu na unaijua CCM kuliko watu wengine. Wote tumezaliwa na kukulia hapa hapa. Pia wengine tuna mchango ndani ya hiki chama kuliko unavyofikiria au kujua.
 

wewe pia ni mnufaikaji wa mfumo mzuri wa ccm na sera za ccm imewezesha watanzania vijana kupewa elimu ya chuoni kusoma bure. juzi kikwete ametangaza kufuta ada za sekondari nchini watoto wenu wasome bure.ccm inawajali sana kama mama mzazi
 
wewe pia ni mnufaikaji wa mfumo mzuri wa ccm na sera za ccm imewezesha watanzania vijana kupewa elimu ya chuoni kusoma bure. juzi kikwete ametangaza kufuta ada za sekondari nchini watoto wenu wasome bure.ccm inawajali sana kama mama mzazi

Rais hakutangaza kufuta ada ila alisema wanaangalia uwezekano wa kutoa elimu bure. Bado hiyo haijawa sera rasmi.

Wewe na wenzio wa aina yako hamjui historia ya Tz, aidha kwa bahati mbaya au kwa malengo. Wengi wa wazee watawala unaowapigia debe wanatokana na wazazi wakulima masikini. Isingekuwa sera ya TANU kutoa elimu bure wasingekuwa ktk ngazi yoyote ya uongozi, labda ubalozi wa nyumba kumi.

Wamejisahau, wanajilipa mishahara minono na marupurupu manene kama hizo laki tatu kwa siku vikao vya Bunge la Katiba, wanasomesha watoto wao vyuo ghali na ng'ambo; na BAADHI ya watoto wa masikini wanakopeshwa na wengi hawana kabisa uwezo wa kusomesha watoto wao hata kwenye hizi shule za kata!

Hali hii inapelekea kuwepo kwa tabaka maalum la watawala na pia tabaka lingine MAALUM la watawaliwa. Tunaposema kweli tunaitwa 'wapinzani'. Tunachotaka ni chama kurudi kwenye misingi ya asili ya kujali watu wanyonge. Kama wao waliwezeshwa kufika walipo kutokana na sera nzuri iweje leo wanadidimiza umma kwa kutumia madaraka waliyoyapata kwa hisani ya umma huo huo?

Si vyema kumuona kila msemakweli kuwa ni mpinzani wa CCM. Kama mtu si mwana CCM hana haki ya kuikosoa? Kwani si ndio wanaotunga sera na kutawala kwa sasa?
 
wewe pia ni mnufaikaji wa mfumo mzuri wa ccm na sera za ccm imewezesha watanzania vijana kupewa elimu ya chuoni kusoma bure. juzi kikwete ametangaza kufuta ada za sekondari nchini watoto wenu wasome bure.ccm inawajali sana kama mama mzazi

leo umekubali kama hizo picha ni za nchi hii au bado unaamini kwamba ni za somalia ?
 

SAFI SANA , UMEMPA ZA USO , kWA KUKUMEGEA SIRI TU HUYO NDIO KIONGOZI WA BUKU 7 FC , HUU UJUMBE WAKO UMETUA LUMUMBA !
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…