LGE2024 CCM: TAMISEMI itambue demokrasia yetu ni changa, ipuuze makosa madogomadogo katika hatua ya rufaa uchaguzi Serikali za mitaa

LGE2024 CCM: TAMISEMI itambue demokrasia yetu ni changa, ipuuze makosa madogomadogo katika hatua ya rufaa uchaguzi Serikali za mitaa

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

CCM: TAMISEMI IPUUZE MAKOSA MADOGO MADOGO, KUKUZA DEMOKRASIA

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeiomba Wizara ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), kuwaelekeza wasimamizi Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, kupuuza makosa madogo madogo yaliyotokea, ili kuruhusu wagombea wengi kushiriki uchaguzi huo.

Akizungumza na wahariri na waandishi waandamizi wa vyombo vya hahari nchini, Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, ametoa mfano wa makosa hayo yanayostahili kupuuzwa ni pamoja na wagombea kukosea herufi.

Kupitia mkutano huo uliofanyika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar es Salaam, leo Novemba 12, 2024, Balozi Nchimbi amesema ni vyema TAMISEMI ikaangalia uwezekano wa kuwarudisha wagombea wote walioenguliwa kutokana na makosa hayo madogo madogo ili kuhamasisha ukuaji wa demokrasia kwenye uchaguzi huo.

Aidha, kuhusu sehemu kubwa ya malalamiko mengi ya kuenguliwa kuonekana ni ya wagombea wa vyama vya upinzani, Balozi Nchimbi amewatoa shaka Watanzania kuwa, si kweli kwamba wagombea walioenguliwa ni wale wa vyama vya upinzani pekee, bali pia hata wagombea wa CCM wapo waliowekewa mapingamizi ya kugombea.

“Waziri wa TAMISEMI tunajua anafuata sheria, lakini ni muhimu kutambua demokrasia yetu hii bado ni changa hivyo tunahitaji muda wa kuendelea kujiífunza…tunaziomba mamlaka hasa TAMISEMI katika nyakati za mwisho za rufaa kuyapuuza makosa madogo madogo ili watu wengi wapate nafasi ya kugombea", alisema Dkt. Nchimbi.
Ccm wanajitekenya na kucheka wenyewe.
 

"Wapo Wanaccm waliowekewa mapingamizi, wapo wa ACT, wapo wa CHADEMA, na majibu ya mapingamizi yalitoka, lakini kwa hatua za rufaa kwa maelekezo ya Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi ambaye ni Rais wa Tanzania nilipofanya naye mazungumzo, ambacho tumekiona wapo wagombea wengi sana wa vyama mbalimbali ambao waliwekewa mapingamizi katika hatua za awali.

Katika maelekezo ya Mwenyekiti wa CCM, tumeelezana kuwa ni vizuri watu wapate nafasi, hivyo nitumie nafasi hii kutoa wito kwa waziri mwenye dhamana ya serikali za mitaa, tunatambua umefuata sheria lakini ni muhimu kukumbuka kwamba demokrasia yetu bado ni changa, ni muhimu tuzidi kukua.

Soma Pia:
Tunaziomba mamlaka hasa TAMISEMI, katika hatua ya mwisho za rufaa kuyapuuza makosa madogomadogo ili Watanzania wengi zaidi wapate nafasi ya kugombea. Yapo makosa makubwa, kwa mfano nafasi ni maalumu kwa wanawake lakini amejaza mwanaume"
Yaani ccm ni washiriki wa uchaguzi halafu ndiyo wasimamizi wa uchaguzi huo huo !!

Huo ni utapeli na dharau ya hali ya juu sana dhidi ya wananchi.
Tlaatlaah Lucas Mwashambwa
 
Safi sana CCM baba wa siasa
Hapa ni ile unatengeneza tatizo na unajaribu kuwaonyesha watu kwamba unalitatua tatizo hilo ,kinacho endelea katika mchakato wa uchaguzi wa serikali za mitaa ni AIBU kwa Taifa, wasimamizi wa uchaguzi walianza kwa kufunga na kukimbia ofisi ili wapinzani wasichukue wala kurejesha fomu, wachache walifanikiwa kuchukua na kurudisha , majina yao yalikatwa, wakati wa kukata rufaa, wamekimbia tena na kufunga ofisi ili wapinzani wasirudishe rufaa zao.

Kama ccm wanataka kujisafisha wamweleze waziri wa TAMISEMI ajiuzulu kwa kuvuruga uchaguzi. Vinginevyo tutajua amevuruga kwa maelekezo yao.

Sijui udhalimu huu utaisha lini nchi hii, halafu watu na akili zao timamu anafurahia udhalimu katika uchaguzi, sasa MTU akivuruga uchaguzi kwa makusudi ataweza vipi kusimamia barabara ijengwe kwa viwango!? Atafamya kwa kiwango cha kuchakachua kama walivyo chakachua uchaguzi
 
View attachment 3150555Ni Samia Tena na Demokrasia, Aagiza Wagombea Walioenguliwa kwa Makosa Madogomadogo Majina yao Yarudishwe

Na Joseph Bulebe, Dar es salaam

Rais Samia Suhuhu Hassan ameendelea kuonesha ulimwengu na watanzania kwa ujumla kuwa demokrasia ndo kitu cha msingi katika uongozi wake unaofuata utawala bora na demokrasia.

Katika hali ambayo haikutegemewa na wagombea wote waliokuwa wameenguliwa kisheria na wasimamizi wa uchaguzi wa serikali za mitaa kwa makosa madogomadogo, Rais Samia ameamuagiza Waziri wa TAMISEMI, Mohammed Mchengelwa kuwarudisha wagombea wote walioenguliwa kwa makosa madogo madogo kama kukosea mwaka wa kuzaliwa, eneo analotoka, tarehe nk.

Akiongea leo na waadishi wa Habari, Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, Balozi Emmanuel Nchimbi amesema Rais Samia amemugiza kumwambia waziri wa TAMISEMI wagombea wenye makosa hayo warudishwe katika kinyanganyilo cha uchaguzi ili kulinda demokrasia changa inayokuwa katika nchi yetu.

Hii sio mara ya kwanza Mh Rais anaonesha ukomavu wa demokrasia nchini katika mambo ya siasa.

Mara tu baada ya kuingia madarakani Mh Rais aliruhusu mikutano ya siasa ya wazi iliyokuwa imekatazwa na mtangulizi wake.

Hakuishia hapo Mh Rais aliunda tume ambayo pamoja na mengine ilipendekeza kuundwa kwa tume huru ya uchaguzi ambayo tayari imeundwa, kuondoa pingamizi ya zuio ya mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa ambalo nalo limeondolewa.

Mh Rais katika kuonesha demokrasia zaidi aliwaondolea kesi mbalimbali wapinzani mahakamani kama vile Mwenyekiti wa CHADEMA na makamu wake pamoja na kuwarudisha nchini wapinzani wote waliokuwa wamekimbia nchi kipindi cha awamu ya tano.

Kama hiyo haitoshi Rais amewakaribisha Ikulu Wapinzani na kuongea nao na chini ya utawala wake wapinzani wanaalikwa karibia kila tukio la kitaifa na dhifa mbalimbali za kitaifa.

Huyu ndo Rais Samia, Mwanamama wa kwanza katika nchi ya Tanzania na ukanda wa Afrika Mashariki anayeipeleka nchi ya Tanzania katika kufanya uchaguzi wa serikali za mitaa kidemokrasia zaidi.

Kongole kwako Rais Samia kwa kulinda demokrasia nchini kwa hali na Mali sasa wagombea waliokuwa mmeenguliwa mkutane katika kampeini tarehe 20/11/2024.
Kwa maana hiyo nchi imethibitika kabisa kuwa haiendeshwi kwa sheria tena, bali kwa utashi wa rais!!!
Kama watu wameenda kinyume na sheria,iweje warudishwe!!??

Hii imenipa wasiwasi mkubwa wa kuwa matendo ya wasimamizi wa uchaguzi ni maagizo kutoka juu,na sio kweli kuwa sheria, taratibu na kanuni zimetumika.
 
Watapojua democrasia Imekula watatafutana maana Nchi imedumaa baada ya kunyoma watu elimu ya uraia
 
Huu uchaguzi haupaswi kugharamiwa na serikali hata shilingi moja. Ni mambo madogo sana ambayo wananchi wenyewe kupitia watendaji kata/kijiji/ mtaa wangeratibu na kusimamia kuchaguana.
Tena hii unaitishisha mkutano mmoja tu hapi, kila mgombea anawepewa dk 15 za kujieleza nabkujibu maswali kisha uchaguzi na majibu yanatolewa.
 
Je sheria isifuate mambo yaende kiholela!

..hata utenguaji umefanyika kiholela.

..na sheria iliyopo ni ya kihuni ambayo imekataliwa na wadau.

..yanayoendelea ni jitihada za Mama Abduli kuiba uchaguzi ila makelele yamezidi.
 
View attachment 3150555Ni Samia Tena na Demokrasia, Aagiza Wagombea Walioenguliwa kwa Makosa Madogomadogo Majina yao Yarudishwe

Na Joseph Bulebe, Dar es salaam

Rais Samia Suhuhu Hassan ameendelea kuonesha ulimwengu na watanzania kwa ujumla kuwa demokrasia ndo kitu cha msingi katika uongozi wake unaofuata utawala bora na demokrasia.

Katika hali ambayo haikutegemewa na wagombea wote waliokuwa wameenguliwa kisheria na wasimamizi wa uchaguzi wa serikali za mitaa kwa makosa madogomadogo, Rais Samia ameamuagiza Waziri wa TAMISEMI, Mohammed Mchengelwa kuwarudisha wagombea wote walioenguliwa kwa makosa madogo madogo kama kukosea mwaka wa kuzaliwa, eneo analotoka, tarehe nk.

Akiongea leo na waadishi wa Habari, Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, Balozi Emmanuel Nchimbi amesema Rais Samia amemugiza kumwambia waziri wa TAMISEMI wagombea wenye makosa hayo warudishwe katika kinyanganyilo cha uchaguzi ili kulinda demokrasia changa inayokuwa katika nchi yetu.

Hii sio mara ya kwanza Mh Rais anaonesha ukomavu wa demokrasia nchini katika mambo ya siasa.

Mara tu baada ya kuingia madarakani Mh Rais aliruhusu mikutano ya siasa ya wazi iliyokuwa imekatazwa na mtangulizi wake.

Hakuishia hapo Mh Rais aliunda tume ambayo pamoja na mengine ilipendekeza kuundwa kwa tume huru ya uchaguzi ambayo tayari imeundwa, kuondoa pingamizi ya zuio ya mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa ambalo nalo limeondolewa.

Mh Rais katika kuonesha demokrasia zaidi aliwaondolea kesi mbalimbali wapinzani mahakamani kama vile Mwenyekiti wa CHADEMA na makamu wake pamoja na kuwarudisha nchini wapinzani wote waliokuwa wamekimbia nchi kipindi cha awamu ya tano.

Kama hiyo haitoshi Rais amewakaribisha Ikulu Wapinzani na kuongea nao na chini ya utawala wake wapinzani wanaalikwa karibia kila tukio la kitaifa na dhifa mbalimbali za kitaifa.

Huyu ndo Rais Samia, Mwanamama wa kwanza katika nchi ya Tanzania na ukanda wa Afrika Mashariki anayeipeleka nchi ya Tanzania katika kufanya uchaguzi wa serikali za mitaa kidemokrasia zaidi.

Kongole kwako Rais Samia kwa kulinda demokrasia nchini kwa hali na Mali sasa wagombea waliokuwa mmeenguliwa mkutane katika kampeini tarehe 20/11/2024.

..huu ni upumbavu.

..Waziri wa Tamisemi ni Rais Samia mwenyewe.

..Mchengerwa sio Waziri kamili, ni Waziri wa Nchi ofisi ya Raisi Tamisemi.
 

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeiomba Wizara ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), kuwaelekeza wasimamizi Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, kupuuza makosa madogo madogo yaliyotokea, ili kuruhusu wagombea wengi kushiriki uchaguzi huo.

Akizungumza na wahariri na waandishi waandamizi wa vyombo vya hahari nchini, Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, ametoa mfano wa makosa hayo yanayostahili kupuuzwa ni pamoja na wagombea kukosea herufi.

Kupitia mkutano huo uliofanyika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar es Salaam, leo Novemba 12, 2024, Balozi Nchimbi amesema ni vyema TAMISEMI ikaangalia uwezekano wa kuwarudisha wagombea wote walioenguliwa kutokana na makosa hayo madogo madogo ili kuhamasisha ukuaji wa demokrasia kwenye uchaguzi huo.

Aidha, kuhusu sehemu kubwa ya malalamiko mengi ya kuenguliwa kuonekana ni ya wagombea wa vyama vya upinzani, Balozi Nchimbi amewatoa shaka Watanzania kuwa, si kweli kwamba wagombea walioenguliwa ni wale wa vyama vya upinzani pekee, bali pia hata wagombea wa CCM wapo waliowekewa mapingamizi ya kugombea.

“Waziri wa TAMISEMI tunajua anafuata sheria, lakini ni muhimu kutambua demokrasia yetu hii bado ni changa hivyo tunahitaji muda wa kuendelea kujiífunza…tunaziomba mamlaka hasa TAMISEMI katika nyakati za mwisho za rufaa kuyapuuza makosa madogo madogo ili watu wengi wapate nafasi ya kugombea", alisema Dkt. Nchimbi.

#Ends
 
Sasa CHADEMA ata wagombea hawana ila wanataka kujitoa kutafuta huruma hii ni akili kubwa sana ya CCM
 
Tunatengeneza tatizo na tunatafuta credit kuliondoa.
Ikiwa sheria,kanuni na taratibu zinafuatwa yanini matamko na maelekezo?
Hii nchi........Mh.
 
hivyo nitumie nafasi hii kutoa wito kwa waziri mwenye dhamana ya serikali za mitaa, tunatambua umefuata sheria
Mstari huo (tunatambua waziri Mchengerwa unefuata sheria) una uvundo
 
Mimi napata tabu Sana, hv tume ya uchaguzi ni ccm? Yaan ishu za rufaa wanatangaza ccm, sababu za kukatwa zinademwa na ccm.
 
Back
Top Bottom