CCM tukiendelea kuwapuuza wananchi iko siku tutalia, 2025 sio mbali

CCM tukiendelea kuwapuuza wananchi iko siku tutalia, 2025 sio mbali

MAHANJU

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2014
Posts
5,252
Reaction score
8,003
Nataka niliseme hili na ninaomba tuweke kumbukumbu hii kwa rejea ya kesho muda ukifika.

Chama changu tulitaka kuungana pamoja na watanzania kuhusu suala la Tozo za kwenye simu baadaye tukaungana na serikali tikakaa kimya, mafuta yakapanda bei tupo kimya,vifaa vya ujenzi vipo juu tupo kimya, bei ya gesi ya kutumia majumbani ipo juu tumeganda kimya, sasa imekuja kodi Majengo ambayo ilikua ilikua ikilipwa na wamiliki moja kwa moja lakini serikali imeagiza kibao hicho kwa mpangaji ambaye ni mtu wa chini kabisa kupitia LUKU eti ukikatwa kodi hiyo nenda kaidai kwa mwenye nyumba(hii siyo sawa). Pamoja na ugumu wote huu wa maisha tunatumia mgongo wa uzalendo kuwaumiza wananchi wa hali ya chini tukidhani watesema kesho watasahsu.

Tukumbuke kua huu ndio uhalisia wa maisha ya sasa na tunawapa wapinzani agenda na sababu za kuongea, kama kweli wananchi wana maumivu makali sana juu ya haya wanatoyapitia tunawapa mwanya wa kuungana na wapinzani kuikataa CCM. Sasa wataungana nao kuidai katiba mpya wakiamini kua huenda ubovu wa katiba hii ndio chanzo cha maumivu yote haya. Tukae tukizipa masikio lakini iko siku utatokea msukumo mbaya toka kwa wananchi tutapoteana.

Chama changu CCM ki ashindwa kujitenga na serikali ispokua chenyewe ndio kimekua na kazi ya kuisemea na kuitetea serikali badala ya kuisimamia na kuishauri kutimiza ilani yake, matokeo yake mwishoni siyo mazuri na muda siyo mrefu tutazungumza.

Tutajivunia kuitumia serikali hiyo hiyo kulilinda chama lakini tunashindwa kuelewa kua wapinzani wetu nao wana akili timamu, tunashindwa kuelewa kua wananchi nao wanabadilisha na kua na uelewa mkubwa kupitia maumivu yanayopitia. Tusizibe masikio tusikilize maoni ya wananchi na siyo ya serikali tusiyapuuze.

Tunasikitika maamuzi ya viongozi wachache wasiokua na huruma wasiojua maumivu ya watu wa chini, mimi nikiwa kama mwanaccm siafiki kabisa hizo Tozo za simu na kodi za majengo tunalazimishwa kitu ambacho wananchi hawako tayari nacho, hii inagharama yake na tutalipa.
 
Nataka niliseme hili na ninaomba tuweke kumbukumbu hii kwa rejea ya kesho muda ukifika.

Chama changu tulitaka kuungana pamoja na watanzania kuhusu suala la Tozo za kwenye simu baadaye tukaungana na serikali tikakaa kimya, mafuta yakapanda bei tupo kimya,vifaa vya ujenzi vipo juu tupo kimya, bei ya gesi ya kutumia majumbani ipo juu tumeganda kimya, sasa imekuja kodi Majengo ambayo ilikua ilikua ikilipwa na wamiliki moja kwa moja lakini serikali imeagiza kibao hicho kwa mpangaji ambaye ni mtu wa chini kabisa kupitia LUKU eti ukikatwa kodi hiyo nenda kaidai kwa mwenye nyumba(hii siyo sawa). Pamoja na ugumu wote huu wa maisha tunatumia mgongo wa uzalendo kuwaumiza wananchi wa hali ya chini tukidhani watesema kesho watasahsu.

Tukumbuke kua huu ndio uhalisia wa maisha ya sasa na tunawapa wapinzani agenda na sababu za kuongea, kama kweli wananchi wana maumivu makali sana juu ya haya wanatoyapitia tunawapa mwanya wa kuungana na wapinzani kuikataa CCM. Sasa wataungana nao kuidai katiba mpya wakiamini kua huenda ubovu wa katiba hii ndio chanzo cha maumivu yote haya. Tukae tukizipa masikio lakini iko siku utatokea msukumo mbaya toka kwa wananchi tutapoteana.

Chama changu CCM ki ashindwa kujitenga na serikali ispokua chenyewe ndio kimekua na kazi ya kuisemea na kuitetea serikali badala ya kuisimamia na kuishauri kutimiza ilani yake, matokeo yake mwishoni siyo mazuri na muda siyo mrefu tutazungumza.

Tutajivunia kuitumia serikali hiyo hiyo kulilinda chama lakini tunashindwa kuelewa kua wapinzani wetu nao wana akili timamu, tunashindwa kuelewa kua wananchi nao wanabadilisha na kua na uelewa mkubwa kupitia maumivu yanayopitia. Tusizibe masikio tusikilize maoni ya wananchi na siyo ya serikali tusiyapuuze.

Tunasikitika maamuzi ya viongozi wachache wasiokua na huruma wasiojua maumivu ya watu wa chini, mimi nikiwa kama mwanaccm siafiki kabisa hizo Tozo za simu na kodi za majengo tunalazimishwa kitu ambacho wananchi hawako tayari nacho, hii inagharama yake na tutalipa.
Utalia wewe na gaidi wako,

USSR
 
Nyie watz na chadema hamna cha kuifanya ccm, tunaposema ccm itatawala milele mtuelewe tu, hizo tozo itafika Muda mtazizoea na sie haturudi nyuma make tunashida na hela.
 
Wataiba uchaguzi na wanajeshi wataingizwa mtani wafagie.
 
Nataka niliseme hili na ninaomba tuweke kumbukumbu hii kwa rejea ya kesho muda ukifika.

Chama changu tulitaka kuungana pamoja na watanzania kuhusu suala la Tozo za kwenye simu baadaye tukaungana na serikali tikakaa kimya, mafuta yakapanda bei tupo kimya,vifaa vya ujenzi vipo juu tupo kimya, bei ya gesi ya kutumia majumbani ipo juu tumeganda kimya, sasa imekuja kodi Majengo ambayo ilikua ilikua ikilipwa na wamiliki moja kwa moja lakini serikali imeagiza kibao hicho kwa mpangaji ambaye ni mtu wa chini kabisa kupitia LUKU eti ukikatwa kodi hiyo nenda kaidai kwa mwenye nyumba(hii siyo sawa). Pamoja na ugumu wote huu wa maisha tunatumia mgongo wa uzalendo kuwaumiza wananchi wa hali ya chini tukidhani watesema kesho watasahsu.

Tukumbuke kua huu ndio uhalisia wa maisha ya sasa na tunawapa wapinzani agenda na sababu za kuongea, kama kweli wananchi wana maumivu makali sana juu ya haya wanatoyapitia tunawapa mwanya wa kuungana na wapinzani kuikataa CCM. Sasa wataungana nao kuidai katiba mpya wakiamini kua huenda ubovu wa katiba hii ndio chanzo cha maumivu yote haya. Tukae tukizipa masikio lakini iko siku utatokea msukumo mbaya toka kwa wananchi tutapoteana.

Chama changu CCM ki ashindwa kujitenga na serikali ispokua chenyewe ndio kimekua na kazi ya kuisemea na kuitetea serikali badala ya kuisimamia na kuishauri kutimiza ilani yake, matokeo yake mwishoni siyo mazuri na muda siyo mrefu tutazungumza.

Tutajivunia kuitumia serikali hiyo hiyo kulilinda chama lakini tunashindwa kuelewa kua wapinzani wetu nao wana akili timamu, tunashindwa kuelewa kua wananchi nao wanabadilisha na kua na uelewa mkubwa kupitia maumivu yanayopitia. Tusizibe masikio tusikilize maoni ya wananchi na siyo ya serikali tusiyapuuze.

Tunasikitika maamuzi ya viongozi wachache wasiokua na huruma wasiojua maumivu ya watu wa chini, mimi nikiwa kama mwanaccm siafiki kabisa hizo Tozo za simu na kodi za majengo tunalazimishwa kitu ambacho wananchi hawako tayari nacho, hii inagharama yake na tutalipa.
Waendelee kuziba masikio,waendelezea uovu na manyanyaso,ili kuwaamsha walio lala,na kuirahisisha kazi yao
 
Tunasikitika maamuzi ya viongozi wachache wasiokua na huruma wasiojua maumivu ya watu wa chini, mimi nikiwa kama mwanaccm siafiki kabisa hizo Tozo za simu na kodi za majengo tunalazimishwa kitu ambacho wananchi hawako tayari nacho, hii inagharama yake na tutalipa.
Mwanzo nilipokusoma nilitaka kukataa kuwa wewe sio mwanaCCM, lakini baada ya kuwaza haya yanayokuliza hapa, nikajuwa kweli wewe ni mwanaCCM hasa, tena wale CCM ambao akili zao zimegota hata hawajui tena ni mambo yapi ya msingi hasa yanayowaumiza wananchi.

Wewe unalia na hizi tozo? Jambo dogo kabisa ambalo haliwezi kamwe kuwasumbua CCM inapokuja kwenye kuwahadaa wananchi?

WaTanzania sasa wameanza kuwa na uelewa wa mambo muhimu zaidi kuliko hizo tozo, na hapo ndipo ungeweka nguvu zako zote kuwalilia hao wenzako wanaofanya mambo mazito yasiyowapendeza waTanzania, ambayo kwako naona huyatambui.

WaTanzania sasa watakataa kuvunjiwa haki zao za msingi, kama kuharibu kura zao mnakokufanya wakati wa chaguzi mbalimbali.

WaTanzania sasa watakataa manayanyaso mengi mnayowafanyia, mkikiuka katiba na sheria zilizopo.

WaTanzania wanataka katiba mpya, kuondokana na 'umungu' anaopewa mwenyekiti wenu.

Haya ndiyo mambo yanayotakiwa yakulize, siyo hizo tozo ambazo inapofika wakati mnazitumia kununua mashati ya kijani na kuwagawia hao hao wananchi ili kuwasahaulisha maumivu mnayowasababishia wananchi hao.
 
Ni akili ndogo sana kujafili tozo za miamala kuliko kutafuta permanent solution ambayo ni Katiba mpya
Hii itaiondolea Serikali ya chama cha Mapinduzi kujiona wao ndio wao hakuna wa kuwafanya chochote
 
Mwenye kumbukumbu nzuri anikumbushe ni lini ccm iliwahi kuwaheshimu au hata kuwathamini wana inchi anikumbushe.
 
Ni akili ndogo sana kujafili tozo za miamala kuliko kutafuta permanent solution ambayo ni Katiba mpya
Hii itaiondolea Serikali ya chama cha Mapinduzi kujiona wao ndio wao hakuna wa kuwafanya chochote
Utakuta mtuu analalamaaa akisikia katiba mpya ghafla anasahau alichokua ana kilalamikia, naananza kupinga mchakato wa kuipata katiba mpya
 
Back
Top Bottom