CCM: Tumepokea kwa mstuko mkubwa taarifa za kifo cha Christina Kibiki aliyeuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiyojulikana

CCM: Tumepokea kwa mstuko mkubwa taarifa za kifo cha Christina Kibiki aliyeuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiyojulikana

Usipoziba ufa, utajenga ukuta.

Kuna mafisadi huko walioanzisha haya mambo kama propaganda chafu kipindi cha Magufuli, wenyewe watakuwa wanashangaa ‘narrative’ waliyoanzisha kumchafua mwenzao, sasa imegeuka mambo ya kweli.

Samia mwenyewe, mawaziri wake bungeni kila saa hatutaki kurudi kule tulikotoka na majizi anayoyalea yamechangia ku-promote hiyo nadharia.

Wamefungua chupa ya jini, katoka: kumdhihiti hawawezi.

Ujinga una madhara
 
CHAMA CHA MAPINDUZI
TAARIFA KWA UMMA
Dodoma, Tanzania


Chama cha Mapinduzi, kimepokea kwa mstuko mkubwa taarifa za kifo cha Katibu wa CCM Wilaya ya Kilolo Mkoa wa Iringa, Bi Christina Kibiki aliyeuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiyojulikana.

Marehemu alikuwa anajindaa kuhudhuria Semina elekezi kwa Makatibu Mjini Dodoma kesho.

Chama Cha Mapinduzi kinatoa pole kwa familia, ndugu, viongozi na wanachama wa CCM Mkoa wa Iringa kufuatia kifo cha ghafla na cha kikatili.

Tunawaomba wanachama wetu wawe watulivu wakati vyombo vya dola vikifuatilia na kuchunguza tukio hili, ili wahusika waweze kufikishwa katika vyombo vya kisheria.

CPA. Amos Gabriel Makalla
KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA CCM TAIFA,
ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO

13 Novemba,2024
Pia soma ~ Iringa: Katibu wa CCM Kilolo avamiwa na kuuawa na Watu wasiojulikana
Ingekuwa aliyeuawawa ni mpinzani, basi kuna wendawazimu wangekimbilia moja kwa moja kumhusisha marehemu na wivu wa mapenzi, kuchukuliana waume, nk!! Na huku wakiwa hawana uthibitisho wowote ule.

Ila kwa upande wangu nitafarijika sana kuona wahusika halisi wakitiwa mikononi mwa vyombo vya dola!
Na ikiwezekana waanze kwanza kuwatia nguvuni wale watekaji na wauaji wa yule kiongozi wa Chadema (Mzee Kibao) kabla ya wauaji wa huyu mama.
 
Mdude ndio huwa anaapa kuua watu, na juzi Mwanamapinduzi katishia kumuua Samia, labda Polisi waanzie hapo
Nape Nnauye na yule wa UVCCM Kagera na yule Mkuu wa Wilaya ya Longido pia wasaidie hapo
 
Usalama wa Taifa imeshindikana kabisa kudhibiti haya matukio?
Wako kwenye usalama wa chakula

 
  • Masikitiko
Reactions: Tsh
Back
Top Bottom