CCM watatoka madarakani kwa njia ya kura ni muhimu kujiandikisha na kupiga kura

Tatizo la wapinzani ni kutokupiga kura hili naliunga mkono ,kila mpinzani sifanyi huo ujinga wa kupiga kura nani apige sasa ?
 
Njia ni mbili tu,

1. Kama walivyofanya Senegal na mara kwa mara wanafanya kenya licha ya ukabila wao.WAUNGANISHE NGUVU WAWE WAMOJA.

2. WAWE NA MAWAZO MAPYA NA FIKRA MBADALA. waaminiane, wapendane na wawe na sera mbadala zenye kuwapa matumani na kushawishi wananchi wengi zaidi kuwaunga mkono. kulalamika, tamaa, uchu wa madaraka, kujipa umuhimu zaidi ya wengine kutawafanya daima upinzani kudhaifu daima na milele..

Maandamano ya upinzani ni useless eti kuitoa serikali ya kidemokrasia madarakani. Hiyo ni nonsense...

Na CCM wakiamua kuandamana je kupinga upinzani dhaifu wasilete fujo?

upinzan wamejisahau kana kwamba wanapigana na serikali sikivu ya kidemokrasia iliyopo madarakani...

nje ya serikali kuna chama, ambacho wanachama wake watawatazama tu...

siku walete fujo zao halafu na wanachama wa CCM wafyumu ndio utajua nchi hii hakuna upinzani kabisa 🐒
 
Make hapa kwanza ncheke.
 
Bado hamjasema hadi mseme. Ni muda mrefu tumekuwa tukisema ccm inashinda kwa kuchezea matokeo ya uchaguzi mnabisha. Hiki kinachoendelea cha watu kutojitokeza kwenye kujiandikisha, ni ujumbe tosha kuwa ccm haikubaliki. Magufuli ndio alikuja kuweka mwisho wa watu kuendelea kushiriki chaguzi za kihuni.

Mlikuwa mnadanganyana kuwa Magufuli anakubalika, tukasema anayekubalika hachezei uchaguzi mkashupaza shingo. Matokea yake akaishia kupika idadi ya wapiga kura ili apate idadi ya kura za hadaa kuonyesha anakubalika, na eti ccm imekuwa imara chini yake! Matokeo yake hata ule wizi watu waliokuwa wamekubaliana nao, sasa wamestuka kuwa hakuna uchaguzi, bali ni upuuzi kama upuuzi mwingine. Hiyo idadi ndogo unayoiona ndio huwa kura za ccm, lakini kwakuwa wapinzani huwa wanajitokeza, watu wanakuwa wengi na nyie ndio huziiba tokea hapo.

Ni hivi, ccm itatoka madarakani kwa njia yoyote ile, mlitakiwa mtoke kwa njia ya kura maana ni ya kistaarabu, mkawa hamko tayari, sasa subirini kutoka madarakani kwa aibu.
 
Nje ya mbeleko ya vyombo vya dola, ccm ni warembo. Chama cha wazee hakina ubavu huo.
 
Mara ya mwisho umepiga kura lini ?
Sijawahi kuacha kupiga kura zaidi ya chaguzi 4 sasa. Lakini enough is enough. Dhalimu magu alikuja kuweka mwisho wa kuendelea kushiriki chaguzi za hadaa. Jilaumuni kwa kumuachia mtu asiyejua siasa afanye atakavyo. Muda wa mabadiliko ni sasa, tena tuko nje ya muda.
 
Mimi huwa simlaumu Magu maana wapinzani walisusia bunge na masihala mengi akaona hakuna haja ya hawa Nyumbu kurudi bungeni
 
Tuko, ila hatuna silaha za kupambana na vyombo vyenye silaha. Tuachiwe ccm tuone chama kipi ni cha vijana, na kipi ni cha wazee.
wakati kujiandikisha kwenyewe hutaki🤣

kupiga kura ndio hutaki hata kuskia. kwanza una kitambulisho kweli hata cha mpiga kura tu?🤣

tafuta wenye mihemko wenzako ili kupambana nao.

CCM iko kazini ina dhamana muhimu ya kuwatumikia waTanzania, haiwezi kubabaika na mihemko yako ya kinyumbu 🐒
 
Hatari sana
 
Watanzania unaosema wajinga ni wewe mmojawapo unalalamika hapa
 
Tuko, ila hatuna silaha za kupambana na vyombo vyenye silaha. Tuachiwe ccm tuone chama kipi ni cha vijana, na kipi ni cha wazee.
Wewe nati hazipo sawa yaani vyombo vya Dola viache raia wapigane kisa vyama
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…