Sangizi
JF-Expert Member
- Nov 9, 2015
- 1,942
- 4,230
Hii nzuri sanaUkomo viti maalumu ni vizur uwekwe kwenye katiba moja kwa moja..
Kimsingi CCM na Upinzani wanakubaliana kwenye hilo
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hii nzuri sanaUkomo viti maalumu ni vizur uwekwe kwenye katiba moja kwa moja..
Kimsingi CCM na Upinzani wanakubaliana kwenye hilo
Ni lini na wapi CCM waliwahi kukubali hili la ukomo wa viti maalumu ndugu!!?Ukomo viti maalumu ni vizur uwekwe kwenye katiba moja kwa moja..
Kimsingi CCM na Upinzani wanakubaliana kwenye hilo
Uchaguzi wa Chadema uliuona lakini? Na wa CCM je?Subiria ya Dikteta Uchwara wa Laigwanan tundu lissu.
Soma page 2Ni lini na wapi CCM waliwahi kukubali hili la ukomo wa viti maalumu ndugu!!?
Akhsante, ni page 3.Soma page 2
Wanavyuo na neto wapate wawakirishi a.s.a.pWakuu,
Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa, imefanya kikao chake maalum jana tarehe 10 Machi, 2025 jijini Dodoma chini ya Mwenyekiti wake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan. Katika kikao hicho, Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa imepokea na kujadili agenda kuu mbili kama zifuatazo:-
(i). Mapendekezo ya Marekebisho ya Kanuni za Uteuzi wa Wagombea Uongozi katika Vyombo vya Dola toleo la 2022 na
(ii). Rasimu ya Ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu wa 2025-2030
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Kuhusu Mapendekezo ya Marekebisho ya Kanuni za Uteuzi wa Wagombea Uongozi katika Vyombo vya Dola, Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa imeridhia mapendekezo ya marekebisho ya Kanuni hizo. Maeneo yaliyofanyiwa marekebisho ni kama ifuatavyo:-
1. Mchakato wa uchujaji na uteuzi wa wagombea wa nafasi za ubunge, uwakilishi wa majimbo na udiwani wa kata/wadi.
2. Mchakato wa uchujaji na uteuzi wa wagombea wa nafasi za ubunge, uwakilishi na udiwani wa viti maalum wanawake.
3. Upanuzi wa wigo wa idadi ya wajumbe wa vikao vya chama na jumuiya zake watakaopiga kura za maoni. Lengo la hatua hii ni kuimarisha misingi ya demokrasia, uwazi na kupanua uwakilishi wa wanachama wa CCM katika kuwapata wagombea wa nafasi za uongozi katika chaguzi za vyombo vya dola. Utaratibu utakuwa kama ifuatavyo:-
(a) Kwa upande wa wabunge wa Jumuiya ya Wanawake (UWT) ngazi ya mikoa, kwa upande wa Tanzania Bara
Mkutano Mkuu Maalumu wa UWT wa Mkoa, ambao utakuwa na wajumbe wafuatao :-
(i) Wajumbe wote wa Mkutano Mkuu wa UWT wa Mkoa (Kama ilivyoainishwa kwenye Kanuni za UWT).
(ii) Wajumbe wote wa Kamati za Utekelezaji wa UWT za Wilaya.
(iii) Wajumbe wote wa Kamati za Utekelezaji wa UWT za Kata.
Kwa upande wa Zanzibar Mkutano Mkuu Maalumu wa UWT wa
Mkoa, utakuwa na wajumbe wafuatao :-
(i) Wajumbe wote wa Mkutano Mkuu wa UWT wa Mkoa.
(ii) Wajumbe wa Kamati za Utekelezaji za Wilaya.
(iii) Wajumbe wa Kamati za Utekelezaji za Jimbo.
(iv) Wajumbe wa Kamati za Utekelezaji za Kata/Wadi.
(v) Wajumbe wa Kamati za Utekelezaji za Matawi.
(b) Kwa upande wa Jumuiya ya UVCCM na WAZAZI
Kura za maoni kwa waombaji nafasi za Ubunge/Uwakilishi wa viti maalumu wanawake kupitia Jumuiya ya UVCCM na WAZAZI zitapigwa na wajumbe wa Mikutano Mikuu Maalumu ya Taifa, kwa utaratibu ufuatao:-
Mikutano Mikuu ya Taifa ya UVCCM/WAZAZI itakua na wajumbe Wanawake tu; wajumbe hao ni kama wafuatao
(i) Wajumbe wote wanawake wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa UVCCM/WAZAZI.
(ii) Wajumbe wote Wanawake wa Kamati za Utekelezaji za UVCCM/WAZAZI za Mikoa.
(iii) Wajumbe wote Wanawake wa Kamati za Utekelezai za Wilaya UVCCM/Wazazi.
Ukomo wa viti maalum
Kuweka ukomo wa vipindi viwili vya miaka mitano kwa nafasi za ubunge/uwakilishi na udiwani wa viti maalum wanawake. Ukomo huo utaanza kutumika katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2030.
Vilevile, Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa imepitisha Kauli Mbiu rasmi kwa ajili ya kampeni za Uchaguzi Mkuu wa 2025 isemayo;
"KAZI NA UTU, TUNASONGA MBELE"
Kauli mbiu hiyo inaakisi dhamira ya Chama ya kuendeleza juhudi za ujenzi wa Taifa lenye maendeleo jumuishi, mshikamano wa kitaifa na ustawi wa watu wenye kujali UTU.
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
Issa Haji Ussi (GAVU)
KATIBU WA NEC ORGANAIZESHENI
11 Machi, 2025
Kwa kuwa jambo hilo linatakiwa liingie kwenye Katiba ya chama,kwa Sasa yanabaki kama mapendekezo ya Halmashauri Kuu kwenda kwenye Mkutano Mkuu.Wakuu,
Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa, imefanya kikao chake maalum jana tarehe 10 Machi, 2025 jijini Dodoma chini ya Mwenyekiti wake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan. Katika kikao hicho, Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa imepokea na kujadili agenda kuu mbili kama zifuatazo:-
(i). Mapendekezo ya Marekebisho ya Kanuni za Uteuzi wa Wagombea Uongozi katika Vyombo vya Dola toleo la 2022 na
(ii). Rasimu ya Ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu wa 2025-2030
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Kuhusu Mapendekezo ya Marekebisho ya Kanuni za Uteuzi wa Wagombea Uongozi katika Vyombo vya Dola, Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa imeridhia mapendekezo ya marekebisho ya Kanuni hizo. Maeneo yaliyofanyiwa marekebisho ni kama ifuatavyo:-
1. Mchakato wa uchujaji na uteuzi wa wagombea wa nafasi za ubunge, uwakilishi wa majimbo na udiwani wa kata/wadi.
2. Mchakato wa uchujaji na uteuzi wa wagombea wa nafasi za ubunge, uwakilishi na udiwani wa viti maalum wanawake.
3. Upanuzi wa wigo wa idadi ya wajumbe wa vikao vya chama na jumuiya zake watakaopiga kura za maoni. Lengo la hatua hii ni kuimarisha misingi ya demokrasia, uwazi na kupanua uwakilishi wa wanachama wa CCM katika kuwapata wagombea wa nafasi za uongozi katika chaguzi za vyombo vya dola. Utaratibu utakuwa kama ifuatavyo:-
(a) Kwa upande wa wabunge wa Jumuiya ya Wanawake (UWT) ngazi ya mikoa, kwa upande wa Tanzania Bara
Mkutano Mkuu Maalumu wa UWT wa Mkoa, ambao utakuwa na wajumbe wafuatao :-
(i) Wajumbe wote wa Mkutano Mkuu wa UWT wa Mkoa (Kama ilivyoainishwa kwenye Kanuni za UWT).
(ii) Wajumbe wote wa Kamati za Utekelezaji wa UWT za Wilaya.
(iii) Wajumbe wote wa Kamati za Utekelezaji wa UWT za Kata.
Kwa upande wa Zanzibar Mkutano Mkuu Maalumu wa UWT wa
Mkoa, utakuwa na wajumbe wafuatao :-
(i) Wajumbe wote wa Mkutano Mkuu wa UWT wa Mkoa.
(ii) Wajumbe wa Kamati za Utekelezaji za Wilaya.
(iii) Wajumbe wa Kamati za Utekelezaji za Jimbo.
(iv) Wajumbe wa Kamati za Utekelezaji za Kata/Wadi.
(v) Wajumbe wa Kamati za Utekelezaji za Matawi.
(b) Kwa upande wa Jumuiya ya UVCCM na WAZAZI
Kura za maoni kwa waombaji nafasi za Ubunge/Uwakilishi wa viti maalumu wanawake kupitia Jumuiya ya UVCCM na WAZAZI zitapigwa na wajumbe wa Mikutano Mikuu Maalumu ya Taifa, kwa utaratibu ufuatao:-
Mikutano Mikuu ya Taifa ya UVCCM/WAZAZI itakua na wajumbe Wanawake tu; wajumbe hao ni kama wafuatao
(i) Wajumbe wote wanawake wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa UVCCM/WAZAZI.
(ii) Wajumbe wote Wanawake wa Kamati za Utekelezaji za UVCCM/WAZAZI za Mikoa.
(iii) Wajumbe wote Wanawake wa Kamati za Utekelezai za Wilaya UVCCM/Wazazi.
Ukomo wa viti maalum
Kuweka ukomo wa vipindi viwili vya miaka mitano kwa nafasi za ubunge/uwakilishi na udiwani wa viti maalum wanawake. Ukomo huo utaanza kutumika katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2030.
Vilevile, Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa imepitisha Kauli Mbiu rasmi kwa ajili ya kampeni za Uchaguzi Mkuu wa 2025 isemayo;
"KAZI NA UTU, TUNASONGA MBELE"
Kauli mbiu hiyo inaakisi dhamira ya Chama ya kuendeleza juhudi za ujenzi wa Taifa lenye maendeleo jumuishi, mshikamano wa kitaifa na ustawi wa watu wenye kujali UTU.
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
Issa Haji Ussi (GAVU)
KATIBU WA NEC ORGANAIZESHENI
11 Machi, 2025
Utueleweshe wakati ccm ni chama cha kidhalimu kwa vitendo?Omba kueleweshwa kwanza sio kupayuka
Mnashindana na nani wakati refa, mshika kibendera, kamisaa wote ni wenu? Chama la majizi bana.Kudumu Chama Cha Mapinduzi
Tunakwenda na wakati
Dalili za ushindi wa kishindo
Joyce Mukya hatakubaliana na mambo ya ukomo.Ukomo viti maalumu ni vizur uwekwe kwenye katiba moja kwa moja..
Kimsingi CCM na Upinzani wanakubaliana kwenye hilo
Chadema kuna nini cha kujifunza ? Katiba yenu haina ukomo wa cheo cha mwenyekiti wala wajumbe nyie.mnaongea mawazo tu msiyoyafanyia kaziNi wazo la chadema wamesoma upepo.Unajua kwa nini wanaogopa chadema wakiambiwa hawana akili utumia wasiojulikana na mwisho ujiona akili zimekosekana wanaamua kufata ya chadema ili wasishitukiwe.