Pre GE2025 CCM waweka ukomo nafasi za ubunge na udiwani viti maalum, waja na kauli mbiu mpya

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ingekuwa jambo la maana kama wangeweka ukomo wa utawala wao kama wangeshindwa kihalali na upinzani..Haya mengine ni mbwwmbwe tu!
 
Kuweka ukomo wa vipindi viwili vya miaka mitano kwa nafasi za ubunge/uwakilishi na udiwani wa viti maalum wanawake. Ukomo huo utaanza kutumika katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2030.

Hii kauli ni hatari,na Haina ukweli na ikianza kutumika,Kuna uwezekano waliokuwa wabunge awali kuchukua Tena fomu kugombea, ili waweze kuanza mfumo huo mpya! CCM hapana😳
 
Hii CCM ya miaka hii, sijui iko wapi tu, mtaani huku husikii watu wakiiongelea kwa madaha au kuipigania, kimekua chama cha vikao vya ndani ndani huko na wanachama wao wakiishi kwa usiri, mtu ana kadi lkn hata mkewe hajawahi itia machoni.Wanaovaa nguo za kijani kwa kujiachia mtaani unakuta ni wale waliojichokea wanavaa sababu walipewa na hawana mavazi ya kutosha.
CCM isome alama za nyakati - hata uwe mzuri vipi watu watakuchoka, ndo hulka ya ubinadamu hiyo--
 
RUBBISH. Ukomo wa mahovyo hovyo yote umewekwa kwenye RASIMU ya Warioba, ambayo CCM na serikali yake WANAPIGA CHENGA kuipitisha iwe KATIBA MPYA.
 
Maoni ya wananchi yangeheshimiwa wabunge wote wawe na ukomo katika ubunge,alafu mawaziri wasitokane katika wabunge bali professional itafanya uwajibikaji na kuondoa hii stereotype ya watu flani kujiona kwamba wao ndio wana title deed ya kushika nafasi flani wizarani
 
Ukomo viti maalumu ni vizur uwekwe kwenye katiba moja kwa moja..

Kimsingi CCM na Upinzani wanakubaliana kwenye hilo
Ccm imeonyesha njia hivyo hadi 2030 itakuwa kwenye katiba mambo mdogo mdogo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…