CDF Mstaafu Mabeyo ametaka kufikisha ujumbe. Je, wananchi tumeuelewa ujumbe?

CDF Mstaafu Mabeyo ametaka kufikisha ujumbe. Je, wananchi tumeuelewa ujumbe?

Ni miaka 3 imepita tangu Rais Magufuli afariki. Ni jambo la kawaida, hasa siku ya maziko au wakati wa kutangaza kifo, kutolewa taarifa za kina za mazingira ya kifo cha marehemu, na kama pengine marehemu alitoa kauli yoyote. Haikuwa hivyo kwa Hayati Magufuli.

Wengi walipenda na walikuwa na shauku, msiba tu ulipotokea, wafahamu kwa kina aliugua lini, alifikishwa hospitali lini, jitihada zilizofanywa katika harakati za kuokoa uhai wa marehemu, mpaka kushindikana, na hatimaye kuyapokea mapenzi ya Mungu. Kukosekana kwa taarifa hizo, kumesababisha maneno mengi, ya kweli na yasiyo ya kweli.

Miaka 3 baadaye, baadhi ya taarifa za kina zimetolewa na CDF. Siamini kama taarifa hizi zimetolewa tu ili kujifurahisha, bali kuna ujumbe umetumwa kwa wananchi.

UJUMBE MUHIMU
Kuna shida kwenye katiba ya nchi. Kuna vitu havijawa sawa na kwa uwazi. Kwa maelezo ya CDF, ni kwamba ni yeye CDF ndiye aliyetoa msisitizo wa kuwa ni Makamu wa Rais ndiye anatakiwa kuwa Rais, na siyo mwingine yeyote. Tena ameeleza kuwa ni yeye CDF ndiye aliyeelekeza kuwa inabidi makamu wa Rais aapishwe kabla ya maziko ya Rais maana bila hivyo jeshi haliwezi kumtambua kama ndiye Amiri Jeshi Mkuu.

Lakini pia Rais mstaafu Kikwete, wakati Ndugai alipoondolewa kwenye nafasi ya uspika, alieleza kuwa Rais alipofatiki, spika alimwendea na kumwambia kuwa kwa mujibu wa katiba, yeye spika ndiye anatakiwa kuwa Rais. Yeye Kikwete alimkatalia.

Lakini pia zipo habari ambazo hazijawekwa wazi, huenda zikawekwa wazi siku za mbeleni, kuwa wale waliokuwa wakipinga Makamu kuchukua nafasi ya Urais baada ya kifo cha Rais, walieleza kuwa katiba inasema kuwa Rais akitoka bara, makamu atatoka visiwani. Na kwa vile aliyefariki alikuwa anatoka bara, urais ulikuwa nafasi ya bara, nafasi ya visiwani ilikuwa ni umakamu, hivyo makamu aendelee kuwa makamu.

HATARI ILIYOPO
Tusistegemee nyakati zote tutakuwa na CDF wa aina ya Mabeyo. **** siku tutakuja kuwa na CDF mwoga wa kutoa maamuzi na wanadiasa wakatii, au tukawa na CDF mwenye tamaa ya madaraka, anaweza kutumia nafasi ya kukosekana maelewano miongoni mwa wanasiasa, akayanyakua madaraka yeye CDF.

HITIMISHO
Tumepewa ujumbe ambao ni angalizo, kuwa tunatakiwa kuiweka sawa katiba ili kila jambo liwe wazi kwenye katiba, na katiba izibe mianya yote ya tafsiri zisizokusudiwa.

Mapungufu yetu ya katiba hayapo tu pale ambapo Rais atafariki akiwa madarakani, yapo maeneo mengi. Tangu enzi za Tume ya Jaji Nyalali, mapungufu ya katiba yamekuwa yakiainishwa, lakini wafanya maamuzi wamekuwa magumegume, wanafanya mabadiliko madogo madogo kwenye maeneo yale tu wanayoona yanawahakikishia kubakia madarakani hata bila ya matakwa ya umma.

Hata Samia ambaye nusura asiwe Rais kwa sababu ya sintofahamu za katiba, baada ya kuipata Urais, hataki katiba mpya kwa vile anaona iliyopo inamhakikisha mamlaka ya kuwa hata dikteta akitaka, bila ya kubughudhiwa. Amesahau kuwa bila ya hekima ya CDF huenda asingekuwa Rais. Manufaa yake binafsi yamefifisha hekima yake katika kuyaangalia maslahi ya Taifa.

Ni lini tutampata Rais mzalendo anayelitazama zaidi Taifa kuliko madaraka yake binafsi na manufaa ya chama chake? Kuwa na hawa viongozi wanaojali zaidi madaraka kuliko madlahi ya Taifa, kuna siku nchi itakwenda kwa namna isiyotarajiwa. Pongezi kwa CDF kwa kujali maslahi ya Taifa.
Mbona katiba iko wazi sana juu ya nani atakua rais kama rais wa madarakani atafariki?? Ni wewe ndio huelewi labda.
 
Kuna mshua mmoja namuheshimu sana aliongoza taasisi ambayo ina historia ya kutoa wabunge, yani si viongozi wakuu tuu, mpaka wale waliowafuatia wakurugenzi walikuwa wakistaafu wanagombea ubunge na kupata.

Sasa, yule mshua alivyostaafu, na yeye akaambiwa, kwa rekodi yako ya utumishi, na nondo unazotoaga kila siku, utafaa sana kugombea ubunge.

Yule mshua mtu fulani wa dini sana, unajua ile kibongobongo maadili maana yake ni dini. Akasema ataliweka hilo suala kwenye maombi na kupata baraka za Mungu kama hilo ni jambo linalofaa au lisilofaa. Kwangu mimi "Komredi" nachukulia hiyo kama ilikuwa namna yake ya kutafakari kwa kina na ku meditate kuhusu uamuzi huo mkubwa.

Baada ya muda fulani, yule mshua alikuja kujibu kwamba hataweza kugombea ubunge. Sababu alizotoa ni kwamba, ile process ya kugombea ubunge imejaa mambo ambayo yanapingana na principles zake za maisha.

1. Kugombea ubunge kulikuwa kama biashara fulani ya gharama kubwa, kulihitaji pesa nyingi sana. Pesa hizi, mtumishi wa umma ambaye alifanya kazi kwa uadilifu ni vigumu sana kuwa nazo, labda atumie kiinua mgongo chake chote. Na akifanya hivyo itakuwa kama anawekeza katika biashara, atalipwa vipi?

Kulikuwa na option ya kupata wafadhili, wafanyabiashara wakubwa, wampe hizo hela. Lakini, yeye maisha yake yote alikataa kuchukua pesa za wafanyabiashara wakubwa, kuna kipindi Muhindi mmoja alikuwa tayari kumsomesha mtoto wake Ulaya au Marekani, akakataa, akisema kuwa ukichukua fadhila hizi, kuna siku moja waliokupa fadhila nao watadai uwalipe kwa kuwafanyia mambo yao wanayoyataka. Hivyo, aliona matatizo mengi sana kwenye chaguzi zinazotawaliwa na fedha na rushwa.

2. Aliona kugombea ubunge kunahusisha siasa nyingi za majitaka, siasa za udini makanisani. Hakutaka kufanya siasa hizo.

3. Aliona kugombea ubunge kunahusisha sana siasa za kudanganya wananchi kwa ahadi zisizotekelezeka, zinahusisha kujipanga kwenye kauli na miongozo ya chama ambayo haitekelezeki na wala haina uhalisia.

Aliona sababu nyingi zinazo compromise principles zake za morality. Akaamua asigombee ubunge.

Na mtu kama huyo angegombea ubunge, pengine angepata nafasi ya kuwa Waziri na Rais.

Na mtu kama huyo, ndiye anayefaa kuwa waziri na rais.

Lakini, hizo sifa zake nzuri ambazo zinamfanya afae kuwa mbunge, waziri na rais, ndizo hizo hizo zilizomzuia kuwa hata mbunge.

Ndiyo maana nasema ngoma yetu ngumu, watu wenye sifa zinazofaa hawawezi kupanda ngazi ya uongozi, kwa sababu hawatakiwi huku juu na sifa zao haziwaruhusu kupanda ngazi ya uongozi wa kisiasa. Watu wasio na sifa, wale ruthless wanaotaka uongozi at any cost, kw auongo, kwa wizi, kwa rushwa, ndio wanaopata uongozi.

Sasa tunategemea rais aliyeanza kujifunza rushwa tangu akiwa kiongozi wa serikali ya wanafunzi chuoni, aka graduate na kupata shahada ya pili ya rushwa akigombea ubunge, akapata Ph.D ya rushwa kwenye uwaziri, akaenda kuwa mkuu wa chuo cha rushwa kwenye urais, aongoze vita dhidi ya rushwa?
Hatari sana mkuu, hiyo ngazi ni ngumu kuipanda kama unapenda haki.


Makando kando ni mengi , mtu anatafuta wadhamini kwa makubaliano ukipata inabidi na mimi uje unipe kitu (katika jimbo either kupitisha biashara ya magendo/kukwepa kodi nk nk) .wengine hufikia kuua wapinzani wao hasa akimuona ni mwiba kihoja kwake
 
Mbona katiba iko wazi sana juu ya nani atakua rais kama rais wa madarakani atafariki?? Ni wewe ndio huelewi labda.
Shida sio kuelewa yeye , inaeleweka shida ilikuwa kwenye kuifuata ndio maana CDF akasema kulitokea mvutano inawezekana watu waliisahau katiba. Sio walisahau hapo kaongea Kiutu uzima
 
Hatari sana mkuu, hiyo ngazi ni ngumu kuipanda kama unapenda haki.


Makando kando ni mengi , mtu anatafuta wadhamini kwa makubaliano ukipata inabidi na mimi uje unipe kitu (katika jimbo either kupitisha biashara ya magendo/kukwepa kodi nk nk) .wengine hufikia kuua wapinzani wao hasa akimuona ni mwiba kihoja kwake
Hiyo ndiyo "paradox of political pugilism".

Ni kama vile ili upiganie principles unazozisimamia, inakulazimu uzivunje hizo principles unazozipigania.

N aukizivunja tu, watu wanachukua faili lako na kulihifadhi, ukifika juu siku moja na kuwasaliti wanawaga mchele wote kwenye kuku wengi.

Matokeo yake, hata wale wanaoanza kwa kusema watavunja principles ili wapande juu wazitetee principles, wakifika juu wanaishia kuwa mateka wa system.
 
Na ile ngazi ni kama imeshikiliwa na wachache ambao wanataka apite ambaye anawafaa wao. Asiyetaka longo longo ambaye sisi wananchi tunamtaka hafiki kwa ile ngazi
Iko vile bandugu !
 
Hiyo ndiyo "paradox of political pugilism".

Ni kama vile ili upiganie principles unazozisimamia, inakulazimu uzivunje hizo principles unazozipigania.

N aukizivunja tu, watu wanachukua faili lako na kulihifadhi, ukifika juu siku moja na kuwasaliti wanawaga mchele wote kwenye kuku wengi.

Matokeo yake, hata wale wanaoanza kwa kusema watavunja principles ili wapande juu wazitetee principles, wakifika juu wanaishia kuwa mateka wa system.
So sad 😞
 
Mbona katiba iko wazi sana juu ya nani atakua rais kama rais wa madarakani atafariki?? Ni wewe ndio huelewi labda.
Iko wazi kimaandishi lakini in reality it’s different !
Ndio maana wale waliotaka kupindua meza wanajua hivyo na wakataka kufanya yao !
 
Hii ilikuwa wazi kabisa tangu anajiuzulu, zile sababu zilikuwa geresha tu.

Sababu halisi ni kwamba kulikuwa na timbwili kubwa tangu enzi za Magufuli. Yale mambo ya "Siongei na mbwa, naongea na mwenye mbwa".

Na ile move ya kuutaka urais kinyume na katiba ndiyo iliyomaliza kila kitu. Ni vigumu sana kuwa na Spika na Rais wana beef Tanzania. Hususan kama beef lenyewe linahusisha issue ya Spika kutaka kumputa Rais urais. Rais atakuwa muda wote anajiona anawekewa mitego tu na Spika.Mwishowe Spika akakubali matokeo tu.

Sasa mara paap, mbwa kageuka mwenye mbwa.

Lazima uwe mdogo tu.
Kelele zote zile za kusema nchi itapigwa mnada alikuwa anajua fika kifuatacho.

Kumtegemea binadam ni risk sana kwa haya maisha yetu ya leo yupo anaekupa jeuri lakini kesho hayupo, lazima ushuke tu taka usitake.
 
Kelele zote zile za kusema nchi itapigwa mnada alikuwa anajua fika kifuatacho.

Kumtegemea binadam ni risk sana kwa haya maisha yetu ya leo yupo anaekupa jeuri lakini kesho hayupo, lazima ushuke tu taka usitake.
Naam.

Halafu jitahidi sana usimdharau mtu kwa kuwa huyu mdogo, huyu hana cheo, huyu mbwa tu si mwenye mbwa, huyu mwanamke.

Maisha yanabadilika sana na juu panakuwa chini wakati chini panakuwa juu.

Sasa Ndugai ubabe wote ule kwa sababu ya kujua Magufuli yupo umekwisha.
 
Naam.

Halafu jitahidi sana usimdharau mtu kwa kuwa huyu mdogo, huyu hana cheo, huyu mbwa tu si mwenye mbwa, huyu mwanamke.

Maisha yanabadilika sana na juu panakuwa chini wakati chini panakuwa juu.

Sasa Ndugai ubabe wote ule kwa sababu ya kujua Magufuli yupo umekwisha.
Hakika mkuu, tatizo madaraka yanawalevya baadhi ya viongozi wetu na kuona washayamaliza maisha kumbe bado safari ni ndefu.

Huwa nasema usimdharau mtu yeyote yule, kushindwa na maanguko mengine ni ya kujitakia.
 
Naam.

Halafu jitahidi sana usimdharau mtu kwa kuwa huyu mdogo, huyu hana cheo, huyu mbwa tu si mwenye mbwa, huyu mwanamke.

Maisha yanabadilika sana na juu panakuwa chini wakati chini panakuwa juu.

Sasa Ndugai ubabe wote ule kwa sababu ya kujua Magufuli yupo umekwisha.
Aibu ikamtengua kabla ya kutenguliwa saivi kimyaa asee dharau na kiburi mafikio yake mabaya
 
Back
Top Bottom