CEO wa mtandao wa Telegram, Pavel Durov akamatwa katika uwanja wa ndege nchini Ufaransa

CEO wa mtandao wa Telegram, Pavel Durov akamatwa katika uwanja wa ndege nchini Ufaransa

Ni tajiri wa 121 duniani
Alipewa uraia wa Ufaransa baada ya kwenda kuishi kisiwa kidogo huko Caribbean
Ila mtandao wake una mambo mengi sana na hakuyadhibiti
Alijua anatafutwa na serikali ya france ila kajipeleka
Atakula mvua za kutosha akicheza
30 years labda daa dunia hii
Jamaa ana utajiri wa $15.5b naona zitapungua sana kwenye kesi hii
 
Hujui kitu. West ndo wanataka sasa afungue waone baadhi ya data zilizoibiwa Israel na Wana suspect mtandao uliotumika ni Telegram.
Hamna kitu unajua. Alianzisha VKontakte ambayo ni kama Facebook ya Russia, ikawa maarufu kuliko Facebook ila raia wakawa huru nayo hadi kwenye maandamano ikatumika ndipo usalama wakataka credentials za users akakataa. Serikali ikalazimisha takeover ikanunua hisa na kuleta masharti yake kwenye mtandao. Akaachana na VKontakte.

Akaanzisha Telegram akasumbuliwa na kutoroka Urusi. Sasa mtu aliomba uraia wa Ufaransa akapewa alafu useme eti West ndio wanamtafuta. Kwahiyo wewe unajua usalama wake kuliko yeye mwenyewe.
Mtu awe wanted kisha anaenda na private jet kwenye airport mji mkuu??

Telegram imefunguliwa kesi kama ambavyo Zuckeberg akisimama kwenye Congress, Apple ilivyopelekwa mahakama na Umoja wa Ulaya, Facebook vilevile ilikuwa na kesi Ulaya, Apple ilikuwa na kesi Urusi. Hamna ajabu hapo.
 
Hamna kitu unajua. Alianzisha VKontakte ambayo ni kama Facebook ya Russia, ikawa maarufu kuliko Facebook ila raia wakawa huru nayo hadi kwenye maandamano ikatumika ndipo usalama wakataka credentials za users akakataa. Serikali ikalazimisha takeover ikanunua hisa na kuleta masharti yake kwenye mtandao. Akaachana na VKontakte.

Akaanzisha Telegram akasumbuliwa na kutoroka Urusi. Sasa mtu aliomba uraia wa Ufaransa akapewa alafu useme eti West ndio wanamtafuta. Kwahiyo wewe unajua usalama wake kuliko yeye mwenyewe.
Mtu awe wanted kisha anaenda na private jet kwenye airport mji mkuu??

Telegram imefunguliwa kesi kama ambavyo Zuckeberg akisimama kwenye Congress, Apple ilivyopelekwa mahakama na Umoja wa Ulaya, Facebook vilevile ilikuwa na kesi Ulaya, Apple ilikuwa na kesi Urusi. Hamna ajabu hapo.
Wewe ndio hujui . Nchi za ulaya wanataka access ya mtandao na jamaa amegoma. Tusubiri tutaona
 
Wewe ndio hujui . Nchi za ulaya wanataka access ya mtandao na jamaa amegoma. Tusubiri tutaona
Sio atoe access. Awe na regulations kwenye mtandao wake mbona simple kabisa. Kuna kipindi TikTok ililalamikiwa kutuma maudhui mara ya mtu amejinyonga, mara ajari. Tiktok wakarekebisha sasa Telegram nao wana mambo ya kawaida ya kurekebisha.
 
Sio atoe access. Awe na regulations kwenye mtandao wake mbona simple kabisa. Kuna kipindi TikTok ililalamikiwa kutuma maudhui mara ya mtu amejinyonga, mara ajari. Tiktok wakarekebisha sasa Telegram nao wana mambo ya kawaida ya kurekebisha.
Hao wengine mkuu wangu walifunguliwa mashtaka lakini hawakukamatwa. Hata Musk anatishiwa kukamatwa na France&Uk juu ya mtandao wake wa X.

Au Kuna siku Mark, alikamatwa juu ya Facebook, insta, whats?.
 
Sio atoe access. Awe na regulations kwenye mtandao wake mbona simple kabisa. Kuna kipindi TikTok ililalamikiwa kutuma maudhui mara ya mtu amejinyonga, mara ajari. Tiktok wakarekebisha sasa Telegram nao wana mambo ya kawaida ya kurekebisha.
Hapo ni kuingilia privacy za watumiaji huwezi kuwapa access.
 
Hao wengine mkuu wangu walifunguliwa mashtaka lakini hawakukamatwa. Hata Musk anatishiwa kukamatwa na France&Uk juu ya mtandao wake wa X.

Au Kuna siku Mark, alikamatwa juu ya Facebook, insta, whats?.
Mark akamatwe kwa makosa yapi? Ni maudhui gani ya Meta yanamfanya Mark ashtakiwe. Meta inafanya regulation kali hata watumiaji wanatoa taarifa zinafanyiwa kazi.

Naweza ingia Telegram chap hapa nikakuletea video za child abuse na molestation kwa searchwords tu, unaweza fanya hivyo kwa Instagram, Facebook, Threads au WhatsApp group?
 
Mark akamatwe kwa makosa yapi? Ni maudhui gani ya Meta yanamfanya Mark ashtakiwe. Meta inafanya regulation kali hata watumiaji wanatoa taarifa zinafanyiwa kazi.

Naweza ingia Telegram chap hapa nikakuletea video za child abuse na molestation kwa searchwords tu, unaweza fanya hivyo kwa Instagram, Facebook, Threads au WhatsApp group?
Na ndicho nachosema ilitakiwa afunguliwe mashtaka na sio kukamatwa.

Sasa kama wanamkamata uhuru wa habari wanaosema Russia anaukandamiza ni upi?. Na vipi makundi ya magaidi yanayonunua magari ya Toyota nakuyatumia kwenye mishe zao haramu mbona mmiliki au wamiliki wa Toyota hawakamatwi kwa Ku Facilitate harakati za magaidi?. Kama Telegram inavyo facilitate shughuri haramu?.

Na kwa nini huko UK&France wanakamata watu wanaopost kukosoa utendaji wa Police mitandaoni?.

Kwa nini wanatishia kumkamata Musk au kufungia X huko west .

Uhuru wa habari upo wapi ambao wao ndio wahubiri wakuu wa free speech?.

Censorship ya habari ndio inayowasumbua nasio kingine.
 
Hawa watu wa hizi platform Huwa Wana misimamo sana si uliona yule wa wiki leaks assange, au yule mdukuzi alikimbilia Russia Snowden Huwa hawatoi passcode labda wamuue.
Ukishakua na hela hasa za kihalali kama hao jamaa, serikali haiwezi kukupelekesha, ni lazma mkae mezani muongee.

Tofauti na sisi njaa kali, simu moja tu unatetemeka 😄
 
Na ndicho nachosema ilitakiwa afunguliwe mashtaka na sio kukamatwa.
Mpaka anakamatwa si ni arrest warranty hiyo mkuu. Au unadhani kakamatwa na wasiojulikana kama sisi huku kwetu.
Sasa kama wanamkamata uhuru wa habari wanaosema Russia anaukandamiza ni upi?. Na vipi makundi ya magaidi yanayonunua magari ya Toyota nakuyatumia kwenye mishe zao haramu mbona mmiliki au wamiliki wa Toyota hawakamatwi kwa Ku Facilitate harakati za magaidi?. Kama Telegram inavyo facilitate shughuri haramu?.
Toyota inauza bidhaa, haifanyi huduma. Ingekuwa ni kampuni ya huduma mfano ya kihasibu kama PWC alafu ikapata tenda ya kufanya auditing kwa kundi la kigaidi hapo ungeleta hoja yako. Mbona Ulaya hawafungii Quran ambayo inakuwa cited na magaidi? Au mbona hawafungii Uislamu ambao una makundi ya kigaidi Al Qaeda, Al Shabaab, Boko Haram, ISIS, et al.

Kwa sheria za Ulaya ukianzisha mtandao hakikisha una uwezo wa kulinda mahudhui, huwezi miliki mgahawa alafu bibi afya akute uchafu humo ndani useme "mimi siuzi uchafu unaachwa na wateja wenyewe".
Na kwa nini huko UK&France wanakamata watu wanaopost kukosoa utendaji wa Police mitandaoni?.
Hii ni justification ya Telegram kutumika kurusha maudhui yasiondana na sheria?
Kwa nini wanatishia kumkamata Musk au kufungia X huko west .
Hajakamatwa na anajulikana alipo, na X haijafungiwa. Still hii sio justification.
Uhuru wa habari upo wapi ambao wao ndio wahubiri wakuu wa free speech?.

Censorship ya habari ndio inayowasumbua nasio kingine.
Telegram iko huru, haina staff wengi na haiko organized sana. Magaidi humohumo, madawa ya kulevya, biashara haramu na mambo mengine ambayo yasingekuwepo hapo ungeitaja hiyo censorship.
 
Mpaka anakamatwa si ni arrest warranty hiyo mkuu. Au unadhani kakamatwa na wasiojulikana kama sisi huku kwetu.

Toyota inauza bidhaa, haifanyi huduma. Ingekuwa ni kampuni ya huduma mfano ya kihasibu kama PWC alafu ikapata tenda ya kufanya auditing kwa kundi la kigaidi hapo ungeleta hoja yako. Mbona Ulaya hawafungii Quran ambayo inakuwa cited na magaidi? Au mbona hawafungii Uislamu ambao una makundi ya kigaidi Al Qaeda, Al Shabaab, Boko Haram, ISIS, et al.

Kwa sheria za Ulaya ukianzisha mtandao hakikisha una uwezo wa kulinda mahudhui, huwezi miliki mgahawa alafu bibi afya akute uchafu humo ndani useme "mimi siuzi uchafu unaachwa na wateja wenyewe".

Hii ni justification ya Telegram kutumika kurusha maudhui yasiondana na sheria?

Hajakamatwa na anajulikana alipo, na X haijafungiwa. Still hii sio justification.

Telegram iko huru, haina staff wengi na haiko organized sana. Magaidi humohumo, madawa ya kulevya, biashara haramu na mambo mengine ambayo yasingekuwepo hapo ungeitaja hiyo censorship.
Hakuna uhuru wa habari bali Kuna uhuru wa mwenye chombo Cha habari & Serikali (wanapoafikiana) popote duniani.
 
Hata mimi jana Telegram imenisumbua. Pavel amekamatwa kwa makosa ya Telegram kuchapisha maudhui yanakokinzana na haki za binadamu na makosa ya jinai. Telegram hamna regulation hata wauza madawa wapo, sexual traffickers wapo.

Sidhani kama ni makosa makubwa sana kwake, angekamatwa kwao Urusi ndio ana kesi kubwa ila cha ajabu serikali ya Urusi inaitumia sana Telegram maana raia hawaziamini sana source rasmi za serikali.
Kumbe Asssange pia alikamatwa Urusi!?? Ona huyu..... Na chuki zake za wazi ...
 
Hawa waseng£ wameona Telegram ni secretive social network ambayo inalinda sana siri za watumiaji na data zao , so mataifa na serikali always huwa zinataka kucompromise social networks na kuzitumia kama surveillance tools ,
Sijajua kama Wote na Signal hali ikoje kwa sasa ila Telegram ilikuwa ni moja ya platform ya usalama sana kufanya mawasiliano , kuna Wire na Signal apps nazo zilikuwa vizuri sana ,sijui kwa sasa kama zilishapandikizwa surveillance tools kama matakataka ya Meta (facebook , what's app , Instagram nk
Mitandaon kama WhatsApp Facebook ndo hutumiwaa na mosadi kuwatrack baadhi ya viongozi wa mataifa mbalimbali kupitia C.A.I halafu wanajisifia hata haniye walimtafuta kupitia wahtspp
 
Sio atoe access. Awe na regulations kwenye mtandao wake mbona simple kabisa. Kuna kipindi TikTok ililalamikiwa kutuma maudhui mara ya mtu amejinyonga, mara ajari. Tiktok wakarekebisha sasa Telegram nao wana mambo ya kawaida ya kurekebisha.
Kwahio warekebishe halafu connection ziwe haziruhusiwi?😂 Hebu kuweni makini jamani. TELEGRAM ndio mtandao pekee ambao ukitaka pisi unaita kama unavyoita bolt tu...Ina faida nyingi sana kuliko hasara. Kikubwa uwe na channel zako tu.

Ukitaka content unashusha tu ziwe movie au vinginevyo. Inatunza contact za toka siku ya kwanza ulipo install. Hata uwe umebadili simu mara 6 watu wako utawapata mle hata kama namba zao ulishapotezaga.
 
Back
Top Bottom