Uchaguzi 2020 CHADEMA, ACT Wazalendo vyapigwa marufuku kunadi wagombea wasio wa vyama vyao. Waambiwa kufanya hivyo ni kuwachanganya Wananchi

kwani kuna ubaya gani kumdadi mgombea wa chama kingine?
 
TLP+CCM Huyu Mrema hawachanganyi watanzania anawachanganya warundi tu
 
Sasa marufuku iko wapi hapo?
 
Ha ha
Sasa ; Chama tawala kinashinda kwa kishindo!
hawa wasomi wanahangaika na nin? Upinzani c umeshakufa?
Kuanzia mkurugenzi hadi msajili wanarukaruka nin
Wasipokuwa makini watajiabisha mbele ya watoto mwaka huu. Yetu macho na masikio
 
CHADEMA waliwahamasisha wapi wakati walikatazwa kufanya siasa?
 
Uchaguzi huchagui MTU unachagua kwanza Sera ya chama husika

Sasa ukisema chagua chadema wewe ukiwa ACT wazalendo wakati unajua kabisa Sera za Chadema na ACT wazalendo ziko tofauti na Maalim Seif wa ACT wazalendo hanadi Sera za Chadema mikutano yake ya kampeni na Lisu wa Chadema hanadi Sera za ACT wazalendo hivi ni nini hicho kama sio upumbavu wag mivyama miwili na wagombea wao?

Msajili yuko sahihi hii kitu ilimpa shida hata Lowasa akiwa UKAWA hakujua anadi Sera gani ya chama kipi kikichomo kwenye UKAWA akaishia tu kuongelea vipau mbele vyake binafsi kama yeye

Hao ACT wazalendo na Chadema ni matapeli wa kisiasa
 
Jiwe tu mbaya sana toka ameingia madarakani 2015 , amewaambukiza kichaa watu wengi sana , hasa viongozi anaowapa maagizo , imebaki kidogo tu wavue nguo .
 
vipi kuhusu mrema na cheyo kumnadi magufuli yenyewe ni halali kwa kuwa mmeshakiri kuwa yeye ni yesu wa chato?
 

Huyu Sister na mwenzie Mihela wanataka kuiendesha NEC kama klabu cha pombe za kienyeji, ambako kila aliyelewa huamua kuimba chochote ambacho kilevi kinamtuma.

Tume inaendeshwa kisheria. Huwezi kutoa katazo lolote na ukasema ni kosa, bila ya kuonesha kwa kufanya hicho unachowazuia wanafanya kosa la kukiuka kifungu gani cha sheria.

Kama hakuna kifungu chochote cha sheria kilichokiukw, ina maana hakuna kosa kisheria, na hivyo hata katazo lenyewe linakuwa ni upuuzi mtupu.

Wagombea wakisikiliza haya makatazo ya kijinga kutoka kwa wajinga waliopo huko Tume, kuna siku wagombea wataambiwa wakiwa kwenye kampeni, wasiongelee zaidi ya mambo mawili au matatu kwa sababu wakiongekea mambo mengi wanawachanganya wapiga kura au kuwafanya wapiga kushindwa kukumbuka yote. Na wapo wajinga watakaosema, Tume ipo sahihi!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
vipi kuhusu mrema na cheyo kumnadi magufuli yenyewe ni halali kwa kuwa mmeshakiri kuwa yeye ni yesu wa chato?
Ulitusikia wana CCM tukishobokea walichokisema?

Two wrongs don't make a right

Sera zetu tofauti na zao ndio maana huwezi ukatusikia tukisema lolote kwa hayo waliyosema tunaendelea kunadi tu sera zetu za CCM hutatusikia tukimtaja Mrema wala Cheyo kwenye kampeni zetu

Sisi tunajielewa na tunaelewa tofauti za vyama ziko Kwenye sio kwe sura ya kichwa cha Lisu na ya Maalim Seif
 
Wameamua kufanya kazi ya shetani mchana kweupe bila ya aibu. Bora niendelee kuwa mkulima kuliko kuwa mnafiki kwa ajili ya tumbo.
 
Watu tulijiandudikisha 2015 mpaka Sasa vituo vyetu ni vile vile.

Kama watu hawakujiandikisha wapiga kura mil29 wametoka wapi kwenye data base ya tume? Mnakwama pakubwa Sana nyie watu.
 
Bado hujajibu swali tena swali rahisi sana "je mwanachama wa tlp (mrema) na wa UDP (cheyo) kumnadi mgombea wa ccm ni halali ila mgombea wa ACT wazalendo kumnadi mgombea wa CHADEMA au wa CHADEMA kumnadi wa ACT ni haramu? hilo tu ndio swali wala sijataka kujua sera zenu
 
Katazo la msajili umlielewa? Kapiga marufuku vyama vyote
Halafu umechanganyikiwa mrema na cheyo sio wagombea uraisi walioteuliwa na vyama vyao ni wapiga kura wa kawaida tu sio wagombea uraisi waliopewa ilani ya vyama waibebe kuinadi
 
Sasa wananchi wanachanganywa vipi wakati wanajua hii ni ACT na hii ni CHADEMA. Kwanini wana wasiwasi na hivyo vyama, kwani vipi mbona TLP ya Mrema na UDP ya Cheyo mbona walimsupport John Magufuli? Haya mambo ya kijinga yanashusha status ya nchi yetu kwa ujinga wa CCM. Tangu lini CCM na huyo msajili wanawaonea huruma wananchi wa Tanzania???
 
This country is going backwards because of such people who are looking after their stomachs.

We need to have a thorough review of this election at the Haque as it is now....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…