CHADEMA amsheni watu kwa kauli za kina Chalamila kwa mjamzito kwamba kama hatoi Shs 50,000 arudi nyumbani mume wake amkate kwa kisu na mkasi ajifungue

CHADEMA amsheni watu kwa kauli za kina Chalamila kwa mjamzito kwamba kama hatoi Shs 50,000 arudi nyumbani mume wake amkate kwa kisu na mkasi ajifungue

Utakuta watu kama nyie mnaosema fanyeni kazi wazazi wenu hawana hata elfu hamsini ndio mlizaliwa mazingira ya umasikini sana lakini mmebahatika kuwa na vijisenti sasa mnawaponda wengine. Wazazi wako walipanga kukuzaa wewe au ulitokea tu wakitarajia ungekuja na baraka zako?
📌📌📌Hii dunia sio mahali salama kwa MASIKINI!!!

YAANI HUNA HATA ELFU HAMSINI YA AKIBA ILA UNAPATA WAPI UJASIRI WA KULETA KIUMBA HAPA DUNIANI🧐🧐🧐

WAAFRIKA BADILIKENI UJAUZITO SIO AJALI.CONDOM ISIYOPASULA INAUZWA BUKU.HAKUNA UFAHARI KWENYE UFUKARA!!!

NI DHAMBI KUBWA SANA KUZAA WATOTO USIOWEZA KUJA KUWAHUDUMIA NA KUWAACHIA URITHI. HAO WATOTO WANAISHIA KUWA CHEAP LABOUR HUKO VIWANDANI KWA WAHINDI WANALIPWE BUKU 4 KWA SIKU.


📌KAMA HUNA HELA NI BUSARA UKAPANGA UZAZI!!!
 
Wanataka kuleta watoto wateseke bila sababu
Hamna dada yako, binamu yako au ndugu yako yeyote aliewahi kudungwa mimba bila kupanga? Kumbuka ni wanyama tu wanao mate kwa lengo la kuzaa, sio wanadamu. Huenda hata mimba yako haikupangwa pia.
 
Watu inatakiwa wawajibike kwa watoto wanaowazaa, serikali ijenge barabara, reli, madaraja, ulinzi n.k bado hatujafikia hatua ya serikali kulipia uzazi wa watu.
 
Jambo moja nililoona kuhusu Chadema ni kwamba mnashindwa kutumia matukio ya kila siku kuwafunua macho wananchi kwa nini serikali ya CCM haipo madarakani kwa faida yao. Hii ni pamoja na matumizi ya kifahari ya fedha ya hivi karibuni ya Mkutano Mkuu wa CCM na kadhalika.

Lakini pale ambapo inatokea viongozi wateuliwa wa CCM kama Chalamila wanatoa kauli za kubeza wananchi, kwa mfano huyu mama aliempigia simu Chalamila kusema analazimishwa kutoa Tshs 50,000 ili wamhudumie kujifungua, halafu Chalamila anamjibu kama hhutaki kutoa hiyo hela chukua bajaji nenda nyumbani kwako mwambie mumeo achukue kisu na mkasi akutoe mtoto, hizo ni kauli zilizokosa staha, zenye kuonyesha kiburi na majivuno ya uongozi wa CCM kwa wananchi wake.

Sababu ni kwamba Watanzania tunatozwa kodi katika maeneo mengi sana, lakini fedha hizi za kodi zetu zinaonekana kuwanufaisha watu wachache kama kina Chalamila katika matumizi yao ya anasa kutia ndani na mambilioni wanayotumia kama posho, kununua magari ya kifahari nk. Na hata kama wananchi, pamoja na mlolongo wa kodi wanazokatwa, wanatakiwa kuchangia gharama za hospitali, wananchi wanapohoji kitu lazima ajibiwe kwa heshima na ustaarabu.

Tumuulize Chalamila; jibu alilompta huyu mama linaendama na imani ya CCM kwamba kila mtu anastahili heshima? Au huo ndio msimamo wa Raisi Samia ambaye nae ni mwanamke anaejua maana ya kujifungua? Vipi wakati Samia akijifungua mwanae Abdul angepewa jibu la namna hii na mkuu wa mkoa wa wakati huo?

Huduma za kujifungua ni mojawapo ya huduma dharula ambazo hazipaswi kuwekewa masharti ya leta hiki na kile kabla hatujakuhudumia. Hizi tozo nyingi mnazotutoza elekezeni huko badala ya kujibadilishia magari makubwa ya serikali kila baada ya miaka mitatu.

Ni wazi hawa watu wa CCM wamelewa madaraka na kujiamini kwamba hata wakiwatukana wanachi na kuwakebehi, wataendelea kuwa madarakani. Chadema, vitu kama hivi vitumieni kuwaamsha wananchi juu ya ukweli wa aina ya watu wanaojiita viongozi wao
View attachment 3214787

Angalia pia: https://www.jamiiforums.com/data/video/5941/5941542-128f28144764987ee2bf3cd653521c1d.mp4
Chadema ndio ina wajawazito? Kule Kenya raia wangeisha lianzisha bila kungoja Chama. Wacha ujinga kuzania kila kitu lazima kianzishwe na chama
 
Point safi sana Mkuu. Hata mie nilivyoelewa ni kwamba uchangiaji kwenye huduma za wajawazito ulikoma, kwa tozo na misaada toka nje kupunguza vifo vya kina mama na watoto. Ndio maana majibu ya huyu mvuta bangi yanatia karaha sana!
IMG_7686.jpeg



Huyo hapo ☝️week iliyopita tu alikuwa anamfanyia mazingaombwe mkurugenzi wa WHO wana huduma nzuri ya uzazi na wamepunguza vifo.

Ndio vitu wanavyochapisha kwenye website yao wapo vizuri. Wakati uhalisia kuna wamama wajawazito na vichanga wanafia mbele ya wauguzi kisa tu kukosa gloves.

Siku chache baadae, mkuu wa mkoa na yeye baada ya bange zake anatoa kejeli kwa raia kama kawaida yao.

Huko serikalini sijui kama kuna hata mmoja ataiona pepo unafiki wa hawa watu sio wa dunia hii.

Mungu anipe nguvu nilisema sitoongelea tena afya huyu mama alipopewa uwaziri maana chaos itakayofuata ni balaa.
 
Watu wenye vichwa mithili ya maboga Huwa wanakera sana.yaani chalamila anapingana na sera ya wizara ya afya ya mama mjamzito kujifungua bure anatuletea ujinga wake.
 
Utakuta watu kama nyie mnaosema fanyeni kazi wazazi wenu hawana hata elfu hamsini ndio mlizaliwa mazingira ya umasikini sana lakini mmebahatika kuwa na vijisenti sasa mnawaponda wengine. Wazazi wako walipanga kukuzaa wewe au ulitokea tu wakitarajia ungekuja na baraka zako?
Kama tungekuwa tumezaliwa mazingira hayo tungekuwa tunatia huruma kama wewe na kusubiri kudra za serikali.

Wewe huna elfu 5 ya groves huyo mtoto utamlisha Nini?
 
View attachment 3214822


Huyo hapo week iliyopita tu alikuwa anamfanyia mazingaombwe mkurugenzi wa WHO wana huduma nzuri ya uzazi na wamepunguza vifo.

Siku chache baadae, mkuu wa mkoa baada ya bange zake anatoa kejeli kwa raia.

Huko serikalini sijui kama kuna hata mmoja ataiona pepo unafiki wa hawa watu sio wa dunia hii.
Mwenye email ya huyu Mkuu wa WHO amtumie hiyo clip ya Chalamila amwambie alivyodanganywa na viongozi wahuni wa Tanzania, hela zote za msaada kwa wajawazito zimenunua mabasi ya CCM!😀
 
Wewe huna elfu 5 ya groves huyo mtoto utamlisha Nini?
KIla mtoto anakuja na baraka yake! Kwanza umesahau tuliambiwa tuzae tu, tufyatue? Si hao hao kina Chalamila walisema tufanye hivyo?
 
Wanataka kuleta watoto wateseke bila sababu
Ni ujinga mkubwa mtu unajijua hohehae na bado unashindwa kutumia CONDOM ukazuia kupata zambi ya kuja kutesa kizazi chako.


Mtu huna mbela wala nyuma ila unang'ang'ana na wewe upate watoto.

📌waafrika waache ujinga kuzaa hovyo sio sifa.Kama mtu hana PESA kabisa ASIZAE!!
 
Jambo moja nililoona kuhusu Chadema ni kwamba mnashindwa kutumia matukio ya kila siku kuwafunua macho wananchi kwa nini serikali ya CCM haipo madarakani kwa faida yao. Hii ni pamoja na matumizi ya kifahari ya fedha ya hivi karibuni ya Mkutano Mkuu wa CCM na kadhalika.

Lakini pale ambapo inatokea viongozi wateuliwa wa CCM kama Chalamila wanatoa kauli za kubeza wananchi, kwa mfano huyu mama aliempigia simu Chalamila kusema analazimishwa kutoa Tshs 50,000 ili wamhudumie kujifungua, halafu Chalamila anamjibu kama hhutaki kutoa hiyo hela chukua bajaji nenda nyumbani kwako mwambie mumeo achukue kisu na mkasi akutoe mtoto, hizo ni kauli zilizokosa staha, zenye kuonyesha kiburi na majivuno ya uongozi wa CCM kwa wananchi wake.

Sababu ni kwamba Watanzania tunatozwa kodi katika maeneo mengi sana, lakini fedha hizi za kodi zetu zinaonekana kuwanufaisha watu wachache kama kina Chalamila katika matumizi yao ya anasa kutia ndani na mambilioni wanayotumia kama posho, kununua magari ya kifahari nk. Na hata kama wananchi, pamoja na mlolongo wa kodi wanazokatwa, wanatakiwa kuchangia gharama za hospitali, wananchi wanapohoji kitu lazima ajibiwe kwa heshima na ustaarabu.

Tumuulize Chalamila; jibu alilompta huyu mama linaendama na imani ya CCM kwamba kila mtu anastahili heshima? Au huo ndio msimamo wa Raisi Samia ambaye nae ni mwanamke anaejua maana ya kujifungua? Vipi wakati Samia akijifungua mwanae Abdul angepewa jibu la namna hii na mkuu wa mkoa wa wakati huo?

Huduma za kujifungua ni mojawapo ya huduma dharula ambazo hazipaswi kuwekewa masharti ya leta hiki na kile kabla hatujakuhudumia. Hizi tozo nyingi mnazotutoza elekezeni huko badala ya kujibadilishia magari makubwa ya serikali kila baada ya miaka mitatu.

Ni wazi hawa watu wa CCM wamelewa madaraka na kujiamini kwamba hata wakiwatukana wanachi na kuwakebehi, wataendelea kuwa madarakani. Chadema, vitu kama hivi vitumieni kuwaamsha wananchi juu ya ukweli wa aina ya watu wanaojiita viongozi wao
View attachment 3214787

Angalia pia: https://www.jamiiforums.com/data/video/5941/5941542-128f28144764987ee2bf3cd653521c1d.mp4
Ni lugha imetumika vibaya tu, watu wasifurahie tu ngono, wawajibike na kinachofuata baada ya hapo.
 
Elfu 50 sio elfu tano. Watanzania wengi sana bado hawana elimu ya kutambua ukiwa huna uwezo usizae sana au usizae kabisa - bado wanaishi kwa filosofia kwamba kila mtoto anakuja na baraka zake. Kwa hiyo viongozi wanapaswa kuchululia level yao ya kuelimika into context.

Mbona wanafurahia u-semi illiteracy wao wa kisiasa kwenye kupiga kura?
Namna nzuri ya kufundisha kwa vitendo ni kuwaacha wapambane na hali zao.
 
Ni lugha imetumika vibaya tu, watu wasifurahie tu ngono, wawajibike na kinachofuata baada ya hapo.
Wanadamu sio wanyama kwamba ngono ni tendo la kuzaa tu. Kuna mimba za kutotarajia. Wewe na mimi huenda mimba zetu hazikutarajiwa. Kwani wewe ulishawahi muuliza mama yako kama mimba yako aliipanga akakuhakikishia kuwa ndivyo ilivyokuwa?
 
KIla mtoto anakuja na baraka yake!
Huu msemo ndo maskini wote walimezeshwa😂😂😂


📌Hakuna baraka ya kizembe hivyo.Bali unawaandalia wahindi CHEAP LABOUR wa kwenda kutumikia huko viwandani kwa ujira wa 4,000/= kwa siku.Hivi hamvionei huruma vizazi na damu zenu!!!

Wengine kutokana malezi mabovu yanayoambatana na UMASIKINI wanaishia kuwa wapiga debe,mawinga,madalali,wezi ,majambazi na machangudoa.
 
Namna nzuri ya kufundisha kwa vitendo ni kuwaacha wapambane na hali zao.
Hapana. Huo ni mtazamo wa Ki-CCM wasiojali wananchi. Bado wananchi wa Tanzania zaidi ya 60% ambao hawahusianishi kuzaa na hali za kipato chao. Bado kwa kaya nyingi za Tanzania wana msimamo kuwa kila mtoto anakuja na baraka zake
 
Ameongea vizuri tu.Ni mapokezi na tafsiri ya maneno.Mkiwapa wake wenu ujauzito muwaandalie vifaa na fedha za dharula.Rahisi tu.Dezodezo hakuna.Kipi kigumu kuelewa?
 
Back
Top Bottom