CHADEMA badilisheni hiyo kauli mbiu ya "No Reforms, No Elections"

Umemkosea heshima Pascal.

Hapo Juu umejibu kwa staha👆Nyani Ngabu kwa Ushauri huo huo ambao ameutoa Mzee wetu Pascal Mayalla Kwamba;

Mwenyekiti wetu CHADEMA, aitathmini kauli mbiu ya chama kuelekea uchaguzi 2025.

Tatizo lipo wapi hapo?

..nadhani unataka tutilie mashaka na hatimaye tumvue dhifa ya U GT mzee wetu Pascal


Hapa chini umeandika kinafiki Unafiki.👇 Why? Kwa sababu ni ya Mzee wetu Pascal Mayalla ?
Mmeshalipwa hela huko saivi mmeanza kujitoa ufahamu?

Tunajua hizi ni sehemu za mbinu za CCM na wajinga wachache waliopo huko TISS kufanya spinning na kueneza propaganda mfu ili kuwakatisha tamaa Watanzania wanaotaka mabadiliko ya kweli.
Interested Observer.
 
Unashindwaje kuelewa kuwa CHADEMA kama chama wana uwezo wa kususia uchaguzi huo?
 
Kwa Mujibu wa katiba Hakunaga Mtu au kikundi cha Watu chenye uwezo wa kuzuia Uchaguzi

Labda watumie njia za Kienyeji za ulozi 🐼
Kwa mujibu wa katiba hiyohiyo ikiwepo dharura mtu au kikundi cha watu haohao wanauwezo wa kuzuia uchaguzi kwa muda usiozidi miaka 5.
 
Naona sasa mnajenga mnara wa Babeli. Mmeanza kukataana wenyewe kwa wenyewe. Ni mwendo wa Lugha gongana tu.
Vipi tayari mmeshaelewana na Traore asiwe anaonesha bastola yake hadharani?! Manake ulisema hufurahishwi na tabia yake hiyo 🤣🤣🤣🤣
Mambo ya CDM achana nayo, siyo ya kiwango cha machawa.
 
Wakati anasubiri wananchi wapate huo uelewa mpana tayari kutakuwa na damage kubwa kwa wapiga kura na izingatiwe muda hautoshi. Nyani Ngabu yuko sahihi.
 
Naona sasa mnajenga mnara wa Babeli. Mmeanza kukataana wenyewe kwa wenyewe. Ni mwendo wa Lugha gongana tu.
Halafu wapiga kura wangapi wanaweza kujua maana ya "No reform"? Wenzetu wana shida kubwa ya kutojua vizuri wapiga kura wa Tanzania ni kina nani. Huwezi kuta CCM inatumia kiingereza kufikisha ujumbe kwa wapiga kura. Imagine unaenda huko Laela, Mpanda, Wampembe, Kirando unawaambia "No reforms, No election" ukitegemea waelewe.
 
CCM kingereza chake ni hongo, vitisho vya kupoteza watu,wasimamizi walimu na mapolisi tu.
 
Kakosea kwenye kuchagua maneno yake.

Sidhani kama katumia lugha ya kisheria.

Kakosea tu katika kuchagua maneno ya kutumia.

It’s okay. Hata Lisu huwa anakosea.
No reform no election ilitangazwa na Mbowe na ni maazimio ya kamati kuuu, Lissu ameendeleza jambo lililopitishwa na kamati kuu sasa why are you calling him out as an individual!!

Kingine no reform no election maana yake kama hakuna mabadiliko uchaguzi haufanyiki it can be chadema wakajiondoa why unachukulia kwamba ni violent option pekee?
 
Mimi sijasema chochote kuhusu no reforms no elections.

Kichwa cha mada kimebadilishwa na mods. Mimi sikuandika hivyo.

Na ndo maana hata ukisoma [na kuelewa] nilichoandika, utaona kuwa hiyo si hoja yangu.

Mimi nimezungumzia Tundu Lisu kusema watazuia uchaguzi kufanyika.

Sikuwahi kumsikia Mbowe akisema watauzuia uchaguzi kufanyika.
 
Kusema mtauzuia uchaguzi kufanyika mnawachanganya watu maana haieleweki mtauzuiaje huo uchaguzi usifanyike.
Hii ndiyo hoja ya msingi..

Na nafikiri toka mwanzo, ungejikita kuanzisha mjadala ili kujibu swali la: KIVIPI? KWA NJIA GANI?

Hata hivyo, Tundu Lissu ameelezea njia za kufanya hivyo very clearly kwamba ni kwa njia za kidemokrasia na kikatiba kabisa; kwa mfano:

1. Maandamano ya amani kudai mabadiliko haya..

2. Mikutano na makongamano ya kisiasa ya kutoa elimu kwa watu waielewe movement hii..

3. Kuzishirikisha taasisi na jumuiya za kiraia za kupigania haki (NGOs) za kitaifa na kimataifa..

4. Kuzishirikisha taasisi na madhehebu ya kidini...

5. Kuongea na jumuiya ya kimataifa na nchi wahisani nk

Ibadilisheni hiyo kauli mbiu.
Iweje? Pendekeza...

Au unataka iwe: JAMHURI YA MUUNGANO? Tujibu: KAZI IENDELEE..??
 
mtaalamu pekee ndani ya chadema si ndio huyo huyo kiongozi wake ambae ni kibaka na tapeli wa siasa gentleman?

hashauriki wala haihitaji ushauri wa yeyote ndani ya chadema kwasabb yeye ndie msomi na memaji wa mwisho na mtaalamu wa mambo yote ya chadema .

Yeye ni alfa na omega, mwanzo na mwisho ndani ya chadema. Hata hiyo no reform no elections anaielewa yeye pekee, wengine inawachanganya tu 🐒
 

Hata kama ni kwa nguvu powa tu hakuna uhuru unaopiganiwa bila nguvu hasa kwa serikali ambazo zina rushwa kubwa hivi
 
Kakosea kwenye kuchagua maneno yake.

Sidhani kama katumia lugha ya kisheria.

Kakosea tu katika kuchagua maneno ya kutumia.

It’s okay. Hata Lisu huwa anakosea.
Unakotafsiri wewe kakosea maneno hiyo ndio credit kubwa kwa wafuasi wake waliompigia kura kuwa mwenyekiti.

Kabla ya uchaguzi tuliweka wazi hapa jukwaani zambi ya Mbowe ni kuwepo madarakani muda mrefu kitu ambacho kwa chama kinachosaka dola hakuna tatizo lolote.

Mbowe ndio Diplomatic figure kwa Chadema mwenye uvumilivu na kuweza kuchaguwa maneno.

Lakini kwakuwa duniani sasa hivi viungozi radical ndio wanaopendwa ukianzia na Trump type basi Tundu Lisu ndio mtu sahihi wa kupambana na ccm, ccm haitaki ustaarabu sasa huyu Lisu ndio kiboko yao.

Kama alimuita Magufuli diteta uchwara wakati Taifa zima limejaa hofu, sasa hivi hakuna wa kuweza kumdhibiti.
 
Kil
Kilaza ktk ubora wako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…