CHADEMA bado haijakomaa kidemokrasia, mioyo na fikra za baadhi ya wagombea uongozi wa kitaifa

CHADEMA bado haijakomaa kidemokrasia, mioyo na fikra za baadhi ya wagombea uongozi wa kitaifa

Tlaatlaah

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2023
Posts
24,665
Reaction score
25,388
Ni wazi ukomavu wa kisiasa na kidemokrasia ndani chama cha demokrasia na maendeleo chadema, miongoni mwa wanaogombea uongozi wa kitaifa, wajumbe wa mkutano mkuu wa chadema taifa wanachama na mashabiki bado haijapevuka vizuri mioyoni na kwenye fikra zao.

Shari inayombatana na masharti juu ya namna gani uchaguzi huo unavyofaa kufanyika ina viashiria vya liwalo na liwe vinavyoashiria kukibomoa na kukisambaratisha kabisa chama hiki kikongongwa cha siasa nchini.

kuna wagombea uongozi na wafuasi wao ndani ya chadema wanaenda kwenye uchaguzi huo muhimu sana ngazi ya taifa wakiwa na dhamira na nia moja tu tena kwa kiapo kwamba nisipokua mwenyekiti mimi bora tukose wote, la sivyo chadema ife.

Vita vya maneno na vijembe vya kisiasa na namna wagombea uongozi wanavyovuana nguo hadharini na kutoa siri za vikao vya ndani, ni wazi chadema haina mwisho mwema kuelekea uchaguzi huo wa Jàn.21, 2025.

My friends ladies and gentlemen,
una maoni gani kwenye hili.
Chadema itavuka salama kweli?
Taharuki, mabishano na malumbano ya nini sasa miongoni mwa wagombea muhimu?🐒

Mungu Ibariki Tanzania
 
Mkikumbuka Lissu kubeba mikoba pendwa hampati usingizi:



Wacha Simba akuje tubujikwe machozi ya furaha!
 
Mkikumbuka Lissu kubeba mikoba pendwa hampati usingizi:

View attachment 3198282

Wacha Simba akuje tubujikwe machozi ya furaha!
maana nia na dhamira za wagombea uongozi wa kitaifa zinakusudia kuivuruga, kubomoa na kuisambaratisha chadema,

huko ni kutopevuka kwa Demokrasia ndrani ya mioyo na fikra za wanachdema kwa ujumla 🐒
 
Ni wazi ukomavu wa kisiasa na kidemokrasia ndani chama cha demokrasia na maendeleo chadema, miongoni mwa wanaogombea uongozi wa kitaifa, wajumbe wa mkutano mkuu wa chadema taifa wanachama na mashabiki bado haijapevuka vizuri mioyoni na kwenye fikra zao.

Shari inayombatana na masharti juu ya namna gani uchaguzi huo unavyofaa kufanyika ina viashiria vya liwalo na liwe vinavyoashiria kukibomoa na kukisambaratisha kabisa chama hiki kikongongwa cha siasa nchini.

kuna wagombea uongozi na wafuasi wao ndani ya chadema wanaenda kwenye uchaguzi huo muhimu sana ngazi ya taifa wakiwa na dhamira na nia moja tu tena kwa kiapo kwamba nisipokua mwenyekiti mimi bora tukose wote, la sivyo chadema ife.

Vita vya maneno na vijembe vya kisiasa na namna wagombea uongozi wanavyovuana nguo hadharini na kutoa siri za vikao vya ndani, ni wazi chadema haina mwisho mwema kuelekea uchaguzi huo wa Jàn.21, 2025.

My friends ladies and gentlemen,
una maoni gani kwenye hili.
Chadema itavuka salama kweli?
Taharuki, mabishano na malumbano ya nini sasa miongoni mwa wagombea muhimu?🐒

Mungu Ibariki Tanzania
Wewe na CCM ambayo imekufa sasa ndio hamjakomaa.
 
maana nia na dhamira za wagombea uongozi wa kitaifa zinakusudia kuivuruga, kubomoa na kuisambaratisha chadema,

huko ni kutopevuka kwa Demokrasia ndrani ya mioyo na fikra za wanachdema kwa ujumla 🐒
Nia za wagombea ni kuboaje chadema? Maana kila mgombea anadai anataka kukitoa hapo kilipo kwama, since njia ya maridhiano haijazaa matunda yoyote
 
Ni wazi ukomavu wa kisiasa na kidemokrasia ndani chama cha demokrasia na maendeleo chadema, miongoni mwa wanaogombea uongozi wa kitaifa, wajumbe wa mkutano mkuu wa chadema taifa wanachama na mashabiki bado haijapevuka vizuri mioyoni na kwenye fikra zao.

Shari inayombatana na masharti juu ya namna gani uchaguzi huo unavyofaa kufanyika ina viashiria vya liwalo na liwe vinavyoashiria kukibomoa na kukisambaratisha kabisa chama hiki kikongongwa cha siasa nchini.

kuna wagombea uongozi na wafuasi wao ndani ya chadema wanaenda kwenye uchaguzi huo muhimu sana ngazi ya taifa wakiwa na dhamira na nia moja tu tena kwa kiapo kwamba nisipokua mwenyekiti mimi bora tukose wote, la sivyo chadema ife.

Vita vya maneno na vijembe vya kisiasa na namna wagombea uongozi wanavyovuana nguo hadharini na kutoa siri za vikao vya ndani, ni wazi chadema haina mwisho mwema kuelekea uchaguzi huo wa Jàn.21, 2025.

My friends ladies and gentlemen,
una maoni gani kwenye hili.
Chadema itavuka salama kweli?
Taharuki, mabishano na malumbano ya nini sasa miongoni mwa wagombea muhimu?🐒

Mungu Ibariki Tanzania
Kwani ccm mnapenda ukomavu wa upinzani? Mngekua mnaupenda kwanini mnaua na kurubuni key members wa upinzani? Mfyuuuuuuu!
 
Nia za wagombea ni kuboaje chadema? Maana kila mgombea anadai anataka kukitoa hapo kilipo kwama, since njia ya maridhiano haijazaa matunda yoyote
huenda huna ukaribu wa kufuatilia maelezo ya wagombea uongozi hususani kwenye nafasi ya uenyekiti wa chadema taifa.

kwa faida yako na ya wadau wengine,
wapo wagombea uongozi ambao wameapa kwamba Lazima wao pekee ndiyo washinde uchuguzi kwa nafasi hiyo ya mwenekiti la sivyo bora chadema ife?

Gentleman,
unadhani huku ni kukibomoa au kuijenga chama?🐒
 
Kwani ccm mnapenda ukomavu wa upinzani? Mngekua mnaupenda kwanini mnaua na kurubuni key members wa upinzani? Mfyuuuuuuu!
gentleman,
hakunaga mapenzi kwenye kuelezea na kufafanua masuala ya kisiasa kitaalamu, mapenzi yenu muyafanye nje ya siasa,

hata hivyo ni wazi bado chadema na baadhi ya wafuasi wake ambao pia ni wagombea uongozi wa nafasi mbalimbali hawajakomaa wala kupevuka vyema kisiasa na kidemokrasia ndiyo maana wanaendekeza vitisho na kuropokaropoka kwa lengo la kuhakikisha chadema inasambaratika kabla hawajaelekea kusambaratisha vyama vingine vya siasa nchini 🐒
 
huenda huna ukaribu wa kufuatilia maelezo ya wagombea uongozi hususani kwenye nafasi ya uenyekiti wa chadema taifa.

kwa faida yako na ya wadau wengine,
wapo wagombea uongozi ambao wameapa kwamba Lazima wao pekee ndiyo washinde uchuguzi kwa nafasi hiyo ya mwenekiti la sivyo bora chadema ife?

Gentleman,
unadhani huku ni kukibomoa au kuijenga chama?🐒
Nafuatilia sana , na kwa taarifa yako kila mtu ana matarajio ya kushinda, swali ni kwamba why baadhi ya wagombea hawasemi watakifanyia nini chama? Wanaleta kitu gani tofauti ambacho huko nyuma hawajawahi kukifanya?
 
Wewe na CCM ambayo imekufa sasa ndio hamjakomaa.
ni muhimu sana kwa wajumbe wa mktano Mkuu wa chadema taifa, kudhibiti wagombea uongozi wa chadema taifa kwa kura, wale wote wanaokusudia kuigawanya, kuibomoa na kuisabaratisha chadema kabla hawajaelekea kusambaratisha vyama vingine vya siasa nchini 🐒
 
gentleman,
hakunaga mapenzi kwenye kuelezea na kufafanua masuala ya kisiasa kitaalamu, mapenzi yenu muyafanye nje ya siasa,

hata hivyo ni wazi bado chadema na baadhi ya wafuasi wake ambao pia ni wagombea uongozi wa nafasi mbalimbali hawajakomaa wala kupevuka vyema kisiasa na kidemokrasia ndiyo maana wanaendekeza vitisho na kuropokaropoka kwa lengo la kuhakikisha chadema inasambaratika kabla hawajaelekea kusambaratisha vyama vingine vya siasa nchini 🐒
Kuelekea uchaguzi mkuu wa Chadema,ninyi chawa wa chama cha Nyerere mtapata taabu sana ..hamtopata usingizi, masikio yote nyumba ya jirani, hakika mtapata uchungu sana ila hamtozaa kwa kuwa nyie ni kizazi cha nyoka wa kijani.
 
Nafuatilia sana , na kwa taarifa yako kila mtu ana matarajio ya kushinda, swali ni kwamba why baadhi ya wagombea hawasemi watakifanyia nini chama? Wanaleta kitu gani tofauti ambacho huko nyuma hawajawahi kukifanya?
Gentleman,
kama unafuatilia vyema siasa za wagombea uongozi wa chadema, kitu ambacho ni wazi sana ni kwamba,
wapo wagombea ambao dhamira yao ni kuibomoa na kuisabaratisha chadema kabisa, kabla hawajaelekea kusambaratisha vyama vingine vya siasa nchini.

ni muhimu sana kwa wajumbe wa mkutano Mkuu wa chadema taifa kuwajibika ipasavyo kuwashikisha adabu kwa kura wagombea uongozi wa kisiasa wa aina hii ili iwe fundisho kwa wengine 🐒
 
ni muhimu sana kwa wajumbe wa mktano Mkuu wa chadema taifa, kudhibiti wagombea uongozi wa chadema taifa kwa kura, wale wote wanaokusudia kuigawanya, kuibomoa na kuisabaratisha chadema kabla hawajaelekea kusambaratisha vyama vingine vya siasa nchini 🐒
Magufuli na kilichokua chama chake waliengua wagonbea wote wa vyama pinzani na kuweka watu wao leo yuko wapi? Its matter of time hata wewe unaipenda tu ccm kwakua inakutekenya ukacheka na si kwamba inakufurahisha.
 
Kuelekea uchaguzi mkuu wa Chadema,ninyi chawa wa chama cha Nyerere mtapata taabu sana ..hamtopata usingizi, masikio yote nyumba ya jirani, hakika mtapata uchungu sana ila hamtozaa kwa kuwa nyie ni kizazi cha nyoka wa kijani.
Gentleman,
hapa hatuzungumzia sijui masuala ya usingizi, maskio wala kuzaa kwa uchungu kama nyoka,

hapa tutajadili ukomavu na kupevuka kwa siasa wagombea uongozi na wafuasi wa chadema kuelekea uchaguzi wao wa ndani Jan 21,2025,
kwamba, wapo wagombea wasio na nia njema kabisa dhidi ya chadema,

wana chuki kupindukia, wana ubinafsi kupindukia, Lakini pia dhamira na nia zao ni kuona chadema inasambaratika kabla hawajaelekea kusambaratisha vyama vingine vya siasa nchini 🐒
 
Gentleman,
kama unafuatilia vyema siasa za wagombea uongozi wa chadema, kitu ambacho ni wazi sana ni kwamba,
wapo wagombea ambao dhamira yao ni kuibomoa na kuisabaratisha chadema kabisa, kabla hawajaelekea kusambaratisha vyama vingine vya siasa nchini.

ni muhimu sana kwa wajumbe wa mkutano Mkuu wa chadema taifa kuwajibika ipasavyo kuwashikisha adabu kwa kura wagombea uongozi wa kisiasa wa aina hii ili iwe fundisho kwa wengine 🐒
Unarudi jibu lile lile kwa maswali tofauti. Stop copying man
Kama mgombea anashindwa au hawezi kusema atakifanyia nini chama basi ana deserve kitakacho mkuta, ataleta nini cha tofauti ambacho hakikufanyikw huko nyuma?

Chama kinahitaji mabailiko sio historia
 
Magufuli na kilichokua chama chake waliengua wagonbea wote wa vyama pinzani na kuweka watu wao leo yuko wapi? Its matter of time hata wewe unaipenda tu ccm kwakua inakutekenya ukacheka na si kwamba inakufurahisha.
Gentleman,
hapa sio suala la vyama vingine, mapenzi au vichekesho,

hapa ni majadiliano ya kisiasa dhidi ya kutopevuka na kukomaa kwa siasa na fikra za kidemokrasia miongoni mwa wagombea uongozi wa chadema taifa, ambao baadhi yao wanalenga kuibomoa na kuisabaratisha chadema,

ni muhimu zaidi kujikita kwenye hoja mahususi mezani gentleman 🐒
 
Unarudi jibu lile lile kwa maswali tofauti. Stop copying man
Kama mgombea anashindwa au hawezi kusema atakifanyia nini chama basi ana deserve kitakacho mkuta, ataleta nini cha tofauti ambacho hakikufanyikw huko nyuma?

Chama kinahitaji mabailiko sio historia
Yes gentleman,
mgombea huyo lengo lake mahususi na dhamira yake ni moja tu muhimu, ni kuhakikisha anaibomoa na kuisabaratisha chadema iwe ameshinda au hajashinda uongozi wa chadema taifa,

Lazima tuwaeleze kwa msisitizo mambo haya muhimu sana gentleman 🐒
 
Yes gentleman,
mgombea huyo lengo lake mahususi na dhamira yake ni moja tu muhimu, ni kuhakikisha anaibomoa na kuisabaratisha chadema iwe ameshinda au hajashinda uongozi wa chadema taifa,

Lazima tuwaeleze kwa msisitizo mambo haya muhimu sana gentleman 🐒
Amna mgombea anadhamira ya kukibomoa chama, hata kwenye matamshi yao hakuna anaesema hivyo
Watu wanataka mabadiliko, kama huwezi kuwapa kitu kipya but kaa pembeni

Huu ni uchaguzi, wagombea waweke facts, si porojo na historia. Historia haitakitoa chama kilipo
 
Gentleman,
hapa sio suala la vyama vingine, mapenzi au vichekesho,

hapa ni majadiliano ya kisiasa dhidi ya kutopevuka na kukomaa kwa siasa na fikra za kidemokrasia miongoni mwa wagombea uongozi wa chadema taifa, ambao baadhi yao wanalenga kuibomoa na kuisabaratisha chadema,

ni muhimu zaidi kujikita kwenye hoja mahususi mezani gentleman 🐒
Kwani wewe ni mchepuko wa Chadema? Kuzozana kwa nyumba kuu inakunyima nini raha ewe nyumba ndogo? Kwanini usitafute bwana wa kukuoa kama ccm imezeeka na haikutimizii?
 
Kwani wewe ni mchepuko wa Chadema? Kuzozana kwa nyumba kuu inakunyima nini raha ewe nyumba ndogo? Kwanini usitafute bwana wa kukuoa kama ccm imezeeka na haikutimizii?
gentleman,
masuala ya kitaalamu hayahitaji kubabaika wala kua na mihemko,

ipo haja ya wajumbe wa mkutano Mkuu wa chadema Taifa kuwashughulikia ipasavyo wagombea uongozi wote wenye nia ovu na chadema ili iwe fundisho kwa wengine wenye nia na dhamira kama hizo,

hiyo itakinisuru na kukisaidia chama kusonga mbele zaidi na kuimarisha mno 🐒
 
Back
Top Bottom