#COVID19 CHADEMA: Chanjo tumechanjwa sasa Kazi iendelee

#COVID19 CHADEMA: Chanjo tumechanjwa sasa Kazi iendelee

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Lilikuwa jambo la msingi kusimama kwa muda kupisha zoezi la chanjo kuanza bila ya kutatizika.

Muda wa kuitumia karata ya wingi wetu vizuri ili kuyajaza magereza yao sawa sawa umewadia.

Ni muhimu sana tukawaweka wazi wakatuelewa pasi na shaka kuwa:

"hatuogopi kukamatwa na tuko tayari mno kukamatwa kuliko hata kubakia majumbani mwetu."

Huu pia ni muda muafaka wa kuziweka tofauti zetu ndogo ndogo pembeni na wote wenye uhitaji wa katiba mpya kama sisi.

Tuombane misamaha faraghani na hadharani. Tanzania ni muhimu zaidi kuliko yeyote mwenye akili zake kichwani.

Tushirikiane sote, tuyashirikishe makundi na vyama vyote tunavyoweza kushirikiana navyo. Hayupo mmoja mwenye umuhimu zaidi kwenye mpambano mtakatifu huu kuliko mwingine.

Aboubakar Mbowe atafarijika mno kusikia tunaendelea kwa kasi ile ile.

Mkakati wa kuwahami wahanga ni wa muhimu sana. Umekuwa ukiombwa huu kwa muda sasa pasipo na mrejesho.

Ifahamike kuwa ni muhimu mapambano ya kudai katiba mpya yakaeleweka kuwa ni kwa kujitolea kwa hali na mali. Hii isifanywe kuwa fursa na mtu yeyote na kwa namna yoyote (hasa na mawakili).

Miito ya kujitolea iwe wazi kwa wote wakiwamo Sirro na serikali kwa ujumla wao. Wajue kuwa tunataka tume huru sasa na si vinginevyo.

Ni Lazima kuwapo uratibu wa karibu ili kuhakikisha wahanga wanatunzwa sawa sawa kama askari wetu mashujaa wa mstari wa mbele.

Wananchi wako tayari, wanachohitaji ni organization na uongozi thabiti kuendelea na mapambano muda wote bila kujali nani watakuwa wamekamatwa. Wananchi hawawezi kuamka kama mvua bila uongozi uliodhamiria.

Uongozi una gharama ni muhimu wenye hofu wakaachia ngazi sasa. Hizi ni zama mpya.

Ifahamike mafanikio ya Zambia au uwepo wa nchi marafiki hakutatusaidia lolote kama tutaendelea kutegeana.

Habari hii iwafikie kwa ufasaha pale ufipa kabla uvumilivu wetu haujafika mwisho.

Ninawasilisha.
 
Hii mbinu polisi wanayoendelea nayo ni ya ku suppress opposition hasa Chadema ili kuwaondoa kwenye lengo lao la kudai Katiba Mpya, tatizo ni hapo unaposema makundi mengine au vyama vingine vya siasa vihusishwe.

Hapa ndipo tatizo litakapoanzia, kuna vyama vipo kwenye ndoa na CCM, hawa sijui watashirikishwa kwa namna ipi, na kuna vyama vinafahamika huwa viongozi wake wana tabia ya kubadilika kama vinyonga, hawa nao sijui watashirikishwa vipi.

Wasiwasi wangu ni kwamba, isijetokea huo ushirikishwaji unaoutaka ukasababisha kucheleweshwa kwa hii movement sababu ya mitazamo tofauti watakayokuwa nayo hao viongozi wa vyama vingine vya siasa.

Najua huu mtazamo wangu utaonekana kama ubinafsi kwa wenye uelewa finyu, lakini muhimu naona bora udhaifu uliopo uwekwe wazi ili ufanyiwe kazi, kuliko kuufumbia macho wakati upo.
 
Hii mbinu polisi wanayoendelea nayo ni ya ku suppress opposition hasa Chadema ili kuwaondoa kwenye lengo lao la kudai Katiba Mpya, tatizo ni hapo unaposema makundi mengine au vyama vingine vya siasa vihusishwe.

Siyo siri kuwa wanaotaka katiba mpya ni wengi hata ndani ya CCM wamo.

Uzi huu unahusika:

Tathmini: Kesho bora ya Tanzania inategemea uwepo wa Katiba Mpya

Tofauti zilizopo ni ndogo sana. Hakipo chama kimoja kisicho hitaji tume huru. Hakipo chama kimoja kisicho hitaji katiba mpya.

Ndani ya CCM wanaopinga vuguvugu la katiba ni wale walio wanufaika wa moja kwa moja madarakani na si wote.

Matokeo yake tuna watu wengi wanasubiri matunda ili kula, badala ya kushiriki kwenye kupambana ili matunda yapatikane.

Kwenye mapambano tatizo si washiriki bali viongozi.

ANC iliunganisha wote wakiwamo PAC, Inkatha Freedom party nk japo wote wakiwa na mitizamo tofauti.

Chadema haiwezi kupigania hili peke yake bali kuongoza vita hivi na akili kichwani ndiyo lililo la msingi zaidi.
 
Makomgamano ya Katiba mpya yaendelee saa ya ukombozi ni sasa.

Chadema wanapaswa kutoa uongozi. Wananchi hawawezi kuamka wenyewe spontaneously.

1. Tuwahami wahanga
2. Hii si fursa
3. Kila mtu kwa nafasi yake awajibike kuchangia kwa hali na mali jitihada hizi
4. Askari wetu wa mstari wa mbele na watunzwe vilivyo
5. Mkakati wa wazi wa kuyajaza Pomoni magereza yao uwepo

Si muda mrefu kama uongozi chadema hautupi mwelekeo wajue wana risk Mapinduzi ndani ya chama.

Tulipo haparidhishi:

a) Uko wapi mkakati wa kuwahami wahanga?

b) Uko wapi mkakati wa wazi wenye kuonyesha tunachangia vipi bila kumnufaisha mtu yeyote kama fursa?

c) Yako wapi maridhiano na wengine wote yenye nia ya kusukuma mapambano mbele?

d) Iko wapi ratiba ya kuendelea na makongamano nchi nzima?
 
Ushujaa wa kipuuzi eti magereza yatajaa ???

Ukijicha JF unajiona kama Big Show, kumbe hunatofauti zuchu.

😂😂!

IMG_20210816_204624_190.jpg


Waambieni wanaowatuma andaeni magereza.

Kwa ajili ya tume huru tuko tayari kubakia jela kuliko kubakia majumbani.

Habari ndiyo hiyo.
 
Chadema wanapaswa kutoa uongozi. Wananchi hawawezi kuamka wenyewe spontaneously.

1. Tuwahami wahanga
2. Hii si fursa
3. Kila mtu kwa nafasi yake awajibike kuchangia kwa hali na mali jitihada hizi.
4. Askari wetu wa mstari wa mbele na watunzwe vilivyo
5. Mkakati wa wazi wa kuyajaza Pomoni magereza yao

Si muda mrefu kama uongozi chadema hautupi mwelekeo wajue wana risk Mapinduzi ndani ya chama.

Tulipo haparidhishi:

a) Uko wapi mkakati wa kuwahami wahanga?

b) Uko wapi mkakati wa wazi wenye kuonyesha tunachangia vipi bila kumnufaisha mtu yeyote kama fursa?

c) Yako wapi maridhiano na wengine wote yenye nia ya kusukuma mapambano mbele?

d) Iko wapi ratiba ya kuendelea na makongamano nchi nzima?
Katibu Mkuu wetu yuko kimya sana au huo mkwara wa Mwanza umefanya aufyate sisi tunasema kama hawezi mapambano basi aachie wengine.
 
Katibu Mkuu wetu yuko kimya sana au huo mkwara wa Mwanza umefanya aufyate sisi tunasema kama hawezi mapambano basi aachie wengine.

Hatupaswi kutishwa na vijamaa vyenye ID za vipindi.

Mtu katuma posts 639 kwa miaka 11 how possible?

Hawatutishi hao. Wakawaambie wanaowatuma, bila tume huru we belong to the jails. For which we are happy.
 
Hatupaswi kutishwa na vijamaa vyenye ID za vipindi.

Mtu katuma posts 639 kwa miaka 11 how possible?

Hawatutishi hao. Wakawaambie wanaowatuma, bila tume huru we belong to the jails. For which we are happy.
Tunawasubiri kwa hamu kubwa karibuni uwanjani.
 
Mtu ambaye kajificha ID yake Ni debe tupu. Wewe Ni kama robot au msukule. Waongee watu kama yeriko na wengine tunawajua kuwa sio Robot. Who are you?

Kumbe wewe umeji expose na real ID?!

What is my identification for? I am who I am. Not only, I also know the sentiment has hit you where you should actually be hit.

The rest, you can take it to the bank.

Meet you soon and expect us at our best. We are coming, in millions.
 
Mimi tangu nimsikie huyo "mwamba" wenu akiitaka serikali ifanye chanjo ya corona iwe ya lazima niliizika rasmi chadema katika akili zangu!!!
 
Mimi tangu nimsikie huyo "mwamba" wenu akiitaka serikali ifanye chanjo ya corona iwe ya lazima niliizika rasmi chadema katika akili zangu!!!

Kwani wewe ni mtalaamu mbobezi wa masuala ya afya, kuwa nawe una usemi wowote wa kutiliwa maanani na mtu yeyote kwenye fani hiyo?

Mpuuzi fulani mahali wewe unaupata wapi ujasiri huu wa kutoa maneno mazito haya yaliyo hifadhiwa kwa wabobezi wachache duniani?

"Mimi tangu nimsikie ......."

😂😂😂😂😂!

Haya si ndiyo maajabu ya dunia yenyewe?!

Hiiiiii bagosha!
 
Siyo siri kuwa wanaotaka katiba mpya ni wengi hata ndani ya CCM wamo.

Uzi huu unahusika:

Tathmini: Kesho bora ya Tanzania inategemea uwepo wa Katiba Mpya

Tofauti zilizopo ni ndogo sana. Hakipo chama kimoja kisicho hitaji tume huru. Hakipo chama kimoja kisicho hitaji katiba mpya.

Ndani ya CCM wanaopinga vuguvugu la katiba ni wale walio wanufaika wa moja kwa moja madarakani na si wote.

Matokeo yake tuna watu wengi wanasubiri matunda ili kula, badala ya kushiriki kwenye kupambana ili matunda yapatikane.

Kwenye mapambano tatizo si washiriki bali viongozi.

ANC iliunganisha wote wakiwamo PAC, Inkatha Freedom party nk japo wote wakiwa na mitizamo tofauti.

Chadema haiwezi kupigania hili peke yake bali kuongoza vita hivi na akili kichwani ndiyo lililo la msingi zaidi.
"Kuongoza vita na akili kichwani".
 
"Kuongoza vita na akili kichwani".

Karata zetu za turufu:

"Utayari wetu wa kuozea jela na utayari wetu kufa."

Wajibu mtakatifu kwa Chadema:

"Kuja na mkakati wa mpambano endelevu usioshindwa. Wenye kuhakikisha wahanga wanatunzwa vilivyo."

Wajibu mtakatifu kwa kila mtu:

"Kujitolea kwa hali na mali bila ya yeyote kuona hii kama fursa binafsi ya kiuchumi."
 
Hatuwezi kuchukua Dola kwa kuogopa Virungu vya Polisi muda ndio huu. No Hate NO FEAR.
 
Chadema Hamna tofauti na mzee yusuph mwimbaji be wa taarabu,nyimbo za nini ??? nyie ingieni mitaani mkaidai hiyo katiba utadhani mitaani ndo Kuna watu wanaohusika kuandaa hiyo katiba mnayoitaka.

Ila niwaambieni tu kuwa badala ya kusisitiza serikali ipanue magereza, mngewahimiza wafuasi wenu wapate Bima ya afya kwanza pamoja na pesa za kuendeshea misiba,nawambie kuwa kitakacho wakuta hakika hakijawahi kutokea katika nchi hii.

Msiseme kuwa sikuwaonya.
 
Back
Top Bottom