Pre GE2025 Chadema fanyeni vikao vya ndani kukosoana, kurekebishana, na kusahihishana

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Nikiona hawa Chadema eti kabisa wanataka Urais hawa???? Hawa hawa??? Kabisa Watu wasiokua hata na adabu wala hawajitambui...Wanamtukana Lissu hivi kweli mtu kama Boni anajiita Yai anawezaje kumtukana Lisu alikaribia kifo kwa ajili ya chama chao?? Ni kwanini Mbowe kila akiiona wanachama wengine wanakua Kisiasa anawaanzishia zengwe??? Mimi nadhani Mbowe jiulize kwanza wangapi wameondoka kisa kupishana na wewe??? Sasa umeanza kudeal na Lissu. Kwa Kutumia magenge yako ya watu ambao mkibakia nao humu hawana uwezo kushinda hata kitongoji kimoja.Kuanzia marehemu Chacha Wangwe mpaka wakina Zitto hao wote ukishindwana nao sasa Lissu akiondoka utabakia na wahuni imefika muda mbowe achia Wengine sio lazima wewe tu
 
Nimekusoma mkuu 'proved'.
Husemwa kwamba hata shetani wakati mwingine hujifanya kufanya mazuri ili awanase wagumu kunasika.
Huyu 'Tlaa' kama sikosei ni 'chawa' wa mama na CCM; lakini hapa katoa ushauri mzzuri.

Lakini binafsi naamini haya yanayosemwa na Tundu Lissu hadharani ni yale ambayo tayari yamekwishazungumzwa ndani ya chama chenyewe. Kama ni hivyo sioni athari yoyote.
 

Mgogoro ni mkubwa
Issue ni hivi sugu ana mzigo wa kutosha na mfuasi wa mbowe
Msigwa kalalamika kwa LISU hana hela na ni mfuasi wake na bila kujizuia kaweka hadharani
Kuna kambi ya mbowe na kambi ya LISU
Pambalu( LISU) vs wenje ( mbowe)
Kambi ya mbowe ina hela Chafu
 
Lissu alitumwa na Chadema
 
Acha waparurane ndio demokrasia hiyo mzee.
 
Umepotezwa kijinga sana!
 
ee eeh sikuyajua kumbe ndivyo yalivyo?

si mchezo πŸ’
 
Lissu alitumwa na Chadema
Alitumwa akamkashifu Mwenyekiti na Katibu Mkuu wake?
Umkisikiliza kwa makini kwenye ile video Lissu ameukashifu uongozi wa chama.
Kwamba yeye hapewi pesa za mikutano kwakuwa chama hakina pesa, lakini kuna pesa za kuhonga kwenye chaguzi za ndani za chama.

Na chama kimemuonya asifanye mkutano Iringa mpaka baada ya uchaguzi, lakini amepuuza.

Kwa kifupi hakuna aliyemtuma.
 
Kwamba Chama kimemuonya umeokota wapi huo uongo ?
 
Kwamba Chama kimemuonya umeokota wapi huo uongo ?
Yeye mwenyewe kwenye mkutano wa hadhara mjini Iringa anasema aliambiwa asifanye mkutano Iringa mpaka uchaguzi wa chama utakapomalizika.
(Hakumtaja aliyemzuia)

Lakini Je unadhani mwanachama wa kawaida anaweza kumzuia Makamu Mwenyekiti wa chama kufanya mkutano mahali popote ndani ya Tanzania?

Uzi uko humu umetokana na habari iliyoambatana na video iliyonakiliwa toka mtandao wa X.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…