Pre GE2025 Chadema fanyeni vikao vya ndani kukosoana, kurekebishana, na kusahihishana

Pre GE2025 Chadema fanyeni vikao vya ndani kukosoana, kurekebishana, na kusahihishana

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Naunga mkono hoja, na katika vikao hivyo, wasisitize heshima kwa viongozi, mtu akiishakuwa kiongozi, lazima aheshimiwe. Mfano Mwenyekiti Mbowe, amefanya vikao vya maridhiano na CCM na vikaleta manufaa makubwa Chadema, ikiwemo kupata ruzuku na kukubaliana kitu kinachoitwa kugawana nusu mkate.

Wakati wote wa vikao hivyo Makamo Mwenyekiti yeye alikuwa zake Ubelgiji kwa wazungu wake.

Chadema ilisaidiwa fedha za vikao vya Baraza Kuu, kufanya ziara nje ya nchi, na fedha za nauli kuwarejesha wakimbizi waliokimbilia nje ya nchi akiwemo yeye.

Aliporudi, badala ya kuwa ni mtu wa shukrani, akaanza kubeza maridhiano na kuwatukana viongozi wenzake hadharani kuwa hawana akili!. Msikie Tundu Lissu Hapa, Anauliza Kama Wenzake Wana Akili Kweli! Maridhiano Ayaita Ujinga. Je, Lissu Bado ni Asset or Sasa ni A Liability? hebu msikilize mwenyewe hapa
View: https://youtu.be/Qa59DIQs2yI?si=9oIbwnDXvO-cDzed

Wakati Lissu anaponda maridhiano, angalia JJ Mnyika anasema nini kuhusu maridhiano,
View: https://youtu.be/x5yFws4dc1U

Hivyo naunga mkono hoja, Chadema lazima waitane, wakalishane chini, wasemezane, na kurekebishana.

P.

licha ya mbowe kufanya mazungumzo mazuri sana ya maridhianao na ccm, KM mnyika anaadmit bayana manufaa ya maridhiano jinsi yalivyowanufaisha waandamizi chadema, lakini pia wanasiasa nchini kwa ujumla, lakini makamu mwenyekiti haoni hayo mpaka anawazodoa wenzie hadharani, ati sijui ilikuaje mpaka BAWACHA wakamualika Raisi mkutano wao, bila kujua huo ulikua utashi wa kipekee sana wa kisiasa kuendeleza maridhiano ya dhati, ambayo yalikua yanaenda vizuri sana.....

mi nadhani yanayoendelea chadema yana sababu kadhaa ambazo miongoni mwao ni pamoja na,
kuna kiongozi mzito mwandamiz miongoni mwao anapanga kuhamia kwenda chama kingine kwasababu ya kutokua na uhakika wa kupewa nafasi kutimiza ndoto zake za kuwania nafasi ya juu nchini, lakini na yeye amekusudia mpaka ahakikishe ameimegua chadema kwa kiasi fulani kisha ndipo aondoke...:BASED:
 
Alichofanya Tundu Lisu ni approach sahihi kabisa. Unapoona upuuzi popote unaukemea hadharani ama ndani. Haya mambo ya kupotezeana muda kwenye vikao vya ndani ndio kulea wapuuzi wanaopewa pesa chafu na ccm.
unakemea kitu kunacho kuathiri wewe mwenyewe na familia yako kisiasa. sawa kemea, si ukae ndani basi na wenzie mkemeane vizuri kama familia:pedroP:
 
Hiyo kukosoana huko ndani ndio kumeifanya ccm kimekuwa chama Cha kupuuzi mno, ni bahati tu Bado katiba hii inaipa nafasi ccm kuchezea chaguzi za nchi hii.

Hata wanaotaka kwenda kwenye destinations nyingine wanaruhusiwa kuondoka muda wowote Ili wakawahi nafasi huko waendako. Na kuhusu uchaguzi, hakuna uchaguzi wowote credible hapa nchini wa kufanya mtu aliye serious eti awe anajiandaa. Kinachoendela kwenye chaguzi zetu ni maonyesho ya upuuzi wa mtu mweusi linapokuja suala la uchaguzi. Ingekuwa kura ndio zinatoa mshindi ungekuwa na hoja, lakini sio ule upuuzi unaofanyika kwenye chaguzi zetu.
kwahiyo uchaguzi wa chadema unaoendelea ni credible?:pedroP:

na,
kwani uchaguzi anao ulalamikia na kuukosoa Lisu unasimamiwa na serikali kupitia tume huru ya uchaguzi?

au uchaguzi wa chadema nao ni upuuzi wa mtu mweusi kama ambavyo unadai, japo ni lugha za mihemko za waliofilisika kwa hoja na kisiasa?
 
unakemea kitu kunacho kuathiri wewe mwenyewe na familia yako kisiasa. sawa kemea, si ukae ndani basi na wenzie mkemeane vizuri kama familia:pedroP:
Kwani amekemea hiyo tabia akiwa nje ya nchi? Hapo ujumbe umefika baina ya wapokea fedha chafu, watoa hizo fedha chafu. Ametusaidia sisi tusioingia kwenye hivyo vikao vya ndani kujua kuhusu hizo fedha chafu.
 
kwahiyo uchaguzi wa chadema unaoendelea ni credible?:pedroP:

na,
kwani uchaguzi anao ulalamikia na kuukosoa Lisu unasimamiwa na serikali kupitia tume huru ya uchaguzi?

au uchaguzi wa chadema nao ni upuuzi wa mtu mweusi kama ambavyo unadai, japo ni lugha za mihemko za waliofilisika kwa hoja na kisiasa?
Hauna credibility, ndio maana Lisu ametoka kutujulisha wananchi juu ya uwepo wa hizo fedha chafu.

Uchaguzi unaosimamiwa na serekali huo sio uwepo wa fedha chafu tu, bali huo ndio uchafu halisi.
 
Hauna credibility, ndio maana Lisu ametoka kutujulisha wananchi juu ya uwepo wa hizo fedha chafu.

Uchaguzi unaosimamiwa na serekali huo sio uwepo wa fedha chafu tu, bali huo ndio uchafu halisi.
kwahiyo kuishia kuwajulisha itawasaidia nini bila kuchukua hatua?
 
Kwani amekemea hiyo tabia akiwa nje ya nchi? Hapo ujumbe umefika baina ya wapokea fedha chafu, watoa hizo fedha chafu. Ametusaidia sisi tusioingia kwenye hivyo vikao vya ndani kujua kuhusu hizo fedha chafu.
kwahiyo yeye anafadhiliwa na fedha safi za mabwenyeye wa magharibi, right? :pedroP:

ni vizuri akaeleza pia ameshapewa ngapi na mabwenyeye ya huko ng'ambo maana ni bayana ni fedha nyingi sana,

na ndio maana waliporuhusiwa kufanya mikutano ya hadhara kwa mara ya kwanza kabisa baada ya kuruhusiwa walifanya nae pamoja, na kama kamati kuu walikubaliana nadhani kuishia mwanza kama sio kahama wakati ule....

but kwa ubinafsi na wingi wa fedha alizokua nazo, yeye pekeyake na kundi lake wakataka kuendelea kufanya mkutano huko ngorongoro akakamatwa baada ya kugalagala barabarani, na viongozi waandamizi wenzie wakamchunia:pedroP:
 
Mbowe tukubaliane hutaki wanasiasa wengine wajitokeze na wewe ni mzee unasema ooh umewasaidia kwani wewe ulipokua jela wengine si walikua huko nje wanakusaidia?? Mbowe utaua hicho chama kwa tamaa zako unataka hela huku unataka uonekane ni mpinzani wa kweli lazima kimoja uharibu
Huko nyuma tulisema humu namna ambavyo ndugu Mbowe anang'ang'ania madaraka hata baada uongozi wake kuishiwa mbinu za kuisogeza mbele Chadema lakini tuliishia kutukanwa.
Sasa ni dhahiri tuliyoyaona miaka kadhaa nyuma yanaletwa hadharani.

Hata hivyo pamoja na mapungufu ya Mbowe sikubaliani na kashfa za Tundu Lisu dhidi ya suala la rushwa.
Kama Abdul na mama Abdul wanatoa , basi kuna wanaopokea rushwa hiyo ndani ya Chadema.
Kwa tuhuma zile tuamini kwamba Mbowe na Mnyika wanafaidika na rushwa hizo kwa manufaa yao binafsi.
Haya ni matusi si kwa mama Abdul tu, ni matusi mazito kwa viongozi wenzake ndani ya chama chake.

Chadema kina vikao mbalimbali vya nidhamu, ni vema wakakutane, wachambane huko, wapigane huko, wakija hadharani waheshimiane na jamii itawaheshimu.
Kuja kulopoka hadharani ni kuishiwa hoja na ushawishi.
 
Huko nyuma tulisema humu namna ambavyo ndugu Mbowe anang'ang'ania madaraka hata baada uongozi wake kuishiwa mbinu za kuisogeza mbele Chadema lakini tuliishia kutukanwa.
Sasa ni dhahiri tuliyoyaona miaka kadhaa nyuma yanaletwa hadharani.

Hata hivyo pamoja na mapungufu ya Mbowe sikubaliani na kashfa za Tundu Lisu dhidi ya suala la rushwa.
Kama Abdul na mama Abdul wanatoa , basi kuna wanaopokea rushwa hiyo ndani ya Chadema.
Kwa tuhuma zile tuamini kwamba Mbowe na Mnyika wanafaidika na rushwa hizo kwa manufaa yao binafsi.
Haya ni matusi si kwa mama Abdul tu, ni matusi mazito kwa viongozi wenzake ndani ya chama chake.

Chadema kina vikao mbalimbali vya nidhamu, ni vema wakakutane, wachambane huko, wapigane huko, wakija hadharani waheshimiane na jamii itawaheshimu.
Kuja kulopoka hadharani ni kuishiwa hoja na ushawishi.
Lisu ni mwanaharakati, siyo Statesman.

Ndio maana yule malaika wa kuzima alishindwa kumvumilia na kumtumia kikosi cha wauwaji, kumvumilia Lisu inataka moyo sana.
 
Huenda kweli usemacho, lakini usisahau wao ni binadamu, na kama walivyo binadamu wote hutokea wakati kuna kuhitilafiana.
Hivyo zikitokea hitilafu za namna hiyo wamalize kwenye vikao vya ndani.
Kauli za Tundu Lissu mjini Iringa zimeacha doa kwenye ulingo wa siasa.
Kwa level yake haikupendeza kuwatuhumu viongozi wenzake mbele ya halaiki.
Lissu ana tamaa ya madaraka mno halafu ana dharau ila hana maisha marefu kwenye siasa bora kuishi na dr Silaa lakini siyo Tundu lissu.Yeye anafikiri ni msomi mwenye uwezo pekee,hana diplomasia,hekima,busara na hoja za kuleta maelewano ndani ya chama chake na Taifa zima. Anatumika nje,chadema wachukue tahadhari naye siyo mtu mzuri
 
Lissu ana tamaa ya madaraka mno halafu ana dharau ila hana maisha marefu kwenye siasa bora kuishi na dr Silaa lakini siyo Tundu lissu.Yeye anafikiri ni msomi mwenye uwezo pekee,hana diplomasia,hekima,busara na hoja za kuleta maelewano ndani ya chama chake na Taifa zima. Anatumika nje,chadema wachukue tahadhari naye siyo mtu mzuri
Tundu Lisu ni dikteta.
Watanzania watafanya kosa kubwa sana kuchagua dikteta wa mfano wake.
Mbowe ingawa anang'ang'ania madaraka lakini hana dharau wala majivuno kama Lisu.
 
Back
Top Bottom