Uchaguzi 2020 CHADEMA inakuwaje mtu anagombea Kiti cha Ubunge wa Jimbo na Viti Maalumu kwa mpigo na anashinda vyote? Kwanini asigombee moja?

Walijaribu huku na kule wasipoteze mkate wao kirahisi, ila aliepata nafasi ya pili ndie atapewa hiyo nafasi ya Viti Maalum, sioni kama kuna ubaya hapo.
Hivi hii ina maana gani sasa ya kupoteza muda kufanya uchaguzi?
 
Wacha ujinga mwamba, huko kwingine kukoje? Kwani CCM hawagombei vyote? Acha ujinga aisee huo ni uchaguzi na mtu yuko huru kuchagua vyote. Unafikri uchaguzi wa jimbo ni rahisi unavyofikria?
 
Je, kanuni za vyama zinasemaje? Kanuni za Uchaguzi zinasemaje? Kuna Sheria imekiukwa? Kuna kanuni imekiukwa? Kama hakuna kuvunjwa kwa kanuni au sheria basi usilalamikie Chadema wala CCM lalamikia kanuni na Sheria zinazotoa loophole hiyo

Hizo sheria na kanuni zinazoruhusu hayo tusipozikemea zitaendelea. Hivyo hapa ninafanya kitendo sahihi kuhakikisha kuwa sheria zisizofaa zinaondolewa.
 
Inaweza kuwa kweli,kama walifanya mikusanyiko isiyohalali unategemea nini?

Hakuna mikusanyiko isiyo halali, cdm sio chama cha kigaidi, mikutano yake kinafanya mchana kweupe, kila mtu akiwaona. Kinachofanyika ni matumizi mabaya ya madaraka, ili kuwatisha watu kutoshiriki mikutano ya cdm, kisha zipigwe propaganda za kizee kuwa cdm haikubaliki.
 
big up men, hilo jibu limefunga uzi mkuu! ni uroho wa madaraka na kutokujiamini!
 
Je, kanuni za vyama zinasemaje? Kanuni za Uchaguzi zinasemaje? Kuna Sheria imekiukwa? Kuna kanuni imekiukwa? Kama hakuna kuvunjwa kwa kanuni au sheria basi usilalamikie Chadema wala CCM lalamikia kanuni na Sheria zinazotoa loophole hiyo
Hakuna kanuni yoyote iliyovunjwa ndio maana hayo mambo yapo, kama wakiona kuna tatizo labda ndio wakabadilishe kanuni.
 
Kuna watu chadema viti maalumu ni kama walizaliwa navyo hata ile maana ya kuwapa uzoefu imepotea
 
Kwahiyo mama salma yy kajiamini maana naona kachukua fomu anagombania ubunge na kwenye viti maalum pia kagombania
Huyo ndio hajiamini zaidi level yake ya first lady mpaka kwenye hayo matakataka ni kukosa washaur tu bora angefungua darasa!
 
Mikusanyiko halali lazima iwe na kibali cha Officer commanding division. Zaidi ya hapo ni kinyume cha sheria. Na Chadema huwa wanakiuka kwa kujifanya wababe.
 
Mbona wewe unaomba kazi makampuni matano-mia moja kwa wakati mmoja?
 
Mikusanyiko halali lazima iwe na kibali cha Officer commanding division. Zaidi ya hapo ni kinyume cha sheria. Na Chadema huwa wanakiuka kwa kujifanya wababe.

Ndio hapo ninapokuambia matumizi mabaya ya madaraka yanapoanzia. Cdm huwa wanafuata taratibu zote, ila hao polisi huwa wanapewa amri za kuwakatalia kimakusudi, kwa lengo la kuwadhoofisha. Hilo limekuwa likifanyika mara zote kwa nia ovu. Na kwakuwa cdm huwa wanajua kuwa wanafanyiwa Katazo kama hujuma za kisiasa, hawana jinsi zaidi ya kukutana kwa lazima.

Kimsingi haki haiombwi, na iwapo cdm wataendelea kusubiri hao viongozi wa polisi wanaojivunia kuwa wanaccm hadharani, kinyume cha maadili ya kazi, hawatakaa wafanye mikutano. Kwa sasa ccm inategemea vyombo vya dola kwa asilimia mia moja kufanya siasa, na vyombo vya dola vinajiona vina haki ya kuitetea ccm, hiyo ndio inayopelekea cdm kunyimwa haki ya kukutana.
 
Kwa nini hao Ocd's wawakatalie bila sababu? Hizo amri toka juu anazitoa nani? Chadema wana nini kipya mpaka amri zitoke juu kuwazuia? Maana hawana mvuto wala nguvu kama 2010-2015, na walipewa vibali vya mikutano iweje hii leo ambapo wameanguka kifo cha mende wanyimwe vibali.
 

Unaongea nini ww? Hiyo ambayo unasema hawana nguvu imetokana na kunyimwa vibali ya kufanya mikutano. Kwahiyo kwakuwa walikuwa wanapewa vibali huko nyuma, sasa hivi hawawezi kunyimwa, tena kwa sababu ya mikakati ya kisiasa? Hebu kaa kimya maana huna jipya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…