Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
Sijui kama CDM wanajifunza ! hivi hii ni kauli ya Mbowe au ya chama?Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe amesema chama chake kinaunga mkono rasimu ya Katiba mpya iliyotolewa na Jaji Joseph Warioba.
Mwenyekiti huyo alikuwa akihutubia maelfu kwa maelfu ya wananchi wa jiji la Mbeya katika mkutano wa kumnadi mgombea udiwani wa kata ya Iyela kwa tiketi ya Chadema Charles Nkelwa.
Kiongozi huyo wa upinzani bungeni amesema sababu kubwa ya kuunga mkono rasimu hiyo ni kwamba mambo mengi yaliyoorodheshwai na chama hicho yamekubaliwa.
Mbowe amesema jambo kubwa lililofanyiwa kazi ni kurejeshwa kwa serikali ya Tanganyika.Mbowe amesema amesikitika kuona baadhi ya wanaCCM wakiipinga serikali ya Tanganyika na kung'ang'ania serikali mbili na kudai watu hao ni wanafiki wanaopaswa kupuuzwa na wananchi.
Kauli ya Mbowe imekuja wakati ambapo mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema Dr Kitila Mkumbo alinukuliwa kusema rasimu mpya ya Katiba iliyotolewa na Warioba ni bora mara mia mbili akilinganisha na katiba ya sasa.
Mara baada ya mkutano huo maelfu ya watu walitanda barabarani kumsindikiza kiongozi huyo anayependwa sana jijini Mbeya.
Source:Mwananchi Jumatatu.
Ile ya Kitila ni yake, hii ya Mbowe je? Kwanini kusiwe na taarifa ya chama kuhusu msimamo wa Chadema
Ina maana wao wamekubali kila kitu, kama sivyo kipi wanadhani kiboreshwe kipi kiachwe n.k. na kwanini wanadhani msimamo wao umekidhiwa katika katiba mpya.
Je, tatizo la katiba ililikuwa kurudi kwa Tanganyika? Mambo mangapi ni muhimu sana katika katiba.
Wameridhika na tume ya uchaguzi, wameridhika na mfumo wa mahakama?
Nadhani walitakiwa watoe statement ya chama na si kila mmoja kivyake. Hivi akiibuka mwingine akasema anapinga, je atakuwa anapingana na chama, mwenyekiti au atakuwa sahihi.