Pre GE2025 CHADEMA Iringa wamkana Mwenyekiti Mungai kauli ya kumuunga mkono Mbowe

Pre GE2025 CHADEMA Iringa wamkana Mwenyekiti Mungai kauli ya kumuunga mkono Mbowe

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu,

Badamu batachuruzika safari hii!

=====


Wajumbe wa Mkutano Mkuu CHADEMA kutoka Mkoa wa Iringa wakiongozwa na makatibu kutoka jimbo la Kilolo, Iringa mjini na wilaya ya Iringa pamoja na viongozi wengine wameibuka kupinga kauli ya mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Iringa, William Mungai aliyeueleza umma kuwa mkoa huo unamtaka Freeman Mbowe kwenye nafasi ya Mwenyekiti wa chama Taifa.

Ikumbukwe William Mungai pamoja na wenyeviti wa CHADEMA kutoka Mikoa 21 nchini, Desemba 18, 2024 walikwenda nyumbani kwa Mbowe(Dar Es Salaam) kumuomba agombee.

Pia soma: Kuelekea 2025 - Mwenyekiti CHADEMA Iringa: Mbowe ni role model, asiogope mtu yeyote hata we nje ya nchi

Ujumbe wa wenyeviti hao ulisomwa na Mungai ambapo kauli yake imepingwa vikali na makatibu hao Disemba 20, 2024 wakisisitiza kauli aliyoitoa ni maoni yake binafsi na sio wajumbe wa mkutano Mkuu wa CHADEMA Iringa.

David Mfugwa katibu wa CHADEMA, Wilaya ya Kilolo kwa niaba ya mwenzake amesema "Mungai ametoa kauli ambayo yeye anasema ni msimamo wetu kitu ambacho sio kweli hatukuwahi kukubaliana kwa kauli moja ya kumuunga mkono Mbowe sisi tunasimama na Tundu Lissu kwani tunaamini anatosha kukiongoza chama chetu"
 
CHADEMA Iringa Mwenyekiti Mungai na katibu wa CHADEMA, Wilaya ya Kilolo ni nani mwenye mamlaka huko iringa Ndani ya Chadema?
Katibu anakataa kwamba hawajakubaliana juu ya hilo na huo sio msimamo wa kamati kuu ni msimamo wa Mungai sijui ni msimamo wake kama mwenyekiti au ni binafsi.
Kama alisema CDM Iringa maana yake vikao vilipaswa kuamua hilo sio yeye binafsi.
Kama aliamua mwenyekiti binafsi kumuunga mkono Mbowe au Lissu unabaki uamuzi binafsi sio wa wajumbe wote na wanapopiga kura watapiga binafsi na mwenyekiti wa mkoa atakua na kura moja tu.
 
Katibu anakataa kwamba hawajakubaliana juu ya hilo na huo sio msimamo wa kamati kuu ni msimamo wa Mungai sijui ni msimamo wake kama mwenyekiti au ni binafsi.
Kama alisema CDM Iringa maana yake vikao vilipaswa kuamua hilo sio yeye binafsi.
Kama aliamua mwenyekiti binafsi kumuunga mkono Mbowe au Lissu unabaki uamuzi binafsi sio wa wajumbe wote na wanapopiga kura watapiga binafsi na mwenyekiti wa mkoa atakua na kura moja tu.
Kwa kawaida! Kauli ya mwenyekiti wa chama Mkoa ni kauli ya Chama!
 
Wote walioshangilia kifo cha Magufuli laana iwatafune
 
Kwa kawaida! Kauli ya mwenyekiti wa chama Mkoa ni kauli ya Chama!
Uchaguzi ni kupiga kura sio kauli ya mwenyekiti wa chama.
Matamko mengine sawa ila uchaguzi una mpaka kampeni sasa ukimshawishi mwenyekiti peke yake na wajumbe wengine haujawashawishi kura yake moja sio kura ya wajumbe wa mkoa kila mmoja anapiga mwenyewe ilipaswa mwenyekiti azungumze yeye na nani waliokubaliana kumuunga mkono FAM.
 
Katibu anakataa kwamba hawajakubaliana juu ya hilo na huo sio msimamo wa kamati kuu ni msimamo wa Mungai sijui ni msimamo wake kama mwenyekiti au ni binafsi.
Kama alisema CDM Iringa maana yake vikao vilipaswa kuamua hilo sio yeye binafsi.
Kama aliamua mwenyekiti binafsi kumuunga mkono Mbowe au Lissu unabaki uamuzi binafsi sio wa wajumbe wote na wanapopiga kura watapiga binafsi na mwenyekiti wa mkoa atakua na kura moja tu.
Na kikao gani kilifanyika CHADEMA Iringa na kufikia maamuzi ya kumkubali Lissu? Nani alikuwa Mwenyekiti wa huo mkutano? Hawa vijana wanatakiwa wajifunze kukaa kimya.

Amandla...
 
Back
Top Bottom