CHADEMA: Kikosi Kazi kiliundwa ili kuchelewesha mchakato wa Katiba Mpya

CHADEMA: Kikosi Kazi kiliundwa ili kuchelewesha mchakato wa Katiba Mpya

Ni wivu tu[emoji23][emoji23][emoji23][emoji16][emoji16]
 
Cha msingi hakuna Tena watu wasiojulikana..,tujifunze kuona unafuu katika maisha haya..,Lile kundi lilikuwa hatari Sana mpaka watu tuliogopa kuweka maoni yetu katika mitandao ya kijamii..,hakuna serikali iliyokamilika asilimia mia Moja.., tujifunze kuwa na shukrani

Binafsi naona wale wanaoendelea kuisakama serikali ya rais Samia hata kwa makosa madogomadogo tu , wanasahau shida na mateso tuliyopewa na yule fashisti dikteta mwendakuzimu wa chato..,mungu katuokoa na kutuondolea Lile dubwana lakini lawama haziishii..,tuna kuwa kama Wana wa islaer katika safari ya nchi ya ahadi[emoji848]

Sent from my Infinix X660B using JamiiForums mobile app
Ungekua na akili tungekushangaa
 
Pia Katibu Mkuu Mnyika ameitaka serikali kuweka wazi gharama ambazo kikosi kazi hicho kimetumia ili kukamilisha kazi yake .

Hela za umma zinapaswa kufahamika jinsi zinavyotumika
Hili halina uzito; lenye uzito na ambalo tayari Samia shaliweka kapuni ni "ruhusa"? ya kufanya mikutano.

Ni sheria zipi zinazohitaji marekebisho ndipo vyama vianze kufanya mikutano? Hizi si ndiyo mbinu za ucheleweshaji tunazozizungumzia kaila mara humu?
 
Kama haitoshi vile Mpokea taarifa anasema wataunda tume nyingine ndogo kushirikiana na baadhi ya waliokuwepo humo kuona wapi wafanye kazi. Huu ni upigaji wa Hela za walipa Kodi! Washauri wa mheshimiwa mwambieni hii sio sawa! Nini kinachoogopesha kutoifuata rasimu ya Warioba ambayo imechukua maoni nchi mzima na Kwa weledi na yeye mwenyewe akiwa mojawapo.
Aiiiseeee!

"Upigaji wa hela za walipa kodi", ni jambo moja, pengine lisilo na uzito zaidi ya jambo zito zaidi..., la kucheza danadana na kupoteza muda, tena kwa maksudi mazima!

Mama wala hapepesi macho, wala kuona aibu kwa hadaa za aina hii anazozitoa mbele za watu wenye akili vichwani mwao.
 
Matumizi mabaya kabisa ya fedha, haiwezekani unaunda kikosi kazi kwa ajili ya kukuletea mapendekezo ya nini kifanyike kuhusu mambo kadhaa, halafu ukishapewa mapendekezo unasema tena mtaenda kupitia sheria [mikutano ya siasa].

Matokeo yake wamepoteza pesa kwenye kikosi kazi, na wataenda kupoteza pesa nyingine kwenye kupitia sheria.
 
giphy.gif
Hakika huyu ni Crimea , Idugunde , Etwege na wenzao wana Chama Cha Mazuzu.
 
Duh!! Sasa John John Mnyika amekuwa CAG anafanya value-for-money audit? Leo anakishambuliaje KK huku CHADEMA walikataa kujiunga nacho wala kutoa maoni? Na anasifia Tume ya Warioba, why, si CHADEMA walitoka nje na kina mariasarungi? Manati ni pale anapotaka Bunge hili tulikwepe, eti lilikuwa ni Uchafuzi, na huku anamtaka Rais aanzishe mchakato. What a collection of rats, to be sure!

Umeelewa alichozungumza J.J. Mnyika!!?!
Anasema kulikuwa na umuhimu gani wa kikosi kazi kukusanya maoni wakati Tume ya Warioba ilishamaliza kila kitu na kufikia hatua ya kuwa na Bunge la Katiba!!??

Kwani CDM & Co. walitoka nnje ya Bunge la Katiba kwa sababu ya Tume ya Warioba au kwa sababu ya sarakasi za mule bungeni!!??

Jitahidi uwe na taarifa sahihi na uzielewe kabla ya kuandika upotoshaji.
 
Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika ameitaka Serikali kuweka wazi gharama ambazo kikosi kazi kimetumia huku akisema hakukuwa na haja ya kuundwa kwa kikosi hicho kwa sababu kazi ya kutafuta maoni ya wananchi ilifanywa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyoongozwa na Jaji Joseph Warioba.

Mnyika ameeleza hayo leo Jumamosi Oktoba 22, 2022 Jijini Dar es Salaam ikiwa ni siku moja baada ya kikosi kazi cha kuratibu maoni ya wananchi kuhusu demokrasia ya vyama vingi, kukabidhi ripoti yake kwa Rais Samia Suluhu Hassan.

Katika ripoti hiyo, kikosi kazi kimetoa mapendekezo 18 kwa Serikali ikiwemo kuruhusiwa kwa mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa, mchakato wa katiba mpya kuendelezwa na ruzuku kwa vyama vyote vya siasa.

Hata hivyo, Rais Samia alitoa angalizo kwamba mapendekezo hayo siyo amri kwa Serikali kuyatekeleza. Alisisitiza kwamba wameyapokea na watayafanyia kazi hasa yale ambayo hayahusishi mabadiliko ya sheria.

Akizungumza na vyombo vya habari, Mnyika amesema kikosi kazi hicho kiliundwa ili kuchelewesha mchakato wa katiba mpya na kwamba hilo limejidhihirisha kwenye mapendekezo waliyoyatoa.

Amesema maoni ya wananchi yalikusanywa na Tume ya Warioba, hivyo hakukuwa na haja ya kuundwa kwa kikosi kazi, bali wangerejea kwenye kitabu cha maoni ya wananchi kilichoandaliwa na Tume ya Warioba.

"Kuundwa kwa kikosi kazi ni matumizi mabaya ya fedha za Watanzania. Tunaitaka Serikali itoke hadharani ituambie kikosi kazi kimetumia fedha kiasi gani," amesema Mnyika.

Amesema walikuwa wakipigania kuruhusiwa mikutano ya hadhara lakini baada ya kuundwa kwa kikosi kazi waliamua kukipa muda ili waone matokeo yake, lakini wameshangazwa na kauli ya Rais Samia wakati akijibu hoja hiyo akisema kuna haja ya kufanyia mabadiliko sheria na kanuni kabla mikutano haijaruhusiwa.

"Tunaitaka Serikali iruhusu mikutano ya hadhara bila kusubiri mabadiliko ya Sheria ya Vyama vya Siasa, bila kusubiri mabadiliko ya kanuni za mwaka 2019, bila kusubiri mabadiliko ya Sheria ya Jeshi la Polisi.

"Zuio la mikutano ya hadhara ni haramu kwa sababu liko kinyume na Katiba ya nchi, liko kinyume na Sheria ya Vyama vya Siasa," amesema Mnyika.

Amesema wameshangazwa na kauli ya Rais Samia kwamba mapendekezo ya kikosi kazi siyo amri kwa Serikali, huku akisisitiza kwamba wanataka kujua gharama zilizotumiwa na kikosi kazi.

Mwananchi
Bila watu kufa hakuna kitakachofanyika. Afrika lazima damu, tena nyingi imwagike , jumuiya ya kimataifa iingilie ndiyo haki itatendeka. haya si rahisi kuyasikiliza CCM. But at present kupiga kelele ni muhimu sana maana ndiyo silaha iliyopo sasa ingawa ni sil;aha dhaifu! Kenya wako walivyo baada ya kufa wengi......
 
Hawa ni maproffessors wa majalalani,eti vyama vya siasa vipate ruzuku Sawa this is craze, chama Chenye 0 MP kipate ruzuku Sawa na chama chenye 50MPs,hawa wanatuchezea sana maana kuna hatari ya kufumuka kwa utitiri wa vyama ili wapate free ruzuku, kupata ruzuku political parties lazima watoe jasho, nilitegemea wangekuja na azimio la kuvitaka vyama vya siasa kutangaza hadharani vyanzo vyao vya mapato, Nina wasiwasi ccm inatumia fedha za serikali kuendesha chama
 
Baada ya kusikiliza press conference ya Katiibu Mkuu Chadema Hon. John Mnyika, nimeconclude kuwa ripoti ya the so called Prof Mkandara Ni another Professorial rubbish output of the year 2022.

Mungu wa mbinguni tuepushe na Rubbish Professors with their Professorial rubbish outputs.maana wanaongezeka kila uchao.
 
Baada ya kusikiliza press conference ya Katiibu Miuu Chadema Hon. John Mnyika, nimeconclude kuwa ripoti ya the so called Prof Mkandara Ni another Professorial rubbish output of the year 2022.

Mungu wa mbinguni tuepushe na Rubbish Professors with their Professorial rubbish outputs.maana wanaongezeka kila uchao.
Tusubiri mwaka uishe,huenda hii ikazidiwa na rubish nyingine ya funga mwaka
 
Back
Top Bottom