CHADEMA kubalini matokeo na m-survive, or shupazeni shingo. You go to hell 6ft under Hao Makamanda 19 ni mashujaa, kuendelea Ubunge wao

Yaani Mccm ageuke kuwa mshauri wa Chama pinzani CDM? Paskali nilitegemea ukiandika hoja zenye mantiki kukemea u dhalimu unaopindisha katiba na sheria za nchi hii.

Lakini umekua kimya ukiandika porojo and most of the very writing here is to point out on CDM..wengi humu hatuna vyama ila tungependa future nzuri ya Taifa Letu. Kuangalia leo Bila kufocus future ya vizazi vijavyo ni uhayawani wa waziwazi kabsa.
 
Swali moja rahisi sana kwako Paskali. CHADEMA ikifa, Watanzania na taifa kwa ujumla tutapata hasara gani? Unaamini NI LAZIMA CHADEMA iendelee kuwepo (exist)?

Maelezo yote hayo marefu sana uliyotoa na ambayo umekuwa ukiyatoa zaidi ya mwaka kuhusu CHADEMA, yanadhihirisha kuwa kwa mazingira ya kisiasa tuliyo nayo Tanzania, HAIWEZEKANI tuwe na mfumo wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini ambao ni BONA FIDE GENUINE.

Ukweli ni kuwa gharama ya uwepo wa CHADEMA hapa Tanzania ni kubwa sana na inazidi kutisha kadiri miaka inavyoendelea. Zaidi ya matumizi makubwa ya hazina ya taifa, watu wanauawa, kutiwa vilema, kupotea, kuteswa na vyombo vya dola na wengine kuharibiwa shughuli zao za kiuchumi. Halafu ikitokea CHADEMA ikawa active sana kisiasa, kampeni ya “kulinda amani ya taifa” huongezeka sana. Viongozi wa dini, jamii, kimila ni kuendesha ibada mfululizo dhidi ya pepo la vurugu, ugaidi na tishio la kutoweka amani ya taifa! TENSION inaongezeka, vitisho vinatolewa muda wote na viongozi wa serikali na vyombo vya dola kwenye media. Sonono zinazidi mitaani. WHAT FOR?

Hivyo, hii kampeni yako (RELENTLESS) ya “kuiokoa” CHADEMA na kifo ina nia njema na Watanzania kweli? Au unataka kuwasaidia viongozi akina Mbowe at the expense of the people?

Au wewe una maslahi binafsi na uwepo tu wa CHADEMA haijalishi kivipi.

Halafu, VERY CURIOUSLY, siioni juhudi yako ya dhati kuwaasa wenye dhamana ya kutengeneza mazingira sahihi ya demokrasia ya vyama vingi Tanzania ili kuwezesha vyama kama CHADEMA kuwepo na kufanya shughuli zake kwa ufanisi. Hapo ungeeleweka badala ya kupania kwa makala kadhaa zilizojaa jazba nyingi kutaka CHADEMA IWEPO na ikubaliane na dola tu hata katika mazingira hatarishi kiasi gani!

WHAT’S YOUR REAL MOTIVE?
 
Mi paragraph ya kwanza tu aliyomalizia kwa kusema uchaguzi ulikuwa huru na haki, ndipo hapo sikutaka kuendelea kuisoma makala yake. Bora angesema "unaodhaniwa", au "unaodaiwa" , au "unaonasibishwa" kuwa ulikuwa huru na haki. Sasa yeye ka-confirm kabisa!!! Nikaachana nayo... Nikapita vile.
 
Chadema kwa kuwafukuza covid 19 imeimarika zaidi kuliko wangesalia ndani ya chama kwani ingefariki kwa kasi ya Hatari na kuwa kama UDP DP TLP NCCR na CUF ya ya Lipumba
 
Hayo matrilioni ya mabeberu mtayala kwa macho tu. Mlionywa sana mkashupaza shingo mkaiba kura kwa nia ya kuufuta upinzani sasa mnawaona wa maana hadi mnajivua nguo kuwabembeleza waingie bungeni, matamanio yenu ya kuufuta upinzani ndiyo yanawatokea puani. Hao mabeberu mnaotaka kuwaaminisha kuwa hili ni Bunge la vyama vingi wanauona huu Utopolo mnaonfanya.
 
Swali moja rahisi sana kwako Paskali. CHADEMA ikifa, Watanzania na taifa kwa ujumla tutapata hasara gani? Unaamini NI LAZIMA CHADEMA iendelee kuwepo (exist)?...
Mkuu Drifter, kwanza asante kwa mchango wako, very objective, kiukweli tangu nimepandisha uzi huu, wewe ndio mtu wa kwanza kunielewa, kwasababu, kiukweli kabisa, hii jf ya sasa, tuna watu wachache sana, wenye kuweza kusoma bandiko na kisha kujiuliza what is the motive behind.

Chama cha Mapinduzi ni chama cha ukweli na haki, kiliasisiwa na Mwalimu Nyerere, mpenda haki na mtenda haki. Baada ya Mwalimu, CCM ilipitia mageuzi na kuishiwa kuhodhiwa na wenye fedha, hivyo kuzalisha kada kubwa ya makada wa CCM ambao ni makada maslahi, na kwenye uchaguzi, wanakuwa wako tayari kutumia mbinu zozote kushinda uchaguzi. JPM alipoingia, amekuja kuibadili CCM kuirudisha ile CCM ya Nyerere. Sasa ndani ya makada wa CCM, kuna makada wa aina mbili, kuna "CCM Die Hard", hawa ndio wanaotaka kuhakikisha CCM inaupondaponda upinzani na kushinda kwa asilimia 99.9% kwa kutumia mbinu zozote.

Tupo sisi makada "Modern CCM" ambao kutokana na good track ya kazi nzuri ya JPM, CCM innashinda kwa mshindi mzuri safi na clear victory, kushinda kwa haki bila kufanya figisu figisu zozote.

Kwa vile Bunge letu ni Bunge la vyama vingi, mimi naamini kuna baadhi ya wana CCM very genuine, hakupenda kuona baadhi ya wapinzani wakishindwa akiwemo mtu kama Zitto!. Lakini kutokana na wapinzani kukataliwa na wananchi, ili Bunge lichangamke, zile kamati 2 za oversight committee, PAC na LAAC, lazima ziongozwe na wabunge wa upinzania ambao ni vichwa vya ukweli, kwenye hao wabunge wote sijaona watu wa kalibre hiyo ndio maana kila siku, tunamuomba Mwenyekiti wetu, JPM, katika zile nafasi zake 10, awateua wapinzani 4, Zitto, JJ Mnyika, Mbatia na kale kabinti Queen Sendiga.

Ili CCM itawale vizuri inahitaji Upinzani makini, ndio maana kila uchao, naibalasa Chadema humu na ACT Zanzibar, waache ujinga wa kususa. Ili kusasa kwa akili ni kususa kama kwa kususa huko utaachieve something, lakini kususa tuu for the sake of kususa, huku you won't achieve anything huu ni ujinga!.

Karibu tena.

P
 
Wanabodi,

Kila nipatapo fursa, huja na makala zangu za kwa maslahi ya taifa, japo mimi ni kada wa chama cha siasa na sio Chadema, ukada wangu, haunizuii kutoa ushauri kwa Chama chochote kukisaidia...

Kama unajua kutoa ushauri mzuri hivi kwa vyama vya siasa, imekuwaje biashara yako sasa hivi inayumba? Aliyeyumbisha biashara yako ndio anayelazimisha kuivuruga CHADEMA.

Ni vyema ungetumia hii nguvu unayolazimisha kuishauri cdm kwa matarajio yako nyuma ya pazia, kujua ni kwanini biashara yako imekwama kwa sasa.

Na ni vyema kujiuliza kwanini ulipata kura moja huku ukiwa na uwezo wa kuishauri CHADEMA. Hii poroji yako ni sawa na mtu hana maji ya kunywa, lakini anaenda kumshauri mwenye shamba amwagilie mboga zake ili zisinyauke.
 
Umeshauri mabadiliko ya katiba katika nyanja Hizi, Ila nadhani umezingatia yanayoendelea Chadema. lakini je umejiridhisha Kama mabadiliko haya yatakuwa na manufaa kwa chama chako? Kama hayana manufaa usitegemee Kama chama chako kitakuwa tayari kufanya mabadiliko hayo kwa sababu wao ndo wanufaika wakubwa wa sheria Hizi dhaifu
 
Kuhusu hoja ya kufutwa ubunge. nani ataitaarifu ofisi ya spika kuhusu kuvuliwa uanachama wa wabunge hao 19?Ikumbukwe Chadema haikuwahi kuwasilisha majina NEC. Hivyo Chadema kuitaarifu ofisi ya Spika kuhusu maamuzi ya Chama ni kuhalalisha barau iliyowatambua kuteuliwa. Kesi hii imeangukia kwenye kesi za kupinga matokeo ya uchaguzi na inatakiwa kuamuliwa mahakamani.
 
Hopples kabsa yaan hapa naelewa sasa tofauti ya kusomea sheria na kuwa msomi wa sheria, yaani wewe msomea sheria unahangaika na kuteseka na cdm really? Hopples
 
Tupo tayari chama kife lakini hatutakubali kutumika kama muhuri wa kuhalalisha mateso kwa Watanzania. DEMOKRASIA NI MUHIMU KULIKO UHAI WA CHADEMA, TANZANIA NA WATANZANIA NI MUHIMU KULIKO UHAI WA CHADEMA. Kikubwa zaidi hatusikilizi ushauri wa WANAFKI.
I have never seen you physically ,paschal! However, by the virtue of understanding, there is no doubt that,you are Quite understanding and bright.
Where are you being quagmired paschal, just to not understand a very simple thing like this?
Halima and her colleagues definitely have had gone astray to norms, regulations , and also their party constitution and laws of the country as well.
And if you really know how to read between the lines, you could have seen how repentant and apologetic Halima was when briefing the press.
You couldn't have seen her propagating for the validity of their parliamentary seats. You know why? She is diplomatically regretting, since she has had discerned the mistakes they did.
I support your brilliance and intellectual capacity. Don't let yourself down Paschal.
Come back to your senses and become realistic again as you used to be.
Bless you.
 
Mbona unatutishia watu.eti "hawatanielewa".huu uchaguzi wa 2020 na uchaguzi wa serikali za mitaa hakuna correlation??hivi umewahi jiuliza hili???
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…