Uchaguzi 2020 CHADEMA kufungua kesi kwa ajili ya kumtafuta aliyesaini Barua ya NEC inayohusu majina ya Viti Maalum

Uchaguzi 2020 CHADEMA kufungua kesi kwa ajili ya kumtafuta aliyesaini Barua ya NEC inayohusu majina ya Viti Maalum

Dar es Salaam. CHADEMA imeanza kutumia nguvu ya mahakama kupinga mchakato wa uteuzi wa wabunge 19 wa viti maalumu na mtu aliyesaini fomu zao kwa nafasi ya katibu mkuu.

Chama hicho kilistahili kupata wabunge wa viti maalum kutokana na kupata idadi ya kura za wabunge inayozidi asilimia tano, lakini kinadai hakukuwa na kikao kilichopitisha majina ya wanachama na kupeleka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kwa ajili ya uteuzi.

Lakini Noveemba 24, makada 19 walijitokeza viwanja vya Bunge na kuapishwa kuwa wabunge wa viti maalumu katika utaratibu mpya unaomruhusu Spika kufanya kazi hiyo bila ya kuwepo na mkutano wa chombo hicho cha kutunga sheria, kitendo kilichosababisha Kamati Kuu ya CHADEMA iliyokutana Novemba 27 kuamua kuwavua uanachama.

Pamoja na kustahili viti hivyo, CHADEMA ilishatangaza kutotambua matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, ikidai kwamba uchaguzi huo ulitawaliwa na ukiukwaji wa sheria na taratibu.

Mkurugenzi wa itikadi, uenezi, mawasiliano na mambo ya nje wa CHADEMA, John Mrema alisema mchakato huo unaendelea na tayari katibu mkuu wa chama hicho, John Mnyika ameiandikia barua NEC.

Katika barua hiyo kwa NEC, alisema CHADEMA inataka kupatiwa nakala ya barua iliyowasilisha majina pamoja na fomu namba 8D ambazo katibu mkuu anatakiwa kujaza ili ijulikane aliyeijaza na hivyo aunganishwe kwenye kesi hiyo.

Mwananchi
Majibu kutoka tume 2021 majibu ya forgery kutoka polisi 2022 kama ikitokea ikiwa kesi .kesi itaendelea mahakamani .hukumu 2025 ,my chadema msipoteze muda bure .tumieni maarifa .wacha wabunge wapige kazi .Na anzeni kudai katiba mpya ile ile iliopitishwa na ccm .ipigiwe kura angalau inayo tume huru na inampunguzia Rais madaraka,
 
Ni hatua nzuri,hiki ndio chama pekee makini cha upinzani kilichobaki Tanzania kwa sasa
Chama kipi mkuu, Unajua Tundu Lissu alifanya nini baada ya kufika belgium kwenye interview yake ya mwanzo? "Alimtaka Rais Magufuli ashirikiane na upinzani kuunda umoja- Sasa kwa kauli hii TL amemtambua Rais Magufuli ata akina Halima mdee hawajaenda bungeni kuapa. Ninachojifunza kwenye mambo haya wanasiasa ni watu wanafiki sana, zaidi ya sana.

Wao siku zote huwatumia wananchi kutekeleza malengo yao, Lissu alipokuwa akiutaka urais alipanda Ndege toka Belgium hadi Tanzania na akapokewa kwa maandamano pale airpot regardless waliompiga risasi bado hawajakamatwa., Alifanya kampeni usiku na mchana akiwa salama bila kudhuriwa mahali popote na hao watu wasiojulikana. Lakini mara baada ya uchafuzi alikimbilia ubalozi eti anataka kuuliwa na mtu aliyempigia simu kwamba ameagizwa kumuua na hatimae akarudi begium bila kutathmini watu waliokuwa wakimuunga mkono waliokuwa na mategemeo naye wamepata ushirikiano gani kutoka kwa kiongozi huyo ambaye yeye ndio anatakiwa atoe fatwa azijuazo kuwa pamoja na wananchi.

Na sasa nimemuamini Magufulikwenye kampeni zake alisema Lissu tayari ana visa ya kuishi belgium anataka kuwatumieni halafu yeye achomoke arudi zake belgium watu waendelee kuumia. Ndivyo sura halisi sasa inaonekana.

Yeye anadai hawezi kuja Tz sababu antaka kuuliwa sasa vipi ataiongoza Tz siku moja akiwa rais ilhali hawezi kurudi ama atawaongoza Watanzania online yeye akiwa belgium?
 
Chadema wanakosea sana kwenda mahakamani. Wabaki na msimamo wao wa kuwafukuza akina Mdee, halafu ukweli ujulikane katika baraza kuu ambapo rufaa itasikilizwa, Maana hapo Mdee atasema fomu aliletewa na nani.
Mahakama itawaumiza sana na hatapata jibu manalofikiria kulipata
 
Yeye anadai hawezi kuja Tz sababu antaka kuuliwa sasa vipi ataiongoza Tz siku moja akiwa rais ilhali hawezi kurudi ama atawaongoza Watanzania online yeye akiwa belgium?
akiwa Rais atakuwa na ulinzi kuzidi ule aliokuwa nao wakati wa kampeni
 
Dar es Salaam. CHADEMA imeanza kutumia nguvu ya mahakama kupinga mchakato wa uteuzi wa wabunge 19 wa viti maalumu na mtu aliyesaini fomu zao kwa nafasi ya katibu mkuu.
Wanataka kuvunja katiba kwa kutumia mahakama sasa!
 
Nongwa tu?...mbona hawamshughulikii yule wa Nkasi?Kuna madiwani wengi tu wameapa
 
Katika barua hiyo kwa NEC, alisema CHADEMA inataka kupatiwa nakala ya barua iliyowasilisha majina pamoja na fomu namba 8D ambazo katibu mkuu anatakiwa kujaza ili ijulikane aliyeijaza na hivyo aunganishwe kwenye kesi hiyo.
safi, kama wakigoma kuitoa hiyo form namba 8D wataitolea mahakamani.
 
Mkuu,

Are they filing a case to challenge a non-existent defaulter? This might be a guise phenomenon of the 21st century to surface on planet earth.
Mkuu: hapa kuna hesabu za permutations, how many pairs can you make out of 19 names? Tundulissu yuko mbioni kuwatafutia hifadhi Canada na Nairobi ba EU. Ilu kuongeza dau Halima atengeneze hifadhi 15, Esta A 10, Esta B 10, yule Mnyantuzu naye 10, na aliyenajinsi wimbo wa taifa naye 10 na waliobaki tano tano. CHADEMA wanataka kuitumia nafasi hii waende Canada na kupewa ruzuku watakayoipoteza iwapo "The 19 Ndungai Heroines" watashinda, of course na legal fees za kibatala. Relax, hawa ni Waarabu wa Pemba hujuaba kwa vilemba.
 
Dar es Salaam. CHADEMA imeanza kutumia nguvu ya mahakama kupinga mchakato wa uteuzi wa wabunge 19 wa viti maalumu na mtu aliyesaini fomu zao kwa nafasi ya katibu mkuu.

Chama hicho kilistahili kupata wabunge wa viti maalum kutokana na kupata idadi ya kura za wabunge inayozidi asilimia tano, lakini kinadai hakukuwa na kikao kilichopitisha majina ya wanachama na kupeleka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kwa ajili ya uteuzi.

Lakini Noveemba 24, makada 19 walijitokeza viwanja vya Bunge na kuapishwa kuwa wabunge wa viti maalumu katika utaratibu mpya unaomruhusu Spika kufanya kazi hiyo bila ya kuwepo na mkutano wa chombo hicho cha kutunga sheria, kitendo kilichosababisha Kamati Kuu ya CHADEMA iliyokutana Novemba 27 kuamua kuwavua uanachama.

Pamoja na kustahili viti hivyo, CHADEMA ilishatangaza kutotambua matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, ikidai kwamba uchaguzi huo ulitawaliwa na ukiukwaji wa sheria na taratibu.

Mkurugenzi wa itikadi, uenezi, mawasiliano na mambo ya nje wa CHADEMA, John Mrema alisema mchakato huo unaendelea na tayari katibu mkuu wa chama hicho, John Mnyika ameiandikia barua NEC.

Katika barua hiyo kwa NEC, alisema CHADEMA inataka kupatiwa nakala ya barua iliyowasilisha majina pamoja na fomu namba 8D ambazo katibu mkuu anatakiwa kujaza ili ijulikane aliyeijaza na hivyo aunganishwe kwenye kesi hiyo.

Mwananchi
Hiyo kesi CDM waliyoifungua wakitaka wamfahamu aliyesaini barua ya kuidhinisha wabunge wa viti maalumu imeishia wapi huku wabunge 19 wakikata rufaa na hoja zao kukubalika kwenye mamlaka ya chama?

*Kitu gani kimetokea? Every talkative and provocative person against others accusing of betrayal is a chameleon to trust
 
Back
Top Bottom