Uchaguzi 2020 CHADEMA kutikisa Dar kwa siku tatu, Uchaguzi Mgombea Urais Tanzania na Zanzibar

Uchaguzi 2020 CHADEMA kutikisa Dar kwa siku tatu, Uchaguzi Mgombea Urais Tanzania na Zanzibar

da umeandika kishabiki sana mkuu yaani maandamano ambyo hayajawahi kutokea tanzania? yepi hayo ?huyuhuyu lissu na ni siku hyo akirudi ? unachekesha kama hayo ndiyo maandamano ambayo hayajawahi kutokea utakua siyo mfuatiliaji wewe au akli yako inashida mahala kwenye medula oblangata
Mwenye macho haambiwi Tazama.Endekea kufunika kichwa kwenye gunia huku mwili wote ukiwa nje
 
Lisu asipopita chadema mtakuwa mmejiangusha wenyewe. Wengine tunasubili jina la mgombea wa chadema ili tuanze kuzisaka kadi zetu za kupigia kura zilipo,

Nje ya hapo hatupigi kura, mimi nawakilisha wengi ambao tunasubili jina la lisu, kama tupo pamoja gonga likes za kutosha
mbuttu
 
Lisu asipopita chadema mtakuwa mmejiangusha wenyewe. Wengine tunasubili jina la mgombea wa chadema ili tuanze kuzisaka kadi zetu za kupigia kura zilipo,

Nje ya hapo hatupigi kura, mimi nawakilisha wengi ambao tunasubili jina la lisu, kama tupo pamoja gonga likes za kutosha
Tunaamini wajumbe wa mkutano mkuu watafanya maamuzi yao kwa busara na weledi mkubwa.Jumanne siyo mbali
 
Chadema ndiyo mpango wa Mungu na si majina ya watu.Chama ndiyo mpango wa Mungu kwa hiyo yeyote anayesimama na chama anafanikiwa
Tukutane hapa Novemba mwanzoni utoe mrejesho.
 
yaani huwaga namshangaaa sana mtu kama wewe unshabikia kitu kisichowezekana hivi kuwa mkweli unategemea kweli chadema washinde u RAIS ? au unaigizia tu nikuache nisikushangae maana unaonekana kama kioja kweli
Acha blah Blah wewe..Kwa akili yako unadhani unaweza kufikiri zaidi ya Mungu aliyetuumba
 
Lissu atahudhuria kweli? Maana yuko karantini kwa mujibu wa PETER KIBATALA, sasa asipokuwepo atapitishwa vipi kugombea Urais, mahakamani alishindwa kutokea sababu yuko karantini
 
Asante kwa habari ya kusisimua sana na sasa siasa zinakaribia kuanza tena watanzania tujiandae kwa kishindo kikubwa. Kuna watu hawalali sasa mnawajua, eeh?
Sasa ni Rasmi.Chama kikuu Cha upinzani nchini Chadema kitaanza vikao vyake kwa siku 3 mfululizo kuanzia Jumapili tarehe 2 mpaka Jumanne tarehe 4 katika ukumbi maarufu nchini wa Mlimani City.

Kikao Cha Kamati Kuu kitafanyika kesho Jumapili huku Baraza Kuu likiwa siku ya Jumatatu na Mkutano Mkuu utakuwa siku ya Jumanne.

Agenda Kuu ya vikao hivi ni kuchambua na hatimaye kupiga kura kumpitisha Rasmi mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chadema.

Tayari wajumbe wa vikao hivi wameshaanza kuwasili jijini Dar es Salaam wakiwa na shauku kubwa ya kutimiza takwa la kikatiba.

Mchuano mkali kwenye nafasi ya Urais ni Kati ya mafahali wawili Lazaro Nyalandu Waziri wa zamani wa Maliasili na Utalii ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kanda ya Kati na Mjumbe wa Kamati Kuu akipambana na Tundu Lissu Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa na mwanasiasa mashuhuri zaidi kwa Afrika.

Ikumbukwe Chadema ilitikisa nchi siku ya Jumanne wiki hii wakati maelfu kwa maelfu ya watu walipojaa majiani kumlaki Tundu Lissu aliyerejea matibabuni huku kukiwa na maandamano makubwa zaidi kuwahi kutokea nchini kumsindikiza mwanasiasa huyo makao makuu ya Chama huku umati huu ukiimba 'Rais' Rais' Rais' kote alikopita ambapo Barabara ilifungwa kwa masaa manne kumsindikiza shujaa huyo.

Sisi wa Molemo Media Kama Sikuzote Tunatarajia kuwaletea matangazo ya moja kwa moja wasomaji wetu wa Jamii Forum ili Dunia kuweza kujua kinachoendelea ndani ya vikao hivyo muhimu.Tuna Imani hatukuwahi kuwaangusha wafuatiliaji wetu.
Endeleeni kujifariji
Mwenye macho haambiwi Tazama.Chadema ni mpango wa Mungu
Asante sana Molemo tupo pamoja tunawaletea Mgombea Urais wa Maono ya Watanzania
Kila la kheri makamanda.
People's........ Power......
FaizaFoxy sijamsoma siku nyingi, tangu Coronavirus ilipoingia rasmi kwenye mapapai, mafenesi, mbuzi, kondooo, kware na kuku Tanzania 🇹🇿
T 2020 TAL
Lazima maccm watafutane...
Mungu awatangulie Chadema. Sasa ni wakati wenu wa kuithibitishia Tanzania, watanzania na dunia kwa ujumla kuwa nyie ni Chama Bora kwa sasa hapa Tanzania.

Nawatakia Heri kwenye vikao vyenu!
Hizo ndo habali watanzania hasa wapenda demokrasia haki na utawala bora ndo huwa wanapenda kuziskia achana na zile habali za kibaguzi
 
Back
Top Bottom