Uchaguzi 2020 CHADEMA: Matukio ya Chato, Kahama yanatishia usalama wa Tundu Lissu

Uchaguzi 2020 CHADEMA: Matukio ya Chato, Kahama yanatishia usalama wa Tundu Lissu

CHADEMA

JF-Expert Member
Joined
Apr 13, 2013
Posts
490
Reaction score
2,471
CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NA UMMA

Chama ch ma Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesikitishwa na kupokea kwa tahadhari kubwa matukio yanayotishia uvunjifu wa haki na uhuru nchini, kuhatarisha amani ya nchi na hata kuwa dalili zingine za wazi za kuharibu na kuvuruga Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 28, 2020 na hivyo kinazitaka mamlaka zinazohusika kuchukua hatua za haraka kuzuia vitendo hivyo.

Kitendo cha Jeshi la Polisi Wilayani Kahama kuvamia msafara wa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chadema, Mhe. Tundu Lissu na kuwashambulia kwa silaha za moto wananchi waliokuwa wakitembea kwa amani kumsindikiza Mhe. Lissu kwenda hotelini na kuwatishia waandishi wa habari, ni mwendelezo wa vitendo vya jeshi hilo kukiuka Maadili ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020 na taratibu zingine za kisheria nchini.

Aidha, tukio la watu ambao hawajakamatwa, waliokuwa na silaha, kuwavamia Mgombea Ubunge wa Chadema, Jimbo la Chato na Katibu wa Chadema katika eneo hilo, kisha wakafanya uharibifu mkubwa wa mali na kutishia usalama wa viongozi hao, ni mwendelezo wa matukio dhidi ya Chadema na viongozi wake maeneo mbalimbali nchi nzima ambayo hakuna hatua zozote za kisheria zimechukuliwa.

Tukio hilo la kuvamia viongozi wa Chadema Jimbo la Chato usiku wa kuamkia leo, linafanana kwa namna moja ama nyingine na lile la kuvamiwa na kuchomwa moto kwa Ofisi ya Chadema Kanda ya Kaskazini, jijini Arusha. Matukio yote yamefanyika muda mfupi kabla Mgombea Urais wa Chadema Mhe. Lissu hajafika maeneo hayo kwa ajili ya vikao na mikutano inayohusu shughuli za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.

Chadema inayachukulia matukio yote hayo mawili yaliyotokea Kahama na Chato kuwa na tishio kwa usalama wa Mgombea Urais Mhe. Lissu na mwendelezo wa dalili za wazi za kuvuruga na kuharibu Uchaguzi Mkuu.

Pamoja na kulaani vikali matendo hayo yanayokiuka Maadili ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020 na taratibu zingine za kisheria za nchi yetu, Chadema inazitaka mamlaka zinazohusika ikiwemo NEC na Jeshi la Polisi kuchukua hatua za haraka kuzuia uhalifu huo unaovunja haki na kutishia amani wakati huu wa kampeni za Uchaguzi Mkuu. Kunyamazia vitendo hivyo itatafsiriwa kuwa vinafanyika kwa baraka za vyombo vyenye mamlaka ya kuzuia visitokee.

Imetolewa leo Jumanne Oktoba 13, 2020 na;

Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
 
1. Ni jambo zuri kuzitahadharisha mamlaka ili zichukue hatua

2. Lakini lazima mfahamu kuwa hiyo ni mikakati inayoratibiwa na dola yenyewe chini ya maRC na maDC kwa baraka zote za NEC..

3. Kumbukeni hawa (RCs na DCs) ni wenyeviti kamati za ULINZI na USALAMA mkoa na wilaya na ndiyo wanaotoa "orders" kwa maRPC na OCDs kuharibu amani kwenye mikutano ya mgombea wenu. OCDs nao wanaamuru askari wao kupiga na kuvuruga..!!

4. Wanafanya hivyo, ili kuipa hoja CCM na mgombea wao ambaye hana kibali kwa UMMA na kwa MUNGU kuongoza nchi, kusema "....mnaona amefika Chato kazomewa kwa sababu hawamtaki..."

Ieleweni mikakati hii kicha kuwa proactive kuchukua hatua. Wao wana polisi, TISS na bunduki na risasi, lakini ninyi mna UMMA....mna NGUVU YA UMMA. Itumieni hii kwa ufasaha...

USHAURI:

¶ There's no going back. Lazima mapambano yaendelee. Kama wanataka kuleta fujo, waanzishe hiyo fujo, SISI TUTAIMALIZA!!

¶ Mgombea Urais, Tundu Lissu lazima afike kila sehemu na afanye mikutano yake kulingana na ratiba!!

¶ Imesemwa na inasemwa sana na mgombea Urais wetu Mh. Tundu Lissu, kuwa kuikomboa nchi toka kwa manyang'au CCM na vibaraka wao is not an easier job, kuwanyang'anya dola hawa inahitaji kulipa huge price..

Gharama yenyewe ndiyo hii..!!

Adui yuko desperate. Anaitetea pumzi yake ya mwisho. Hawezi ku - survive. Amechoka. Yuko tayari ku - surrender. ALUTA CONTINUA...
 
1. Ni jambo zuri kuzitahadharisha mamlaka ili zichukue hatua

2. Lakini lazima mfahamu kuwa hiyo ni mikakati inayoratibiwa na dola yenyewe chini ya maRC na maDC kwa baraka zote za NEC

3. Wanafanya hivyo, ili kuipa hoja CCM na mgombea wao ambaye hana kibali kwa UMMA na kwa MUNGU kuongoza nchi, kusema "....mnaona amefika Chato kazomewa kwa sababu hawamtaki..."

USHAURI:

¶ There's no going back. Lazima mapambano yaendelee. Kama wanataka kuleta fujo, waanzishe hiyo fujo, SISI TUTAIMALIZA!!

¶ Mgombea Urais, Tundu Lissu lazima afike kila sehemu na afanye mikutano yake kulingana na ratiba!!

¶ Imesemwa na inasemwa sana na mgombea Urais wetu Mh. Tundu Lissu, kuwa kuikomboa nchi toka kwa manyang'au CCM na vibaraka wao is not an easier job, kuwanyang'anya dola hawa inahitaji kulipa huge price..

Gharama yenyewe ndiyo hii..!!

Adui yuko desperate. Anaitetea pumzi yake ya mwisho. Hawezi ku - survive. Amechoka. Yuko tayari ku - surrender. ALUTA CONTINUA...
Yaani mfa maji kweli haishi kutapatapa. Maji yako shingoni TAL anatafuta njia tuu ya kuleta vurugu. Waliochoma nyumba huko Arusha ni wao wao ili kutaka vurugu ianze. Hatudanganyiki. TAL na kundi lake mwageni sera zenu za nini mtafanya mkipata dola. Msiendelee kutafuta huruma kwa wananchi. Anayetafutwa hapa ni Rais atakayewaletea maendeleo Watanzania; na siyo anayelialia akitafuta huruma. Tueleze utatufanyia nini zaidi ya tulichopata kwa JPJM.
 
Polisi ongeza bidii juu ya hawa chadema maana wao ndio upanga matukio ya vurugu ili kutafuta huruma ya wananchi, narudi adui mkubwa wa chadema ni chadema wenyewe..wengi wao ni majambazi wastaafu na matapeli!
 
Acheni mambo ya kipumbavu kufanya mambo kwa makusudi
mnasababisha watu wasio hatia kuumia sababu ya upuuzi wenu
"kupuuza sheria kuhusu mikusanyiko"

Hovyo sana nyie watu.
 
Yaani mfa maji kweli haishi kutapatapa. Maji yako shingoni TAL anatafuta njia tuu ya kuleta vurugu. Waliochoma nyumba huko Arusha ni wao wao ili kutaka vurugu ianze. Hatudanganyiki. TAL na kundi lake mwageni sera zenu za nini mtafanya mkipata dola. Msiendelee kutafuta huruma kwa wananchi. Anayetafutwa hapa ni Rais atakayewaletea maendeleo Watanzania; na siyo anayelialia akitafuta huruma. Tueleze utatufanyia nini zaidi ya tulichopata kwa JPJM.
Ni vema kuandika comment zenye uhalisia. Haya mambo ya watu kufanyiwa fujo au kuharibiwa mali zao, kuumizwa au kuuawa tusichukulie ushabiki wa vyama. Tuwe wamoja kukemea hayo mambo yasiyo ya kibinadamu.
 
Kwani ameenda kwa mujibu wa ratiba ya NEC?

Nec ya CCM inayo ng'ata upande mmoja tu !!!.Mbona hauulizi na upande wa pili Ratiba ina vurugwa na hatuioni hiyo NecCCM ikijitokeza !?.Mh Magufuli anasimama popote na anafanya lolote na habugudhiwi ,Raia kwa mapenzi yao wana msindikiza Mgombea wao kwenda Hotel mnawa shambulia.Nna sikitika Wapinzani Nchi hii kuchukiwa na kuchukuliwa kama maadui na Dola inayoongozwa na CCM,dola inayotakiwa kukaa katikati.
 
Ni vema kuandika comment zenye uhalisia. Haya mambo ya watu kufanyiwa fujo au kuharibiwa mali zao, kuumizwa au kuuawa tusichukulie ushabiki wa vyama. Tuwe wamoja kukemea hayo mambo yasiyo ya kibinadamu.

Sijui kama wengine ni waelewa au mpaka na wao waeleweshwe kwa vitendo ,wanaumiza Watu sana kwa kuharibu Mali zao kuumiza Raia kwa vipigo kisa Policeccm na wanao wabeba.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
John wewe ni mpumbavu kumbe?..... kwenye ule uzi wako mwingine joka kuu alikutumia kabisa ratiba, na ukashukuru!


sasa hapa unauliza nini tena? umechanganyikiwa?[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Meku, mimi nashangaa kwanini afanyiwe figisu kama safari yake ni halali!
 
Back
Top Bottom