Uchaguzi 2020 CHADEMA mna mpango wa kumsimamisha nani kama mgombea urais?

Uchaguzi 2020 CHADEMA mna mpango wa kumsimamisha nani kama mgombea urais?

Nafikiri ungefuatilia ile hukumu ya Mahakama ya rufaa juu hili suala la tume huru wala usingerudia mara kwa mara kulizunguzia. Sababu kile ndio chombo cha juu na cha mwisho kutafasiri sheria. Hukumun ilishatoka na iliwekwa wazi kuwa tume ya uchaguzi inafanya kazi kwa uhuru kama chombo huru, ambacho kinafanya kazi kwa mujibu wa katiba na sheria.
Mahakama ya yule Jaji aliyewekwa kukaimu kwa miaka 2?
Yule kishaungana na huu muhimili kuu, hamna kitu pale, tunasubiri hawa mahakimu wa sasa akina Sachore waje kupata ujaji mkuu ndio watakuwa na maamuzi yasiyo ya ki-pwuzyi
 
Wahenga wanasema siku hazigandi na kama ilivyokawaida October 2020 inakaribia. Na kila chama kitaweka mgombea kuanzia ngazi ya udiwani,ubunge na urais.

Kwa walioshika dola tayari inajulikama nani atapeperusha bendera ya Chama chake yaani CCM

Mwenyekiti wa Tlp yeye pamoja na kuwa sio mwana CCM amekiri atamuunga mkono John Pombe Magufuli hii ni kwa sababu amefanya kazi kubwa ya kudhibiti rushwa na ubadhirifu,kujenga miundo mbinu,kujenga miradi kama Sgr,JNHHP n.k na kwa mantiki hii ameamua kumuunga mkono.

Nakuja kwa hichi chama ambacho kuanzia wafuasi wake na viongozi wake hawana uzalendo. Maana wao kila siku ni kuitakia mabaya nchi yao ati kisa tu CCM ndio imekamata dola.

Sasa wamebaki kuwa watu wa vurugu na matusi mitandaoni na wameonyesha kukata tamaa ya kisiasa. Na swali linakuja watamsimamisha nani ili apambane na JPM? Ni Mh Mbowe? Au Mnyika? au Halima Mdee? Au Esther Matiko?
Ngoja tusubiri maana siku hazigandi.

Au ndio hawataweka mgombea kabisa? Maana naona kama hamna wa kupambana na JPM!
JPM huyu aliyekimbia kacorona au yupi?Naomba nikufahamishe ya kuwa CCM ya sasa ikikubali Tume Huru ya Uchaguzi na uchaguzi ukiwa Huru na haki hawatoboi hata akisimama nani?
JPM na chama chake hawakuwahi kushinda uchaguzi wowote hapa nchini bila magumashi.Hilo wanalielewa wazi ndiyo maana wakisikia Tume Huru/Katiba Mpya utawaona wanavyobadilika kauli na matendo. They turn into killer monsters instantly.
 
Watu si watasagana hadi ikulu?


Sent from my iPhone using Tapatalk
Bora hata hilo maana litakuwa haliwaumizi wapiga kura na wananchi wengine kama maumivu wanyopitia chini ya utawala huu wa magaidi.
Mabeberu na Ushoga mnauhubiri na kuuwazia sana watu wa CCM,au ndicho vijazavyo mioyo yenu?Kila hoja ngumu kwenu jibu lake ndilo hilo?
 
Mahakama ya yule Jaji aliyewekwa kukaimu kwa miaka 2?
Yule kishaungana na huu muhimili kuu, hamna kitu pale, tunasubiri hawa mahakimu wa sasa akina Sachore waje kupata ujaji mkuu ndio watakuwa na maamuzi yasiyo ya ki-pwuzyi
Mh.. Hayo yako binafsi na huyo Mh Sachore. Lakini jopo la majaji watatu wa mahakama ya rufaa walichambua hoja za pande mbili na wakaona tume ipo huru.
 
Nafikiri ungefuatilia ile hukumu ya Mahakama ya rufaa juu hili suala la tume huru wala usingerudia mara kwa mara kulizunguzia. Sababu kile ndio chombo cha juu na cha mwisho kutafasiri sheria. Hukumun ilishatoka na iliwekwa wazi kuwa tume ya uchaguzi inafanya kazi kwa uhuru kama chombo huru, ambacho kinafanya kazi kwa mujibu wa katiba na sheria.

Ww ndio una imani na hizo mahakama. Narudia tena, tume hii ya uchaguzi sio huru, hata kama ingekuwa imeandikwa kwenye biblia acha hiyo unayosema mahakama ilisema. Hiyo mahakama tunaona wazi inafanya kwa kufuata amri toka juu ndio useme tuiamini? Uhuni na uhayawani unaofanyika kwenye chaguzi zetu, tena kwa uratibu wa vyombo vya dola na tume ya uchaguzi huwa tunaona na wala hatuhadithiwi, tukisema tume hii ya uchaguzi sio huru, hatukosei kwenye hilo.
 
M
Wapo wengi tu.Mtu yoyote mwenye akili timamu anaweza kuongoza nchi hii, kazi ambayo JK na Magufuli wameweza, nani ataishindwa? Magufuli kama Magufuli hawezi ushindani, pitia rekodi yake toka akiwa mbunge ni mara ngapi aliwahi kushinda kwa box la kura zaidi ya mizengwe. Tunahitaji katiba mpya ili tupate kiongozi bora na sio kiongozi katili.
Mkuu mada haiongelei kiongozi katiri mbona upo nnje ya mada? Mada inaongelea mtasimamisha Mgombea yupi?
 
MboNa
Mkujua itawasaidia nn !?
Mnataka kumpiga risasi !?
Mumbambikie kesi ya kutakatisha fedha !?
Kuhoji uraia wake !?
Kuhoji uraia wa wazazi wake !?
Au muanze kumpaka matope mitandaoni !?

Tulizeni kiraro, hii game haihitaji hasira wala kukamiana.
Mbona haya maneno ni Ishara ya kutokujiamini.
 
Wahenga wanasema siku hazigandi na kama ilivyokawaida October 2020 inakaribia. Na kila chama kitaweka mgombea kuanzia ngazi ya udiwani,ubunge na urais.

Kwa walioshika dola tayari inajulikama nani atapeperusha bendera ya Chama chake yaani CCM

Mwenyekiti wa Tlp yeye pamoja na kuwa sio mwana CCM amekiri atamuunga mkono John Pombe Magufuli hii ni kwa sababu amefanya kazi kubwa ya kudhibiti rushwa na ubadhirifu,kujenga miundo mbinu,kujenga miradi kama Sgr,JNHHP n.k na kwa mantiki hii ameamua kumuunga mkono.

Nakuja kwa hichi chama ambacho kuanzia wafuasi wake na viongozi wake hawana uzalendo. Maana wao kila siku ni kuitakia mabaya nchi yao ati kisa tu CCM ndio imekamata dola.

Sasa wamebaki kuwa watu wa vurugu na matusi mitandaoni na wameonyesha kukata tamaa ya kisiasa. Na swali linakuja watamsimamisha nani ili apambane na JPM? Ni Mh Mbowe? Au Mnyika? au Halima Mdee? Au Esther Matiko?
Ngoja tusubiri maana siku hazigandi.

Au ndio hawataweka mgombea kabisa? Maana naona kama hamna wa kupambana na JPM!
Hashim Rungwe Sipunda ili atuletee mabomba ya asali na Maziwa. 🤣🤣🤣🤣
 
Ww ndio una imani na hizo mahakama. Narudia tena, tume hii ya uchaguzi sio huru, hata kama ingekuwa imeandikwa kwenye biblia acha hiyo unayosema mahakama ilisema. Hiyo mahakama tunaona wazi inafanya kwa kufuata amri toka juu ndio useme tuiamini? Uhuni na uhayawani unaofanyika kwenye chaguzi zetu, tena kwa uratibu wa vyombo vya dola na tume ya uchaguzi huwa tunaona na wala hatuhadithiwi, tukisema tume hii ya uchaguzi sio huru, hatukosei kwenye hilo.
Sasa hao wabunge sabini mliwapataje kama sio huru? Maana kuanzia ngazi ya kituo,jimbo na taifa mnatakiwa muwe na mawakala na hii ni kwa mujibu wa sheria na kanuni. Sasa hao mawakala wenu huwa wanasinzia wakati wa kuhesabu kura? Na form zote huwa zinakusanya na kusainiwa na mawakala kisha wagombea kwa kila ngazi.
 
Uchaguzi wa nini wakati Covid-19 tu hatuwezi kudhibiti...??
Si bora hizo hela za uchaguzi tujipange kutoa rambi rambi??
 
M
Mkuu mada haiongelei kiongozi katiri mbona upo nnje ya mada? Mada inaongelea mtasimamisha Mgombea yupi?

Mkuu hapa sio kwenye somo la hesabu kwamba 2+2=4, hapa ni jukwaa la siasa ambapo kwenye mjadala mifano ni mingi ili kutoa mtazamo wa mchangiaji yoyote. Ningekuwa nimejadili mambo ya soka, au dini hapo ndio ningekuwa nje ya mada.
 
Kampeni za 2020 zitakuwa tamu sana!!! Kuna mgombea ataulizwa jinsi yake ni ke au me???
 
Sasa hao wabunge sabini mliwapataje kama sio huru? Maana kuanzia ngazi ya kituo,jimbo na taifa mnatakiwa muwe na mawakala na hii ni kwa mujibu wa sheria na kanuni. Sasa hao mawakala wenu huwa wanasinzia wakati wa kuhesabu kura? Na form zote huwa zinakusanya na kusainiwa na mawakala kisha wagombea kwa kila ngazi.

Hao wabunge 70 walipatikana enzi za JK wakati huo demokrasia na utawala bora ulikuwa na afadhali kwa mbali. Toka ameingia Magufuli madarakani tumeona na kumsikia akitishia maafisa wa tume kutokumtangaza mpinzani kisa yeye ndio anawalipa. Mimi binafsi na watu wengine tuliona kupitia kituo cha ITV kwenye kituo cha uchaguzi wa marudio maboxi ya kura yakitolewa kituoni na kwenda kujazwa kura za ccm, hali hii ilitokea mbele ya vyombo vya dola na msimamizi wa uchaguzi, na bado msimamizi wa uchaguzi alimtangaza mgombea wa ccm mbele ya huo uhayawani. Mtindo ulitumika kwenye vituo vingine vyote vya uchaguzi, na aliyetoa maagizo hayo ni rais ili kuhadaa umma kuwa ccm inakubalika.

Pia niliona baadhi ya vituo karatasi zisizo halali za matokeo, mawakala wa upinzani wakilazimishwa kujaza tena kwa kipigo cha polisi. Haya yalifanyika kwenye vituo vyote vya uchaguzi kwa maagizo maalumu. Wasimamizi wa uchaguzi walikuwa wakifunga ofisi ili wasipokee fomu za wagombea wa upinzani. Fomu za wagombea wa upinzani hata zile zilizopokelewa zikifanyiwa hujuma za wazi. Tabia hii ya kwenye chaguzi za marudio zilifanyika hata kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa.

Ukiangalia hizi tabia za kwenye chaguzi zetu ni tabia binafsi za Magufuli hata alipokuwa mbunge. Ninaposema Magufuli ndio anayenajisi chaguzi za nchi hii kwa matumizi mabaya ya madaraka, sisemi hivyo kwa kubahatisha. Ndio tunasema tunataka tume huru ya uchaguzi, kwani ccm chini ya Magufuli haiwezi ushindani wala sio imara, bali inaendesha ukatili kwenye chaguzi zetu ili kutangazwa washindi. Nitawashangaa wapinzani kushiriki huu ushenzi wa mtu mweusi uitwao uchaguzi. Na sisi wananchi tunaojitambua hatutashiriki huo upuuzi bila tume huru ya uchaguzi fullstop.
 
Hao wabunge 70 walipatikana enzi za JK wakati huo demokrasia na utawala bora ulikuwa na afadhali kwa mbali. Toka ameingia Magufuli madarakani tumeona na kumsikia akitishia maafisa wa tume kutokumtangaza mpinzani kisa yeye ndio anawalipa. Mimi binafsi na watu wengine tuliona kupitia kituo cha ITV kwenye kituo cha uchaguzi wa marudio maboxi ya kura yakitolewa kituoni na kwenda kujazwa kura za ccm, hali hii ilitokea mbele ya vyombo vya dola na msimamizi wa uchaguzi, na bado msimamizi wa uchaguzi alimtangaza mgombea wa ccm mbele ya huo uhayawani. Mtindo ulitumika kwenye vituo vingine vyote vya uchaguzi, na aliyetoa maagizo hayo ni rais ili kuhadaa umma kuwa ccm inakubalika.

Pia niliona baadhi ya vituo karatasi zisizo halali za matokeo, mawakala wa upinzani wakilazimishwa kujaza tena kwa kipigo cha polisi. Haya yalifanyika kwenye vituo vyote vya uchaguzi kwa maagizo maalumu. Wasimamizi wa uchaguzi walikuwa wakifunga ofisi ili wasipokee fomu za wagombea wa upinzani. Fomu za wagombea wa upinzani hata zile zilizopokelewa zikifanyiwa hujuma za wazi. Tabia hii ya kwenye chaguzi za marudio zilifanyika hata kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa.

Ukiangalia hizi tabia za kwenye chaguzi zetu ni tabia binafsi za Magufuli hata alipokuwa mbunge. Ninaposema Magufuli ndio anayenajisi chaguzi za nchi hii kwa matumizi mabaya ya madaraka, sisemi hivyo kwa kubahatisha. Ndio tunasema tunataka tume huru ya uchaguzi, kwani ccm chini ya Magufuli haiwezi ushindani wala sio imara, bali inaendesha ukatili kwenye chaguzi zetu ili kutangazwa washindi. Nitawashangaa wapinzani kushiriki huu ushenzi wa mtu mweusi uitwao uchaguzi. Na sisi wananchi tunaojitambua hatutashiriki huo upuuzi bila tume huru ya uchaguzi fullstop.
Uongo uliopitiliza ,yaani kama ni kuforce basi ni balaa.
 
Mkuu hapa sio kwenye somo la hesabu kwamba 2+2=4, hapa ni jukwaa la siasa ambapo kwenye mjadala mifano ni mingi ili kutoa mtazamo wa mchangiaji yoyote. Ningekuwa nimejadili mambo ya soka, au dini hapo ndio ningekuwa nje ya mada.
ha ha ha mkuu unaruka ruka tu, hujatoa jibu sahihi.
 
Wanategemea kapi la ccm[emoji23][emoji23][emoji23]
Wahenga wanasema siku hazigandi na kama ilivyokawaida October 2020 inakaribia. Na kila chama kitaweka mgombea kuanzia ngazi ya udiwani,ubunge na urais.

Kwa walioshika dola tayari inajulikama nani atapeperusha bendera ya Chama chake yaani CCM

Mwenyekiti wa Tlp yeye pamoja na kuwa sio mwana CCM amekiri atamuunga mkono John Pombe Magufuli hii ni kwa sababu amefanya kazi kubwa ya kudhibiti rushwa na ubadhirifu,kujenga miundo mbinu,kujenga miradi kama Sgr,JNHHP n.k na kwa mantiki hii ameamua kumuunga mkono.

Nakuja kwa hichi chama ambacho kuanzia wafuasi wake na viongozi wake hawana uzalendo. Maana wao kila siku ni kuitakia mabaya nchi yao ati kisa tu CCM ndio imekamata dola.

Sasa wamebaki kuwa watu wa vurugu na matusi mitandaoni na wameonyesha kukata tamaa ya kisiasa. Na swali linakuja watamsimamisha nani ili apambane na JPM? Ni Mh Mbowe? Au Mnyika? au Halima Mdee? Au Esther Matiko?
Ngoja tusubiri maana siku hazigandi.

Au ndio hawataweka mgombea kabisa? Maana naona kama hamna wa kupambana na JPM!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ganja bhana!,[emoji41]
Wapo wengi tu.Mtu yoyote mwenye akili timamu anaweza kuongoza nchi hii, kazi ambayo JK na Magufuli wameweza, nani ataishindwa? Magufuli kama Magufuli hawezi ushindani, pitia rekodi yake toka akiwa mbunge ni mara ngapi aliwahi kushinda kwa box la kura zaidi ya mizengwe. Tunahitaji katiba mpya ili tupate kiongozi bora na sio kiongozi katili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom