CHADEMA mwendo mdundo

CHADEMA mwendo mdundo

Wewe acha kuzungumzia marehemu,
Kuweka record yako vizuri Kighoma Malima ni muadilifu wala hakuwa fisadi...mafisadi unawajua vizuri kina mkapa, yona, mramba, chenge, RA, edward lowassa, ...
ama unataka kubadilisha hii thread kwenye mkondo uliopo kwenye mkondo mwingine kabisaaa..maana wanaomtuhumu kighoma wamejazwa na chuki za "Kidini" hasa wakristo nothing more..call a spade a spade...hakuna kiongozi muadilifu kama kighoma
kwani Rais alie mfukuza kazi alikua Mkristo, jadili hoja ilio muhusisha, kwani Kikwete akiwa waziri hazina aligundua nini, umesahau maafisa kumi n mbili makamishna alifukuzwa nao......mfumo wa kulindana ndio umeua nchi hii.
 
Chadema hakujatulia, Mbowe ashambuliwa
Imeandikwa na Theopista Nsanzugwanko; Tarehe: 27th November 2009 @ 23:58

ALIYEKUWA kiongozi wa mambo ya Bunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Juju Danda, amejiondoa katika Chama hicho.

Danda amesema jijini Dar es Salaam kuwa, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) anapaswa kukagua hesabu ya Chadema na kwamba, hati zikiwa safi yupo tayari kufungwa jela.

Amedai kuwa, taratibu za manunuzi hazifuatwi katika chama hicho, na kwamba, manunuzi yote ya chama yanafanywa na Antony Komu ambaye ni mtu wa karibu na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe.

Danda amedai kuwa, Mbowe ameifanya Chadema kama kampuni yake binafsi.

“Nikiwa mmoja wa walipa kodi wa nchi hii, nina wajibu wa kuhakikisha fedha zinazotolewa kama ruzuku kwa vyama vya siasa zinatumika kwa mujibu wa sheria hivyo basi naomba mkaguzi mkuu wa fedha za Serikali aikague Chadema na ikipata hati safi mkondo wa sheria uchukue hatua dhidi yake” amesema Danda.


Kwa mujibu wa Danda, Mbowe tu anafahamu zilipo fedha za ruzuku, makusanyo yanayopatikana kupitia ujumbe wa simu, na fedha zinazotoka kwa wahisani.

Amesema, wananchi wengi wanakichangia chama hicho lakini Mbowe amekuwa akibadili michango hiyo kuwa yake binafsi na kudai kukikopesha Chama.

Ametoa mfano kwa kudai kuwa, kuna mfanyabiashara jijini Dar es Salaam aliyechangia milioni 43 kwa ajili ya uchaguzi wa ubunge Tarime mwaka 2008 lakini Mbowe alidai kukikopesha chama.

“Chadema wamekuwa wakilia na wimbo wa ufisadi kila siku lakini,shilingi milioni 35 alizochota Mbowe katika ruzuku ya Desemba mwaka jana ni sawa na asilimia 52 ya ruzuku ya chama kwa mwezi, wakati Sh.bilioni 133 za EPA ni sawa na asilimia 23 tu ya matumizi ya serikali kwa mwezi” amedai Danda.

Danda amesema,yeye na aliyekuwa afisa habari wa chadema, walifukuzwa kwa kuwa walitofautiana kimtazamo na 'mmiliki huyo' hasa baada ya kuonesha hisia zao za kumuunga mkono Zitto Kabwe alipotaka kugombea uenyekiti wa chama hicho.

Amedai kuwa, baada ya kufukuzwa alitakiwa kuomba msamaha ili arudishwe kwenye chama lakini alikataa.

Danda amedai kuwa, hajafikiria atahamia chama gani lakini akishaamua ataondoka na wanachama wengi toka Chadema.

Alisema ndani ya Chadema kuna makundi mawili, kundi la Mbowe lenye maisha mazuri na magari ya kifahari na lile la Zitto lenye wanachama wanaomuunga mkono mwanasiasa huyo.

- Huwa sio kawaida yangu kuingilia ishus za ndani za vyama vya siasa, tatizo langu hapa ni kwa nini huyu mkuu hakusema haya kabla hajafukuzwa? Na yeye anakuwa kama majaji wakuu wa Tanzania, mpaka saa ya ku-retire ndio tunajua kuwa hata kama walikuwepo!

Respect.


FMEs!
 
Nimeaga nimerudi tena kidogo tu nitoe jibu la sentensi moja: NAAMINI WAZEE WALIMSHAURI ZITTO AJITOE NA ZITTO AKAKUBALI KWA SABABU CHADEMA NI ZAIDI YA MBOWE NA ZITTO. Alamsiki, siku nyingine Kituko.
JJ

pamoja na kuwa ndani ya CHADEMA kama kiongozi, Pamoja na kupewa mamlaka ya kuandika huo waraka ulioubandika hapo kwenye website yenu, still hujuhi kinachoendelea unaishi humo kwa IMANI TU, mi nadhani majibu yako yanapaswa kuwa ya uhakika na sio mambo ya imani, siku zote ukiwa mtu wa kuaminiamini tu thinking yako lazima iwe zero, na kama wewe unaishi kwa imani ndani ya CHADEMA je sisi wa nje?
SWALI KWA NINI WAZEE WALIMSHAURI ZITTO AJITOE kama hilo ni gumu hebu jibu hili KWA NINI WAZEE HAWAKUMSHAURI MBOWE AMBAYE KAKAA MUDA MREFU AJITOE,
naomba majibu ya uhakika sio ya IMANI
 
ukianza na Wangwe,Kafulila hakuna hata mmoja ambae alifukuzwa nnje ya utaratibu uliopo ndani ya katiba ya CHADEMA, sema shida yako umelelewa kwenye mfumo wa kubembelezana na kuamini kua bila mtu fulani hakuna maisha.
Hakuna alie juu ya Chama, maana Chama ni taasisi, ndio maana alikuwepo Mtei Mtei , akaja Bob, sasa Mbowe.....maisha yanakwenda.
Tumaini kama kiongozi mfano JK ANAYOVYOSHINDWA kuwawajibisha wasaidizi wake, kwako huo ni mfano wa demokrasia, amakweli kiwi cha macho huletwa na malezi mabaya ya tangu udogo.

Dogo JK siyo role model wa kiongozi wa siasa ninaye admire...what a joke?

Ungeniuliza ni kiongozi gani wa chama cha siasa una-appreaciate uongozi wake so far ningesema..ni "Ibrahimu Lipumba" wa CUF

Kwanini, chama kimelaumiwa sana kuwa na cha kidini lakini kila siku wanajitahidi na unaona viongozi wanafanya hivyo kwa vitendo...kuwa chama cha kitaifa...inapenetrate sehemu na kona zote za nchi.. hajalaumiwa uadilifu wake iwe katika kuonea mwanchama au kufisadi fedha za chama, hana njaa na ni msomi muadilifu..that is my take.

on the other hand, chadema wanaendeleza nepotism na ubabe usio na maana...kwa wanachama wake eti kisingizio tunalinda heshima

kulazimisha heshima au kuheshimwa wakati wewe huna heshima ni ugonjwa mbaya sana ambao chadema itakufa kifo cha mende kwa uongozi wa kina slaa na mbowe
 
[/COLOR]

Ha ha haa! Kuna ngoma inaitwa mduara.

Ulishaharibu mkuu, mbaya zaidi wewe ni injinia wa forums

Forum; A public facility to meet for open discussion-SAGE

Ulichofanya mara ya kwanza hakikuwa 'forum' ila ushabiki.kama wewe unaonyesha mfano huu, mkuu tutegemee nini kuja humu?

Hata kama una ushabiki weka kando, kwa nafasi yako ndani ya JF..wewe uwe kama mwenyekiti wa 'debate' kama mtu hajatukanwa whats wrong?

I am dissaponted!

Na usije kwa mamlaka yako ukanifungia au kunizushia mambo ya ajabu
 
Ungeniuliza ni kiongozi gani wa chama cha siasa una-appreaciate uongozi wake so far ningesema..ni "Ibrahimu Lipumba" wa CUF
mimi najiepusha kuzungumzia CUF, kwasababu zangu binafsi, ila swala la UDINI linawatafuna sana, watajuana na CCM, ila siioni falsafa maridhawa ndani ya ya chama hiko, ndo maana niko CHADEMA. kwanza CUF sio tishio kwetu, ni kama TLP tu, sisi tuwaza kupambana na CCM ALIE Madarakani, anaetuletea unasikini....nyinyi mnapambana na asie na mamlaka....ama dola, ama kweli.
kwangu issue sio kua Muislamu , mpagani , mpare , mpemba au Mmasai, cha muhimu ni namna gani unaweza kuongoza na kuleta mambo mema kwa nnchi yako....
 
mimi najiepusha kuzungumzia CUF, kwasababu zangu binafsi, ila swala la UDINI linawatafuna sana, watajuana na CCM, ila siioni falsafa maridhawa ndani ya ya chama hiko, ndo maana niko CHADEMA. kwanza CUF sio tishio kwetu, ni kama TLP tu, sisi tuwaza kupambana na CCM ALIE Madarakani, anaetuletea unasikini....nyinyi mnapambana na asie na mamlaka....ama dola, ama kweli.
kwangu issue sio kua Muislamu , mpagani , mpare , mpemba au Mmasai, cha muhimu ni namna gani unaweza kuongoza na kuleta mambo mema kwa nnchi yako....

Sababu zako binafsi ni "UDINI" kama kawaida unajificha sehemu tambarare

CUF siyo tishio..kwako..lol unafurahisha baraza au?...CUF ni wa pili kwenye uchaguzi wa serikali za mitaani uliopita...tlp sijui ni ya ngapi wapi na wapi?

Ibrahimu hajalaumiwa na wanachama for nepotism, kuonea wanachama wa CUF na ubadirifu wa fedha...lakini huyo jamaa yako mbowe na slaa kila siku wanachama wanalalamika je wakipewa dola..

Namna gani gani unaweza kuongoza na kuleta mambo kwa nchi yako ha ha ha ..hayo ni matokeo ya uadilifu wako binafsi na uadilifu wa taasisi yako..kusimamia hayo..tumeshuhudia CCM na Chadema kwenye swala la kusimamia uadilifu....wanaboa...long way to go for chadema as an institution.
 
Kesho tutakuwa na Kongamano la Vijana, halafu kuanzia tarehe 30 Novemba, 2009 mpaka tarehe 3 Disemba 2009 tutakuwa kwenye mfululizo wa vikao vya juu vya chama tukiutathmini mwaka 2009 na kupanga mwelekeo wa chama kwenda mwaka 2010.

Ndugu Mnyika maswali yangu utayajibu , japo sidhani kama nitaweza kusoma kwa sasa. Ila ondoeni huo wingu unaotanda mkijua kuwa ndio mtaji wa wapinzani wenu kuwakosesha kura.

Pili, sijajua ile sera ya nyumba tano imeishia wapi na ni kwa kiasi gani inakuwa reinforced that was brilliant idea, na inawezekana

Tatu kitengo chenu cha siasa bado kiko poor katika vyama hicho kitengo ni kama ;department ya marketing kwenye makampuni kama Tigo. Tatizo sijaona kama mnachukua opportunity zilizopo kwa kiasi gani.Mathalan Sofia Simba alisema CCM mafisadi-mnaweza kuweka postal kubwa ya Sofia simba na kuandika maneno yake chini ''CCM wote mafisadi' na kuisambaza. Sijajua kama kuna kitengo kama hiki na sijajua kiko efficiency kiasi gani

Nne chukulieni kuwa Changamoto hizi ni kwa ajili ya nyie kukomaa na kukua.Forum hizi zinasaidia sana kuona watu wanawaza nini.Kupata kura ni ishu nyingine mkuu, hata ukijibu tuhuma zote na watu wote JF wakaelewa lakini kupata Kura is another art Kumbuka,

"The ballot is stronger than bullet" J.A.Schumpeter.

Tunataka mpate kura, THATS ALL

Kazi njema
 
Sababu zako binafsi ni "UDINI" kama kawaida unajificha sehemu tambarare

CUF siyo tishio..kwako..lol unafurahisha baraza au?...CUF ni wa pili kwenye uchaguzi wa serikali za mitaani uliopita...tlp sijui ni ya ngapi wapi na wapi?

Ibrahimu hajalaumiwa na wanachama for nepotism, kuonea wanachama wa CUF na ubadirifu wa fedha...lakini huyo jamaa yako mbowe na slaa kila siku wanachama wanalalamika je wakipewa dola..

Namna gani gani unaweza kuongoza na kuleta mambo kwa nchi yako ha ha ha ..hayo ni matokeo ya uadilifu wako binafsi na uadilifu wa taasisi yako..kusimamia hayo..tumeshuhudia CCM na Chadema kwenye swala la kusimamia uadilifu....wanaboa...long way to go for chadema as an institution.
ni wapi nimezungumzia udini, wewe na CUF wako mtajuana kama vikao vya kuhamasishana mnafanyia misikitini ama laah, ila nijuacho mimi moja ya malengo ya CHADEMA nikushika dola, kwa maendeleo ya Taifa, lengo letu sikupambana na vyama visivyo na dola.......
CCM wenyewe wanajua nani ni adui yao kwanza, maana wanapambana kwa nguvu zao zote.
 
Ngoja awaudhi wenye chama ndio atajua unachooongea..dogo bado anabebwa kwa nepi...

Awaudhi wenye chama kwa kukubali kununuliwa na RA ili awe anawapigia ndogondogo -- kumtetea kujananja katika ufisadi wake na kujaribu kuibomoa Chadema. Na kila mara huwa ni Mbowe dikteta, Mbowe anatafuna ruzuku -- hivi hakuna hoja nyingine? Hoja hii inachosha sana -- imeshatumika huko nyuma na wengi tu viongozi waliotimuliwa kutoka vyama vingine vya siasa kama NCCR, TLP, CUF etc.Halafu naunga mkono akina kafulia na huyu dandi ni sisimizi tu -- na nawahakikishia RA hatawajali tena, kwani hawawezi kumsaidia wakiwa katika chama ambacho kimepoteza kabisa mwelekeo -- yaani NCCR. Mbatia aliaibika Tarime kutokana na kukubali kuwa wakala wa CCM kujaribu kuizuia Chadema.mbatia aliweza kufanikiwa Pemba miaka kadha iliyopita alipoisaidia CCM kuchukua viti kule alikopiga kambi -- huku hao hao CCM wakimnyang'sanya kiti katika jimbo Kigoma. Akina Dandi wawe tayari kufanya hiyo kazi ya UWAKALA -- kwa RA na CCM!!!
 
ni wapi nimezungumzia udini, wewe na CUF wako mtajuana kama vikao vya kuhamasishana mnafanyia misikitini ama laah, ila nijuacho mimi moja ya malengo ya CHADEMA nikushika dola, kwa maendeleo ya Taifa, lengo letu sikupambana na vyama visivyo na dola.......
CCM wenyewe wanajua nani ni adui yao kwanza, maana wanapambana kwa nguvu zao zote.

Wewe na chadema mtajua kama vikao vyenu vya kuhamasishana ni kanisani au laah,! au uchagani

Malengo yenu si kupambana na vyama visivyo na dola...recall sherehe mliyofanya baada ya kumchukua Lwakatare! lol

CCM wenyewe wanajua nani adui yao wa kwanza! joking! CCM iwaogope viongozi ambao si waadilifu ambao bei yao ni kununua muasisis moja kutoka kilimanjaro na kubadilisha uamuzi mzima...wa chama kwa faida yake na familia yake...

CCM haina shida na mtu ambaye ni fisadi mwenzao kama mbowe ambaye anaweza kununuliwa kwa kufunguliwa biashara ya kuuza pombe...etc..get your record right..na inajua chadema hai-function kitaasisi (family show institution)
 
CHADEMA, HALI NI SHWARI...........
Kesho tutakuwa na Kongamano la Vijana, halafu kuanzia tarehe 30 Novemba, 2009 mpaka tarehe 3 Disemba 2009 tutakuwa kwenye mfululizo wa vikao vya juu vya chama tukiutathmini mwaka 2009 na kupanga mwelekeo wa chama kwenda mwaka 2010.
Vijana wote wapenda mabadiliko haya shime tuungane, maana adui yetu CCM ametangaza vita tayari kuelekea uchaguzi mkuu, tukutane kesho.
 
Tumaini

Asante kwa mchango wako, ugonjwa upi huo? Kelele zipi hasa unatushauri tuzingatie kama sauti maridhawa za kuchochea mabadiliko ndani ya CHADEMA na taifa letu kwa ujumla? Naomba uziweke kwenye mpangilio ili tuzielewe maana tuliwahi kufundishwa tukiwa watoto kuwa kelele ni sauti zisizo katika mpangilio maalum?

Iddi njema kwa watanzania wote hususan waislamu.

JJ

Si kweli kelele ni sauti zisizo na mpangilio maalum.

Kelele ni sauti yoyote iliyo ktk frequency(masafa) ambayo hupendelei kusafiri nayo na hayo masafa (frequency).

Mfano sauti yako inasikika na unapendelea kuisikia ikiwa ktk frequency(masafa) ya 40 Hz, hivo ikija sauti nyingine iliyo ktk mpangilio mzuri na sauti ya kuvutia na murua na iko ktk frequency (masafa) ya 100Hz,hii itakuwa kelele ktk bandwidth yako.

Kwa hiyo angalia unapoita sauti iliyo ktk frequency nyingine ni sauti isiyo ktk mpangilio unakosea sana maana unajilimit sana.

Na kwa kukushaurini fanyeni mpango wa kuzi intergrate pamoja hizo sauti zilizo ktk frequency tofauti.
 
Awaudhi wenye chama kwa kukubali kununuliwa na RA ili awe anawapigia ndogondogo -- kumtetea kujananja katika ufisadi wake na kujaribu kuibomoa Chadema. Na kila mara huwa ni Mbowe dikteta, Mbowe anatafuna ruzuku -- hivi hakuna hoja nyingine? Hoja hii inachosha sana -- imeshatumika huko nyuma na wengi tu viongozi waliotimuliwa kutoka vyama vingine vya siasa kama NCCR, TLP, CUF etc.Halafu naunga mkono akina kafulia na huyu dandi ni sisimizi tu -- na nawahakikishia RA hatawajali tena, kwani hawawezi kumsaidia wakiwa katika chama ambacho kimepoteza kabisa mwelekeo -- yaani NCCR. Mbatia aliaibika Tarime kutokana na kukubali kuwa wakala wa CCM kujaribu kuizuia Chadema.mbatia aliweza kufanikiwa Pemba miaka kadha iliyopita alipoisaidia CCM kuchukua viti kule alikopiga kambi -- huku hao hao CCM wakimnyang'sanya kiti katika jimbo Kigoma. Akina Dandi wawe tayari kufanya hiyo kazi ya UWAKALA -- kwa RA na CCM!!!

Umenena ndugu yangu -- ingawa huyo dandi bado hajaenda NCCR. Labda ataenda CUF -- lakini kule pia RA ana mkono. Tumeliona hilo.Lakini kuondoka kwa kiongozi/mwanachama kutoka chama cha siasa ni hiari ya mtu, na hakuna haja ya kuondoka kwa maneno, matusi nk. Hii imekuwa ndiyo utamaduni wa siku hizi, hawezi kiongozi kuondoka kimyakimya kutoka katika chama bila kuwabwatukia viongozi wa juu.Itakumbukwa huko nyuma guninita alitimuliwa Chadema na alibwatuka hayo hayo -- utafunaji wa ruzuku. Kumbe alikuwa kihiyo wa kutupa! Mwingine ramadhani Mzee alitimuliwa CUF na akataja hayo hayo ya kutafuna ruzuku. Hivi yuko wapi huyu?Ninachotaka kusema ni kwamba hao na wengine waliondoka hakukutokea kukuzwa au maneno mengi magazetini nk na masuala yalisahauliwa kwa siku chache tu. Siku hizi "sisimizi" (nami nakubali ni sisimizi) akiondoka Chadema, basi linakuwa jambo kubwa kweli kweli -- magazeti ya RA yanaliendeleza mpaka vichwa vya habari vinasikitisha na kutia doa katika fani ya uandishi. lakini sababu ya hii inajulikana -- ufisadi tu.
 
CHADEMA, HALI NI SHWARI...........
Kesho tutakuwa na Kongamano la Vijana, halafu kuanzia tarehe 30 Novemba, 2009 mpaka tarehe 3 Disemba 2009 tutakuwa kwenye mfululizo wa vikao vya juu vya chama tukiutathmini mwaka 2009 na kupanga mwelekeo wa chama kwenda mwaka 2010.
Vijana wote wapenda mabadiliko haya shime tuungane, maana adui yetu CCM ametangaza vita tayari kuelekea uchaguzi mkuu, tukutane kesho.
Siyo vibaya kijipa moyo...endelee

Je unaonaje ukianzia kanisani na uchagani kuhamasisha watu kuja huko ..lol just curious
 
Umenena ndugu yangu -- ingawa huyo dandi bado hajaenda NCCR. Labda ataenda CUF -- lakini kule pia RA ana mkono. . Kumbe alikuwa kihiyo wa kutupa! Mwingine ramadhani Mzee alitimuliwa CUF na akataja hayo hayo ya kutafuna ruzuku. . Siku hizi "sisimizi" (nami nakubali ni sisimizi) akiondoka Chadema, basi linakuwa jambo kubwa kweli kweli -- magazeti ya RA yanaliendeleza mpaka vichwa vya habari vinasikitisha na kutia doa katika fani ya uandishi. lakini sababu ya hii inajulikana -- ufisadi tu.
kumbe kuna mafungamano , sasa naanza kuelewa haya mambo.....
 
Wapendwa wanaJF wenzangu:

Nimekuwa mchangiaji wa nadra sana wa JF kutokana na sababu ambazo nilishawahi kueleza hapa siku za nyuma, mojawapo ukiwa ni ushauri wa baadhi yenu ambao niliuheshimu.

Nimekuwa msomaji wa majadiliano yanayoendelea kuhusu mustakabali wa taifa letu, na katika baadhi ya mijadala imetajwa CHADEMA na jina langu limekuwa likijitokeza tokeza. Aidha baadhi yenu mniandikia ujumbe nije hapa kufafanua baadhi ya mambo yanayohusu CHADEMA hususani yale yanayonihusisha kwa namna moja au nyingine.

Niliwahi kuandika hapa kwa kirefu naichukuliaje JF, lakini moja ya mtazamo wangu kuhusu JFni kuwa hivi ni chombo cha habari, pia ni kama kijiwe cha kijamii cha mijadala, lakini pia ni kama mkutano wa majadiliano katika mji(town hall meeting), naitazama pia JF kama mkutano wa hadhara ambao kila mmoja yuko huru kuhutubia!.

Katika muktadha huo, kama ambavyo nashiriki mijadala katika matukio yenye sura ya hayo hapo juu, najihisi nina wajibu kwangu binafsi na kwenu kuja kushiriki mijadala mara kadhaa.

Kwa kuanzia nawaletea taarifa hii rasmi, ambayo nimeitoa leo kwa niaba ya ya CHADEMA. Taarifa hii inajibu baadhi ya maswali ambayo yamekuwa yakiulizwa hasa kuhusu yanayoendelea ndani ya chama katika siku za karibuni.

Tamko hilo mnaweza kulipata kwa kubonyeza hapa: http://www.chadema.or.tz/habari/habari.php?id=103

Kesho tutakuwa na Kongamano la Vijana, halafu kuanzia tarehe 30 Novemba, 2009 mpaka tarehe 3 Disemba 2009 tutakuwa kwenye mfululizo wa vikao vya juu vya chama tukiutathmini mwaka 2009 na kupanga mwelekeo wa chama kwenda mwaka 2010.

Hivyo, naomba muendelee na mjadala na kama kuna maswali yatakayoulizwa nitakuja kuyajibu moja baada ya jingine baada ya tarehe hizo.

Salamu zangu za baraka ya Iddi kwa waislamu, ni siku nzuri ya kutafakari aya kwenye kurani tukufu mathalani Al Heed 57:25, Al-Nisa 4:35, Al-Maidah 5:8

chadema pambaneni sana maana hizi gharika ni vitu vya kawaida. Kwani katika kondoo kuna na mbuzi hivyo hivyo kujua kondoo ni yupi na mbuzi ni yupi ni kazi kubwa. Cha muhimu wekeni misingi bora itakayowezesha kondoo kuchujwa kwa urahisi. Upinzani ni kawaida ila upatapo upinzani unajua jinsi ya kujipanga kwani huwa unaonyesha mapungufu yako na ya adui.
 
Hivi kwanini watu wapenda sana ushabiki? Issue ya mbowe kuwa fisadi ilishaongelewa hapa jamvini sasa watu wanarudia ili kubadilisha mada au? Wewe ukisema kuwa CHADEMA mfano wanachama wake wanalalamika kuwa mbowe, slaa ni wadini, mafisadi, wanatumia hela la ruzuku vibaya. Je wanachama kwanini wanawapigia kura? Kwanini hawaambiwi haya kwenye vikao tena vya wazi siyo vya siri kama vya chama fulani? CUF huwezi kuilinganisha na Chadema kwani inanguvu sehemu zenye waislamu wengi hilo halina ubishi. Mifano michache zanzibar, kondoa, rufiji, temeke, mikoa ya kusini. Huwezi kukuta CUF imefanya vizuri mikoa ya kaskazini labda mtu awe anakubalika hivyo watu wamchague. Hata Lwakatale kushinda mwaka 2000 ni kwasababu kulikuwa na support ya chadema pia.

Tumezoea sasa kila chama kinapojaribu kusimama kinashambuliwa plus kuplant mamruki ili kiyumbe kife cheki NCCR, TLP, CUF na sasa wanafanya kwa CHADEMA. Lakini for information chama hiki kiko makini hivyo sidhani kama kitayumba.
 
Alisema ndani ya Chadema kuna makundi mawili, kundi la Mbowe lenye maisha mazuri na magari ya kifahari na lile la Zitto lenye wanachama wanaomuunga mkono mwanasiasa huyo.


Huyu Ms Nsanzugwanko anajua anachosema? Kundi la Mbowe lina maisha mazuri na magari ya kifahari halafu la Zitto lina wanachama wanaomuunga mkono.

Jamani! Mambo ya Chini Ya Muti School of Journalism.
 
Back
Top Bottom