CHADEMA mwendo mdundo

CHADEMA mwendo mdundo

Hivi kwanini watu wapenda sana ushabiki? Issue ya mbowe kuwa fisadi ilishaongelewa hapa jamvini sasa watu wanarudia ili kubadilisha mada au? Wewe ukisema kuwa CHADEMA mfano wanachama wake wanalalamika kuwa mbowe, slaa ni wadini, mafisadi, wanatumia hela la ruzuku vibaya. Je wanachama kwanini wanawapigia kura? Kwanini hawaambiwi haya kwenye vikao tena vya wazi siyo vya siri kama vya chama fulani? CUF huwezi kuilinganisha na Chadema kwani inanguvu sehemu zenye waislamu wengi hilo halina ubishi. Mifano michache zanzibar, kondoa, rufiji, temeke, mikoa ya kusini. Huwezi kukuta CUF imefanya vizuri mikoa ya kaskazini labda mtu awe anakubalika hivyo watu wamchague. Hata Lwakatale kushinda mwaka 2000 ni kwasababu kulikuwa na support ya chadema pia.

Tumezoea sasa kila chama kinapojaribu kusimama kinashambuliwa plus kuplant mamruki ili kiyumbe kife cheki NCCR, TLP, CUF na sasa wanafanya kwa CHADEMA. Lakini for information chama hiki kiko makini hivyo sidhani kama kitayumba.


Michango hii inafurahisha sana.
Kwanini RA anapigiwa kura? kwanini wananchi hawaambiwi ktk vikao vya wazi??
 
Nani kasema kosa la jinai, kwanza ndo nalisikia toka kwako.Acha upotoshaji kubali chalenges
Ninyi mliodai apelekwe jela. Ninavyofahamu mtu hupelekwa jela kwa kosa la jinai na si kwa kusema uwongo au kukashifu.
 
Nimeaga nimerudi tena kidogo tu nitoe jibu la sentensi moja: NAAMINI WAZEE WALIMSHAURI ZITTO AJITOE NA ZITTO AKAKUBALI KWA SABABU CHADEMA NI ZAIDI YA MBOWE NA ZITTO. Alamsiki, siku nyingine Kituko.

JJ
Basi hapo hao wazee wenu mnaowaita ndipo walipo chemka. Wangeacha kura ziamue,na wewe kama unawasupport wazee upo wrong kabisa. Demokrasia si kuamuliwa na wazee, demokrasia ingeamuliwa na wanachama cha demokrasia[CHADEMA]
 
Wewe na chadema mtajua kama vikao vyenu vya kuhamasishana ni kanisani au laah,! au uchagani

Malengo yenu si kupambana na vyama visivyo na dola...recall sherehe mliyofanya baada ya kumchukua Lwakatare! lol

CCM wenyewe wanajua nani adui yao wa kwanza! joking! CCM iwaogope viongozi ambao si waadilifu ambao bei yao ni kununua muasisis moja kutoka kilimanjaro na kubadilisha uamuzi mzima...wa chama kwa faida yake na familia yake...

CCM haina shida na mtu ambaye ni fisadi mwenzao kama mbowe ambaye anaweza kununuliwa kwa kufunguliwa biashara ya kuuza pombe...etc..get your record right..na inajua chadema hai-function kitaasisi (family show institution)
kwani unabisha kua Vikao vya CUF hufanywa misikitini, kwani kunapokua na maandamano kwa nini vipeperushi husambazwa misikiti yote.
Uongozi wote wa CUF ni waislamu tena nasikia kuna harufu ya pesa chafu toka kwa vyama vya Mujahidina kule arabuni.
 
kwani unabisha kua Vikao vya CUF hufanywa misikitini, kwani kunapokua na maandamano kwa nini vipeperushi husambazwa misikiti yote.
Uongozi wote wa CUF ni waislamu tena nasikia kuna harufu ya pesa chafu toka kwa vyama vya Mujahidina kule arabuni.
Kwani unabisha kua vikao vya Chadema hufanywa kanisani kwani kunapokuwa na maandamano kwanini vipeperushi husambazwa makanisa yote

Uongozi wote wa chadema ni wakristo tena nasikia kuna harufu ya pesa chafu kutoka vyama vya lord resistance army kutoka kule vatican city
 
Kwani unabisha kua vikao vya Chadema hufanywa kanisani kwani kunapokuwa na maandamano kwanini vipeperushi husambazwa makanisa yote

Uongozi wote wa chadema ni wakristo tena nasikia kuna harufu ya pesa chafu kutoka vyama vya lord resistance army kutoka kule vatican city
Mwenyekiti ni Freeman Mbowe
Makamu mwenyekiti znz: Said Issa Mohamed
Makamu mwenyekiti bara: Said Arfi 315
Hao ndio viongozi wakuchaguliwa, sasa leta viongozi wako wajuu hapo CUF
 
‘Zitto haondoki Chadema’
Imeandikwa na Na Lucy Lyatuu; Tarehe: 28th November 2009 @ 19:59

Habari Leo

KAIMU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleao (Chadema), John Mnyika amewahakikishia wanachama wao kuwa Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe hakusudii kukihama chama hicho.

Aidha, Mnyika pia amedai kuwa chama hicho kimefanyiwa propaganda za kukichafua zinazoendana na Uchaguzi Mkuu wa 2010.

Mwanasiasa huyo kijana alitoa kauli hiyo jana katika taarifa aliyoitoa kwa vyombo vya habari kujibu tuhuma zilizotolewa na aliyekuwa kiongozi wa Mambo ya Bunge wa chama hicho, Juju Danda ambaye alijiondoa katika chama hicho.

Juzi Danda alijiengua katika chama hicho na kumtuhumu Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe kwa kukigeuza chama hicho kama kampuni yake na kwamba Zitto yuko njiani kukihama.

Kiongozi huyo ambaye ni wa pili kujiengua katika chama hicho baada ya aliyekuwa Ofisa Habari wa Chama hicho David Kafulila, pia alishauri Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, (CAG) akague mahesabu ya chama hicho ili aoneshe alichodai kuwa ni ubadhirifu wa ruzuku za chama hicho.

Akizungumzia hali hiyo, Mwenyekiti wa chama cha TLP, Augustine Mrema amewataka viongozi wa CHADEMA kuacha alichodai kuwa ni jeuri na ubabe badala yake waungane ili kukiokoa chama hicho ambacho alidai kiko katika hali tete ya kudidimia.

Mrema alisema hayo jana Dar es Salaam wakati akitoa ushauri kwa viongozi wa chama hicho ambao hivi karibuni chama chao kimekumbwa na sakata la kujivua uanachama kwa baadhi ya wanachama wa chama hicho.

“Ushauri wangu wa bure kwa Mtei (Edwin), Mbowe na Dk. Slaa waelewe kuwa mambo yanaelekea kubaya, chadema inaporomoka, hivyo acheni jeuri na ubabe ili muokoe chama hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu,” alisema Mrema.

Aliongeza kuwa viongozi hao wafanye masahihisho na kuhakikisha wanawarejesha vijana waliowatimua katika chama hicho, waelewe kuwa hao ndio nguvu kazi ya chama na kwamba wasione aibu kwani pindi Zitto akitoka, chama hicho kitabaki historia.
 
Hayo ni mawazo ya Mtanzania anaejisifu kuwa na upeo, amakweli kunufaika kwako na UFISADI Kumekutia kiwi cha macho, unadhani kama hali ya klisiasa ikiharibika utaona thamani ya hako kaposho kako, siasa inaathiri kila nyanja, waulize Zimbabwe kama kuna mtu wa ZANU PF aliefaidi wakati wa crisis, mimi ni mwanachama wa chama cha siasa maana sio kosa, wewe unategeme mshahara mwisho wa mwezi sio kosa, ila tambua siasa inaathiri mifumo yote ya maisha.

Kutokuwa mwanachama au mfuasi wa chama chochote cha siasa haimaanishi kwamba haufuatilii siasa! Nafikiri ili ni tatizo mojawapo kubwa sana hapa JF ndio maana mtu akionekana kupinga baadhi ya mambo ya CHADEMA ataambiwa yeye CCM, na akipinga ya CCM ataambiwa ni CHADEMA, the list goes on. Hali hii imejengeka katika misingi ya kutopenda kukoselewa kwa tulio wengi hivyo kushindwa kutambua uhuru wa mtu kukosoa bila kujali ni mlengo upi au chama gani kitaathirika. Kwa maelezo yako hapo juu ni kama vile ili aweze kutoa comment zozote za kisiasa au kukosoa ni lazima awe mwanachama wa chama fulani! Kwanini hatuwezi kufikiri kwamba mtu anaweza kuwa independent when it comes to politics?! Kwa maoni yangu, Independents ni watu muhimu sana katika mfumo wowote wa kiasa wenye kujali demokrasia ya kweli. I'm proud to be one of them.
 
Akizungumzia hali hiyo, Mwenyekiti wa chama cha TLP, Augustine Mrema amewataka viongozi wa CHADEMA kuacha alichodai kuwa ni jeuri na ubabe badala yake waungane ili kukiokoa chama hicho ambacho alidai kiko katika hali tete ya kudidimia.

“Ushauri wangu wa bure kwa Mtei (Edwin), Mbowe na Dk. Slaa waelewe kuwa mambo yanaelekea kubaya, chadema inaporomoka, hivyo acheni jeuri na ubabe ili muokoe chama hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu,” alisema Mrema.

Mzoefu wa kuua vyama Mrema, na yeye pia ameona kasheshe la CHADEMA lakini bwana mdogo Mnyika anatuambia eti mambo yote shwari, who do you think you are lying to. For CHADEMA to survive, just like the original NCCR, Mbowe and Mtei had to go.
 
Unajua mara nyingi kila naposoma hoja za watu kama LibabaPM, hunipa fikra za kufikiria pengine kuna ukweli kuwa Chadema ni chama cha Kikristu ama cha Kidini..Hoja hapa inazungumziwa matatizo ya Chadema inakuwaje watu mnaingiza maswala ya CUF as if kuna mashindano..Wanachoshindwa kuelewa watu kama Libaba ni kwamba wao wanaandika hapa kama wakristu hivyo kuwakilisha mawazo ama msimamo wa wanachama wa Chadema against CUF au CCM..Hatuwezi kujenga nchi kwa fikra finyu kama hizi, hata kama Tumain ni CUF na Muislaam ni lazima Chadema wayatazame matatizo yao kama chama na sii kujilinganisha na CUF au Tumain ambaye tayari mmekwisha mbatiza chama na dini yake.

Kuna tatizo kubwa sana ndani ya Chadema na hili haliwezi kuepukwa kwa kuandika sana hapa JF ama ktk magazeti na muhimu sana tuyaweke wazi bila kumwonea mtu aibu wala kumung'unya maneno.

1. Kwanza kabisa Zitto has become a thorn...
Yeye kama kiongozi na mwana Chadema anafanya mambo mengi sana kinyume, kama vile ni mbunge Independent jambo ambalo linamweka katika kona ya kuta mbili za kisiasa..Ni makosa makubwa sana kwa kiongozi yeyote kutangaza msimamo wake ktk magazeti kinyume cha makubaliano ndani ya chama unless mtu huyo anataka kujiengua.
Nimemsoma sana Zitto ktk maswala mbali mbali na hasa kuhusiana na majukumu alokabidhiwa na bunge amekuwa akitoa maoni yake binafsi pasipo kufikiria kwanza maslahi ya Upinzani..
Inaonyesha wazi hafahamu maana ya Upinzani na kwa nini ameshiriki ktk kamati hizo za bunge kuwakilisha Upande upi..CCM hawashindwi kuweka wajumbe wote wa kamati hizi toka chama chao na hawana sababu ya kufanya hivyo isipokuwa ni kutokana Upinzani unaotazama upande wa pili wa sarafu moja kuleta hoja zao kuipa sura inayokubalika hiyo sarafu.

Zitto kisiasa anachemsha sana inapofikia hapa..(maswala ya Umeme) Kufikiria kwamba unaweza kuwa independent kuwakilisha kamati hizi hali, yeye ni mteule kutokana na uwakilishi wa chama chake na sii kwa sababu yeye ni Zitto..hivyo ni makosa makubwa kisiasa kuwa independent mahala ambapo unawakilisha Ubunge wa chama.. Hilo lazima alikubali na ajirekebishe laa sivyo sioni sababu yake kubakia Chadema kama kiongozi kwani atakivuruga chama. Inabidi awe mgombea independent kuwakilisha mawazo yake binafsi, na ndio maana halisi ya mbunge independent.

2. Viongozi wa Chadema..
Hawa pia wamekuwa na matatizo makubwa sana kujieleza wazi ktk maswala yote wanayotuhumiwa. Wanachokifanya hakina tofauti na viongozi wengine wote wanaojaribu kuweka pazia ktk machafu ambayo wanatuhumiwa.. Mbowe ni mshikaji na nampa heshima zote kama kiongozi, lakini inapofikia hali mbaya kama hii ni muhimu sana ajitenge na uongo...kukaa kimya hakuwezi kuondoa matatizo na wala sii sifa nzuri ya kiongozi... Ni hadithi kama hizi tunazotufanya wengi tufikirie Kikwete sii kiongozi mzuri kwa sababu hakubali ukweli na wala hata siku moja hajihusishi na hoja nzito zinazowahusu watu wake wa karibu.

Rostam akiwa mweka hazina wa CCM alishutumiwa kwa mengi sana na ndiye haswa aliyeharibu jina la Kikwete kwa sababu ya kinga aliyomwekea. Ni huyu huyu Rostam anaye sababisha mvurugano mkubwa ndani ya CCM toka awe mweka hazina hadi kuenguliwa..Hali kama hiyo naiona tena Chadema, ambako kuna huyu mweka fedha mwingine - KOMU asiyewezekana. Simjui, lakini ajabu ni kwamba ktk vijiwe vyote sijawahi kuona watu wakimzungumzia huyu mtu wakati kila jina la Mbowe linapotajwa huyu Komu huwa ndiye kiambatanisho. Who is he?

Kwa hiyo Mbowe , Dr. Slaa, Mzee Mtei pamoja na viongozi wote ndani ya CVhadema wanaposhindwa kuyatazama madai na kuyapa kipaumbele ktk kurudisha hadhi ya chama, basi sintashangaa kusikia Chadema imesambaratika. Na hakika lawama zote zinatakiwa kupewa Uongozi wa chama kwa kushindwa kuthibiti lawama zote zinazo kielemea chama..
 
Uko sahihi Nguvumali

1.Migogoro haikosi

2.Tunataka viongozi watakaoweza kumaliza hii migogoro in peaceful manner, bila kuharibu saikolojia ya wanachama wao,mathalan , leo unasema Kafulila anatoa siri za chama-kupitia magazetini.Kesho unataka same Kafulila abaki ndani ya chama na akitoka asiseme kitu.Makosa

3.Chadema iwe na usiri sana katika kila kitu, ni chama kinaangaliwa kama dhahabu ya Mwanza! CCM kumbukeni bado wana hasira ya kuwataja mafisadi! na wanataka watoto wao waje kushika madaraka!,SIRI ZA CHADEMA NI MUHIMU akipatikana mto siri(ikawa proved) mwiteni mwonyeni,kwa siri... siyo tunasikia kuna vikao vya siri sehemu.Chadema kama chama hakiwezi kikamfanyia kikao cha siri KAFULILA WHO IS THIS GUY?? tabia hii kwa sisi wengine tunashtuka kama kuna uwazi, katiba inajulikana, ANAOGOPEWA NINI MPAKA MFANYE KIKO CHA SIRI PASI YEYE KUJUA?? HII NI DALILI YA CHAMA CHA WATU WACHACHE MKUU, sauti ya pamoja usema kwa pamoja kwa mujibu wa katiba yenu!

4.Chadema , iwe na vision ya muda mrefu, kwa mfano sijaona uhumuhimu wa kutangaza uchaguzi kama wazee walishaona Mbowe aendelee! simple and clear, waambieni wanachama jamani, tutafanya uchaguzi wa Mwenyekiti baada ya miaka 15! mkiamua wote kwa pamoja hizi kelele zisingekuwepo mkuu!
Nafikiri hapa unakosea, usiuite uchaguzi. Hakuna uchaguzi wa mtu mmoja bila alternative, ilikuwa mkutano wa kumtambulisha mwenyekiti.
 
Nimeaga nimerudi tena kidogo tu nitoe jibu la sentensi moja: NAAMINI WAZEE WALIMSHAURI ZITTO AJITOE NA ZITTO AKAKUBALI KWA SABABU CHADEMA NI ZAIDI YA MBOWE NA ZITTO. Alamsiki, siku nyingine Kituko.

JJ
Kwa nini wasimshauri Mbowe ajitoe?
 
Ulishaharibu mkuu, mbaya zaidi wewe ni injinia wa forums

Forum; A public facility to meet for open discussion-SAGE

Ulichofanya mara ya kwanza hakikuwa 'forum' ila ushabiki.kama wewe unaonyesha mfano huu, mkuu tutegemee nini kuja humu?

Hata kama una ushabiki weka kando, kwa nafasi yako ndani ya JF..wewe uwe kama mwenyekiti wa 'debate' kama mtu hajatukanwa whats wrong?

I am dissaponted!

Na usije kwa mamlaka yako ukanifungia au kunizushia mambo ya ajabu
Waberoya,
Nafikiri unaconfuse kati ya "Invisible" (the MOD) na "The Invincible" (JF Member kama wewe na mimi).
 
Ni kweli Zitto sio mtu wa kuhama Chadema, unless otherwise na sio leo au kesho!
 
John,
Kelele ni sauti zisizo na mpangilio au sauti ambazo hupendi kuzisikia (kero) inategemea uko upande na unapenda kuchukua definition ipi? nakupa mfano:-

Ukiwa polisi mzuri wewe ni kelele (kero) kwa majambazi unaleta usumbufu

Ukiwa kiongozi ambaye si muadilifu (mla rushwa, asiye toa haki na fursa sawa kwa watu wake, mbabe) wanao dai mabadiliko na haki zao ni wapiga kelele (kero)

Sasa kwa chadema na wewe ...wale wote wanaondoka, wanaoondolewa kwa kukosa uhuru, haki na wenye vyeo including yourself mtasikia kelele hizo kila siku kwakuwa ni human nature kudai haki na fursa zilizo sawa na heshima mbele ya jamii

kuita wanachama sisimizi baada ya kuacha kazi kwenye chama chenu ni dalili kwamba hakuna viongozi hapo wenye vision na ambao watavumilia uhuru wa mtu ila ni kikundi cha wababe na wahuni wanaotaka dola itakuwaje tukiwapa jeshi,polisi nk...si mtaua watu wakiwa tofauti na nyinyi ..shame on you and your leaders! esp.slaa and mbowe si wavumilivu

kupuuzia madai ya ufisadi wa matumizi ya fedha ya chama na upendeleo wa kikanda bila kufanya jitahada za maalum kupata wanachama upande mwingine wa nchi (zenj) ni dalili chafu na ni kelele kwenu nyinyi mliopewa dhamana...kwa sasa

Hamuwezi kusikia, wala hamuwezi kuona(sikio la kufa haliskia dawa) kwakuwa mko ndani mnadanganyana chadema ni family club poleni..sana you have long way to go ...
Tumain salaam,
naona uchangiaji wako umeegemea zaidi kwenye personal attacks na ushabiki.tuhuma unazozitoa kwa viongozi wa chadema ni majungu na fitna ambazo hazina proof zozote.mwenyekiti wa chadema tayari keshasema wako tayari kuruhusu mkaguzi wa mahesabu au mtu mwingine mwenye wasiwasi kwenda kukagua mahesabu ya chama.Hao wakina kafulila na wenzake ni njaa za madaraka,pesa na kutaka umaarufu kupitia migongo ya watu.Ni watu wadogo sana ndani ya chama na ndo maana slaa akawaita sisimizi.kwa taarifa yako chadema haitakufa wala kuyumba kwasababu ya hao wakina kafulila kuondoka.Hongera kamanda Mnyika kwa kutoa maoni yako na kutujulisha mambo yanayojiri ndani ya chama.keep it up!
 
Wangapi wametimka? Au ndiyo huu uandishi wa Bongo wa wishful thinking?
 
Ndugu yangu Kituko,
utakuwa unamatatizo ya akili kama kweli unafikiria Zito anauwezo wa kuwa mwenyekiti wa chama kwa sasa.kuwa mzungumzaji mzuri majukwaani hakumfanyi awe na sifa za kuwa mwenyekiti.it need more than that.uwenyekiti wa chama si mchezo hata kidogo wewe.una upeo mdogo sana wa kufikiria na huangalii mbali.una ushabiki wa kitoto bila kuchambua mambo kiundani
 
Back
Top Bottom