CHADEMA na Udikteta Makao Makuu


tumeshindwa kuelewana sikuwa na maana kuwa mkjj ametetea CHADEMA kwenye hii thread nimemtolea mfano kwa sababu wanamlaumu sana kuwa ni mtetezi wa CHADEMA kama KADA anavyolaumiwa kwa CCM, pole kwa hilo
 

Mwafrika wa Kike,
Hebu acha uvivu kidogo na usome hizo pages nilizokupatia. Maeneo ya kila mhusika anakotoka yameandikwa. Kweli waafrika tunachukia kusoma.

Halafu kama posting ya matumizi ya Chadema ya mwaka 2005, tena yenye nia tu ya kuwaumbua CCM, ni valid kwa matumizi ya 2008 na inatatua manung'uniko na makunyanzi ndani ya chama, basi nafikiri hakuna sababu ya kuchapisha tena matumizi yao, milele na milele. CCM kama waliwahi kuchapisha hata kama ni wakati chama kikitwa TANU, basi inatosha hadi leo. Hii argument yako inafurahisha sana.
 


Mkuu KJ,

Point yako nimeigusa kuwa kama the idea ni ku-balance ishus, basi ziwe ishu za uhakika, tuache uvivu wa kutafuta ishus na kutegemea internent, tuende tutafute real ishus against Chadema, so far sijaiona ya maana ya kuweza kuiweka meza moja na za CCM,

Seif, Lipumba, na Mrema hata wangekuwepo bungeni leo wasingefanya kitu maana wote walishapitwa na wakati, wote walishashika nafasi nzito sana serikalini na CCM, hebu onyesha one thing walichofanya kinachoweza kumshawishi mwananchi kuwa wanafaa? Nothing! Hao nao wajitoe ili kina Duni waingie huko CUF na kuleta akili mpya,

Maneno yako ni kweli, lakini tatizo ni kwamba ishu mnazowashambulia nazo upinzani ni weak sana the matter of fact ni completely none ishus kwa taifa letu, especially at this time, kwa hiyo fanyeni basi home work nzito, otherwise turudi kwenye kumkoma nyani wakuu, kuanzia juzi tumepiga kelele kuhusu Chenge, si umeona leo CCM wajikanyaga, kwa hiyo tuendelee kumkoma nyani wakuu taifa liko njia panda!

Lakini tafuteni ishu za kweli na nzito, hizi za viongozi njaa waliotemwa huko ni none ishus kwa taifa, maana hata kina Tambwe nao walisema hizo hizo, motive yake ni nothing but njaaa ya binafsi, sio ya taifa!
 

Unaona sasa. Jitahidi uwe unasoma. Umesema ruzuku iliyochapishwa ni ya matumizi ya 2010 tu? Mbona hii hapa ya 2008 nayo imesemwa?
"Kwa msingi huo tunapenda kuwataarifu watanzania kuwa CHADEMA katika uchaguzi huu tumetumia shilingi milioni 48, milioni 15 ikiwa ni mchango wa chama na milioni 33 ikiwa ni michango ya wanachama"

Halafu ujue kwamba hizi ni za uchaguzi. Kila Kamati Kuu CHADEMA inatoa taarifa ya matumizi. Na mara mbili kila mwaka kwa Baraza Kuu. Jiunge na CHADEMA kama mwanachama utapata? Sasa jiulize lini Chama Cha Mafisadi kimewaeleza wanachama wake matumizi? Halafu soma pia sheria inavitaka vyama kufanya nini.

Ama kwa madai yako ya UKABILA nimekwambia utoa ushahidi wa kwamba sekretariati imejaa wachagga, na kwamba wabunge wa viti maalum wote ni wakilimanjaro. Links ulizozitoa zote zimeonyesha sivyo. Ukweli ni kuwa ukitazama majina ya watendaji makao makuu; wasukuma ni wengi zaidi. Tumbo, Mnyika, Sabula, Shija, Kafulila nk. Na kwenye viti maalum, ni kweli watu wenye asili ya uchagga ni wengi lakini si wote. Wako sita; wenye asili ya kilimanjaro ni wanne, na wawili wana asili tofauti kabisa. Na hata hao wanne wenye asili ya uchagga, aliyetokea kilimanjaro ni mmoja tu; wengine watatu wameteuliwa kutoka Dar es salaam na wanajulikana kabisa kuwa ni wakazi wa DSM miaka na miaka. Inasemekana wawili kati yao hata kichaga hawakijui kabisa

Asha
 
Si kweli kwamba CHADEMA imejaa Wachagga!

Kwa akili za kawaida, shutuma kwamba CHADEMA imejaa wachaga maana yake ni kwamba CHADEMA ina viongozi na wanachama wengi wachagga kuliko kabila lolote hapa Tanzania. Je ni kwa kiasi gani kauli hiyo ina ukweli?.

Katika safu ya juu ya uongozi wa kitaifa wa CHADEMA yenye viongozi sita: wenyeviti na makatibu mchaga ni mmoja tu-Mwenyekiti wa chama Taifa, Freeman Mbowe. Viongozi wengine wanatoka makabila mengine kama MuIraq, Myao, Mpemba na Mu-Unguja.

Aidha katika sekretariati ya chama taifa ambacho ndio chombo kinachosimamia utekelezaji wa kila siku wa shughuli za chama kikiwa na kurugenzi 9, kati ya wakurugenzi wake mchaga ni mmoja tu. Na wasukuma ni watatu. Kwa nini hawasemi kwamba CHADEMA ni chama cha wasukuma?

Kadhalika mpaka sasa Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe ameteua wajumbe wanne wa Kamati Kuu, kati yao hakuna mchaga hata mmoja na kati yao wawili ni wahaya, Profesa Mwesiga Baregu na Balozi Ngaiza. Kwa nini hawakusema kwamba CHADEMA ni chama cha wahaya?

Kwa upande mwingine kwa mujibu wa matokeo ya uchaguzi uliopita, jimbo ambalo CHADEMA iliongoza kwa uwingi mkubwa zaidi wa kura ni Tarime ikiwa asilimia zaidi ya 64. Kama CHADEMA ni chama cha wachaga kwa nini jimbo la kwanza lisingekuwa la mkoa wa Kilimanjaro?

Kati ya majimbo kumi ambayo CHADEMA ilifanya vizuri zaidi, jimbo la Kilimanjaro ni moja tu la Moshi mjini huku mikoa kama Kigoma, Rukwa ikiwa na majimbo mawili ambayo CHADEMA imefanya vizuri zaidi.

Kama CHADEMA ingekuwa chama cha wachaga si ingefanya vizuri zaidi katika majimbo ya Kilimanjaro?

Je, wanataka kutuambia kuwa Mara, Kigoma, Rukwa na mikoa mingine ambayo CHADEMA imefanya vizuri kote kumejaa wachaga?

Kwa mantiki hiyo basi, si kweli kwamba CHADEMA ni chama kilichojaa wachaga. CHADEMA ni chama cha kitaifa. Kinachojumuisha wanachama na wapenzi wa asili na hali mbalimbali.

Soma zaidi hapa:http://www.chadema.net/tamko/2007/mwanri.php
 
Asha,
Inaelekea wewe ni mndani kabisa wa Chadema, jambo ambalo ni zuri na litasaidia kufikisha haya malalamiko.

KJ

Umesema vyama vilipoanzishwa vimeanzishwa kwa malengo ya kikabila, kimajimbo na kidini- PROVE KAMA CHADEMA ilianzishwa kikabila.

PROVE kwamba CHADEMA ilianza na misingi mibaya tofauti na katiba yake.

Hapa nakuletea makala ya Mzee Mtei aliyoiandika mwaka 2005, itakupa historia kiasi ya kuanzishwa kwa CHADEMA.
CHADEMA NI NINI NA NI NANI

 
Bi. Asha pole sana, majibu uliyotoa yametolewa hapa mwaka mmoja na ninakuhakikishia miezi michache ijayo atakuja mwingine na madai yale yale. Sasa utachoka wangu, next time ni bora kuwapatia link tu maana wengine ni wavivu hata kubonyeza keyboard kutafuta majibu wao wenyewe. Ukiwaambia nenda kwenye tovuti inakuwa kama umewatumia kisimani kuchota maji!
 


Heshima Mbele Asha,

Nashukuru kwa maelezo yako ingawa hata hivyo bado hayatatui madukuduku yaliyomo ndani ya baadhi ya wanachama na wapenzi wa Chadema. Naomba uelewe haya mawili;
  1. Hakuna matumizi yoyote yaliyopo kwenye www ya Chadema zaidi ya yale ya uchaguzi wa mwaka 2005 ambayo yaliwekwa zaidi kuiumbua CCM. Kama yapo nipe link ili tumalizane. Malalamiko yaliyotolewa ni kuwa, mikoani hawapati ruzuku ukilinganisha na makao makuu. Hili ndio la kujibu. Kama matumizi ni uchaguzi tu, basi Chadema hawatashinda hata siku moja, maana mpiga kura huandaliwa mikoani kabla ya uchaguzi.
  2. Kuhusu ukabila, hili liko wazi na ndio maana linapigiwa kelele mwaka hadi mwaka. Kama Chadema wanataka kulifumbia macho, ni juu yao, lakini lipo. Wewe mwenyewe unakiri kuwa kati ya wabunge 6 wa kuteuliwa, 4 wanatokea ya Kilimanjaro, kwa hiyo kama huoni kuwa hili ni doa, basi huwezi kuona mengine. Si unajua tena ukipenda hata chongo inakuwa ni kengeza.
Mwanakijiji amesema vema, ingawa alikuwa na nia ya kukutetea lakini badala yake ameelezea yanayokusibu, kuwa kila wakati haya masuala yatakuzukia, kwa sababu moja tu, hayajarekebishwa. Mzee Mtei atasema asemalo, lakini ukweli utabaki pale pale kuwa, wakati wake Chadema kilikuwa ni chama cha kikabila zaidi na ngome yake ilikuwa Kilimanjaro tu, mpaka Kaborou alipoigombea Kigoma.

Muhimu ni kuwa, ikubalike tu kuwa tatizo lipo na linahitaji ufumbuzi. Chadema ni chama kichanga na isingekuwa rahisi kikawa a national party over night, hili linaeleweka. TZ ilikubikwa na msululu wa vyama wakati vilipoanzishwa kwani waanzilishi hawakuweza kukubaliana kutofautiana. Walichoweka mbele ni ubinafsi wao kwanza, huku wakipeperusha makaratasi ya Demokrasia. Ndio maana vyama vikuu vyote, isipokuwa NCCR kabla ya Mrema, vilikuwa identified na makundi fulani, kijimbo na kidini.

Bahati nzuri ni kuwa, hii awamu ya pili ya viongozi ambao wengi wao wamevikuta hivi vyama na hawafungwi sana na ubinafsi wa waanzilishi labda ndio watakaoviokoa hivi vyama. Lakini hii haina maana kuwa mizizi na ushawishi wa waasisi haupo, la hasha, bado upo na ndio maana unaona kunakuwa na mapungufu hayo yaliyorithiwa tokea awali.

Asha, kama unaiombea mema Chadema, basi pigia debe ili hayo yanayopigiwa kelele yatatuliwe badala ya kujitahidi kuyakingia kifua, kinyume na hapo, yatarudi kulalamikiwa kila kukicha maana wanachama nao wana macho na masikio. Tunahitaji Chadema ya kutukomboa, sio Chadema ya kutugawa zaidi.
 

Hii statement kwenye red ndiyo inakuonyesha jinsi usivyo na hoja bali viroja. Yaani wewe CHADEMA kuweka mapato na matumizi yake kwenye mtandao ni kuiumbua CCM na sio kuwa wazi.

Kwa hili umeonyesha ni mtu wa namna gani so keep exploding maana umenipa sababu ya kukamata chupa nyingine ya pepsi!

Malalamiko yaliyotolewa ni kuwa, mikoani hawapati ruzuku ukilinganisha na makao makuu. Hili ndio la kujibu. Kama matumizi ni uchaguzi tu, basi Chadema hawatashinda hata siku moja, maana mpiga kura huandaliwa mikoani kabla ya uchaguzi.

Hao watu wa Tarime na Kigoma walishinda vipi? Kwa argument yako basi CHADEMA ingeshida Dar na sio mikoani? Mkuu unaaibisha hadi inatia huruma!


Hili limekuonyesha ulivyo na chuki za kikabila na vikorosho vya ubaguzi. Jana nilikuuliza uweke majina unayosema kuwa ni ya mkoa wa Kilimanjaro na hukufanya hivyo. Hivi unawezaje kujua kabila la mtu kwa kuona jina lake?

Mbona hao waliotajwa ni watu waliokulia Dar es salaam na wote wanajulikana zaidi kama wana darisalama kuliko hiyo mikoa wewe unayotaka kuwapandikizia.

Babu punguza chuki za kikabila utakuwa na maisha marefu kidogo!

Mzee Mtei atasema asemalo, lakini ukweli utabaki pale pale kuwa, wakati wake Chadema kilikuwa ni chama cha kikabila zaidi na ngome yake ilikuwa Kilimanjaro tu, mpaka Kaborou alipoigombea Kigoma.

Katika hili umekamatwa ukidanganya mchana kweupe na sasa wewe mwenyewe umejithibitishia jinsi usivyo na data. Poor guy, mwaka 1995, Bob Makani aligombea jimbo la Shinyanga mjini. The last time I checked, yeye ni miongoni wa viongozi wa mwanzo wa Chama na pia kati ya waliokieneza chama mikoani kuchuana na NCCR.

Get your facts utaabika hapa mzee!


Hizi statement zinakuabisha mzee bora utulie tuli maana ni wewe tu waliokuwa paranoidi huko ccm ndio mnajaribu kuleta issue kuwa chadema ni chama cha wachaga huku facts zikionyesha vinginevyo. Na kama kawaida ya JF, utafunuliwa hadi moyo wako wenye chuki za kikabila na uongo wenye udaku ndani yake uwekwe hapa kwa kila mtu kuona!


Wewe na chuki zako za kikabila ishia huko huko ccm kwenye wizi na ufisadi huku mkitafuta namna ya kuwagawa watanzania kama vile ilivyofanyika kwa Dr Salim Ahmed Salim!

Katika hili, ushauri wako wa kinafiki unafutwa na chuki zote zile ulizozionyesha hapo juu!

Next ........
 


MwK,
Hebu punguza jazba kidogo na kusoma tena ujumbe wangu kwa uangalifu ili ujibu hoja badala ya kuendeleza mayowe. Mimi ni Mdanganyika, sishabikii chama chochote kama mwenzangu ambaye umemchagua Mrema. Kama uteuzi wenye ratio ya 4 out of 6 kiukabila sio controversial basi tunaweza ku-ignore wanaolalamika, otherwise Chadema ni vema wakarekebisha hiyo hali. Halafu narudia tena kuwa, matumizi yaliyotangazwa na Chadema ni ya mwaka 2005 tu. Kingine cha muhimu ni kuangalia statement ya mwisho kabisa kwenye hiyo page ya matumizi, kuhusu CCM, ili uelewe kwa nini matumizi hayo yaliwekwa na pengine kwa nini mengine hayajawekwa wazi hadi leo ambapo wanachama mikoani wanalalamika.


Gharama za Kampeni Uchaguzi Mkuu 2005 - Chadema
http://www.chadema.net/uchaguzi/gharama.php

Mapato
1. Ruzuku kutoka Serikalini 22,770,712
Agosti mpaka Novemba
2. Michango ya Wanachama na Wapenzi wa Ndani 246,723,543
3. Michango ya Wahisani wa Nje ya Nchi 83,500,000
Conservative Party
4. Mikopo ya Wanachama na Wapenzi wa Ndani 399,574,543
Jumla 752,568,798

Matumizi
1. Gharama za Helikopta 223,030,726
Kukodisha helikopta 186,500,800
Mafuta ya helikopta 31,057,786
Vibali, Kodi viwanja vya ndege, Uendeshaji n.k. 5,472,140
2. Kampeni kupitia vyombo vya habari 60,576,450
Malazi, chakula na posho za waandishi wa habari 21,186,050
Matangazo kwenye luninga, radio na magazeti 39,390,400
3. Nyenzo za Kampeni 61,363,660
Machapisho - mabango, vipeperushi 51,113,500
Nyenzo za kampeni - bendera, fulana 8,580,000
Gharama za uchapishaji Makao Makuu 1,670,160
4. Gharama za Vikao vya Uteuzi 87,386,659
Kura za awali (Primaries) 43,490,959
Kamati Kuu, Baraza Kuu & Mkutano Mkuu 43,895,700
5. Misaada ya fedha taslim kwa Wagombea Ubunge 59,250,000
6. Gharama za Usafiri 160,558,084
Kukodisha magari 35,580,000
Kununua magari 79,200,000
Matengenezo ya magari 15,867,850
Mafuta ya magari 26,725,234
Usafiri wa ndege 3,185,000
7. Uendeshaji wa Makao Makuu kipindi cha Kampeni 17,500,000
8. Gharama za kuendesha mikutano 68,615,000
Kukodisha vipaza sauti 44,095,000
Kununua Majenereta kwa ajili ya mikutano 17,720,000
Kununua vipaza sauti kwa Wagombea Ubunge 6,800,000
9. Gharama za Simu/Mawasiliano 1,112,000
10. Gharama za Mazishi 1,300,000
11. Posho za Watendaji wa Kampeni 7,780,000
12. Malazi na chakula kwa Watendaji wa kampeni 5,021,826
13. Gharama nyinginezo 292,100
Jumla 753,786,505

Chama cha Mapinduzi kimepata kigugumizi na kimeshindwa kukanusha tuhuma kwamba kilitumia zaidi ya shilingi bilioni 40 (40,000,000,000,000) katika kampeni za Uchaguzi wa 2005. Aidha, Chama cha Mapinduzi kimekuwa kikipinga kwa nguvu zake zote mabadiliko yeyote kwenye sheria za uchaguzi ambayo yataweka ukomo wa matumizi ya fedha katika kampeni. Huu ni mkakati wa makusudi kabisa wa chama hiki cha mafisadi wakuendelea kung'ang'ania madaraka kwa kuhakikisha uchaguzi hauwi wa huru na haki.


http://www.chadema.net/uchaguzi/gharama.php
 

Sasa ulichohakikisha hapa ni nini hasa?

Nimekushauri uachane na chuki ya kikabila na utareason zaidi ya kutoa mambo ambayo sio tu yanakanusha unachosema, bali pia yanakufunua zaidi ulivyo - unataka kuanzisha issue out of nothing!

Next ......
 

Ukisikia bangi na kuhishiwa hoja kwa ccm soma kinachoandikwa hapa na mswahili!
 
Poa tu yote maisha ulitaka niwe wapi? au ulitaka nile ruzuku za makao makuu ambazo wewe unapata?

Ulirudishwa kwa ufisadi sasa utakoma kuringa maana kesi dhidi yako inaandaliwa! Watu kama wewe mnatumainiwa na serikali na kuwekwa nchi za nje kisha mnaaibisha watanzania.... grrrrr
 
Sasa ulichohakikisha hapa ni nini hasa?

Nimekushauri uachane na chuki ya kikabila na utareason zaidi ya kutoa mambo ambayo sio tu yanakanusha unachosema, bali pia yanakufunua zaidi ulivyo - unataka kuanzisha issue out of nothing!

Next ......

MwK,
Nashukuru sana kwa kunifahamisha kuwa kuhubiri usawa ni chuki ya kikabila. I hope huo ni msimamo binafsi na sio wa Mh. Mrema na TLP kwa ujumla. Ila sitabadilisha msimamo wangu kuwa kuteua wabunge wanne (4) kati ya sita (6) kutoka mkoa mmoja ni upendeleo na sio Demokrasia. Hii ina maana kuwa kati ya hao wabunge 6 wa kuteuliwa, Kilimanjaro ina wawakilishi (4) na the rest of the country inawakilishwa na wawili (2) tu. MwK tuwe wakweli na kuacha ushabiki wa kitoto.
 

Mimi nimekuuliza swali rahisi sana lakini naona unakimbia kama vile sijui nini. Nimekuomba utaje majina ya wabunge wa kuteuliwa wa CHADEMA, kisha utaje mikoa au makabila yao maana mimi sina utaalamu huo wa kujua hili.

Simple and clear
 

Good points, bado CHADEMA hawajashika usukani kwa hiyo issue zao sio nzito kama zile zilizoibuliwa na Slaa, Zito na wengine. Vile vile sio guarantee kwamba watashinda uchaguzi ujao.

Tatizo ni hawa vibaka ambao wanakula pesa ya walipa kodi kwa ridhaa ya CCM.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…