CHADEMA ni balaa, Afisa wa makao makuu atoa Siri nzito za Mbowe

CHADEMA ni balaa, Afisa wa makao makuu atoa Siri nzito za Mbowe

1. Kwa sasa! Tundu Lissu anatosha ili aje aisuke upya Makao Makuu ya CHADEMA maana imeyumba sana!

2. HQ ya Chama chetu inaendeshwa kimazoea sana; watu wenye fikra pevu hawawezi kudumu na kuonyesha uwezo. Hujuma ni nyingi kuliko kitu chochote. Tatizo linaanzia kwenye Secretariat!

3. Mwenyekiti Mbowe Hana uwezo wa kuwafanya chochote wanamumudu sana kwa sababu ni washikaji zake sana!

4. Uchaguzi huu linda taasisi na sio mtu/watu. Na Mtu anayeweza kututoa hapa tulipo ni Tundu Lissu!

5. Kama wanabisha, nitaachia hadharani mpango kazi mzima wa kuipata TV ya Chama uliokwamishwa na hata email zao zote walizokuwa wanawasiliana na mwekezaji husika ninazo.

6. Tundu Lissu pekee ndiye anayeweza kuturekebishia utendaji wa hapa CHADEMA Makao Makuu.

Remigius Selestine,
Afisa wa IT - Chadema HQ.
Huyu ni pandikizi la Msigwa na Lissu. Ila Mbowe ndo kayataka haya. Halushughulikia nidhamu kwenye chama chake ndo maana wanachama wanashambuliana hadharani bila aibu. Matusi imekuwa sera ya CHADEMA chini ya Mbowe. Sasa hivi wanaanza kumtukana yeye mwenyewe aliyelea upumbavu.
 
Bogus!

Kama bado una amini kwamba mtu mmoja atakuja kufanya mabadiliko ya taasisi badala ya mfumo, basi wewe ni mjinga na mpumbavu kwa pamoja.
Na huo mfumo LAZIMA awepo mtu mmoja wa kuhakikisha huo mfumo unakuwepo.
 
Bogus!

Kama bado una amini kwamba mtu mmoja, (badala ya mfumo) atakuja kufanya mabadiliko ya taasisi, basi wewe ni mjinga na mpumbavu kwa pamoja.
Kwa hiyo, kwa maoni yako, huyo mtu mmoja hana 'impact' yoyote katika kutafuta mabadiliko/marekebisho ya huo "mfumo"?

Kwa maana yako Mwenyekiti wa chama hawezi kuwa na ushawishi juu ya hao wanao ukalia na kuhodhi "mfumo" wako!

Hao watu wa "mfumo" wanao koga roho yako sana, hasa ni akina nani hao; wewe ni mmoja wao?
Naona maneno "Bogus" na "mfumo" ndiyo hasa yaliyo ichota akili yako hadi ukaona ueleze kitu ambacho huna uwezo wa kukifafanua.
 
Mbowe na Mnyika fukuza haraka huyo Remigius anayejiita afisa wa IT HQ hafai
Nawakumbusha tu bila mwamba Mbowe aliyesimamia matibabu ya Lissu alipopata dhahma saa hizi Lissu angekuwa shimo la Tewa !
Ni mtu mwenye akili kubwa tu ndo angeweza kufanya yale na si vinginevyo.Jamani acheni mzaha
Yule daktari aliyemzalisha mama yako ukaja duniani ulimrudishia fadhila?

Mnakuja na sababu za kipuuzi sana… sasa mlitaka alambe viatu vya mbowe?

Yes alimsaidia so what? ‘ilikuwa wajibu wake kama mwanadamu sio kiongozi!

Kama kuna mapungufu lazima yafanyiwe kazi chama kikomaee sio hizi sababu za kitoto za kupeana peremende usinisemelee!

Mageuzi ni sasa
20 yrs tupo pale pale! It’s time for a change!

Wachache wananeemeka mkiendelea kuwapaka Wananchi mafuta na mgongo wa chupa.
 
Kwa hiyo, kwa maoni yako, huyo mtu mmoja hana 'impact' yoyote katika kutafuta mabadiliko/marekebisho ya huo "mfumo"?

Kwa maana yako Mwenyekiti wa chama hawezi kuwa na ushawishi juu ya hao wanao ukalia na kuhodhi "mfumo" wako!

Hao watu wa "mfumo" wanao koga roho yako sana, hasa ni akina nani hao; wewe ni mmoja wao?
Naona maneno "Bogus" na "mfumo" ndiyo hasa yaliyo ichota akili yako hadi ukaona ueleze kitu ambacho huna uwezo wa kukifafanua.

Kwa vile upo behind the keyboard unadhani kila mmoja ana upeo mdogo wa kufanana na wewe siyo!
 
Mtu mmoja anaweza fanya mabadiliko makubwa sana ikiwa yeye ndo CEO na ni center ya maamuzi,kwani hyo mifumo mpaka ibadilishwe pia inahitaji mtu mmoja mwenye maamuzi.

Si kweli. Ingekuwa hivyo, basi JK angewezesha Katiba Mpya(mfumo) kupatikana.
 
Unaweza ukawa wewe ni Bogus zaidi Kwa sababu ya kushindwa kufikiri na kuwasilisha fikra tunduizi.

Siku zote visionary leader (individual) Ndio anayetakiwa kuyatafsiri maono ya wanataasisi na kuyaweka in practice Ili yalete hayo mabadiliko ya kitaasisi unayoyataka. Taaisisi lazima uwe na kiongozi. These are social systems na kwa maana hiyo lazima ziwe na kiongozi, mbeba maono.

So what is leadership kama tulivyosoma?
Ana ability of a person to influence others to share a common vision towards a common goal! Uko hapo jamaa yangu! Kama una ability ya kuwainfluence watu waongane na wewe kufikia common goal, jua hakuna taaisisi itakayosimama! Wake up upo kwenye platform ya great thinkers:
Hebu soma hii hapa kama darasa kwako na wale wenye akili na mtazamo kama wewe:


Nguvu ya kiongozi mmoja kuleta mabadiliko ndani ya taasisi au chama cha siasa inatokana na uwezo wake wa kuwa na maono ya mbali, mikakati thabiti, na uwezo wa kuwahamasisha wengine. Kiongozi wa mabadiliko huathiri utamaduni, muundo, na utendaji wa taasisi kwa lengo la kuboresha maendeleo ya muda mrefu. Katika vyama vya siasa, viongozi wenye dira sahihi wana uwezo wa kuvibadilisha vyama na kuviimarisha ili viweze kukidhi mahitaji ya jamii.

Moja ya nguzo muhimu za kiongozi wa mabadiliko ni kuwa na maono na madhumuni wazi. Kiongozi wa aina hii hutoa mwelekeo wa wazi juu ya mahali chama kinapaswa kuelekea na jinsi ya kufanikisha lengo hilo. Katika vyama vya siasa, kiongozi mwenye maono anaweza kuwaunganisha wanachama na wafuasi wake kuelekea malengo ya pamoja kama vile kuleta mageuzi, haki, au utawala bora. Maono ya kiongozi huwezesha chama kuendana na mabadiliko ya kijamii na kupata imani ya wananchi.

Pili, fikra za kimkakati na maamuzi sahihi ni muhimu kwa kiongozi wa mabadiliko. Uwezo wa kiongozi kutambua changamoto, kuona fursa, na kufanya maamuzi madhubuti unachangia sana katika mafanikio ya chama. Katika vyama vya siasa, hii inaweza kujumuisha kufanya mabadiliko ya kimfumo ndani ya chama, kuanzisha sera mpya, au kuimarisha mikakati ya kuwafikia wananchi. Viongozi wanaofanya maamuzi ya kimkakati wanaweza kufufua vyama vilivyodorora na kuvifanya viwe na nguvu katika uwanja wa kisiasa.

Aidha, kuhamasisha na kuwapa watu motisha ni kipengele kingine cha uongozi wa mabadiliko. Viongozi wa vyama vya siasa wanawahamasisha wanachama na wananchi kuamini katika maono yao. Wanawaunganisha watu, kuwapa matumaini, na kuwafanya wajisikie kuwa sehemu ya mafanikio ya chama. Uwezo huu wa kuhamasisha juhudi za pamoja mara nyingi huamua mafanikio ya harakati na kampeni za kisiasa.

Viongozi wa mabadiliko pia huonyesha uvumilivu na uwezo wa kubadilika wanapokutana na changamoto. Vyama vya siasa mara nyingi hukumbana na migogoro ya ndani, shinikizo kutoka kwa upinzani, au mabadiliko ya mitazamo ya umma. Kiongozi shupavu anaweza kuliongoza chama kupitia changamoto hizo, kurekebisha mikakati inapohitajika, na kuhakikisha lengo kuu halipotei. Uwezo huu wa kustahimili changamoto hujenga imani miongoni mwa wafuasi.

Viongozi wa mabadiliko pia hujenga utamaduni wa ushirikiano na usawa ndani ya taasisi. Katika vyama vya siasa, hili linahusisha kuwaunganisha wanachama kutoka makundi tofauti chini ya misingi ya pamoja. Kwa kusikiliza sauti za makundi mbalimbali na kushirikiana nao, viongozi huimarisha mshikamano wa chama, kutatua migogoro, na kuvifanya vyama vionekane vyenye mvuto zaidi kwa wananchi.

Mwisho, viongozi wa mabadiliko huonyesha mfano bora kwa tabia na maadili ya juu. Kwa kuonyesha uwajibikaji, uadilifu, na kujitolea, wanajenga imani na uaminifu kutoka kwa wanachama na umma kwa ujumla. Kiongozi mwenye maadili anapoweka mbele maslahi ya chama na wananchi, anaimarisha taswira ya chama na kuvutia wafuasi zaidi.

Maneno ya chawa.
 
Moja ya fundamental principle ya utumishi, usimponde boss wako anayeondoka kwa boss mpya ukitegemea boss mpya atakupeda.
Najua wakati kama huu sarakasi nyingi sana,chotote kwa maslahi ya yeyote yanaweza semwa.
 
Kwa vile upo behind the keyboard unadhani kila mmoja ana upeo mdogo wa kufanana na wewe siyo!
Ulitaka niwe wapi mkuu 'Kindeena', ndiyo niwe na uhakika wa kuyasema maneno hayo.
 
Bogus!

Kama bado una amini kwamba mtu mmoja, (badala ya mfumo) atakuja kufanya mabadiliko ya taasisi, basi wewe ni mjinga na mpumbavu kwa pamoja.

Sasa mfumo si unaundwa na watu mmoja mmoja au? 😀
 
Back
Top Bottom