CHADEMA: Ole wenu mkiipokea Mizoga ya CCM!

CHADEMA: Ole wenu mkiipokea Mizoga ya CCM!

CCM wameshaamua nani watawawakilisha kwenye Ubunge, wamechuja chuya, wametupa makapi na mizoga.

Sasa natoa tahadhari kwa CHADEMA; Ole wenu mkiipokea hii mizoga ya CCM na kuipa kadi na hata kuwafanya wagombea wenu kwenye majimbo, mtajishushia hadhi na kuonekana chama kisicho na maana na ni hifadhi ya mizoga na makapi.

Jiulizeni kwa nini hawa mizoga, makapi na pumba kwa nini walisubiri kuenguliwa na CCM ndipo wakakimblia kwenu? Kwa nini tangu awali hawakufanya uamuzi wa kuhamia CHADEMA kabla ya kushindwa ndani ya CCM na hivyo baada ya kutalikiwa wanakuja kwenu nanyi mnawapa Ufestiledi kwenye majimbo?

Mkuu wamerudia tena 2015 .. sasa sijui utasemaje? Umeona Sikonge na Bunda mambo yameenda mrama?!
Ni kazi sana.
 
Asiyefunzwa na mamaye, atafunzwa na ulimwengu!

Haya Sumaye huyoo ndani ya nyumba! Alafu anasema ukaskazini
Hawa jamaa wameshavurugana! Ila safari hii ndo wanaishia. Sikonge na Bunda ni tip of the iceberg. Bado sasa mvurugano wa CUF bara!
 
Haya Sumaye huyoo ndani ya nyumba! Alafu anasema ukaskazini
Hawa jamaa wameshavurugana! Ila safari hii ndo wanaishia. Sikonge na Bunda ni tip of the iceberg. Bado sasa mvurugano wa CUF bara!

Lack of long term strategy and vetting of some of these folks! They are going for short term gains and even awed with some sensational 15 seconds of fame rather than clear conscious and strategy.

Hapakuwa na haja kumharakisha Bulaya au Nkumba wagombee, tayari kulikuwa na watu waliojijenga kwa muda mrefu ndani ya chama...same rule applies to EL when it comes to Slaa.

Sasa hivi with Mngeja, Guninita and others party stalwarts crossing the river, Chadema kitabadilika sana in 2-3 years. Ile Upinzani makini kutoka ndani ya CCM will now starting shaping up maana ndani ya CCM kuna vita kubwa ya kiitikadi, maslahi, generational difference na hata personalities.

Hii dhana na kulazimishana "Umoja ni Ushindi" will not survive for that long especially kama Mkapa na Kikwete still have significant say ndani ya Chama.

Kuna majeruhi wa Kichama na Kiitikadi na hata walionyimwa fursa kutokana na mizengwe.

Hopefully Magufuli will stand by his first promise "Umoja wa Kitaifa" na aanze aggressively kusafisha Chama Sekretarieti na Kamati Kuu ambazo ndio kidogo anaweza kuwa na nguvu kuleta msukumo na mabadiliko ya kweli anayoyataka yatokee katika Serikali yakisukumwa na kuhakikiwa na Chama.

CCM sasa ni lazima iendelee kumeguka (si suala la ufisadi tuu au kigezo cha ufisadi), fursa hii imeanza na Lowassa, wenyeviti wa mikoa wabunge wachache na sasa Sumaye.

Kuna makapi wanaokimbilia uchaguzi, lakini pia kuna wanaoondoka kwa hiari wakijua mfumo wa sasa wa Chama haufai au unahitaji marekebisho na hasa tofauti za kiitikadi na dira ya Chama.

CCM haiewezi kuwa na dira au uimara kama kuna mgongano wa kiitikadi ndani ya chama.

CCM ilianzishwa kusimamia haki za wanyonge, kusimamia utu na kupiga vita utajiri wa kupita kiasi hasa kutokana na viongozi wake.

Azimio la Zanzibar, liliruhusu viongozi kuwa matajiri kupindukia na msuguano kati ya wananchama na wananchi wanaoamini ujamaa na viongozi wanaoamini ubepari, umezaa chuki na ufisadi.

Chadema ni chama cha mabepari, wanaokihama CCM kwa kudiriki leo iwe ni fursa (au tamaa) ya kupata mamlaka na uongozi au ni mvuto wa kuchoka CCM na ni watu wenye mwelekeo wa Kiubepari, watakuwa salama Chadema na huko ndiko itabidi waingize nguvu zao na kushindana na wajamaa (Dr. Slaa na wenzake) ambao waliamini kutumia itikadi za ujamaa walipoanza wimbi la kuing'oa CCM kupiga kelele za Ufisadi (UTAJIRI).

Yetu macho.
 
Rev. Kishoka

Katika uchaguzi wa rais baada ya kusimamisha vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Liberia, Charles Taylor alitumia slogan: He killed my pa he killed my ma I'll vote for him.

Kutokana na watu wa Liberia kuchoshwa na vita, walimchagua Taylor. Kwa matumaini ya kuwa atabadilika na kumaliza vita. Lakini haikuwa hivyo. Mara baada ya kuchaguliwa kuwa rais, Taylor aliendeleza udikteta, rushwa na udhalimu kwa watu wake. Na matokeo yake vita vilirudi na vilevile kuendelea katika nchi jirani.

Kwa kuchoshwa na rushwa na umasikini naona watanzania wako tayari kuchagua mtu yoyote yule kwa matumaini kuwa mchaguliwa anabadilika. Hata standards imebidi zishushwe sasa. Nchi imekuwa kama mtu alikwenda baa kutafuta mchumba na kukubali mtu yoyote (desperation) atakayemsalimia.

Historia ya Liberia na Ujerumani inatuonyesha kuwa kutumia kigezo cha matumani bila kufikiri kunaweza kuifanya jamii au nchi kuchagua kiongozi mbaya kwa kupitia misingi ya kidemokrasia. Ukweli wa mambo ni vigumu kwa watu kubadilisha tabia zao pale wapatapo madaraka. Charles Taylor alichaguliwa kwa matumaini. So did Hitler.

Hapa simpigi dongo Lowassa au Magufuli. Na vilevile sisemi kuwa wao watakuwa kama Taylor or Hitler. Lakini historia inajionyesha yenyewe. Nyerere hakuingia madarakani akiwa na tabia mbaya na baadaye kubadilishwa na cheo. Kagame hakuingia madarakani hakiwa mla rushwa na baadaye kubadilika akiwa madarakani.

Je kuna uwezekano wa uchaguzi wa mwaka huu kutoa Charles Taylor or mini-wake?
 
Zakumi,

..how about Mkapa?

..unafikiri aliingia madarakani akiwa na tabia nzuri au mbaya?

..je, madaraka yalimbadilisha tabia au hayakumbadilisha?

..nadhani tunapozungumzia mabadiliko tusiangalie Uraisi peke yake.

..yanahitajika mabadiliko hata ktk ngazi za serikali za mitaa, udiwani, na ubunge.

..mimi nadhani imetosha. yale matusi aliyoporomosha Mkapa pale jangwani, halafu JK na Magufuli wanacheka, proved to me that these ppl need to go.

..nchi hii ina watawala/wanasiasa ambao hawaheshimu na hawaogopi wananchi/wapiga kura.
 
Last edited by a moderator:
Rev. Kishoka

Katika uchaguzi wa rais baada ya kusimamisha vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Liberia, Charles Taylor alitumia slogan: He killed my pa he killed my ma I'll vote for him.

Kutokana na watu wa Liberia kuchoshwa na vita, walimchagua Taylor. Kwa matumaini ya kuwa atabadilika na kumaliza vita. Lakini haikuwa hivyo. Mara baada ya kuchaguliwa kuwa rais, Taylor aliendeleza udikteta, rushwa na udhalimu kwa watu wake. Na matokeo yake vita vilirudi na vilevile kuendelea katika nchi jirani.

Kwa kuchoshwa na rushwa na umasikini naona watanzania wako tayari kuchagua mtu yoyote yule kwa matumaini kuwa mchaguliwa anabadilika. Hata standards imebidi zishushwe sasa. Nchi imekuwa kama mtu alikwenda baa kutafuta mchumba na kukubali mtu yoyote (desperation) atakayemsalimia.

Historia ya Liberia na Ujerumani inatuonyesha kuwa kutumia kigezo cha matumani bila kufikiri kunaweza kuifanya jamii au nchi kuchagua kiongozi mbaya kwa kupitia misingi ya kidemokrasia. Ukweli wa mambo ni vigumu kwa watu kubadilisha tabia zao pale wapatapo madaraka. Charles Taylor alichaguliwa kwa matumaini. So did Hitler.

Hapa simpigi dongo Lowassa au Magufuli. Na vilevile sisemi kuwa wao watakuwa kama Taylor or Hitler. Lakini historia inajionyesha yenyewe. Nyerere hakuingia madarakani akiwa na tabia mbaya na baadaye kubadilishwa na cheo. Kagame hakuingia madarakani hakiwa mla rushwa na baadaye kubadilika akiwa madarakani.

Je kuna uwezekano wa uchaguzi wa mwaka huu kutoa Charles Taylor or mini-wake?
Hii habari ya kuchagua mtu yeyote kwa sababu wamechoshwa na rushwa siku zote huwa ni maamuzi magumu na sio sahihi. Tumeyaona Liberia, Zambia, Malawi na hta Uganda wakati wa Idd Amin.. Na kinachonichosha zaidi, nimewasoma watu wakisema "Hata likiwekwa jiwe kugombea dhidi ya mwana CCM watachagua jiwe!" really?

Kwa hiyo sio swala la kuichoka CCM tu, mimi nina mashaka sana na akili za wadanganyika ambao wanasema wapo tayari kuchagua JIWE! mimi nadhani akili zao wenyewe ndio zimechoka! I mean japo ni msemo lakini inatisha zaidi kusikia kuwa wananchi wako tayari kuchagua mtu yeyote lakini sio kutoka CCM..Na ndio maana safari hii nimeona sura za wagombea wa ajabu ajabu kabisa ambao sijui kama wataweza kuisimamia serikali, kutunga sheria na kupitia bajeti zaidi ya kuuuza sura mule wakipokea millioni 11.

Mimi ningepomba tu, kabla ya uchaguzi huu washushe mishahara ya Bunge kufikia Millini 3 - 5 kwa mwezi halafu tuone kama kweli hawa watu wameyataka mageuzi ama wametaka kubadilisha tu mfuko unaoingia kodi za wananchi..
 
Zakumi,

..how about Mkapa?

..unafikiri aliingia madarakani akiwa na tabia nzuri au mbaya?

..je, madaraka yalimbadilisha tabia au hayakumbadilisha?

..nadhani tunapozungumzia mabadiliko tusiangalie Uraisi peke yake.

..yanahitajika mabadiliko hata ktk ngazi za serikali za mitaa, udiwani, na ubunge.

..mimi nadhani imetosha. yale matusi aliyoporomosha Mkapa pale jangwani, halafu JK na Magufuli wanacheka, proved to me that these ppl need to go.

..nchi hii ina watawala/wanasiasa ambao hawaheshimu na hawaogopi wananchi/wapiga kura.

JokaKuu;

I agree with you that they have to go. Lakini wakati huohuo hawawezi kuondoka iwapo Tanzania intelligentsia inaendelea kukaa kimya without taking a stance. Hatuwezi kupata wabunge na viongozi wengine wazuri wa kuchaguliwa iwapo mifumo ya vyama haifai na haitoi wenye vipaji kushika nafasi.

Jamii inapohamua kuwa smart, viongozi watafikiria mara mbili kabla ya kuongea. Mkapa anaongea utumbo kwa sababu jamii imekubali kuusikiliza utumbo. Lowassa anasafishwa siku moja tu kwa kuhamia CDM.

Mmoja wa watia nia alisema kuwa akichaguliwa kuwa rais anataka Tanzania iwe kama Kenya. Itafika siku mwingine atasema iwe kama Rwanda au Burundi. Wakati wa Mwalimu, pamoja na kuwa sikubaliani na siasa zake, watu walitaka nchi zao ziwe kama Tanzania.
 
Hii habari ya kuchagua mtu yeyote kwa sababu wamechoshwa na rushwa siku zote huwa ni maamuzi magumu na sio sahihi. Tumeyaona Liberia, Zambia, Malawi na hta Uganda wakati wa Idd Amin.. Na kinachonichosha zaidi, nimewasoma watu wakisema "Hata likiwekwa jiwe kugombea dhidi ya mwana CCM watachagua jiwe!" really?

Kwa hiyo sio swala la kuichoka CCM tu, mimi nina mashaka sana na akili za wadanganyika ambao wanasema wapo tayari kuchagua JIWE! mimi nadhani akili zao wenyewe ndio zimechoka! I mean japo ni msemo lakini inatisha zaidi kusikia kuwa wananchi wako tayari kuchagua mtu yeyote lakini sio kutoka CCM..Na ndio maana safari hii nimeona sura za wagombea wa ajabu ajabu kabisa ambao sijui kama wataweza kuisimamia serikali, kutunga sheria na kupitia bajeti zaidi ya kuuuza sura mule wakipokea millioni 11.

Mimi ningepomba tu, kabla ya uchaguzi huu washushe mishahara ya Bunge kufikia Millini 3 - 5 kwa mwezi halafu tuone kama kweli hawa watu wameyataka mageuzi ama wametaka kubadilisha tu mfuko unaoingia kodi za wananchi..

Bob,

I hear you very well. Lakini kama Bobu Mlay alivyosema "them belly full but we hungry, a hungry man is an angry man"..Watanzania hawajali tena maana kwa ustaarabu wao wa kuamini kuwa CCM will go back kuwa chama cha utu na kupigania maslahi ya wanyonge, imekuwa wazi ni chama cha wanaogombea maslahi binafsi na hata kufikia kuwakejeli na kuwadharau wananchi.

Kauli ya wapumbavu, malofa na mchawi zilizotolewa Jangwani, hazikuwa na staha hata kidogo ukizingatia waliozitoa kauli hizo ndio walioongoza kugota kwa meli ya maendeleo ya Taifa na kuhamishia kila kitu vipuri, mafuta, chakula kwenye Yatch zao.

Si siri tena kuwa vita kati ya Lowassa, Mkapa na Kikwete si itikadi au kutokea damu Tanzania bali ni vita vya maslahi binafsi na CCM imekaa mguu pande kabisa ikiachia mashindano ya ujuaji, ufahari na uroho wa madaraka ili kujipatia mali.

Sasa ukianza kutafakari kwa nini Wananchi wengine wanaona potelea pote sisi tutamjaribu Lowassa na Chadema kuliko hawa CCM wa miaka nenda rudi, utaona ni lile suala la "hungry man who is angry".

Wakulaumiwa kwa haya wala si Wananchi tena bali viongozi wa CCM na mfumo wake uliozalisha uroho na uchu wa madaraka ili kujipatia mali na utajiri.

Ndio maana naendelea kuuliza, tunamshupalia na kumkaba koo Lowassa kuwa fisadi (tajiri wa kupindukia) lakini Mkapa, Kikwete na matajiri wengine viongozi ndani ya chama tunawafumbia macho na tunayaamini maamuzi yao hata walipoamua kutuchagulia kupitia mchujo maridhawa na kutuletea Pombe Magufuli.

Shangwe walioonyesha Mkapa na Kikwete na wanavyopigia debe mwanafunzi wao Magufuli ni ya kushangaza na inasikitisha. Hawa mahasimu wawili wameamua kuungana sasa kushindana na bepari mwenzao ili waendelee na uharamia wa Kiserikali na Sera za halali kuendeleza mfumo wao wa kujipatia utajiri na kwa manufaa ya marafiki wao matajiri na wala si Watanzania.

Watanzania wanaendelea kula na kuambulia makombo chini ya meza, tukiambiwa tuna wivu wa kike, wavivu na sasa wapumbavu na malofa huku watu hawa hawa wakiachama midomo na kutoa kauli hawaelewi ni vipi Watanzania ni masikini!

Ukawa na Watanzania wamejionea kuwa "why not'? kwa nini nao wasijaribu na kuacha njia zote zenye akili ya maana na msingi na wafuate mkumbo wa unyang'au kama CCM na tuone hiyo sandakalawe ya October 25, wakikosa si shida maana wamezoea kukosa na wamezoea shida, wanachofanya sasa hivi ni kutafuta ahueni na aliye na njaa pamoja na malegeza ana hasira na hajali tena kupoteza maisha yake huku yule aliyevimbiwa kalewa kupita kiasi na kutemea watu mate!
 
Hii habari ya kuchagua mtu yeyote kwa sababu wamechoshwa na rushwa siku zote huwa ni maamuzi magumu na sio sahihi. Tumeyaona Liberia, Zambia, Malawi na hta Uganda wakati wa Idd Amin.. Na kinachonichosha zaidi, nimewasoma watu wakisema "Hata likiwekwa jiwe kugombea dhidi ya mwana CCM watachagua jiwe!" really?

Kwa hiyo sio swala la kuichoka CCM tu, mimi nina mashaka sana na akili za wadanganyika ambao wanasema wapo tayari kuchagua JIWE! mimi nadhani akili zao wenyewe ndio zimechoka! I mean japo ni msemo lakini inatisha zaidi kusikia kuwa wananchi wako tayari kuchagua mtu yeyote lakini sio kutoka CCM..Na ndio maana safari hii nimeona sura za wagombea wa ajabu ajabu kabisa ambao sijui kama wataweza kuisimamia serikali, kutunga sheria na kupitia bajeti zaidi ya kuuuza sura mule wakipokea millioni 11.

Mimi ningepomba tu, kabla ya uchaguzi huu washushe mishahara ya Bunge kufikia Millini 3 - 5 kwa mwezi halafu tuone kama kweli hawa watu wameyataka mageuzi ama wametaka kubadilisha tu mfuko unaoingia kodi za wananchi..


Mkandara;

Mifumo ya maisha sio black and white, au kwa Tanzania maisha sio Simba na Yanga. Lakini kwa watanzania naona tumeshazoezana hivyo. Tumeshazoea kuwa wewe kama sio Simba basi ni Yanga. Wewe kama sio Mkristo basi ni Mwislamu. Maisha sio mfumo wa pande mbili zinazotofautiana au kuvutana.

Kwa maoni yangu watanzania wana choices nyingi. Inabidi wawe wabunifu tu na kufanya maamuzi magumu. Ukisema kama umeichoka CCM unapigia jiwe, basi una-trivialize maisha. CCM inakupa plan A na plan B. Kwa hasira zako unaamua kuchagua plan B na kusubiri miaka mingine mitano. Swali kwanini Tanzania intelligensia isihamke na kudai mfumo mzuri?
 
Hii habari ya kuchagua mtu yeyote kwa sababu wamechoshwa na rushwa siku zote huwa ni maamuzi magumu na sio sahihi. Tumeyaona Liberia, Zambia, Malawi na hta Uganda wakati wa Idd Amin.. Na kinachonichosha zaidi, nimewasoma watu wakisema "Hata likiwekwa jiwe kugombea dhidi ya mwana CCM watachagua jiwe!" really?

Kwa hiyo sio swala la kuichoka CCM tu, mimi nina mashaka sana na akili za wadanganyika ambao wanasema wapo tayari kuchagua JIWE! mimi nadhani akili zao wenyewe ndio zimechoka! I mean japo ni msemo lakini inatisha zaidi kusikia kuwa wananchi wako tayari kuchagua mtu yeyote lakini sio kutoka CCM..Na ndio maana safari hii nimeona sura za wagombea wa ajabu ajabu kabisa ambao sijui kama wataweza kuisimamia serikali, kutunga sheria na kupitia bajeti zaidi ya kuuuza sura mule wakipokea millioni 11.

Mimi ningepomba tu, kabla ya uchaguzi huu washushe mishahara ya Bunge kufikia Millini 3 - 5 kwa mwezi halafu tuone kama kweli hawa watu wameyataka mageuzi ama wametaka kubadilisha tu mfuko unaoingia kodi za wananchi..

..mabadiliko yanaweza kuleta matokeo mazuri au mabaya.

..umetoa mifano ya nchi ambazo hazikufaidika na mabadiliko ya uongozi.

..lakini pia zipo nchi ambazo zimefaidika na mabadiliko ya uongozi.

..naweza kukupa mifano ya Ghana, Nigeria, Kenya, Liberia[tangu aingie Mama Sirleaf], na kwengine kwingi.

..mimi ni mmoja wa ambao niko radhi kuchagua JIWE kuliko kuwapigia kura CCM. nasema hivyo kwasababu nimechoshwa na hawa CCM. naona hakuna njia yoyote ile ya kupata mabadiliko bila kwanza kuwaondoa hawa CCM.

..baadhi ambao tuko radhi kuchagua jiwe tulii-support CCM katika chaguzi zote kabla ya huu unaokuja mwezi October. Lakini tumefika mahali tumechoshwa na KIBURI na VITIMBI vya CCM. Tumefika mahali CCM hawaheshimu wenzao ktk vyama vingine, na zaidi hawaheshimu hata wapiga kura.

..CCM ndiyo kikwazo cha mabadiliko nchi hii. It is too big and is suffocating the political space. Inabidi iondolewe ile kuwa na balance ambapo wapiga kura watakuwa na choice na hawatalazimika kupiga kura za hasira na jazba --kuchagua JIWE.

NB:

..kichachonitisha zaidi ya huu umati mkubwa unaokwenda kwenye mikutano ya hadhara.

..hawa watu wote walitakiwa wawe viwandani wanapiga shift, lakini hapa kwetu wako mitaani kusikiliza siasa.

..tunashangilia mambo haya lakini yanaathiria hatari huko mbele. lakini aliyetufikisha hapo ni CCM.
 
..mabadiliko yanaweza kuleta matokeo mazuri au mabaya.

..umetoa mifano ya nchi ambazo hazikufaidika na mabadiliko ya uongozi.

..lakini pia zipo nchi ambazo zimefaidika na mabadiliko ya uongozi.

..naweza kukupa mifano ya Ghana, Nigeria, Kenya, Liberia[tangu aingie Mama Sirleaf], na kwengine kwingi.

..mimi ni mmoja wa ambao niko radhi kuchagua JIWE kuliko kuwapigia kura CCM. nasema hivyo kwasababu nimechoshwa na hawa CCM. naona hakuna njia yoyote ile ya kupata mabadiliko bila kwanza kuwaondoa hawa CCM.

..baadhi ambao tuko radhi kuchagua jiwe tulii-support CCM katika chaguzi zote kabla ya huu unaokuja mwezi October. Lakini tumefika mahali tumechoshwa na KIBURI na VITIMBI vya CCM. Tumefika mahali CCM hawaheshimu wenzao ktk vyama vingine, na zaidi hawaheshimu hata wapiga kura.

..CCM ndiyo kikwazo cha mabadiliko nchi hii. It is too big and is suffocating the political space. Inabidi iondolewe ile kuwa na balance ambapo wapiga kura watakuwa na choice na hawatalazimika kupiga kura za hasira na jazba --kuchagua JIWE.

NB:

..kichachonitisha zaidi ya huu umati mkubwa unaokwenda kwenye mikutano ya hadhara.

..hawa watu wote walitakiwa wawe viwandani wanapiga shift, lakini hapa kwetu wako mitaani kusikiliza siasa.

..tunashangilia mambo haya lakini yanaathiria hatari huko mbele. lakini aliyetufikisha hapo ni CCM.
Hiyo akili ya kuchagua hata jiwe ndio mimi yaniacha hoi kwa maana ya kwamba hamtumii tena akili bali ya kushikizwa kama wale walochagua Ukuta badala ya Nyerere enzi za chama kimoja. Sikuelewa maana yake na sintoelewa inafikiaje mtu kuchagua jiwe au Ukuta!

Mtu mwenye akili timamu utasemaje bora kuchagua jiwe likuongoze wewe! hii ina maana wenye matatizo ya kiakili ni watu wanaoongozwa sio CCM kwa sababu CCM ni chama tu, ni taasisi ambayo Ubaya wake unatokana na watu wake, sasa hao watu wake waondoke wahamie kwingine useme bora huko walikohamia kuliko chama kilichobakia!. Aidha kuna kutoelewa nini maana ya chama na kwamba ukiwa CCM basi ni muumini wa dhulma kulingana na Katiba yao!

Kifupi mkuu wangu wewe akili kubwa, utanishangaza sana ikiwa unaamini wanasiasa wenye mrengo wa KULIA wapo kutetea wanyonge kama Lowassa anavyowaahidi maskini akiwa upande wa pili. Huu kama sio uongo ni kitu gani, Uliona wapi Wahafidhina(Conservative) kudai kutoa Elimu na Afya bure wakaacha kutetea mashirika! Uliona wapi Wahafidhina wakitetea ujenzi wa misingi ya kukuza uchumi kwa kuwapa kipaumbuele walalahoi? Hii kama sii kutafuta kura kwa udanganyifu nini zaidi!

Hii mikutano ni matokeo ya akili zenu wenyewe kutaka mabadiliko..Leo hii tunashuhudia Chadema Asilia wasipewe hata nafasi ya kusimama majukwaani, Hoja ya kumnadi kiongozi mkuu imekuwa hoja ya kunadi wanaoondoka CCM kama vile kuondoka kwao kutawaletea wananchi mabadiliko. Sasa nambie mbona mabadiliko tunayoyaona ni Chadema yenyewe inabadilika toka ndani kina Lema, Mnyika, Lissu, mndee, Slaa sasa watabeba mikopa ya Lowassa wakiahidiwa majimbo wakati yeye akijenga jeshi lake la kukodisha majukwaani. Leo hawa wapambanaji watawaambia nini wananchi?, watauza sera gani ikiwa Wahafidhina CCM B ndio wamekamata usukani?
 
Mkandara,

Politics is a dirty game. It is a crazy thing kama hapa kwa Uncle Sam ambapo watu wanaamua kuchagua jiwe.. can you eve imagine kuwa Donald is better than Jeb?

Nafikiri hasira za watu ni imani na matumaini waliyokuwa nayo 2005 hayakutimia na kwa miaka 10 wamekiona CCM kikidorora na watu wa CCM wakineemeka.

Chama hujengwa na watu, huandika katiba, kanuni sera na itikadi. Chama ni tofauti na dini. Dini ni static, ila watu tunataka kuifanya dynamic.. chama cha siasa si Static, ni dynamic, hivyo Chama hakikai kama gogo tulaumu sisimizi wanaoingia ndani maana Chama hakijisemei wala kujifanyia mambo.

Dhambi kuu ya CCM ilianza na Azimio la Zanzibar, hilo liliachia mianya ya viongozi kuhodho mali, kujilimbikizia mali na kujiingiza katika biashara.

Katika kipindi hicho, ni wazi yule aliyekuwa na akili na bila woga alichukua fursa hiyo na kujipatia "riziki" mapema kupitia mkondo wa kibiashara huku wengine wakianza kujiongezea marupurupu kikazi. Nafikiri hapa ndipo grayhound la Kimaasai lilitimka na kuwaacha wenzake wakishangaa na ndio kisa cha maugomvi yote.

Nchi inawekwa njia panda kutokana na ugomvi wa watu watatu au wanne, ambao wanashindana maslahi na wanafanyiana visa kuzidiana akili.

Wananchi wameng'amua hilo na kutokana na chuki dhidi ya dharau na udanganyifu wa wawili wa hawa wapigania maslahi, jiwe linaonekana bora!
 
Mkandara,

..YES.

..Tumechoka.

..ukiweka jiwe vs ccm tunachagua jiwe.

..hiki kiburi na dharau za ccm ndiyo zimetufikisha hapa.

..tutachagua ukawa mwaka huu. Wakishindwa tunachagua act 2020.
 
Last edited by a moderator:
Nafikiri mtu anapochagua jiwe au ukuta si kwamba anataka ukuta au jiwe limuongoze bali ni hali ya kumuonyesha mtawala/mchaguliwa kuwa sina imani na wewe na sikutaki.. Mkandara , JokaKuu

Nilikuwa bado nasita sita kuhusu kura yangu lakini baada ya Mkapa kutuita sisi ni Malofa na wapumbavu basi kura yangu nitampa Lowassa.. Simpi Lowassa kura yangu kwa vile ni kiongozi mahiri, shupavu, mkakamavu, mchapakazi au penda haki bali ninampa Lowassa kura yangu ya kutaka kuwaonyesha watawala kuwa sasa imetosha.

Hawezekani mtu anayepata mlo wake kutokana na jasho langu (yaani kodi), huyu mtu analindwa, ninamlipia kodi ya maji, umeme, ninatuza watoto wake, wajukuu na vitukuu wake leo hii shukurani anayopita ni kuniita Mpumbavu, halafu na mimi kwa akili nilizojaliwa na Mwenyezi Mungu siku ya 25.10 niamke asubuhi, nipange foreni halafu nichangue chama chake/mtu wake. Nikifanya hivi atakuwa na haki ya kunita Lofa na Mpumbavu x 10.

Ni lazima watanzani tufike sehemu tuwafundishe wanasiasa heshima kwani sisi ndo waajiri wao, sisi ndo tunalipa mishahara yao, sisi ndo tunawapeleke kutibwa ulaya,. sisi ndo tunawasomesha watoto wao kwenye "International school" na nk.Haiwezekani hao hao watuite sisi ni wapumbavu au "kama kula nyasi tutakula lakini ndege ya rais ni lazima inunuliwe" hizi ni kejeli si kwangu tu, bali nii kejeri kwako, ni kejeri kwa mkeo/mmeo na ni kejeri kwa mtoto wako na hizi kejeri tusipe nafasi wakati ndio huu tusisubiri miaka mingine 5 wakati wao wakazidi kujitajirisha kwa migogo yetu.

Piga kura yako kwa Ukawa au chama chochote cha upinzani.
 
Last edited by a moderator:
Alinda,

..Exactly.

..hakuna uwezekano wa Tume ya Uchaguzi kuweka jiwe lipigiwe kura.

..kusema tutachagua jiwe ni namna tu ya kuonyesha ni kwa kiwango gani TUMECHOKA.

..mimi nisichopenda ni hii MONOPOLY ya ccm ambayo inasababisha ulaghai, dharau, uzembe, ukatili, ufisadi, na mambo mengine mengi.

..watu wanaboronga kazi, wanatesa watu, wanatukana, and nothing happens to them. That needs to change.

..hata mazingira yale ya kwamba mtu hawezi kufanya siasa nchi hii akafanikiwa bila kuwa mwana-ccm, that needs to change too.

..ninaamini hayo yanaweza kupatikana kwa kuipigia kura ukawa ktk uchaguzi huu. baada ya hapo tutawapima, na kama wataboronga, na wao tutawaweka pembeni.

cc Mkandara
 
Last edited by a moderator:
Wanajukwaa mimi sitamjibu mtu yeyote in particular ila kuna mambo matatu yamejitokeza humu yanayonishangaza na kuniacha hoi kwa sababu moja tu, wanaoyasema ni watu waliotakiwa kujua lililo bora zaidi; nilitegemea wawe better than the majority ya Watanzania lakini in truth I am disappointed, nabaki nikijiuliza kama wasomi ndio hivi je ambao hawakuuona mlango wa shule?

Kabla sijayataja hayo mambo matatu naomba nieleweke; mimi ni katika watu wanaoisubiri kwa hamu kubwa siku chama tawala cha CCM, kitakapopigwa chini. Yeyote atakayesoma huu mchango wangu naomba azingatie hilo kwamba kwenye haya mapambano, mimi nilishachagua upande. Upande huo niliuchagua hata kabla upepo wa mageuzi kuanza mwishoni mwa miaka ya 1980s.

Mambo yanayonishangaza ni haya;

1. Watu kuendela kudhani kwamba Watanzania ni viumbe tofauti na binadamu wengine duniani, kwamba mifarakano inayotokea katika nchi zingine mbali na jirani haiwezi kutokea Tanzania, kwamba siasa ya Tanzania ni ya pekee na hivyo kujaribu kuilinganisha kwa kutoa mifano ya mataifa mengine si sahihi.

Kwa hili lazima nikiri jinsi Chama cha Mapinduzi na awali TANU ilivyoweza kupandikiza kwa mafanikio makubwa imani hii potofu ya utofauti wetu na hao tunaowaita wengine. Linalonisikitisha zaidi ni kwamba hata wachache wetu tulioweza kupata ka mwanga ka elimu (exposure) nje ya nchi bado tumejifunga ndani ya box hili.

2. Watu kuendelea kuwa na mtazamo potofu kuhusu neno mabadiliko na hivyo kuhubiri dhana potofu ya heri zimwi likujualo katika jitihada za kutokuwa tayari kupokea mabadiliko. Nakumbuka jinsi mbinu hii ilivyotumika mwanzoni mwa 1990s katika kuwaonya wananchi kuwa kuruhusu upinzani nchini ni sawa na kukaribisha vita.

Mifano iliyotolewa kwenye redio na television na wahafidhina ni kuonesha yaliyokuwa yakitokea kwa jirani zetu kama Rwanda, Sudan na kwingineko. Ingawa baada ya miaka ishirini upinzani haujatupeleka vitani, walioko madarakani hadi leo wanaendelea kuwatisha wananchi kuhusu hatari ya kuikabidhi nchi kwa Watanzania wenzao.

3. Matumizi ya maneno uroho wa madaraka! Kwamba chama cha upinzani kuwaomba wananchi wakipe kura na wao wakamate dola ni kusukumwa na uroho wa madaraka. Lowassa kutaka kutimiza ndoto yake ya kuwa Raisi wa nchi hii anasukumwa na uroho wa madaraka na hivyo yuko tayari kutumia fedha kuwanunua wananchi wampe kura.

Kwamba chama tawala kukaa madarkani kwa miaka hamsini na ushee si uroho wa madaraka bali chama cha CUF au Chadema kutaka kuing'oa CCM madarakani, naam, huo ndio hasa uroho wa madarka. Kinachosikitisha hapa ni kwamba hadi leo wapo baadhi ya wananchi wanaweza kuhadaika kirahisi na kuamini propaganda kama hii ya kijinga!

Baada ya huo utangulizi naomba nijibu pia mambo kadhaa niliyoyasoma humu katika mada hili;

1. La kusimamisha jiwe: huu ni msemo tu na haukuanza kutumika leo na kama nakumbuka vizuri ni mojawapo katika misemo ya CCM iliyokuwa ikitumika kama namna ya kuwakatisha tamaa wapinzani. Tunao madiwani na wabunge ambao sifa yao pekee ya kuchaguliwa ni kwa sababu walikuwa ni wagombea wa chama tawala. CCM ilikuwa kila mara inatamba jinsi upinzani ulivyo dhaifu na kwamba hata wakisimaisha jiwe litapita tu. Leo mambo yanageuka wanatokeza watu wanatupia lawama UKAWA? Huu ndio unafiki nisioupenda hata kidogo.

2. La ushindi ni lazima: jamani tuwe wakweli, kutolewa kwa kauli kama hii na Raisi wa nchi na kunyamaza kwa vyombo husika bila kukemea kunaonesha udhaifu mkubwa katika hivyo vyombo katika kusimamia na kutoa haki sawa. Hapa kwa kweli upinzani lazima upongezwe kwa uvumilivu wanaoonesha vinginevyo hatari ya hali ya hewa kuchafuka ingekuwa kubwa tu. Pamoja na hayo upinzani kutotendewa haki katika vyombo vya dola na Usalama vinaonesha woga wa chama tawala kushindwa kwenye uchaguzi huru na wa haki.

3. La mtandao: Ni ukweli usiopingika kwamba CCM inao mtandao mkubwa, mtandao ambao Lowasaa alikuwa ni sehemu yake, mtandao ambao ulimwingiza Kikwete madarakani mwaka 2005 na mtandao ambao ulimliza na kummaliza kabisa Salim Ahmed Salim kisiasa na hadi leo hana hamu. Ujasiri aliouonesha Lowassa katika kujitoa CCM umeupa kiwewe huo mtandao kiasi kwamba nguvu ya ziada imebidi itafutwe ndani na nje ya mtandao (pamoja na JF) katika jitihada za kuuzima moto aliouwasha kwa kujiunga na Chadema.

4. La CCM na ufisadi: Raisi Mwinyi wakati anagombea Uraisi wa Jamhuri mwaka 1985 alipewa sifa tatu kubwa; ni mwenzetu, mpole na hana makuu. Raisi Mkapa naye mwaka 1995 alipewa sifa tatu; msafi asiye na kashfa (Mr. Clean), mwajibikaji na mwana diplomasia. Raisi Kikwete naye mwaka 2005, alipewa sifa kuu tatu; mpenzi wa wengi (chaguo la Mungu?), kijana na tumaini la taifa. Hakuna hata moja kati ya hawa alihusishwa na ufisadi na wananchi waliwapa kura nyingi tu lakini baada ya muda mfupi, walijikuta wakijutia uamuzi wao.

5. La ufisadi na mfumo: Wana CCM ni wananchi wenzetu; ndugu zetu, marafiki wetu na jirani zetu...tulizaliwa pamoja, tukakulia pamoja, tukaishi pamoja, tukasoma pamoja; je kitu gani kinachotutofautisha? Nadhani jibu ni UCCM wao unaowafanya waamini kwamba bila CCM hakuna maisha, hakuna amani, hakuna maendeleo na kwa msingi huo hakuna Tanzania. Mfumo uliojengwa na CCM hauioni Tanzania bila CCM na badala yake unaona vurugu, vita na uhasama, hauoni ndugu bali unaona adui asiye na malengo mema na adui asiyefaa kukabidhiwa nchi.

6. La Lowassa na ufisadi: Dr Slaa wa Chadema alitaja orodha ya mafisadi 11 mwaka 2008 na miaka mitatu baadaye akaiongeza na kufikia mafisadi 17. Mafisadi hawa wote walikuwa ni viongozi waandamizi wa serikali na chama tawala CCM wawili wao wakiwa viongozi wakuu wa nchi. Moja katika waliotajwa, Edward Ngoyai Lowassa, kwa sasa kaihama CCM na kujiunga na Upinzani akijitetea kwamba hakuhusika na ufisadi kama alivyotuhumiwa bali kujizulu kwake kulikuwa ni katika kuisetiri serikali na kiongozi wake Mkuu wakati huo Raisi Jakaya Mrisho Kikwete.

7. La UKAWA na ufisadi:
Inadaiwa kwamba Lowassa alitumia hela alizopata kifisadi kuinunua Chadema na kupewa fomu ya kugombea Uraisi kupitia chama hicho. Baadaye UKAWA ikiwa ni umoja wa vyama vikuu vinne; Chadema, CUF, NCCR na NLD ukampitisha kuwa mgombea Uraisi kupitia umoja huo. Pia inadaiwa pia kuwa kwa Chadema kumpokea aliyetuhumiwa kwa ufisadi, chama tawala CCM kimejitakasa na kuwa safi ila UKAWA kwa kumpitisha huyo fisadi kimechafuka na kurithi taji la ufisadi lililokuwa linashikiliwa na chama tawala CCM.

8. La CCM na usafi: Katika orodha ya mafisadi 17, CCM sasa imebakiwa na mafisadi 16 baada ya fisadi moja kuhamia Upinzani na kampeni zimepamba moto. Swali linaloumiza vichwa vya wengi ni jinsi CCM inavyojinadi kama chama safi huku mgombea wake akiwa moja wa watu waliokuwa kwenye orodha ya awali ya mafisadi 17. Watanzania wengine kama mimi pia twajiuliza, inawezekanaje kwa mtu moja, ambaye kwa miaka minane hayuko jikoni, aondoke na masufuria yote ya pilau yaliyoandaliwa tayari kwa walaji akiwaacha wanateseka na njaa?
 
Mkandara,

Politics is a dirty game. It is a crazy thing kama hapa kwa Uncle Sam ambapo watu wanaamua kuchagua jiwe.. can you eve imagine kuwa Donald is better than Jeb?

Nafikiri hasira za watu ni imani na matumaini waliyokuwa nayo 2005 hayakutimia na kwa miaka 10 wamekiona CCM kikidorora na watu wa CCM wakineemeka.

Chama hujengwa na watu, huandika katiba, kanuni sera na itikadi. Chama ni tofauti na dini. Dini ni static, ila watu tunataka kuifanya dynamic.. chama cha siasa si Static, ni dynamic, hivyo Chama hakikai kama gogo tulaumu sisimizi wanaoingia ndani maana Chama hakijisemei wala kujifanyia mambo.

Dhambi kuu ya CCM ilianza na Azimio la Zanzibar, hilo liliachia mianya ya viongozi kuhodho mali, kujilimbikizia mali na kujiingiza katika biashara.

Katika kipindi hicho, ni wazi yule aliyekuwa na akili na bila woga alichukua fursa hiyo na kujipatia "riziki" mapema kupitia mkondo wa kibiashara huku wengine wakianza kujiongezea marupurupu kikazi. Nafikiri hapa ndipo grayhound la Kimaasai lilitimka na kuwaacha wenzake wakishangaa na ndio kisa cha maugomvi yote.

Nchi inawekwa njia panda kutokana na ugomvi wa watu watatu au wanne, ambao wanashindana maslahi na wanafanyiana visa kuzidiana akili.

Wananchi wameng'amua hilo na kutokana na chuki dhidi ya dharau na udanganyifu wa wawili wa hawa wapigania maslahi, jiwe linaonekana bora!
Mkuu wangu, Donald hawezi kuwa rais wa Marekani (REALITY) hivyo wanaokuwa Optimistic na hili ni wale wasotumia akili zao barabara ama kujua siasa za Marekani juu ya kwamba Umaarufu hauwezi kukupeleka IKULU (White House)..Maana akichaguliwa yeye kuna uwezekano mkubwa Conservative wakapoteza both Senate na Congress, jambo ambalo Conservative hawawezi kuliafiki hata kidogo na wataikosa hata IKULU yenyewe!. Watu Ma Chale Champlin kama Donald wapo wengi na huruhusiwa ili kuonyesha Demokrasia yao na sii kweli kwamba huyu jamaa atashinda uchaguzi wamepita wengi kama yeye na waliongoza vile vile!. Donald anataka umaarufu zaidi na kaupata, na ndio maana watu wamefikia kusema Donald Trump apambane na Kanye West kugombea kiti cha Urais - Unafikiri wako serious that they hope, one of these dudes to be their President!

Mkuu nakubaliana kabisa na wewe juu ya madhambi ya CCM na kwamba walijisahau wakadhani wao ndio Miungu watu lakini kama ulivyosema chama hujengwa na WATU na kati ya wajenzi wa hiii CCM baada ya Azimio la zanzibar, Lowassa na Sumaye walikuwa Contactors wakuu na wasimamizi wa kila tunalolaumu leo hii, iweje nyumba hii ilojengwa na CCM tuikatae kuwa ni mbovu na haifai lakini wajenzi wake ndio tuwakubali kwa sababu wamehama shirika! Hii akili kweli, hata kama umelichoka shirika lazima kutambua wajenzi wake na haswa Contractors ndio walojenga na hivyo kufukuzwa na shirika mama ili kuondoa lawama. CCM wapo tayari kulipa kwa mabaya waloyafanya na sidhani kama wananchi watawasamehe lakini vile vile ni ujinga kulikataa shirika wakati unajua mjenzi ni nani!...

Hivi kweli Kesho Lowassa anayemiliki hisa kubwa katika mashirika nchini iwe Voda na mengine tusoyajua kesho awe rais kwa ktiba ya mwaka 1977 iloondoa miiiko ya viongozi mnategemea ujenzi wa Mawasiliano nchini ataujenga vipi? Bila shaka sii ajabu Voda wakachukua ama kununua mashirka mengine yote watake wasitake! Je, Lowassa yupo tayari kuachia Biashara zake zote ili aongoze Taifa kama mkombozi? Sidhani. Fikirieni hilo hata kama mnaichukia vipi CCM.. Je, sii ndio kwanza ataliboresha Azimio la Zanzibar akashika miradi yote ya miundombinu toka Umeme, Usafiri,Mawasiliano hadi Maji tukitaka kuishi kumuombe yeye!..Jiulizeni kwa nini reli ilipobomoka kule Dodoma haifanyiwa ukarabati (repaired) toka awe waziri mkuu hadi anaondoka!.

Huyu mtu atakuwa na sio tu conflict of interest bali FISADI mkubwa maana kisha waahidi watu Uwaziri, wengine RC na umiliki wa mashirika ya Umma, viwanda na miradi ya serikali kama watamfuata. Tunayajua yote haya toka kina Rostam, Mwapachu Masheikh hadi Wachungaji! Ananunua Urais kwa nguvu zote. Leo yeye na Sumaye wamejiita wakombozi wakati wananchi wanataka mabadiliko!..Hamuoni kama haendani kabisa na Chadema tuloijua iwe ILANI, kisera ama ahadi zake!

Halafu basi tumeaswa na mwalimu japo hakuwa Mungu lakini mambo kama haya hutokana na exposure, Uzoefu na Fikra ukiwa rais wa nchi jambo ambalo sisi hatukuweza kufikia kina hicho kiasi kwamba watu wengine wanafikiri Mwlaimu Alikuwa mchawi. Alijuaje mambo haya kutokea!.

Huyu jamaa yetu nasikia wakati wa vita na Uganda, yeye alikuwa mkuu storage ya vyakula, bidhaa na zana zote alipiga fedha toka wakati ule na sisi tulokuwepo wakait huo tunajua wanajeshi wengi walitajirika wakati ule wa Vita! sasa wewe chukulia wakati ule na shida zote hizo Mmasai umempa warehouse ya vyakula katajirikayeye wakait watu wengine wanakufa vitani..

Leo mnampa nchi ati kwa sababu mmeichoka CCM kwa ahadi ya kuwatoa katika Umaskini. Agenda yake kubwa ELIMU, hao watoto wake mwenyewe wamesoma hadi wapi maana fedha anayo kashindwa nini wanawe kuwa mfano bora!

Mkuu niilipenda sana Chadema na tena nikawa member wa Friends of Slaa jambo ambalo watu wengi humu hawakuwahi kulifanya. Na niliukubali msimamo wake kisiasa hadi pale alipoingizwa kizani nna kuwa msukule!.. leo hii nikubali kufungwa kamba za shingo wakati najua kabisa napelekwa machinjioni? Ama kweli tusishangae wazee wetu kuuzwa Utumwani kwa maelfu yao wakilindwa na waarabu wawili wenye magobole ya kushindilia!
 
Alinda,

..Exactly.

..hakuna uwezekano wa Tume ya Uchaguzi kuweka jiwe lipigiwe kura.

..kusema tutachagua jiwe ni namna tu ya kuonyesha ni kwa kiwango gani TUMECHOKA.

..mimi nisichopenda ni hii MONOPOLY ya ccm ambayo inasababisha ulaghai, dharau, uzembe, ukatili, ufisadi, na mambo mengine mengi.

..watu wanaboronga kazi, wanatesa watu, wanatukana, and nothing happens to them. That needs to change.

..hata mazingira yale ya kwamba mtu hawezi kufanya siasa nchi hii akafanikiwa bila kuwa mwana-ccm, that needs to change too.

..ninaamini hayo yanaweza kupatikana kwa kuipigia kura ukawa ktk uchaguzi huu. baada ya hapo tutawapima, na kama wataboronga, na wao tutawaweka pembeni.

cc Mkandara
Kama kweli watanzania mngekuwa mmeichoa CCM basi mngeanza kukataa uchaguzi huu hadi KATIBA MPYA ipatikane. Hapa ningewaelewa kwa sababu huwezi kuzuia Utawlaa dhalimu ikiwa ni RUKSA kwao kujitajirisha! Tunaweza walaumu CCM lakini nionyeshe Mbunge hata mmoja iwe wa CCM ama vyama vya Upinzani ni MASIKINI kama wewe na mimi hapa? HAKUNA hata mmoja wao, na ndio maana wamekubali uchaguzi huu haraka haraka ufanyike hata pasipo Katiba Mpya kwa visingizio kwamba CCM wamelazimisha! Well still UKAWA na wananchi kwa pamoja wangeweza kukataa uchaguzi huu usifanyike hadi Katiba Mpya ipatikane kwanza. Burundi wameweza kumkataa kiongozi kwa sababu tu kagombea mihula mitatu. Leo katiba iwe swala la baadaye! Misri walifanya hivyo kwa madai tu ya Katiba Mpya hawakutaka kuahidiwa maana walishahidiwa kwa miaka 20!

Leo mnaacha Katiba Mpya ambayo ingewabana wote katika MIIKO ya Uongozi kiasi kwamba hata huyu Lowassa akichaguliwa hataweza kuendesha Ufisadi wala biashara zake kujitajirisha. Katiba ambayo ingevipa mamlaka kamili vyombo kama TISS na Msajili wa vyama leo tunaahidiwa tu na tunaamini miujiza hii!..Hivi sasa umchague Lowassa au Magufuli hutabadilisha kitu isipokuwa kuwapa maisha mazuri viongozi wa wabunge wote watakao chaguliwa kuwahakikishia UTAJIRI wao kwa Mil. 11 kwa mwezi, Shangingi, posho na UHESHIMIWA wenye uwezo wa kupata liseni na vibali vyote vya kumiliki biashara, ardhi kusumbua wananchi huku akienda Bungeni anajifanya mwana mageuzi!..

Tumewaona miaka 10 tu ilopita wengine hata salamu barabarani hawatupi hufunga vioo vya magari yao wakituachia vumbi - Mheshimiwa kapita! Lowassa hakusaidii kitu ni sawa na kuweka chunvi katika kidonda! maana wengi walidhani UKAWA itagombea Ubunge zaidi kupambana na CCM bungeni kumbe changa la macho!. Mwenzenu miye niliisha liona hilo sikushangaa hata kidogo. Mabadiliko mangapi mnayataka! Mbowe mshikaji nadhani baada ya kuhadaiwa na watu huko nyuma akapoteza dira ya chama, akapoteza hadi marafiki wa kweli kisiasa ndani kaamua kumaliza kabisa!..ANAKAMUA hadi tone la mwisho!
 
Wakuu Mkandara na Rev Kishoka naomba pia mtafakari kuwa Lowassa, Sumaye na Mungai are owners of large tracts of land that they acquired in dubious ways particularly by buying national ranches at throw away prices.
Hawa wamiliki wa ardhi kubwa kwa nini wameamua kuungana ghafla na kudandia treni ya mabadiliko bila hata mmoja wao kuonyesha kutubu au kubadili fikra au mtazamo wa awali uliowapelekea kupora ardhi hizi?
 
Back
Top Bottom