CHADEMA: Ole wenu mkiipokea Mizoga ya CCM!

CHADEMA: Ole wenu mkiipokea Mizoga ya CCM!

Mkuu niilipenda sana Chadema na tena nikawa member wa Friends of Slaa jambo ambalo watu wengi humu hawakuwahi kulifanya. Na niliukubali msimamo wake kisiasa hadi pale alipoingizwa kizani nna kuwa msukule!.. leo hii nikubali kufungwa kamba za shingo wakati najua kabisa napelekwa machinjioni? Ama kweli tusishangae wazee wetu kuuzwa Utumwani kwa maelfu yao wakilindwa na waarabu wawili wenye magobole ya kushindilia!

Bob Mkandara,

Unakumbuka miaka ile nilipouliza siasa zetu ni za itikadi gani na mirengo gani na jibu ulilonipa?

Kama tangu nyakati zile tungeweza kujikita na kubaini aina za itikadi na mirengo, leo hii tusingekuwa hapa tukiwa tumechanganyikiwa.

Mwalimu Nyerere alipochukia kitendo cha Azimio la Arusha na siasa ya ujamaa na kujitegemea kunajisiwa na Azimio la Arusha na hasa kufutwa kwa miiko ya kuzuia "wabenzi" waliokuwa viongozi wa Chama na Serikali kujilimbikizia mali kupitia biashara na kusahau majukumu yao ni utumishi (Bhoke Munanka aliacha Siasa na kuwa mfanya biashara na kuna rafiki yetu mpaka leo anaumita ni fisadi), alitoa chachu ya kuanzishwa kwa vyama vya upinzani ili mpasuko wa ki-itikadi utokee ndani ya CCM na walio wajamaa ama waondoke au wawe na nguvu kukichukua chama.

Kilichotokea kupitia Azimio la Zanzibar ni rukhsa kwa viongozi kujihusisha na biashara na kuwa wenye hisa kwa makampuni binafsi. TUnajua Lowassa alinunua hisa Voda, akanunua mashamba na ardhi kwa urahisi kabisa na kuwapiku washindani (wananchi, wawekezaji na viongozi wenzake). MKapa akajiuzia Kiwira, akaunda kampuni ya kibiashara AnnBen na kuendela kukusanya mali. Hata Mramba na Yona wakaendela na ujuzi wao wa kibiashara na kujipatia mali.

Waliokuwa wakisitasita kwa kutokuwa na uhakika wakifikiria dhana ya Conflict of Interest (Sitta, Mwakyembe, Chenge, na wengine), wakabakia wakikamua kila fursa ndani ya Serikali na Chama kupitia mishahara, posho, marupurupu na hata uhujumu (scandals zetu, Meremeta, EPA, Radar, IPTL nk.)

Slaa na wewe ni wajamaa ambao pamoja na mimi tulilikosea somo kwa kushindwa kuuliza swali kuu kwa Chadema, je wao wako upande gani wa Kiitikadi?

Hata Zitto naye na ujamaa aliona wazi hii COI na ndipo chimbuko la misuguano ndani ya Chadema ingawa tulipoona anadhulumiwa haki, tuliangalia madhaifu yake kama binaadamu na kumdis-qualify kuwa anatufaa.

LOwassa ni tajiri kutokana na mfumo wetu ambao umeshindwa kuwa na vizingiti na milango ya uwazi yenye kupima na kulazimisha full disclosure ya mali (tumeambiwa ana ng?ombe 800 je wmehesabiwa na kuwa audited na nani?

Ikaja Richmond nayo mikono ikajaa nta na michongo ikachongeka.

Upinzani makini utatokana na CCM na hata la Rais bora atakuwa wa CCM, hayo yalikuwa maono ya Mwalimu Nyerere ili walio matajiri waende kwao (Chadema) walio wajamaa wabakie au wajamaa waondoke.

Chadema walitumia fursa ya "vita vya ufisadi" (by the way nini maana ya ufisadi?) kujijenga karibu na wananchi waliokuwa na taabu.

Sasa ndani ya CCM, vita vya maslahi vimesababisha kuitana majina na kuchafuana. Si JK, Mkapa, Kinana, Nape au wengine waliobakia kuwa sasa watarudi kwenye ujamaa na kujitegemea. Na Slaa na Zitto wakatemwa ndani ya chama hiki cha kibepari.

Chadema sasa kimekuwa chama rasmi cha kiliberali wa ubepari, CCM kinaupenda ubepari, lakini kinautraka ujamaa hapo hapo, ACT wameamua wao ni wajamaa.

Tuyapokee haya kwa heri na hata matamanio ya wananchi wengi ili kile kizingiti cha vyama kujijenga kwa itikadi tofauti na hata kuleta uwiano wa kweli bungeni na kudhibiti madaraka ya uraisi kutokee.

KUogopa kwenda njia hii kwa amani, kunaweza kutuletea vurugu huko mbeleni pindi wananchi wakiona kuwa ahadi (hasa za CCM) zilikuwa changa la macho.

Haijali nani ni Rais, lakini Bunge la mseto ndio hatua ya kwanza ya kuleta mabadiliko ya kweli ya kujenga maadili na kupembua Conflict of Interest (unakumbuka Sitta alisema ni Takrima?) na kuweka miiko mikali kuwazia viongozi wasijihusishe na biashara.
 
Wakuu Mkandara na Rev Kishoka naomba pia mtafakari kuwa Lowassa, Sumaye na Mungai are owners of large tracts of land that they acquired in dubious ways particularly by buying national ranches at throw away prices.
Hawa wamiliki wa ardhi kubwa kwa nini wameamua kuungana ghafla na kudandia treni ya mabadiliko bila hata mmoja wao kuonyesha kutubu au kubadili fikra au mtazamo wa awali uliowapelekea kupora ardhi hizi?

Nimemjibu Mkandara utata huu wa fursa zilizotokana na Azimio la Zanzibar. Hawa watatu walijinunulia ardhi mapma na kiulaini, MKapa alijinunulia Kiwira na majumba, Magufuli alijinunulia majumba (inasemekana), hivyo hatuwezi kuwka kipimo cha kurunzi kali kwa watatu, na hawa wengine kutumia kamshumaa kadogo.

Ubovu wa Ufisadi ni mfumo uliokubalika ndani ya CCM na kisha kwa kuzidiana maarifa ndani ya chama na wenye kujua lipi la maana kushika ndio tulipo hapa.

KUna waliothamini kununua ardhi na ranchi kwa kua uelewa wao ulikuwa mkubwa kujua ardhi ina thamani kubwa. Kuna waliokimbilia magari na nyumba au kujipachika kwenye bodi za mashirika ili wapate posho.

At end of day, CCM imejiunguza kwa kufungua pandora box la kuruhusu viongozi kujihusisha na biashara na wale waliozidiwa akili na maarifa analalamika na kujifanya watetea haki za watu.

Nina hamu sana kujua ni nani aliandika orodha ya list of shame na nia yake ilikuwa nini!

Kama tulishindwa kumfikisha Mkapa na associate wake mahakamani kwa ajili ya Kiwira, hatutaweza kumfikisha Lowassa, Sumaye na Mungai kwa kujinunulia ranchi za mifugo na mashamab makubwa.

TUnahitaji truth and reconcilliation na kama kweli CCM inataka kujirudi, basi ilifute azimio lake la Zanzibar na kushurtisha viongozi wake walifuate azimio la arusha, miiko na maadili ya uongozi kufuatana na siasa ya ujamaa na kujitegemea.

Chadema kama wao ni mabepari na hawalitambui Azimio la Arusha (liliundwa katika mfumo wa Chama kimoja na kwa manufaa ya kisiasa ya Tanu is mfumo wa vyama vingi), waachiwe na mfumo wao unaoruhusu viongozi wao kujihusisha na biashara.

Ila, Katiba yetu itamke wazi bila ambiguity masharti ya uongozi wa utumishi wa umma, iwe ni kuchaguliwa kwa kura au kuteuliwa.
 
Wakuu Mkandara na Rev Kishoka naomba pia mtafakari kuwa Lowassa, Sumaye na Mungai are owners of large tracts of land that they acquired in dubious ways particularly by buying national ranches at throw away prices.
Hawa wamiliki wa ardhi kubwa kwa nini wameamua kuungana ghafla na kudandia treni ya mabadiliko bila hata mmoja wao kuonyesha kutubu au kubadili fikra au mtazamo wa awali uliowapelekea kupora ardhi hizi?


Hivi kuna sheria inayozuia mtanzania kumiliki ardhi? Nisije kuwa nimeingiwa mkenge maana nimenunua zaidi ya heka 50.. Na hivi niko njiani kuongezea tuheka twingine..Naomba ufafanuzi hapo kama una uelewa wa mambo ya ardhi.
 
Hivi kuna sheria inayozuia mtanzania kumiliki ardhi? Nisije kuwa nimeingiwa mkenge maana nimenunua zaidi ya heka 50.. Na hivi niko njiani kuongezea tuheka twingine..Naomba ufafanuzi hapo kama una uelewa wa mambo ya ardhi.

Ni hivi: walijilimbikizia ardhi hizi za umma. Siyo kwamba walizirudisha mikononi mwa serikali yaani Wizara ya Ardhi na serikali ya vijiji na kusibiri itangazwe. Hapana. Waligawana kimyakimya. Na walikomba ardhi yote. Mfano ardhi ya Magereza. Natumai umemsikiliza Dr Slaa!
 
Ni hivi: walijilimbikizia ardhi hizi za umma. Siyo kwamba walizirudisha mikononi mwa serikali yaani Wizara ya Ardhi na serikali ya vijiji na kusibiri itangazwe. Hapana. Waligawana kimyakimya. Na walikomba ardhi yote. Mfano ardhi ya Magereza. Natumai umemsikiliza Dr Slaa!


Yaani walikomba ardhi ni hao wawili tu kati ya viongozi wote? vpi na yule aliuza nyumba za umma kwa ndugu na mahawala zake? au vip yule aliyejiuzia mgodi wa Kiwira? au umesahau mikataba 16 ya wachina na kisa cha mwana wa mfalme? (rejea Dr. Slaa)

Kwa hayo ninaweza kukubalina na rev.Kishoka kuwa hawa watu walizidiwa kete sana wanaaza kumchafua wenzao.

Hata ukiwauliza ufasadi wa Lowassa ni nini kiila mtu anainamisha kichwa chini au wanakuja na story za Richmond sasa ukiwauliza kama ni Richmond mlishindwa nini kustisha mkataba na kumpeleka Lowassa mahakamani?

hakuna jibu ukiuliza zaidi ufisadi wa Lowassa wanaibuka na hoja ya kusema "hata baba wa taifa alisema.." yaani hakuna mtu anayeweza kutaja ufisadi wa Lowassa zaidi ya Richmond ambayo amesema yeye hausiki na hata Mwakyembe aliacha kusoma pg fulani kumfunika Rais na ndivyo iliyokuwa kwa pesa za Escrowa na kamati ya Zitto waliposema kuwa wao hawawezi kumchukulia hatua rais.. Agizo la kutoa bil.365 lilitoka kwenye ofisi ya rais.
 
Last edited by a moderator:
Yaani walikomba ardhi ni hao wawili tu kati ya viongozi wote? vpi na yule aliuza nyumba za umma kwa ndugu na mahawala zake? au vip yule aliyejiuzia mgodi wa Kiwira? au umesahau mikataba 16 ya wachina na kisa cha mwana wa mfalme? (rejea Dr. Slaa)

Kwa hayo ninaweza kukubalina na rev.Kishoka kuwa hawa watu walizidiwa kete sana wanaaza kumchafua wenzao.

Hata ukiwauliza ufasadi wa Lowassa ni nini kiila mtu anainamisha kichwa chini au wanakuja na story za Richmond sasa ukiwauliza kama ni Richmond mlishindwa nini kustisha mkataba na kumpeleka Lowassa mahakamani?

hakuna jibu ukiuliza zaidi ufisadi wa Lowassa wanaibuka na hoja ya kusema "hata baba wa taifa alisema.." yaani hakuna mtu anayeweza kutaja ufisadi wa Lowassa zaidi ya Richmond ambayo amesema yeye hausiki na hata Mwakyembe aliacha kusoma pg fulani kumfunika Rais na ndivyo iliyokuwa kwa pesa za Escrowa na kamati ya Zitto waliposema kuwa wao hawawezi kumchukulia hatua rais.. Agizo la kutoa bil.365 lilitoka kwenye ofisi ya rais.

Alinda:

Lowassa anagombea urais. Na moja ya sifa ya kuwa kiongozi ni kuwa communicator mzuri. Kama Lowassa sio fisadi hakuna sababu ya wewe au watu wengine kumtetea. Kinachotakiwa ni yeye kutumia nafasi aliyonayo kueleza kwanini yeye sio fisadi.

Napenda CDM/UKAWA washinde. Lakini ni kiongozi lazima ajue kujieleza na kujibu shutuma.
 
Hivi kuna sheria inayozuia mtanzania kumiliki ardhi? Nisije kuwa nimeingiwa mkenge maana nimenunua zaidi ya heka 50.. Na hivi niko njiani kuongezea tuheka twingine..Naomba ufafanuzi hapo kama una uelewa wa mambo ya ardhi.

Wewe unanunua heka 50 tena kwa makubaliano. Wenzio wanunua ranchi za taifa.
 
Nimemjibu Mkandara utata huu wa fursa zilizotokana na Azimio la Zanzibar. Hawa watatu walijinunulia ardhi mapma na kiulaini, MKapa alijinunulia Kiwira na majumba, Magufuli alijinunulia majumba (inasemekana), hivyo hatuwezi kuwka kipimo cha kurunzi kali kwa watatu, na hawa wengine kutumia kamshumaa kadogo.

Ubovu wa Ufisadi ni mfumo uliokubalika ndani ya CCM na kisha kwa kuzidiana maarifa ndani ya chama na wenye kujua lipi la maana kushika ndio tulipo hapa.

KUna waliothamini kununua ardhi na ranchi kwa kua uelewa wao ulikuwa mkubwa kujua ardhi ina thamani kubwa. Kuna waliokimbilia magari na nyumba au kujipachika kwenye bodi za mashirika ili wapate posho.

At end of day, CCM imejiunguza kwa kufungua pandora box la kuruhusu viongozi kujihusisha na biashara na wale waliozidiwa akili na maarifa analalamika na kujifanya watetea haki za watu.

Nina hamu sana kujua ni nani aliandika orodha ya list of shame na nia yake ilikuwa nini!

Kama tulishindwa kumfikisha Mkapa na associate wake mahakamani kwa ajili ya Kiwira, hatutaweza kumfikisha Lowassa, Sumaye na Mungai kwa kujinunulia ranchi za mifugo na mashamab makubwa.

TUnahitaji truth and reconcilliation na kama kweli CCM inataka kujirudi, basi ilifute azimio lake la Zanzibar na kushurtisha viongozi wake walifuate azimio la arusha, miiko na maadili ya uongozi kufuatana na siasa ya ujamaa na kujitegemea.

Chadema kama wao ni mabepari na hawalitambui Azimio la Arusha (liliundwa katika mfumo wa Chama kimoja na kwa manufaa ya kisiasa ya Tanu is mfumo wa vyama vingi), waachiwe na mfumo wao unaoruhusu viongozi wao kujihusisha na biashara.

Ila, Katiba yetu itamke wazi bila ambiguity masharti ya uongozi wa utumishi wa umma, iwe ni kuchaguliwa kwa kura au kuteuliwa.
Mkuu kusema kweli mimi hapa nitapingana nawe kidogo juu ya MFUMO wa CCM, kwa sababu AZIMIO LA ZANZIBAR sio mrengo wa chama bali ilikuwa MWONGOZO wa KItaifa ndani ya Katiba yetu. Hata ukiwaondoa CCM miaka ilopita bado sheria na kipengele hicho kingekuwepo na kipo hadi leo ndani ya katiba ya mwaka 1977.

Walojilimbikiza mali wapo kila chama, Maalim Seif, Bilal kina Karume wote hawa ni matajiri walonufaika na mfumo huo toka mwaka 1985, Ukirudi Bara hawahesabiki toka viongozi wa nchi, mashirka ya Umma hadi Taasisi wote wameutumia mfumo huo kujinufaisha na haikuwa sera wala mrengo wa CCM. Wamo watu kibao na wanachama wa Chadema walonufaika na Mfumo huo na hata kina Rostam na Mengi huyu ambaye leo ni kikaragosi wa Lowassa alifaidika sana tu. Lakini Lowassa kafisadi toka wakati wa Mwalimu hata kabla ya Azimio hili. Sema tu ujio wa Azimio hili kulimpa nguvu zaidi kujikita ndani ya chama..

Kwa hiyo chochote kinachoingia ndani ya KATIBA ya nchi hakina mrengo maana hii ni Sheria Mama ambayo haina chama na hii ndio sababu kubwa sisi wananchi tukaiomba KATIBA MPYA, sio kwa sababu tulitaka kuindoka CCM madarakani ama tulitaka serikali 3! Hawa wanasiasa wakatuchezea akili zetu tukaamini wana nia thabiti ya kuipata katiba Mpya yenye kurudisha MIIKO na MAADILI ambayo sii sera wala mrengo kumbe wao wana yao ya kisiasa kututenganisha wananchi. Leo tazama tulivyotengana humu na pengine hata kuchukiana na yote inatokana na wao wala sii kosa la CCM, UKAWA wala Lowassa ni watu tulokosa Mwongozo!.

Nilisema toka mwanzo swala la serikali ngapi ni sura moja tu, kuna sura 120 mule (kama sikosei) zitazamwe zote kwanza kisha hili swala la serikali ngapi liachwe kiporo maana limetokea sii mara moja wala mbili na tumeshindwa kufikia muafaka juu ya serikali ngapi huko nyuma. Lakini UKAWA wakaona mwanya wa kupiga bao la penalty kwa kutumia katiba ilihali tumeachwa pale pale tulipokuwa miaka 50 ilopita. Utailaumu CCM kwa kutoleta maendeleo kwa miaka 50 wakati makosa yapo katika mwongozo wake halafu unatajka kuiondoka CCM kwa mwongozo ule ule ulotufikisha hapa tulipo! AZIMIO LA ZANZIBAR ndio lilikuwa kaburi la Uzalendo, Uadilifu, uwajibikaji, Usawa na Haki! na vyote hivi viliondolewa ndani ya katiba ya Taifa tukawa na makundi ya Waheshimiwa na Watawaliwa!

Huwezi kuwalaumu Wakristu kwa kula nguruwe ikiwa agano jipya limeihalalisha! na huwezi sema kwamba ni wakristu fulani ndio waloharibu, hapana ni mwongozo wenyewe kama kweli umekosewa na kufanyiwa marekebisho ambayo hayakustahili basi turudi toka mwanzo. Hivyo hata kama Lowassa atachukua Ushindi ama mgombea yeyote toka vyama vingine hawezi kuzuia Confilct of interest, Takrima wala Kupendeleana (Nepotism) kwa sababu sio haramu ndani ya Katiba yetu.. Yaweza kuwa vibaya lakini sio haramu!
 
Yaani walikomba ardhi ni hao wawili tu kati ya viongozi wote? vpi na yule aliuza nyumba za umma kwa ndugu na mahawala zake? au vip yule aliyejiuzia mgodi wa Kiwira? au umesahau mikataba 16 ya wachina na kisa cha mwana wa mfalme? (rejea Dr. Slaa)

Kwa hayo ninaweza kukubalina na rev.Kishoka kuwa hawa watu walizidiwa kete sana wanaaza kumchafua wenzao.

Hata ukiwauliza ufasadi wa Lowassa ni nini kiila mtu anainamisha kichwa chini au wanakuja na story za Richmond sasa ukiwauliza kama ni Richmond mlishindwa nini kustisha mkataba na kumpeleka Lowassa mahakamani?

hakuna jibu ukiuliza zaidi ufisadi wa Lowassa wanaibuka na hoja ya kusema "hata baba wa taifa alisema.." yaani hakuna mtu anayeweza kutaja ufisadi wa Lowassa zaidi ya Richmond ambayo amesema yeye hausiki na hata Mwakyembe aliacha kusoma pg fulani kumfunika Rais na ndivyo iliyokuwa kwa pesa za Escrowa na kamati ya Zitto waliposema kuwa wao hawawezi kumchukulia hatua rais.. Agizo la kutoa bil.365 lilitoka kwenye ofisi ya rais.

Hivi ufisadi wa Lowassa ulisikia ni Richmond tu wakati nimekuwekea hapo kununua renchi za taifa kwa bei ya kutupa bila zabuni unaona siyo ufisadi? Bado kuna suala la kuwa na fedha nje, mamilioni ya pauni Uingereza na na dola katika offshore accounts ambazo ameshindwa kutetea. Dili nyingi amepiga Lowassa za kukatiwa percent na wafanyabiashara hasa wa kihindi. Na hajaanza leo.
Unamtetea mtu ambaye kumbe hujui hata 10% yake! Na yote yaliwekwa pembeni kumstahi ingawa wengine tulipiga kelele sana kuhusu ufisadi wake. Lakini leo hii CCM iliyomlea imemwacha aje huku baada ya kushindwa kumfuga.
Lowassa ana madhambi mengi niliyokutajia. Ukitaka tuanze kumwanika mzee wa watu zaidi basi humtakii mema ye na familia yake.
 
Last edited by a moderator:
Hivi ufisadi wa Lowassa ulisikia ni Richmond tu wakati nimekuwekea hapo kununua renchi za taifa kwa bei ya kutupa bila zabuni unaona siyo ufisadi? Bado kuna suala la kuwa na fedha nje, mamilioni ya pauni Uingereza na na dola katika offshore accounts ambazo ameshindwa kutetea. Dili nyingi amepiga Lowassa za kukatiwa percent na wafanyabiashara hasa wa kihindi. Na hajaanza leo.
Unamtetea mtu ambaye kumbe hujui hata 10% yake! Na yote yaliwekwa pembeni kumstahi ingawa wengine tulipiga kelele sana kuhusu ufisadi wake. Lakini leo hii CCM iliyomlea imemwacha aje huku baada ya kushindwa kumfuga.
Lowassa ana madhambi mengi niliyokutajia. Ukitaka tuanze kumwanika mzee wa watu zaidi basi humtakii mema ye na familia yake.

Nimekuuliza hivi kama swala ni ranchi alizonunua, je vipi kuhusu nyumba za serikali kupewa mahawala? Je kuhusu bil.265 zilizopotea katika ujezi wa barabara? na je vipi kuhusu vifuko kibovu chenye thamani ya bil.8??

Ni lini na wapi alishindwa kutetea hizo account zilizoko nje ya nchi? Swala si kutoa tuhuma bila ushaidi maana kama ni hivyo hata mimi ninaweza kusena Susuviri ni fisadi ana account nje.. Swala ni kuleta vielelezo vya kusapoti tuhuma zako..

Na je kama huyu mtu ni fisadi kama mnavyotaka kutuhubiria je nini kinawashinda kumfikisha mahakamani?


Je kuna ushaidi wowote unaonyesha hizo tuhuma zako?
 
Last edited by a moderator:
Nimekuuliza hivi kama swala ni ranchi alizonunua, je vipi kuhusu nyumba za serikali kupewa mahawala? Je kuhusu bil.265 zilizopotea katika ujezi wa barabara? na je vipi kuhusu vifuko kibovu chenye thamani ya bil.8??

Ni lini na wapi alishindwa kutetea hizo account zilizoko nje ya nchi? Swala si kutoa tuhuma bila ushaidi maana kama ni hivyo hata mimi ninaweza kusena Susuviri ni fisadi ana account nje.. Swala ni kuleta vielelezo vya kusapoti tuhuma zako..

Na je kama huyu mtu ni fisadi kama mnavyotaka kutuhubiria je nini kinawashinda kumfikisha mahakamani?


Je kuna ushaidi wowote unaonyesha hizo tuhuma zako?

Supporting documents ziliwekwa humu humu ni ya kufukua tu.
Kufikisha mahakamani ni kazi ya DPP na hapo tuko pamoja kuwa ilitakiwa Lowassa awe jela siku nyingi. CCM ilifanya kosa kumlea nyoka.
 
Last edited by a moderator:
Supporting documents ziliwekwa humu humu ni ya kufukua tu.
Kufikisha mahakamani ni kazi ya DPP na hapo tuko pamoja kuwa ilitakiwa Lowassa awe jela siku nyingi. CCM ilifanya kosa kumlea nyoka.

Kama ni swala la kwenda jela basi tuanze na Mkapa mgodi wa Kiwira
halafu tuje Kikwete Richmond, Escrow, Buzwagi,Epa na madudu mengine
Halafu tuje Kinana pembe za ndovu
halafu tuje Sitta Chenji ya bunge la katiba
halafu tuje Mwakyembe mabehewa mabavu bil.220
Halauf tuje Magufuli nyumba za serikali, upoteaji wa shs. Bil.265 hela za barabara, ununuaji wa kivuko kibovu bil.8,
tukimaliza hao ndio tuje kwa Lowassa na tuhuma zisiso na ushaidi. kinyume na hapo kutakuwa ni kumuonea Lowassa..
 
KUna utamaduni mmoja tumeulea Watanzania na ni mbaya sana. Utamaduni wa kusitasita kufamya yale yaliyosahihi kutokomezaa yanaoyounguza Taifa.

Mfano, ndugu yangu Susuviri umesema, kuna mengi sana ya Lowassa na mengine yana-impact familia yake. Granted yapo, yanajulikana, kuna ushahidi. Lakini bado tunasubiri DPP afanye kazi.

DPP anasubiri nini? Polisi wanasubiri nini?

Ama kuna namna ingine ya kutishiana kumwaga mboga..

Mwakyembe juzi kasema kuwa Lowassa anaweza kufikishwa mahakamani sijui kama ilikuwa kauli ya kisiasa zaidi kuzolea kura au ni kauli ya umakini ki-uanasheria. Kama ni kweli, basi swali la wapiga kura kwa Mwakyembe, Sita na hata Dr. Slaa jana ni hili: Kwa nini Lowassa bado anapeta kama kuna ushahidi wa wazi kuwa anaweza funguliwa mashitaka? Swalilitaendelea kucheleweshwa kufunguliwa mashitaka au kuchukua hayua za sheria kunatokana na nini?

Sasa vidole hivi vitarudi kuitazama Serikali na tutajiuliza ni nani mkuu wa Serikali? THen tutaanza kujiuliza ni nani chama tawala? kisha tuajikumbusha ya Chavda, Loliondo, na kuendelea mpaka Escrow tutakuta viongozi wa Serikali ni wale wale, chama ni kile kile na ubutu ni uleule!

Aidha Dr. Slaa jana kasema ana mwengi anayajua "hataki" kuyamwaga hadharani anasubiri Lowassa na Sumaye wayajibu mapigo yake. Kitendo hicho tuu cha kutoa kauli kama za blackmail au kutishia kuna mengine wakati theme ya mkutano wake ilijijenga kuwa ni anakuja kusema ukweli na hata alipoanza kutoa maelezo ya Richomond na Ranchi za magereza, kimepunguza maana ya yeye kuongea uadilifu in my humble opinion.

Kama kuna mengi, kwa nini yachukue mkondo wa vita na majibishano ya kisisasa ya kutegeana?

NItarudi kwa Mwakyembe, Sitta na Slaa na hoja ya Richmond. Kujirudiarudia kwa hii hoja kunafungua maswali zaidi ambayo labda awali hatukuyatafakari na kisha inatuleta kwenye hitimisho moja ambao ni tata mno.

Je uchunguzi wa Richmond ulikuwa ni kuhusu namna Seikali ilivyoingia mkataba au ni kuuchunguza mchakato na mkataba wenyewe? Kwa maana kama ilijulikana kwa upande mmoja kuwa Serikali ilifanya uzembe, lakini pia kwa upande wa pili inaonekana wazi kuwa Richmond walishindwa kazi kutokana na masharti ya mkataba na hata kuna uwezo wa kuvunja mkataba, kwa nini Kamati ya Mwakyembe ilipokuja na matokeo yake, haikutoa pendekezo la kwanza kuwa ni kuvunja mkataba immediately na la pili ni kwa Waziri Mkuu kuwajibika?

Hapo linafungua mlango mwingine: Spika Sitta alizuia kamati ya Mwakyembe isichunguze Dowans iliyokuwa mrithi wa mkataba wa Rchmond. Kwenye mkataba wa Richmond na Tanesco, imeandikwa wazi kuwa mkataba hauwezi kuuzwa kwa mtu mwingine bila idhini ya Tanesco.

Ilikuwaje tukakubali mapungufu haya yaendelee, Richmond kauza kwa Dowans, Dowans kauza kwa Symbion, na bado tunalipa capacity charges kwa umeme usiozalishwa?

NImefafanua kwa kina maswali haya ya Richmond kuonyesha wazi ni jinsi gani mambo tunayafanya shaghalabaghala, kisha tuko mstari wa mbele "kutoa kweli" lakini ukichunguza ndani ya kweli kuna ama uwongo au makusudi ya kuficha mambo.

Lowassa ni fisadi, tuanike kila kitu bila kuweka nyuma kitu. Kama ni ushahidi, uwekwe wazi na tuwaulize Polisi, Takukuru, DPP, AG , TISS na Ikulu wanafanya nini kukaa kimya?

Maana kazi hii ya kufukua madudu si ya Kishoka, Susuviri, Mkanda na Ailinda pekee!

Hivyo, huu utamaduni wa kusema "niseme nisiseme" unaua uadilifu na wajibu.

Ndio maana nashindwa kuelewa leo tunachagua chagua ovu lipi tupigie kelele kwa sauti kuu, ni mwovu yupi tumshikie bango na vuvuzela, lakini mengine tunasema haya baadaye..

Tulikosea huko nyuma kwa kusema Lowassa tutamshughulikia huko mbeleni, sasa tunafanya kosa hilo hilo kwa Magufuli, Mbowe, Mwakyembe, Makamba, Mnyika, Jussa, Makaidi, Azzan na wengine wengi maana tunaona umuhimu kuwatumia kwa sasa, na hakuna haja ya kuwafungulia mashitaka au kusema hawafai (natoa mfano kutumia majina si kuwa natamka kuwa wote hawa nana madhambi au tuhuma).

Turusi kwenye mstari kwa kuanza kushughulikia mamatizo bila kutishiana ya niseme nisiseme na tujiulize, ukaaji kimya wa Serikali ya CCM miaka yote hii, bado tuamini kuwa sasa itabadilika?

NI sisi ndio tubadilike kwanza kisha wao tuwalazimishe wabadilike!
 
Rev. Kishoka,

..jana Dr.Slaa kasema richmond alianza wakati wa Mkapa.

..wakati wa Mkapa richmond waliingia kwa gia ya kujenga bomba la mafuta dar-to-mwanza.

..walisaini MOU na serikali, wakatokomea kwenda kutafuta pesa za mradi, na mpango huo ukajifia wenyewe.

..nakumbuka kusoma toka kwako, au kwa mchangiaji mwingine, kuhusu wazawa kunyang'anywa mradi huo na kupewa hawa jamaa wa richmond.

..baada ya jamaa kushindwa kupata fedha za kujenga bomba la mafuta, kukatokea crisis ya uhaba wa umeme. sasa hapo ndipo wajanja wakaja na hii RICHMOND tunayoiongelea sasa hivi.

..nilitaka tu niweke kumbukumbu sawa, na kukumbusha the old good days za JF.

cc Alinda, Mkandara, Nguruvi3, Mwalimu
 
Kama ni swala la kwenda jela basi tuanze na Mkapa mgodi wa Kiwira
halafu tuje Kikwete Richmond, Escrow, Buzwagi,Epa na madudu mengine
Halafu tuje Kinana pembe za ndovu
halafu tuje Sitta Chenji ya bunge la katiba
halafu tuje Mwakyembe mabehewa mabavu bil.220
Halauf tuje Magufuli nyumba za serikali, upoteaji wa shs. Bil.265 hela za barabara, ununuaji wa kivuko kibovu bil.8,
tukimaliza hao ndio tuje kwa Lowassa na tuhuma zisiso na ushaidi. kinyume na hapo kutakuwa ni kumuonea Lowassa..

Ukiwa mpenda haki, huwezi kumtetea mtu kwa sababu wenzake nao wamefanya makosa yanayofanana. Lowassa na uliowataja hapo juu ni mafisadi. Wanachofanya sasa hivi ni kutumia demokrasi hili wabakie madarakani.

Niliudhuria mkutano wa CDM na Mbowe alikuwa mtoa hotuba. Alisema CDM ikichukua madaraka wataunda tume ya usuluhishi kama hile ya Africa ya Kusini kupatana na CCM. Maneno hayo yalirudiwa na Mr. Duni, mgombea mwenza kupitia CDM/UKAWA.

Kwa maneno mengine, ufisadi ni neno la kampeni ya uchaguzi tu. Lakini hakuna mtu mwenye nia ya kumfunga mwenzake. Hivi kweli Lowassa awe rais atampeleka Mkapa au Kikwete gerezani?
 
Rev. Kishoka,

..jana Dr.Slaa kasema richmond alianza wakati wa Mkapa.

..wakati wa Mkapa richmond waliingia kwa gia ya kujenga bomba la mafuta dar-to-mwanza.

..walisaini MOU na serikali, wakatokomea kwenda kutafuta pesa za mradi, na mpango huo ukajifia wenyewe.

..nakumbuka kusoma toka kwako, au kwa mchangiaji mwingine, kuhusu wazawa kunyang'anywa mradi huo na kupewa hawa jamaa wa richmond.

..baada ya jamaa kushindwa kupata fedha za kujenga bomba la mafuta, kukatokea crisis ya uhaba wa umeme. sasa hapo ndipo wajanja wakaja na hii RICHMOND tunayoiongelea sasa hivi.

..nilitaka tu niweke kumbukumbu sawa, na kukumbusha the old good days za JF.

cc Alinda, Mkandara, Nguruvi3, Mwalimu

So they gang-rape the country?
 
Mkuu kusema kweli mimi hapa nitapingana nawe kidogo juu ya MFUMO wa CCM, kwa sababu AZIMIO LA ZANZIBAR sio mrengo wa chama bali ilikuwa MWONGOZO wa KItaifa ndani ya Katiba yetu. Hata ukiwaondoa CCM miaka ilopita bado sheria na kipengele hicho kingekuwepo na kipo hadi leo ndani ya katiba ya mwaka 1977.

Kwa hiyo chochote kinachoingia ndani ya KATIBA ya nchi hakina mrengo maana hii ni Sheria Mama ambayo haina chama na hii ndio sababu kubwa sisi wananchi tukaiomba KATIBA MPYA, sio kwa sababu tulitaka kuindoka CCM madarakani ama tulitaka serikali 3! Hawa wanasiasa wakatuchezea akili zetu tukaamini wana nia thabiti ya kuipata katiba Mpya yenye kurudisha MIIKO na MAADILI ambayo sii sera wala mrengo kumbe wao wana yao ya kisiasa kututenganisha wananchi. Leo tazama tulivyotengana humu na pengine hata kuchukiana na yote inatokana na wao wala sii kosa la CCM, UKAWA wala Lowassa ni watu tulokosa Mwongozo!.
!


Bob Mkandara,

Kwa mujibu wa Katiba (hata ya 1977) , hakuna mahali popote iliposema ni mwiko kwa kiongozi kujihusisha na biashara!

Kilichoko kwenye katiba ambacho ni very vague bila limitations ni wajibu kwa kila mwananchi. Kabla sijaanza chambua vipengele hivi, lazima nirudishe hoja kwenye Azimio la Arusha na kwa nini vipengele pingamizi vya Viongozi kujihusisha na biashara hasa viongozi wa Serikali, Mashirika ya Umma na Chama yalibainishwa wazi ndani ya Azimio na hata kuundwa kwa leadership code ambayo ndio ilikuwa Sheria kuu kubana watu kwa uwajibikaji wa kuzuia Viongozi kujihusisha na biashara wakiwa kazini na hata kubainisha Conflict of Interests.

Azimio la Zanzibar, lilivunja na kutengua maana nzima ya Leadership Code. Azimio lilipotamka wazi kuwa Wanasiasa waliochaguliwa na wananchi, watendaji wa Serikali na Mashirika wanaweza jihusisha na biashara, ililazimisha leadership code kufutwa kutokana na conflict ya wazi ya Ruksa yya kufanya biashara versus vipingamizi vya leadership code- miiko ya uongozi.

Hata hivyo, pamoja na miiko ya uongozi iliyokuwepo kwa miaka mingi tangu Azimio la Arusha, wafanyakazi wa Serikali, Mashirika na Taasisi za umma, Wanasiasa na hata mawaziri, waliruhusiwa kujiongezea kipato kupitia shughuli za uzalishaji kama kilimo, mifugo na uvuvi. Ndio maana Oysterbay na Masaki harufu ya mavi ya ng'ombe na kuku ilikuwa jambo la kawaida.

Hii ilitokana na mishahara na marupurupu kutotosheleza (lakini hapa kuna kasoro; watu walikaa nyumba za serikali na mashirika, walipata huduma za afya hata usafiri kwenda kazini bure) na njia moja kupunguza vishawishi vya watu kujiingiza katika usanii ilikuwa ni kutoa subsidies (nilizoonyesha kwenye mabano) na kuruhusu shughuli hizi ambazo zilikuwa part and parcel ya Siasa ya Ujamaa na kujitegema na haswa suala la Kilimo kuwa uti wa mgongo.

Katiba ya 1977 na hata marekebisho ya 1984 inaashiria vitu vifuatavyo kama msingi wa kuhakikisha haki na kupata kipato halali kutokana na jasho. Aidha kinazungumzia wajibu wa Wananchi kulinda mali ya umma dhidi ya ubadhirifu na upotevu (hapa mkazo wa sehemu hii ya katiba ulikuja kutokana na lile zoezi la kupiga vita ulanguzi na magendo la 1984).

Kwa makusudi kabisa nitaanza na kipengele cha 27 cha katiba:

Duty tosafeguardpublic propertyAct No.15 of 1984 Art.6

27.-(1) Every person has the duty to protect the natural resources of theUnited Republic, the property of the state authority, all property collectivelyowned by the people, and also to respect another person's property.

(2) All persons shall be required by law to safeguard the property of thestate authority and all property collectively owned by the people, to combat allforms of waste and squander, and to manage the national economy assiduouslywith the attitude of people who are masters of the destiny of their nation.

Huu ndio msingi na ngao ya kuundwa sheria za kuzuia uhalifu wa zizi wa mali, rushwa, magendo, ubadhirifu na uhujumu.

Tukirudi kifungu cha 25 cha katiba hiyohiyo kuhusiana na kazi, Katiba inasema hivi:

Duty toparticipate inworkAct No.15of 1984Art.625.-and Act No. 7 of 1994 Art.8(1)(k)

(1) Work alone creates the material wealth in society, and is thesource of the well-being of the people and the measure of human dignity.Accordingly, every person has the duty to –
(a) participate responsibly and honestly in lawful and productive work;
(b) observe work discipline and strive to attain the individual andcollective production targets desired or set by law.
(2) Notwithstanding the provisions of subarticle (1), there shall be noforced labour in the United Republic.

Halafu ukirudi kifungu cha 24, kinazungumzia kuwa na mali:

Right to ownpropertyAct No.15of 1984Art.6Act No.1of 2005Art.9
24.-(1) Every person is entitled to own property, and has a right to theprotection of his property held in accordance with the law.
(2) Subject to the provisions of subarticle (1), it shall be unlawful for anyperson to be deprived of his property for the purposes of nationalization or anyother purposes without the authority of law which makes provision for fair andadequate compensation.

Ukirudi kwenye kifungu cha 22 na 23, kinazungumzia tena mambo ya kazi ambayo yamezungumziwa kifungu cha 25:

Right to work Act No.15 of 1984 Art.6
22.-(1) Every person has the right to work.
(2) Every citizen is entitled to equal opportunity and right to equal termsto hold any office or discharge any function under the state authority.

Right to justremunerationAct No.15of 1984Art.6

23.-(1) Every person, without discrimination of any kind, is entitled toremuneration commensurate with his work, and all persons working according totheir ability shall be remunerated according to the measure and qualification forthe work.

(2) Every person who works is entitled to just remuneration

Sasa hata kifungu cha 9 cha katiba hiyo (pungufu ni vipengele vilivyobadilishwa 1984 na 1992) haionyeshi mahali kuwa Viongozi na Watendaji wanapigwa kabali kuwa na biashara.

The pursuit ofUjamaa andSelf-RelianceAct No.15of 1984Art.6Act No.4of 1992Art.6

9. The object of this Constitution is to facilitate the building of the UnitedRepublic as a nation of equal and free individuals enjoying freedom, justice,fraternity and concord, through the pursuit of the policy of Socialism and SelfReliance which emphasizes the application of socialist principles while taking intoaccount the conditions prevailing in the United Republic.
Therefore, the stateauthority and all its agencies are obliged to direct their policies and programmestowards ensuring -(a) that human dignity and other human rights are respected andcherished;
(b) that the laws of the land are upheld and enforced;
(c) that activities of the Government are conducted in such a way as toensure that the national wealth and heritage are harnessed,preserved and applied for the common good and also to prevent theexploitation of one person by another;
(d) that the national economy is planned and promoted in a balancedand integrated manner;
(e) that every person who is able to work does work, and work meansany legitimate activity by which a person earns a living;
(f) that human dignity is preserved and upheld in accordance with thespirit of the Universal Declaration of Human Rights;
(g) that the Government and all its agencies accord equal opportunitiesto all citizens, men and women alike without regard to their colour,tribe, religion or station in life;
(h) that all forms of injustice, intimidation, discrimination, corruption,oppression or favouritism are eradicated;
(i) that the use of national wealth places emphasis on the development of the people and in particular is geared towards the eradication ofpoverty, ignorance and disease;
(j) that economic activities are not conducted in a manner that mayresult in the concentration of wealth or the major means ofproduction in the hands of a few individuals; and
(k) that the country is governed according to the principles ofdemocracy and socialism.

Nafikiri tutakubaliana kuwa mawazo ya kuweka miiko ya uongozi ni sheria (hata katiba inazungumzia sheria za miiko ya uongozi) na si suala lililoandikwa kwenye katiba.

An interesting thing kwenye katiba ni kibano wanachopewa Wabunge versus Rais na makamu wa Rais. Rais na Makamu hawabanwi na hawana kitu kama hiki kifungu cha 70.

Members tosubmitstatement ofpropertyAct No.12of 199570. Art.12-

(1) Every Member of Parliament shall be required to submit to theSpeaker two copies of a formal statement regarding his property and the propertyof his spouse. The statement shall be made on a special form prescribed by a lawenacted by Parliament and shall be submitted from time to time as shall bedirected by such law.
(2) The Speaker shall transmit to the Ethics Commissioner, a copy ofevery formal statement submitted to him in accordance with the provisions of thisArticle.

Tume ya maadili imewekwa katika katiba, na kazi yake ni kuhakiki na kuratibu viongozi, lakini hakuna sheria maalum au vipingamizi vilivyoelezewa kwenye katiba.

Public Leaders'EthicsSecretariatAct No.1of 1980Art.15Act No.15of 1984Art.39Act No.4of 1992Art.35Act No.12of 1995Art.18

132.-
(1) There is hereby established a Public Leaders' Ethics Secretariatwhich shall have power to inquire into the behaviour and conduct of any publicleader for the purpose of ensuring that the provisions of the law concerning theethics of public leaders are duly complied with.
(2) For the purposes of this Article, the meaning of "public leader" and"code of ethics for public leaders" shall be construed in accordance with theprovisions of the law concerning the ethics of public leaders or the provisions ofany other law enacted by Parliament in so far as such provisions relate to thequestion of leadership and its interpretation. (3) The Public Leader's Ethics Secretariat shall consist of the EthicsCommissioner and such other employees whose number shall be as specified by alaw enacted by Parliament.
(4) Parliament shall enact a law stipulating basic rules of ethics for publicleaders which shall be complied with by all persons holding public office whichshall be specified by such law.
(5) Basic rules of ethics for public leaders shall -
(a) spell out public offices the holders of which shall be subjectthereto;
(b) require persons holding certain public offices to make a formaldeclaration from time to time concerning their income, assets andliabilities;
(c) prohibit conduct and behaviour which tend to portray that a leaderis dishonest, practices favouritism or lacks integrity, or which tendsto promote or encourage corrupt practices in public affairs orjeopardizes public interest or welfare;
(d) prescribe penalties which may be imposed for breaches of the codeof ethics;
(e) provide for procedure, powers and practice to be applied in order toensure compliance with the code of ethics; and(f) prescribe any other provisions as are appropriate or necessary forthe purpose of promoting and maintaining honesty, transparency,impartiality and integrity in the conduct of public affairs and forthe protection of public funds and any other public property.
(6) Parliament may, by law, provide for the dismissal or removal of aperson from office for breaches of the code of ethics regardless of whether theoffice is elective or appointive.

Kumalizia, tuna sheria na miiko ambayo imeundiwa sheria na hata kuhalalishwa na katiba, lakini kinachogomba ni specifics kuzuia watu kuwa na biashara.

Ubaya ni kuwa hakuna mwenye kumkagua Tume ya maadili!

Na nafikiri hata nyaraka na rekodi ni siri na si public information. Aidha tume haina meno makali kutokana na kuwepo kwa sheria na miiko tata, kushindwa kwa tume kufungua mashitaka (hata ya jinai) dhidi ya waliokiuka miiko na kufanya ukaguzi wa kina wa kikosi cha uchunguzi (mamlaka kama ya polisi, Takukuru, DPP).

Siyasemi haya kusema basi kwa kuwa hayako kwenye katiba basi tusiyazungumze, bali katiba inapounda Tume ya maadili, ni lazima miiko ile ya Azimio la Arusha dhidi ya viongozi kujipatia mali zaidi ya mishahara au kujihusisha na biashara iandikwe kuzuia Conflict of Interest.
 
Rev. Kishoka,

..jana Dr.Slaa kasema richmond alianza wakati wa Mkapa.

..wakati wa Mkapa richmond waliingia kwa gia ya kujenga bomba la mafuta dar-to-mwanza.

..walisaini MOU na serikali, wakatokomea kwenda kutafuta pesa za mradi, na mpango huo ukajifia wenyewe.

..nakumbuka kusoma toka kwako, au kwa mchangiaji mwingine, kuhusu wazawa kunyang'anywa mradi huo na kupewa hawa jamaa wa richmond.

..baada ya jamaa kushindwa kupata fedha za kujenga bomba la mafuta, kukatokea crisis ya uhaba wa umeme. sasa hapo ndipo wajanja wakaja na hii RICHMOND tunayoiongelea sasa hivi.

..nilitaka tu niweke kumbukumbu sawa, na kukumbusha the old good days za JF.

cc Alinda, Mkandara, Nguruvi3, Mwalimu

Nafikiri watu hawa wa Richmond walikuwa pamoja na NatOil ambayo kama nakumbuka vizuri, ilikuwa ya yule Brigadia wa Oman ambaye alihusishwa na Dowans.

Pandora linafunguka zaidi kuhoji walipoingia mkataba wa kumnyang'anya Elisante Muro ilikuwa mwaka gani na walikuwa wamesajiliwa wapi hapa Tanzania au hata Marekani au Oman?

Walipataje tenda mara ya kwanza? Nani aliidhinisha hiyo tenda? nani walikuwa watendaji wa bodi ya uzabuni na hata kutoa maamuzi? Wizara ya fedha, Wizara ya viwanda na biashara, Wizara ya madini, Mwanasheria Mkuu au Ikulu au ni vyombo hivi vyote?
 
Bob Mkandara,

Kwa mujibu wa Katiba (hata ya 1977) , hakuna mahali popote iliposema ni mwiko kwa kiongozi kujihusisha na biashara!

Kilichoko kwenye katiba ambacho ni very vague bila limitations ni wajibu kwa kila mwananchi. Kabla sijaanza chambua vipengele hivi, lazima nirudishe hoja kwenye Azimio la Arusha na kwa nini vipengele pingamizi vya Viongozi kujihusisha na biashara hasa viongozi wa Serikali, Mashirika ya Umma na Chama yalibainishwa wazi ndani ya Azimio na hata kuundwa kwa leadership code ambayo ndio ilikuwa Sheria kuu kubana watu kwa uwajibikaji wa kuzuia Viongozi kujihusisha na biashara wakiwa kazini na hata kubainisha Conflict of Interests.

Azimio la Zanzibar, lilivunja na kutengua maana nzima ya Leadership Code. Azimio lilipotamka wazi kuwa Wanasiasa waliochaguliwa na wananchi, watendaji wa Serikali na Mashirika wanaweza jihusisha na biashara, ililazimisha leadership code kufutwa kutokana na conflict ya wazi ya Ruksa yya kufanya biashara versus vipingamizi vya leadership code- miiko ya uongozi.

Hata hivyo, pamoja na miiko ya uongozi iliyokuwepo kwa miaka mingi tangu Azimio la Arusha, wafanyakazi wa Serikali, Mashirika na Taasisi za umma, Wanasiasa na hata mawaziri, waliruhusiwa kujiongezea kipato kupitia shughuli za uzalishaji kama kilimo, mifugo na uvuvi. Ndio maana Oysterbay na Masaki harufu ya mavi ya ng'ombe na kuku ilikuwa jambo la kawaida.

Hii ilitokana na mishahara na marupurupu kutotosheleza (lakini hapa kuna kasoro; watu walikaa nyumba za serikali na mashirika, walipata huduma za afya hata usafiri kwenda kazini bure) na njia moja kupunguza vishawishi vya watu kujiingiza katika usanii ilikuwa ni kutoa subsidies (nilizoonyesha kwenye mabano) na kuruhusu shughuli hizi ambazo zilikuwa part and parcel ya Siasa ya Ujamaa na kujitegema na haswa suala la Kilimo kuwa uti wa mgongo.

Katiba ya 1977 na hata marekebisho ya 1984 inaashiria vitu vifuatavyo kama msingi wa kuhakikisha haki na kupata kipato halali kutokana na jasho. Aidha kinazungumzia wajibu wa Wananchi kulinda mali ya umma dhidi ya ubadhirifu na upotevu (hapa mkazo wa sehemu hii ya katiba ulikuja kutokana na lile zoezi la kupiga vita ulanguzi na magendo la 1984).

Kwa makusudi kabisa nitaanza na kipengele cha 27 cha katiba:



Huu ndio msingi na ngao ya kuundwa sheria za kuzuia uhalifu wa zizi wa mali, rushwa, magendo, ubadhirifu na uhujumu.

Tukirudi kifungu cha 25 cha katiba hiyohiyo kuhusiana na kazi, Katiba inasema hivi:



Halafu ukirudi kifungu cha 24, kinazungumzia kuwa na mali:



Ukirudi kwenye kifungu cha 22 na 23, kinazungumzia tena mambo ya kazi ambayo yamezungumziwa kifungu cha 25:



Sasa hata kifungu cha 9 cha katiba hiyo (pungufu ni vipengele vilivyobadilishwa 1984 na 1992) haionyeshi mahali kuwa Viongozi na Watendaji wanapigwa kabali kuwa na biashara.



Nafikiri tutakubaliana kuwa mawazo ya kuweka miiko ya uongozi ni sheria (hata katiba inazungumzia sheria za miiko ya uongozi) na si suala lililoandikwa kwenye katiba.

An interesting thing kwenye katiba ni kibano wanachopewa Wabunge versus Rais na makamu wa Rais. Rais na Makamu hawabanwi na hawana kitu kama hiki kifungu cha 70.



Tume ya maadili imewekwa katika katiba, na kazi yake ni kuhakiki na kuratibu viongozi, lakini hakuna sheria maalum au vipingamizi vilivyoelezewa kwenye katiba.



Kumalizia, tuna sheria na miiko ambayo imeundiwa sheria na hata kuhalalishwa na katiba, lakini kinachogomba ni specifics kuzuia watu kuwa na biashara.

Ubaya ni kuwa hakuna mwenye kumkagua Tume ya maadili!

Na nafikiri hata nyaraka na rekodi ni siri na si public information. Aidha tume haina meno makali kutokana na kuwepo kwa sheria na miiko tata, kushindwa kwa tume kufungua mashitaka (hata ya jinai) dhidi ya waliokiuka miiko na kufanya ukaguzi wa kina wa kikosi cha uchunguzi (mamlaka kama ya polisi, Takukuru, DPP).

Siyasemi haya kusema basi kwa kuwa hayako kwenye katiba basi tusiyazungumze, bali katiba inapounda Tume ya maadili, ni lazima miiko ile ya Azimio la Arusha dhidi ya viongozi kujipatia mali zaidi ya mishahara au kujihusisha na biashara iandikwe kuzuia Conflict of Interest.


Rev. Kishoka;

Tumeshajadili sana kuhusu Azimio la Arusha. Ukweli wa mambo Azimio la Arusha ilikuwa si sheria ya nchi. Lakini wakati wa mfumo wa utawala wa chama kimoja, hili uwe kiongozi au hata kupata kazi serikalini, ulitarajiwa kuwa mwanachama wa TANU/CCM. Kwa mtaji huu vipengele vya Azimio la Arusha vililazimishwa kuwa sheria wakati si sheria.

Kwa ujumla waandishi wa Azimio la Arusha hawakutegemea mfumo wa soko uria au vyama vingi kurudi Tanzania. Mabadiliko ya kisiasa ya mwanzoni mwa 90 yalibadilisha yote. Kwa mfano vyeo vya makamisaa jeshini vikafutwa. Azimio la Arusha likabaki kuwa document ya CCM na sio mwongozo wa nchi.

Kuna kipindi Katibu wa CCM wa chama wa wilaya na mkoa walikuwa ni wakuu wa wilaya na mikoa. JK alikuwa ni kada wa chama. Hivyo miaka ya mfumo wa chama kimoja, wanasiasa wengi walikuwa na kazi zao na walitegemea kazi zao. Lakini baada ya mabadiliko, nchi iliwataka wanasiasa kuwa professional politicians.


My point ni kuwa nchi haikufanya transtition nzuri kutoka katika kwenye mfumo wa chama kimoja kwenda kwa vyama vingi. Kwa mfano CDM kilianzishwa kama chama cha mkondo wa kulia. Huwezi kuwaambia wao wafuate Azimio la Arusha. Kinadharia vyama vya mkondo wa kulia havizuii wafanya biashara kuchukua nafasi za uongozi.

Kwa mtaji huu Azimio la Arusha halina nguvu. Halina nguvu sio kwa sababu halina maana. Lina maana zake. Lakini halina nguvu kwa sababu halikutangazwa kuwa mwongozo wa nchi ya vyama vingi.

Tukirudi kwenye ufisadi unaofanywa ndani ya nchi, ufisadi unafanyika kwa kuvunja sheria za nchi. Unapofungua kampuni hewa hili uibie serikali, unavunja sheria ya nchi. Unapotoa rushwa hili upate nafasi kupitia CDM/CCM, unavunja sheria ya nchi. Swali ambalo watanzania wanatakiwa kujiuliza ni kwanini wanaachia watu kuvunja sheria?
 
Rev. Kishoka;

Tumeshajadili sana kuhusu Azimio la Arusha. Ukweli wa mambo Azimio la Arusha ilikuwa si sheria ya nchi. Lakini wakati wa mfumo wa utawala wa chama kimoja, hili uwe kiongozi au hata kupata kazi serikalini, ulitarajiwa kuwa mwanachama wa TANU/CCM. Kwa mtaji huu vipengele vya Azimio la Arusha vililazimishwa kuwa sheria wakati si sheria.

Kwa ujumla waandishi wa Azimio la Arusha hawakutegemea mfumo wa soko uria au vyama vingi kurudi Tanzania. Mabadiliko ya kisiasa ya mwanzoni mwa 90 yalibadilisha yote. Kwa mfano vyeo vya makamisaa jeshini vikafutwa. Azimio la Arusha likabaki kuwa document ya CCM na sio mwongozo wa nchi.

Ndugu yangu Zakumi,

Kwenye bandiko langu la 161 na 162 hapo juu, nimeelezea kuwa Azimio la Arusha lilikuwa la TANU/CCM na kama Chadema watalitaka, yawezekana wakalienzi au kuweka miiko yao.

NItaitafuta hiyo leadership code ya miaka hiyo na hii ya miaka hii tuoanishe.
 
Back
Top Bottom