CHADEMA siwaelewi. Bado siku 2 mwezi uishe lakini Kamati Kuu haijakutana. Why?

CHADEMA siwaelewi. Bado siku 2 mwezi uishe lakini Kamati Kuu haijakutana. Why?

Sipendi uwongo ktk maisha yangu. CHADEMA msinichokonoe. Toeni taarifa kuelezea sababu kwann imeshindikana KK kukutana ama kama mliudanganya umma ombeni radhi.

Moja ya sababu kubwa kwann namchukia sana JPM, ukiachilia mbali roho mbaya na ukatili aliokuwa nao ni UWONGO. Yule jamaa alikuwa anawaongopea Sana watanzania. Uwongo kwangu ni sumu. KATU sitamsamehe JPM. Nimemnanga mwaka mzima na nitaendelea

Sasa chadema niwatahadharishe, tukiufunga mwaka bila tamko lenu juu ya uwongo huu, tarehe moja January naanza kushughulika na ninyi.

Sitakagi ujinga mimi.
Kila mjumbe wa kamati kuu amepewa "mkono wa krismas" watu waache kujali familia zao wahangaike na majitu hayafanyi kazi, yanacheza pool table, yakisubiri maendeleo
 
Hii itabakia kuwa ngonjera inayoimbwa na kila chama na kila mgombea. Lkn suala la ukosefu wa ajira na matataizo ya kiuchumi ni endelevu hakuna wa kulimaliza Ila yupo wa kulipunguza.

Kwahiyo tusidanganyane. Sipendi uwongo.
Zitatangazwa ajira mpya za CHAWA kuelekea 2025
 
Naweza Nika tofautiana na Mbowe Kwa mambo mengi lakini Sina chuki nae , maana tofauti ni za kisiasa tu.

Suala LA Mbowe na chadema kumteua Lowasa mwaka 2015 ilikuwa ni strategy nzuri, data zote CCM zilionyesha Lowasa kukubalika zaidi kupita walinzani wote, hata watalaam (consultant) team ambayo iliundwa na chadema kukusanya maoni ya wagombea wa Urais wakati huo Bado Ina onyesha Lowasa alikuwa ana kubalika sana ukilinganisha na Dk Slaa.

Sasa wewe kama mwenye kiti wa chama dhamira Yako ni kushika dola , na ili ushike dola lazima uangalie mtu sahihi anae kubalika ndo uamuzi uliofanywa na Mbowe na chadema, uamuzi ule binafsi ulikuwa sahihi, sasa outcome yake iwe nzuri au mbaya ni hali ambayo tuna takiwa tukubali.

Kitu ambacho pengine walikosea kidogo ni kuruhusu Dk Slaa na Lipumba kuondoka, wange waandaa kwanza hawa watu kabla ya ujio wa Lowasa ili wabaki na waunganishe nguvu.

Kuhusu Lowasa kuachia wengine katika nafasi ya uenyekiti nadhani Hilo ni sahihi, pia ni njia mojawapo ya uwajibikaji na ni democracy pia , yeye anaweza kubaki kuwa mshauri wa chama.
 
Kwa taarifa yako hata CCM sio chama makini, kipo madarakani hadi hii leo sio kwasababu ya umakini wake, bali ni kwa sababu za kihistoria, katiba ya mfumo wa chama kimoja, tume isiyo huru ya uchaguzi, na uoga wa wananchi. Hiyo migogoro michache unayoiona ndani ya vyama vya upinzani, hata CCM ipo, ila kwakuwa CCM inafaidika na uwepo wake madarakani ndio maana unataka kudhani CCM ni chama makini. Siku CCM ikitoka madarakani pamoja na ukubwa wake, itakufa kirahisi mno kama ilivyokufa KANU ya Kenya. Unapoona chama kimekaa madarakani zaidi ya miaka 50, lakini inategemea tu nguvu ya dola kukaa madarakani, basi ujue hicho sio chama.
mimi nimezungumzia vyama vya upinzani wala sikuvilinganisha na ccm.

ninacho kisema bado sijakiona chama cha upinzani makini na madhubuti ambacho kinaweza kuitikisa ccm achilia mbali kuking'oa.
 
mimi nimezungumzia vyama vya upinzani wala sikuvilinganisha na ccm.

ninacho kisema bado sijakiona chama cha upinzani makini na madhubuti ambacho kinaweza kuitikisa ccm achilia mbali kuking'oa.

CCM sio chama cha siasa bali ni kikundi cha dola kilichojivika koti la chama cha siasa. Labda useme vyama vingine havijapata silaha ya kupambana na hiyo CCM. Lakini kwa njia ya kura, CCM ni takataka kama takataka nyingine.
 
CCM sio chama cha siasa bali ni kikundi cha dola kilichojivika koti la chama cha siasa. Labda useme vyama vingine havijapata silaha ya kupambana na hiyo CCM. Lakini kwa njia ya kura, CCM ni takataka kama takataka nyingine.
hilo halina ubishi hata kidogo, kwasababu chama tawala sikuzote ndio chama kilicho shika dola wala sio ajabu.

Malengo ya chama chochote kile ni kushika na kumiki dola.
sasa nenda kaangalie tafasiri ya neno "dola" kwenye kamusi ya kiswahi Tuki.

kushika dola sio kupigana kwa mtutu bali ni mbinu na ushawishi wa either kuingia kwenye dola na kulinda uendelee kushika dola.
 
hilo halina ubishi hata kidogo, kwasababu chama tawala sikuzote ndio chama kilicho shika dola wala sio ajabu.

Malengo ya chama chochote kile ni kushika na kumiki dola.
sasa nenda kaangalie tafasiri ya neno "dola" kwenye kamusi ya kiswahi Tuki.

kushika dola sio kupigana kwa mtutu bali ni mbinu na ushawishi wa either kuingia kwenye dola na kulinda uendelee kushika dola.

Upuuzi huo wanao CCM tu, vyama vya kisiasa hukaa madarakani kwa ushawishi wa kisiasa na sera tu. Hiyo kukaa madarakani kwa kutumia dola wanafanya CCM baada ya kupoteza ushawishi kwa umma. Kama kukaa madarakani ni kwa kutumia dola, kwanini wasikae viongozi wa kijeshi kwenye madaraka.
 
Back
Top Bottom