Chadema,Tumesikia sana na kuona kuhusu Magufuli. Mna nini Jipya?

Chizi Maarifa

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2013
Posts
10,931
Reaction score
24,816
Bado naona Sera ya sasa ya Chadema ni suala la Awamu ya 5. Ndo imekuwa issue kubwa. Unawasoma hata wengine wanamuda sana chadema but wakizungumzia ujio wa Lissu na kuanza na mikutano wanarudi kumzungumzia marehemu Magufuli.

Je hakuna jambo jipya?hoja mpya?sera zao zikoje ukilinganisha na yaliyopo sasa nchini?

Je tutaendelea kusikia matusi dhidi ya Magufuli mpaka lini? Nlitamani watu wachambue uchumi,katiba,siasa n.k but bado wanaendelea kumchamba marehemu.
 
Hayo maandalizi tu lazima shamba lisafishwe kabla ya kulima na then kupandwa hiyo mikutano itakuwepo kwa muda mrefu sana hayo unayose ma yatapata airtime ya kutosha tu
 
Neno "maridhiano" ni gumu sana kueleweka kwa baadhi ya watu.
 
Mwisho wao wa kufikiri ndio huo!

Wale wajenga sera wote walikwisha timka toka huko uchagani!

Sasa waliobaki ni tumbolistic watupu!
 
Wanachambua kwa sababu ya ushetani wake! Hata shetani halisi anachambuliwa tangu Mungu amtupe duniani na ataendelea kuchambuliwa hadi kiama!
 
Wamepata wasaa wa kusema ukwel wa yaliyomoyon mwao acha waseme!! Pia hiyo sio agenda yao nadhan ukihitaj agenda yao nenda kwa wahusika utapewa. Lkn kuhusu maumiv waliyopitisha nasapoti ni haki yao kusema!!! Vaa uhusika wa Lisu then feel that pain, vaa uhusika wa mbowe then feel that pain kweny mali zako, vaa uhusika wa jamaa zao ambao walipotezwa kweny huu ulimwengu then feel that pain!!! Ni rahis san kuongea kama hujawah feel pain like those painful!!!
 

Hata kwenye nyumba za ibada shetani anasemwa kila siku. Kwenye mikutano ya CDM kunaongelewa mambo mengi, ila nyie sukuma gang mnasikiliza neno Magufuli tu, likitajwa mnarushiana kwenye group lenu.
 
Na bado, atasimangwa mpaka age ageukie upande wa pili
 
Hata kwenye nyumba za ibada shetani anasemwa kila siku. Kwenye mikutano ya CDM kunaongelewa mambo mengi, ila nyie sukuma gang mnasikiliza neno Magufuli tu, likitajwa mnarushiana kwenye group lenu.
Karibu mama tulambe asali...😁
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…