CHADEMA/UKAWA: Uwekezaji usiotabirika

CHADEMA/UKAWA: Uwekezaji usiotabirika

Mag3; Kujibu swali lako: Lowassa si adui wa CCM. Matamanio ya kile anachokitaka (Urais), ndio chanzo cha mgogoro wa Lowassa na wenzake. Kwa vitu vingine vilivyobaki, CCM na Lowassa ni damu damu.
Nafikiri hapa ndipo tunapotofautiana, mimi nasema Lowassa kwa sasa ni adui nambari one wa CCM. Ni kweli aliutaka Uraisi kupitia CCM lakini nani kweli anajua kwa uhakika malengo yake? Je yawezekana kwamba moyoni ni kweli alitaka kuleta mabadiliko from within? Kikwete anapewa benefit of doubt, Magufuli anapewa benefit of doubt, kwa nini Lowassa hapewi benefit of doubt kwa tuhuma zozote zile?
Nafasi aliyoleta Lowassa kwenye upinzani ni kubwa. Lakini inategemea jinsi gani wananchi wataitumia nafasi hiyo. Wakimwachia Lowassa, hakutakuwa na mabadiliko yoyote. Atafanya kama yale aliyofanya akiwa CCM.
Hapana, I disagree, Lowassa hakuwahi kuwa Mkuu wa nchi na hakuwahi kuwa kiongozi mkuu wa chama chake, sasa aliwezaje kufanya anayodaiwa kuyafanya bila idhini ya wakubwa wake? Hizo nguvu alizitoa wapi? Pamoja na hayo tayari kasema anazikubali sera na ilani ya Chadema lakini kama ilivyo kwa malowassa-phobia hawako tayari kumpa hata hiyo benefit of doubt, kwa nini?
Wachangiaji maarufu katika ukumbi huu walituambia kuwa Lowassa ali-sponsor ACT, kuisambaratisha CDM. Lowassa ali-sponsor watu mbalimbali wachaguliwe kuwa wajumbe wa NEC. Na hawa watu ndio waliokuwa wamchague Lowassa kupitia CCM. Leo baadhi ya hawa wachangia wanamkumbatia Lowassa as a game changer.
Zakumi si kila kinachosemwa humu ni ukweli uliothibitika, zingine ni hisia tu kulingana na utashi wa mchangiaji. Mimi ni katika waliokuwa mstari wa mbele kumkataa Lowassa lakini wakati huo alikuwa bado yuko kundini huko CCM. Sasa ukweli usioweza kupingika ni kwamba katoka, na ushahidi kwamba hawako tena pamoja ni, kwa mfano, uwanja anaopewa Dr Slaa na status quo kumkandia Lowassa. Miaka yote Dr. Slaa hakuwahi kupewa nafasi kama hiyo TBC hata alipokuwa anagombea Uraisi mwaka 2010, kwa nini sasa?
 
Last edited by a moderator:
My two cents;

Wachangiaji wote humu kwenye jukwaa, hakuna hata moja anayeongelea kiini cha matatizo yaliyotufikisha hapa tulipo nacho ni haki. Imefikia mahali wengi mnaona tendo la kukosa haki ama kunyimwa haki ni la kawaida tu kama sehemu ya maisha. Mnachosahau ni kwamba bila haki hakuna amani, haki hujenga ustaarabu na hivyo kuwezesha maisha kuendeshwa kiutaratibu kwa kufuata sheria.

Ukosefu wa haki hustawisha uonevu kwa mnyonge na kumjengea kiburi mwenye nguvu, kiburi ambacho bila kudhibitiwa hufungua milango ya uhalifu wa aina zote. Binadamu kwa hulka yake hakubali uonevu na ingawa anaweza akavumilia uonevu kwa muda, iko siku uvumilivu wake utafikia mwisho. Hakuna kiumbe hatari kama binadamu anapofikia hali hiyo ya kukata tamaa ya maisha.

Watu mnaongea kama vile uwanja wa ushindani kisiasa upo sawa, mnaongea kama vile uchaguzi ujao, kama zilizopita, utaendeshwa kwa uhuru na haki na mnaongea kama vile vyama vyote vitakayoshiriki vina haki sawa na chama tawala. Manongea kama vile hamuishi Tanzania, mnaishi nchi nyingine tofauti...nchi iliyostaarabika na inayoheshimu misingi ya utawala unaofuata sheria.

Siku Dr. Slaa alipoongea, aliondoa mashaka yote yaliyokuwa moyoni mwangu kuhusu kuteuliwa kwa Lowassa kugombea Uraisi na UKAWA kupitia chama cha Chadema. Mwanzoni, pamoja na kutaka CCM iondoke, nilipokea uteuzi huo shingo upande kidogo nikisubiri msimamo wa Dr. Slaa...naam, nilimsikiliza kwa makini sana na baada ya kumsikiliza sikuwa na wasi wasi tena, UKAWA walikuwa sahihi.

Kauli zinazoendelea kutolewa na viongozi na wafuasi wa CCM si kauli za kiungwana, ni kauli za walevi wa madaraka,kauli za waliojawa kiburi na kauli zisizo na chembe cha ustaarabu...naam ndiko walikotufikisha CCM na kama Lowassa atatusaidia kuondokana na kadhia na manyanyaso haya ya miaka 50 naunga mkono. Dr. Slaa nitaendelea kumheshimu lakini kwangu hapa kapotoka.

Sitaki kuingia ndani sana kwenye swala la Dr. Slaa kwani ni moja katika watu niliokuwa na imani kubwa nao lakini kwa kitendo chake ameonesha ama hakuwa tayari kwa mabadiliko au alijiaminisha bila yeye mabadiliko hayawezekani. Ninachoomba ni wananchi wapewe haki na wawe huru kumchagua watakaye. Serikali isitoe upendeleo kwa CCM bali itoe fursa sawa kwa vyama vyote vinavyoshiriki.

Ndugu zangu, gari (Tanzania) limekwama, limegota kwenye tope...Magufuli anataka kulinasua kwa kulisukuma bila kutoka ndani ya gari, Lowassa kavua buti katoka kwenye gari alisukume. Nawaacha na usemi huu, adverse circumstances need desperate measures...kama hakuna upepo wa kusukuma boti, dawa si kusubiri upepo bali ni kupiga makasia. UKAWA wanapiga makasia.

Mag3,

Unayosema kuhusu haki ni kweli kabisa. Amani ina ingredients zake, na ya muhimu zaidi ni haki. Mchango wako umeenda kidogo nje ya msururu wa michango ya hivi karibuni kwenye huu mjadala. Na napenda niseme uliyoyasema ni mambo ambayo wataka mabadiliko walitakiwa wayashikie bango mwanzoni kabisa. Ila uchaguzi unapokuja unakuja na yake mapya kabisa.

Wakati wa mchakato wa katiba (ambako baadae ilikuja kuzaliwa UKAWA), kuna watu walitahadharisha kuhusu haki. Kwamba kwa jinsi mchakato unavyoenda tangu mwanzo ilikuwa hakuna nafasi ya haki kupatikana na ilikuwa ni bora kwa wale wadai haki wa ukweli wasiruhusu kuwa distracted na quick gains ya kukimbilia katiba mpya. CCM iliiba wazo la katiba mpya na ikalifanya kuwa ni la kwao na wakalifanya wanavyopenda wao kwa masilahi yao wenyewe. The fact that UKAWA ya leo, ilikubali kushiriki mchakato ule tangu mwanzo wakijua kabisa mapungufu yake na kukosekana kwake kwa misingi ya haki ndio kulikotufikisha hapa leo. Sasa kwa sababu tu walishiriki mwanzo, hakuwafanyi leo hii kukosa haki ya kuukosoa mchakato wa katiba kwa sababu tu na wao walikuwepo. Kama unakubaliana na hili, naomba linganisha na hili la Dr. Slaa kwa jinsi utakavyoona vinaingiliana na muktadha wa Slaa kumkaribisha Lowasa (Japo sio muhimu sana).

Katika hiyo aya ya juu nnachojaribu kukisema ni kuwa, kuna uhusiano mkubwa sana kati ya kuwa na wazo zuri na kutumia njia SAHIHI kulifikia hilo wazo zuri. Usipotumia njia SAHIHI basi utapoteza gharama zako za mali, wakati na afya yako kwa sababu hutakaa ufike katika wazo zuri ulilokusudia. Mwisho wa siku, ili kufika katika malengo ya lile wazo lako zuri itakubidi ni lazima urudie mchakato mzima wa utekelezaji wako kwa kutumia njia SAHIHI. Mimi ni mfuasi mkubwa wa msemo, "Measure twice and cut once". One should always measure carefully (double check, tripple check) and make the decision to cut only once. Nikileta nadharia hii katika suala zima la madaliko hapa nchi ndio na kutana na mabadiliko yanahubiriwa kwenye uchaguzi huu.

Tatizo kubwa ninaloliona katika madadiliko haya yanayo huburia ni kuwa yako vague. Hayako specific tunabadilisha nini ili kuleta nini. Na hapa sizungumziii utitiriri wa ahadi kama anazotoa Magufuli kwa sababu surprisingly nae anahubiri mabadiliko, na pia sizungumzii kelele za mfumo mfumo bila kusema ni nini huo mfumo na mfumo unaokuja baaada ya huu mfumo mbovu ni upi. Hapa nazungumzia an actual road plan ya kuyafikia hayo madiliko ambayo haiishi tu kwa kusema CCM itoke madarakani. Baada ya hapo, tutajua mbele ya safari. Labda kuna watu kwa uelewa wao (mdogo au mkubwa) wanaweza kuafford kusema "tutajua mbele ya safari" ila mimi siko katika mtazamo huu. Na kinachonifanya niamini hivi ni kuwa, mabadiliko ya kweli hayaangalia leo tu, mabadiliko ya kweli yalenga kuweka msingi leo ili vizazi na vizazi vije kufaidi matunda yatokanayo na mabadiliko hayo.

CDM hapo mwanzo walikuwa na a glimpse ya hayo mabadiliko ninayozungumzia hapa. Nasema glimpse kwa sababu hoja yao kuu ilikuwa imejikita kwenye jambo moja tu, UFISADI. Toa UFISADI, weka serikali ambayo haina watu MAFISADI then huo ndio utakuwa msingi wa Tanzania bora. Sasa anapokuja Lowasa hili suala linabadilika kabisa. Ni kweli hajawahi kuwa convicted, lakini kufumbia macho yote anayokuja nayo ni kuamua tu kuvuka barabara huku umefumba macho. Makala baaada ya makala zimeandikwa juu Lowasa. The fact kuwa hajawahi kuwa convicted ni moja ya sababu kwa nini CCM inatakiwa kuondoka madarakani. Sasa huyu akiwa leo ndio kiongozi wa mabadiliko halafu tukategemea matunda ya mabadiliko yale yale tuliyo yatamani ni kujidanganya wenyewe. Na kinachonifanya niyaangalie zaidi mabadiliko haya ya Lowasa kwa jicho la tatu, ni over expectations kwa kundi la vijana ambao kwa maoni yangu wanafata tu who is the most popular candidate at that time ndio maana tunawaona na boda boda zao ( boda boda ni mfano tu) kwenye kampeni za wagombea wote wote. Tunategemea taifa la aina gani hii expectation isipofikiwa. Niliwahi kuandika humu JF sio kwenye jukwaa hili, "The future of the entire nation, can not be reduced into one big social experiment of seeing if we can get CCM out". Haya ni matusi kwa hili taifa zima. Nimesema hapo juu kuhusu kutumia njia SAHIHI, hii ya LOWASA sidhani kama ni njia SAHIHI. Tukipata matokeo kama tuliyoyapata kwenye mchakato wa katiba, sie tunaojinadi kutaka mabadiliko tusirudi kushangaa na kugeuka kwenye kutoa lawama kama tulivyofanya kwenye mchakato wa katiba.

Wengi tumeshangilia CCM kugawanyika. Je ilimeguka kwa misingi ya tofauti za kiitikadi na maono au kwa misingi ya kutaka ukuu? Tumebaki na CCM yenye mafisidi inayomnadi Magufuli, na CDM inayoongozwa na sura za CCM mafisadi wengine ikimnadi Lowasa. Wote wanatumia mapesa na mapesa wanayoyapata toka kwa matajiri ili wawalinde kwenye uongozi wao, na wanatafuta kura kwa masikini ambao wanawaahidi watawabana matajiri hao hao ili walete mabadiliko! Khaa. Mambo ya ajabu sana.

Mimi naomba unishawishi tu nimchague mgombea unayemtaka kwa sababu zingine na sio unitajie msusururu wa ahadi ambazo husemi utazitekeleza vp au kunipa matumaini ya mabadiliko ambayo najua kabisa yatanirudishe hapa hapa nilipo.

Ukiona unapata hamu ya kuniuliza kwa hiyo kama wote hawafai sasa conclusion ni nini kama baadhi ya watu walivyo muuliza Dr. Slaa kwenye press yake? Kwanza nikwambie rudi kwenye jibu la Dr. Slaa, pili KWANI WANAOGOMBEA URAISI NI WAWILI TU?
 
GalaxyS3,

..kile kitendo cha kuiondoa tu CCM ni a big step kuelekea kwenye mabadiliko.

..pia sidhani kama wananchi walioweza kuiondoa CCM watashindwa kumuondoa Lowassa ikiwa atawasaliti.

..mabadiliko tunayoyataka yatapatikana baada ya kuweka msingi wa wa-Tanzania kuwa na UJASIRI wa kubadilisha vyama vilivyoko madarakani kwa njia ya kura.

..wengi wamejikita kumuangalia Lowassa peke yake, and that is understandable. Lakini nadhani tunapaswa kuangalia the entire post-ccm political landscape, kuanzia bungeni, baraza la wawakilishi, cdm, cuf, nccr, act-wazalendo, uamsho, na hata ccm wenyewe watakapokuwa nje.

NB:

..binafsi naiogopa sana CCM ya Magufuli, Nape Nnauye, Mwigulu Nchemba, January Makamba, Harrison Mwakyembe, William Lukuvi, na wengine.

..kwa kweli watu hawa mimi wananitisha, na nadhani tusiposhughulika nao mwaka huu, then demokrasia yetu ya vyama vingi itapitia kipindi kigumu sana.
 
Last edited by a moderator:
Mag3,

Unayosema kuhusu haki ni kweli kabisa. Amani ina ingredients zake, na ya muhimu zaidi ni haki. Mchango wako umeenda kidogo nje ya msururu wa michango ya hivi karibuni kwenye huu mjadala. Na napenda niseme uliyoyasema ni mambo ambayo wataka mabadiliko walitakiwa wayashikie bango mwanzoni kabisa. Ila uchaguzi unapokuja unakuja na yake mapya kabisa.

Wakati wa mchakato wa katiba (ambako baadae ilikuja kuzaliwa UKAWA), kuna watu walitahadharisha kuhusu haki. Kwamba kwa jinsi mchakato unavyoenda tangu mwanzo ilikuwa hakuna nafasi ya haki kupatikana na ilikuwa ni bora kwa wale wadai haki wa ukweli wasiruhusu kuwa distracted na quick gains ya kukimbilia katiba mpya. CCM iliiba wazo la katiba mpya na ikalifanya kuwa ni la kwao na wakalifanya wanavyopenda wao kwa masilahi yao wenyewe. The fact that UKAWA ya leo, ilikubali kushiriki mchakato ule tangu mwanzo wakijua kabisa mapungufu yake na kukosekana kwake kwa misingi ya haki ndio kulikotufikisha hapa leo. Sasa kwa sababu tu walishiriki mwanzo, hakuwafanyi leo hii kukosa haki ya kuukosoa mchakato wa katiba kwa sababu tu na wao walikuwepo. Kama unakubaliana na hili, naomba linganisha na hili la Dr. Slaa kwa jinsi utakavyoona vinaingiliana na muktadha wa Slaa kumkaribisha Lowasa (Japo sio muhimu sana).

Katika hiyo aya ya juu nnachojaribu kukisema ni kuwa, kuna uhusiano mkubwa sana kati ya kuwa na wazo zuri na kutumia njia SAHIHI kulifikia hilo wazo zuri. Usipotumia njia SAHIHI basi utapoteza gharama zako za mali, wakati na afya yako kwa sababu hutakaa ufike katika wazo zuri ulilokusudia. Mwisho wa siku, ili kufika katika malengo ya lile wazo lako zuri itakubidi ni lazima urudie mchakato mzima wa utekelezaji wako kwa kutumia njia SAHIHI. Mimi ni mfuasi mkubwa wa msemo, "Measure twice and cut once". One should always measure carefully (double check, tripple check) and make the decision to cut only once. Nikileta nadharia hii katika suala zima la madaliko hapa nchi ndio na kutana na mabadiliko yanahubiriwa kwenye uchaguzi huu.

Tatizo kubwa ninaloliona katika madadiliko haya yanayo huburia ni kuwa yako vague. Hayako specific tunabadilisha nini ili kuleta nini. Na hapa sizungumziii utitiriri wa ahadi kama anazotoa Magufuli kwa sababu surprisingly nae anahubiri mabadiliko, na pia sizungumzii kelele za mfumo mfumo bila kusema ni nini huo mfumo na mfumo unaokuja baaada ya huu mfumo mbovu ni upi. Hapa nazungumzia an actual road plan ya kuyafikia hayo madiliko ambayo haiishi tu kwa kusema CCM itoke madarakani. Baada ya hapo, tutajua mbele ya safari. Labda kuna watu kwa uelewa wao (mdogo au mkubwa) wanaweza kuafford kusema "tutajua mbele ya safari" ila mimi siko katika mtazamo huu. Na kinachonifanya niamini hivi ni kuwa, mabadiliko ya kweli hayaangalia leo tu, mabadiliko ya kweli yalenga kuweka msingi leo ili vizazi na vizazi vije kufaidi matunda yatokanayo na mabadiliko hayo.

CDM hapo mwanzo walikuwa na a glimpse ya hayo mabadiliko ninayozungumzia hapa. Nasema glimpse kwa sababu hoja yao kuu ilikuwa imejikita kwenye jambo moja tu, UFISADI. Toa UFISADI, weka serikali ambayo haina watu MAFISADI then huo ndio utakuwa msingi wa Tanzania bora. Sasa anapokuja Lowasa hili suala linabadilika kabisa. Ni kweli hajawahi kuwa convicted, lakini kufumbia macho yote anayokuja nayo ni kuamua tu kuvuka barabara huku umefumba macho. Makala baaada ya makala zimeandikwa juu Lowasa. The fact kuwa hajawahi kuwa convicted ni moja ya sababu kwa nini CCM inatakiwa kuondoka madarakani. Sasa huyu akiwa leo ndio kiongozi wa mabadiliko halafu tukategemea matunda ya mabadiliko yale yale tuliyo yatamani ni kujidanganya wenyewe. Na kinachonifanya niyaangalie zaidi mabadiliko haya ya Lowasa kwa jicho la tatu, ni over expectations kwa kundi la vijana ambao kwa maoni yangu wanafata tu who is the most popular candidate at that time ndio maana tunawaona na boda boda zao ( boda boda ni mfano tu) kwenye kampeni za wagombea wote wote. Tunategemea taifa la aina gani hii expectation isipofikiwa. Niliwahi kuandika humu JF sio kwenye jukwaa hili, "The future of the entire nation, can not be reduced into one big social experiment of seeing if we can get CCM out". Haya ni matusi kwa hili taifa zima. Nimesema hapo juu kuhusu kutumia njia SAHIHI, hii ya LOWASA sidhani kama ni njia SAHIHI. Tukipata matokeo kama tuliyoyapata kwenye mchakato wa katiba, sie tunaojinadi kutaka mabadiliko tusirudi kushangaa na kugeuka kwenye kutoa lawama kama tulivyofanya kwenye mchakato wa katiba.

Wengi tumeshangilia CCM kugawanyika. Je ilimeguka kwa misingi ya tofauti za kiitikadi na maono au kwa misingi ya kutaka ukuu? Tumebaki na CCM yenye mafisidi inayomnadi Magufuli, na CDM inayoongozwa na sura za CCM mafisadi wengine ikimnadi Lowasa. Wote wanatumia mapesa na mapesa wanayoyapata toka kwa matajiri ili wawalinde kwenye uongozi wao, na wanatafuta kura kwa masikini ambao wanawaahidi watawabana matajiri hao hao ili walete mabadiliko! Khaa. Mambo ya ajabu sana.

Mimi naomba unishawishi tu nimchague mgombea unayemtaka kwa sababu zingine na sio unitajie msusururu wa ahadi ambazo husemi utazitekeleza vp au kunipa matumaini ya mabadiliko ambayo najua kabisa yatanirudishe hapa hapa nilipo.

Ukiona unapata hamu ya kuniuliza kwa hiyo kama wote hawafai sasa conclusion ni nini kama baadhi ya watu walivyo muuliza Dr. Slaa kwenye press yake? Kwanza nikwambie rudi kwenye jibu la Dr. Slaa, pili KWANI WANAOGOMBEA URAISI NI WAWILI TU?

GalaxyS3, kila ulichosema kina mantiki na siwezi kupinga ila kumbuka kitu kimoja nilichokisisitiza kwa nukuu hii; "adverse circumstances need desperate measures." Adui wa mabadiliko tunayepambana naye ndani ya taifa hili si wa kawaida, ni adui aliyejizatiti kwa muda wa miaka zaidi ya hamsini na ni adui ambaye kwa muda wote huo amehakikisha anaziba mianya yote inayoweza kutoa nafasi kwa mabadiliko ya kweli. Wahenga walisema heri nusu shari kuliko shari kamili hivyo pamoja na makosa, kidogo kidogo tunapiga hatua.

Tulipolazimika kuafiki kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi kwa masharti ya maadui wa mfumo huo, swali ni je tulifanya makosa? Jibu ni ndiyo, tulifanya makosa lakini tusisahau kwamba kwa hayo makosa tulibahatika kupata upenyo ambao umetuwezesha kupiga hatua japo kidogo. Tunapolazimika kuingia kwenye chaguzi kwa katiba ile ile inayoipa chama tawala upendeleo maalum tunafanya makosa? Jibu ni ndiyo tunafanya makosa lakini makosa yenyewe yanatupa fursa angalau ya kupenyeza ndani na nje ya bunge sauti pinzani.

Binadamu hujifunza kutokana na makosa na Watanzania tumefanya makosa mengi tu kama taifa na swali ni je tumejifunza lolote kutokana na makosa hayo. Jibu ni kwamba tumejifunza mengi tu na tutaendelea kujifunza kwa kila kosa tunalolifanya. Ni kweli kama usemavyo tulifanya makosa kushiriki katika mchakato wa kuandika katiba mpya lakini kwa kufanya kosa hilo ukweli ni kwamba tumepiga hatua, tumepata UKAWA. Bandu bandu huisha gogo na tayari ishara zipo gogo linachungulia kaburi na pole pole ndio mwendo.

Je kwa UKAWA kumpokea Lowassa, tumefanya makosa? Hili swali nakosa muda wa kulijadili kwa sasa lakini nawaachia wenzangu waendelee kulidodosa, nikipata muda nitarudi.
 
Nguruvi3,

..upande wa kwanza: diwani wa ukawa, wabunge wa ukawa, na waziri mkuu na serikali ya ukawa. Raisi Lowassa.

..upande wa pili ni diwani: ccm, wabunge wa ccm, Raisi, waziri mkuu na serikali ya ccm.

..I am just tired na hiki kiburi cha CCM. I cant take it no more. I am going with the first choice hapo juu.

cc GalaxyS3, Mag3
 
Last edited by a moderator:
Nguruvi3,

..upande wa kwanza: diwani wa ukawa, wabunge wa ukawa, na waziri mkuu na serikali ya ukawa. Raisi Lowassa.

..upande wa pili ni diwani: ccm, wabunge wa ccm, Raisi, waziri mkuu na serikali ya ccm.

..I am just tired na hiki kiburi cha CCM. I cant take it no more. I am going with the first choice hapo juu.

JokaKuu,

Umenifurahisha. Ila kwenye chagua namba moja mbona Lowasa hujamnasibisha na UKAWA. Umemtaja kama mgombea binafsi bana.

Mimi siko kwenye hizo chaguzi zote mbili. Kwa nini sitachajua hilo chaguo la pili, well its CCM halihitaji maelezo zaidi. Kwanini sitachagua hilo chaguo la kwanza kama ulivyoliweka hapo, well, historia ya nchi imenifundisha nisikipe chama kimoja serikali na bunge.

Atakae pata kura yangu ya uraisi, hatapata kura yangu kwenye ubunge. Nakushauri sana ndugu kama kweli unataka serikali ijayo iwe accountable usifanye uamuzi wa kutoa kura zako zote kwenye chama kimoja. Haijalishi nani ataend up madarakani, kwa maslahi ya taifa hili tunahitaji upinzani imara.

Natamani ningekuwa na uwezo kufanya kampeni inayosema "Ewe mtanzania, usiweke mayai yako yote kwenye kikapu kimoja. Acha kucheza ngoma ya wanasiasa".
 
Kumchagua LOWASA na genge lake alafu uite ni mabadiliko kwa hali za wananchi,nikujipumbaza kwa hali ya juu sana
 
JokaKuu,

Umenifurahisha. Ila kwenye chagua namba moja mbona Lowasa hujamnasibisha na UKAWA. Umemtaja kama mgombea binafsi bana.

Mimi siko kwenye hizo chaguzi zote mbili. Kwa nini sitachajua hilo chaguo la pili, well its CCM halihitaji maelezo zaidi. Kwanini sitachagua hilo chaguo la kwanza kama ulivyoliweka hapo, well, historia ya nchi imenifundisha nisikipe chama kimoja serikali na bunge.

Atakae pata kura yangu ya uraisi, hatapata kura yangu kwenye ubunge. Nakushauri sana ndugu kama kweli unataka serikali ijayo iwe accountable usifanye uamuzi wa kutoa kura zako zote kwenye chama kimoja. Haijalishi nani ataend up madarakani, kwa maslahi ya taifa hili tunahitaji upinzani imara.

Natamani ningekuwa na uwezo kufanya kampeni inayosema "Ewe mtanzania, usiweke mayai yako yote kwenye kikapu kimoja. Acha kucheza ngoma ya wanasiasa".

..I took the worst case scenario kwamba Lowassa siyo Ukawa.

..lakini baada ya kutafakari, hata katika mazingira ambayo Lowassa siyo ukawa, bado nimeangukia kwenye kwenye scenario namba 1.

..I like ur strategy ya kutokuweka "mayai yote ktk kikapu kimoja." It is something I have toyed with for some time. lakini ktk kampeni hizi, CCM inaendelea kufanya mambo yanayozidi kunitibua, na ndiyo maana nimeshawishika kuwapumzisha kila mahali.

..Tangu Magufuli aanze kufanya kampeni kwa nia ya kupotosha waziwazi, nimepoteza hata ile heshima ndogo niliyokuwa nayo kwake. Hivi kweli miaka 20 aliyokaa serikalini, na exposure aliyoipata, hafahamu tofauti ya kilichotokea Libya, Iraq, Zaire, na hiki kinachoendelea hapa Tanzania?

NB:

..unaweza kutuletea uzi wa hii theory yako ya kutokuweka mayai yote ktk kikapu kimoja.

..choice ya kwanza itakuwa ni Lowassa Raisi, Waziri Mkuu toka CCM, chama cha kikuu cha upinzani CDM/UKAWA.

..choice ya pili itakuwa ni Raisi Magufuli, Waziri Mkuu toka CDM/UKAWA, chama kikuu cha upinzani CCM.

..choice ya tatu ni Raisi na waziri mkuu kutoka chama kimoja, lakini chama tawala kina very slim majority.

cc Rev. Kishoka, Zakumi, Nguruvi3, NasDaz
 
Kumchagua LOWASA na genge lake alafu uite ni mabadiliko kwa hali za wananchi,nikujipumbaza kwa hali ya juu sana

..fortunately Lowassa ameliacha genge lake CCM.

..hata Dr.Slaa amesema wale wabunge 50 na wenyeviti wa mikoa wa chama 20 waliokuwa wahame na Lowassa kwenda chadema, wamebadilisha mawazo na kubakia CCM.

cc Alinda, King Suleiman
 
Last edited by a moderator:
Sitaki kuingia ndani sana kwenye swala la Dr. Slaa kwani ni moja katika watu niliokuwa na imani kubwa nao lakini kwa kitendo chake ameonesha ama hakuwa tayari kwa mabadiliko au alijiaminisha bila yeye mabadiliko hayawezekani. Ninachoomba ni wananchi wapewe haki na wawe huru kumchagua watakaye. Serikali isitoe upendeleo kwa CCM bali itoe fursa sawa kwa vyama vyote vinavyoshiriki..

Mag3,

Hii ndio hoja kuu ambayo inazungukwa zungukwa tuu na kelele za kuna waliotoa damu, makamasi, maisha na kujiona Miungu watu wa mambo.

Ni sawa na CCM walivyojiaminisha kuwa Tanzania bila CCM, hakuna maendeleo.

Mwalimu alitoa TAHADHARI kuwa bila CCM MADHUBUTI Tanzania itayumba. Aliyasema haya kwa nia njema sana wala si kuiharamisha kasi, kazi na umuhimu wa Demokrasia ya vyama vingi.

Mwalimu alipowapaka mbovu Chadema na hata Mrema aliyafanya kwa kuwa yeye ni mwanachama wa CCM, lakini pia aliyafanya hayo kutokana na ukweli uchanga wa vyama vya upinzani mwaka 1995 na alijua uchanga uliandamana na udhaifu wa organization na wala si ki-itikadi.

CCM imeshindwa kuwa MADHUBUTI miaka 20 tangu mfumo wa vyama vingi uanze. Imacha kuongoza Taifa kwa manufaa ya Taifa, ila inatawala wananchi kwa manufaa ya KIchama na haswa viongozi wake, wapambe na maslahi ya Wawekezaji.

Ni kukwama huko kwenye hilo tope na kung'ang'ania kuijiona yenyewe ndio yenye uwezo wa pekee (si ajabu wa kiroho mtakatifu kutoka sijui mbungu gani) ndio maana CCM inang'ang'ania kusema ni CCM pekee.

Dr. Slaa naye anaingia mkumbo huu sawa na wale walioamini ni Chadema pekee ndio yenye uhalali na haki miliki ya kuleta mabadiliko au kuwa chama pekee cha upinzani chenye mshiko.

Zitto alipigiwa mizengwe kwa kuwa alikuwa na mvuto na mwamko uliojikita katika hoja nyingi zaidi ya vilio vya ufisadi pekee!

Zitto huko aliko ameonyesha ustadi mzuri tuu na maarifa kwa kuyachukua mawazo yetu, tulivyomkosoa yeye kama mtu na kiongozi, na amekwenda kuanzisha chama ambacho kinaanza kujijenga wa kasi kwa itikadi moja inayoeleweka sana kwa wananchi.

Kujisahau huku kwa Dr. Slaa kwa kuwa na hoja moja au kujiaminisha kuwa ni yeye pekee, ndiko kunamtatiza kuona ni jinsi gani wenzake walibadilika "ghafla" na kumkaribisha Lowassa ambaye yeye Slaa mwenyewe alimleta na wakaamua kwa umoja kumpa ngao na mkuki kuongoza vita vya kwenda kwenye uchaguzi.

Ama mvuto wa "ghafla" wa umoja wa vyama kukaa pamoja na kukubaliana pamoja na madhaifu mengine tunayoyaona, ni kitu ambacho hakikutegemewa kabisa si na CCM pekee bali hata na Dr. Slaa na wapambe wake ndio maana kuna maneno mengi ya kujibagua kutoka Ukawa na kutaka kuleta Uchadema pekee.

Kamati kuu ya Chadema was smart enough hata kumkubali Duni kujiunga kuwa mgombea mwenza kwa maana mpaka leo hii, Chadema hakikuwa na Mzanzibari mwenye umahiri na mvuto wa kukipa kura.

Hivyo tide has change na Dr. Slaa hajaelewa kuwa samaki wamebadilisha mkondo wa kuogelea na wamemuacha yeye pekee kisiwani na upweke.

Kumsema Lowassa ni haki yake, kumchambua ni haki yake, lakini ajihoji ni kwa nini sasa kauli na sauti yake inaonekana ni ya kilalamishi, manung'uniko na hasira dhidi ya mtu au matendo yake?

Je leo Lowassa akiungama kwa Watanzania akasema kweli (nasi tusiweke masharti eti huu ukweli tutauthibitishaje, mbona tunakubali kauli za CCM na Magufuli kwa wepesi na uharaka?) kuwa ana mapungufu kama mwanadamu mwingine na kuna maamuzi na matendo aliyoyafanya anayajutia na hii ni fursa yake kutumikia Taifa kwa usahihi na umakini zaidi, je Dr. Slaa ataridhika?

Tofauti na CCM, CCM "wanaungama" kila mwaka na tunawapa nafasi kila miaka mitano na wanarudia yale yale. Je tumempa Lowassa japo nafasi mpya?

Je kwanini tuwanyime Ukawa hiyo nafasi?

Mabadiliko ni inevitable na attitude za Watanzania wanasema haijali hata kama ni jiwe, tumeichoka CCM na ahadi zake na maungamo kila miaka mitano.
 
Dr. Slaa aliharibu toka ile press conference ya Serena, yeye na CCM wanajua hilo.
Wamekaa na kusoma upepo wakaona wazi kuwa kuna sehemu wamekosea kuchanga karata zao.
Ile ya jana Star TV imezidi kumchafulia Dr. Slaa.
Amejikanyaga sana.

Hii kasi ya kujiadhirisha mbele ya kadamnasi inamfuta kabisa kutoka kuwa mtu mahiri na mwenye busara.

Inaelekea baada ya Serena, kafuata interview ya Tido na sasa Star TV kujitetea mno na kuendelea kutoa hoja ambayo ni kutwanga ngumi kwenye maji.

Lakini pia hii ni mbinu ya kuondoa wanahabari kufuatilia kampeni za Ukawa. Propaganda za CCM ni distortation na mis-information.

Dr. Slaa anajitangaza kana kwamba kaonewa haki ya kuwa mgombea wa Chadema/Ukawa (his tone and choice of words says it in plain english despite his continuous refusal kuwa hautaki Uraisi) hivyo anatafuta sympathy ya wananchi ambao wanahamasishwa kuanza maandamano ya kumuaga na yeye eti anaanza kampeni ya kuaga wananchi kutembelea mikoa.

Go figure mtu anayedai kuwa na roho safi kabisa!
 
Hii kasi ya kujiadhirisha mbele ya kadamnasi inamfuta kabisa kutoka kuwa mtu mahiri na mwenye busara.

Inaelekea baada ya Serena, kafuata interview ya Tido na sasa Star TV kujitetea mno na kuendelea kutoa hoja ambayo ni kutwanga ngumi kwenye maji.

Lakini pia hii ni mbinu ya kuondoa wanahabari kufuatilia kampeni za Ukawa. Propaganda za CCM ni distortation na mis-information.

Dr. Slaa anajitangaza kana kwamba kaonewa haki ya kuwa mgombea wa Chadema/Ukawa (his tone and choice of words says it in plain english despite his continuous refusal kuwa hautaki Uraisi) hivyo anatafuta sympathy ya wananchi ambao wanahamasishwa kuanza maandamano ya kumuaga na yeye eti anaanza kampeni ya kuaga wananchi kutembelea mikoa.

Go figure mtu anayedai kuwa na roho safi kabisa!

..WHAT?!

..R U SERIOUS kuwa Dr ataanza ziara za kuaga mikoani?

..unajua itafika wakati watu wataona mabadiliko hayawezi kuleta na vyama au sanduku la kura.

..kwa kweli ccm wasipokuwa makini tutaishia kuwa kama Libya, Misri, au hata Zaire.
 
..WHAT?!

..R U SERIOUS kuwa Dr ataanza ziara za kuaga mikoani?

..unajua itafika wakati watu wataona mabadiliko hayawezi kuleta na vyama au sanduku la kura.

..kwa kweli ccm wasipokuwa makini tutaishia kuwa kama Libya, Misri, au hata Zaire.

Mbatia anasema UKAWA hawatamvumilia Dr. Slaa akiamua kuzunguka mikoani 'kuaga' wananchi na tayari wameshaandika barua NEC kuhoji kuhusu hiyo ziara na NEC wamesema Slaa anatakiwa afuate taratibu zilizopo....

Nikiunganisha dots naanza kuamini kuwa Dr. Slaa anatumika kudhoofisha mbio za Lowassa kwa maslahi ya CCM au Magufuli...Dr. Slaa might be the last card CCM has...kwamba kila mtu ana 'price' imejidhihirisha kwa Slaa...

Nilichofurahi ni kuona Lowassa na Sumaye hawajamjibu, na wamuache tu azunguke mikoani, I'm confident atajiabisha...
 
Hii kasi ya kujiadhirisha mbele ya kadamnasi inamfuta kabisa kutoka kuwa mtu mahiri na mwenye busara.

Inaelekea baada ya Serena, kafuata interview ya Tido na sasa Star TV kujitetea mno na kuendelea kutoa hoja ambayo ni kutwanga ngumi kwenye maji.

Lakini pia hii ni mbinu ya kuondoa wanahabari kufuatilia kampeni za Ukawa. Propaganda za CCM ni distortation na mis-information.

Dr. Slaa anajitangaza kana kwamba kaonewa haki ya kuwa mgombea wa Chadema/Ukawa (his tone and choice of words says it in plain english despite his continuous refusal kuwa hautaki Uraisi) hivyo anatafuta sympathy ya wananchi ambao wanahamasishwa kuanza maandamano ya kumuaga na yeye eti anaanza kampeni ya kuaga wananchi kutembelea mikoa.

Go figure mtu anayedai kuwa na roho safi kabisa!
Mkuu wangu nikwambie tu kwamba Mbowe is too smart than all of them japo Zitto alimshtukia toka zamani. Mbowe mshikaji lakini inapofika katika maslahi ya nchi niseme ukweli tu kuwa Mbowe mwenyewe alihujumiwa na ile status Quo maadam ana Ambitions zake anataka kuwa someone powerful. A Legend kabla Mola hajamchukua nje ya fikra za Kichama na hawezi kuachia nafasi zinapotokea ama kuzuiwa.

Hapa wote wamekutana kama walivyokutana huko CCM kina Salim, Sumaye, Malecela na wengineo wanazidiana tu how far can I go! Mtu akionekana a threat kisiasa kwa umaarufu kumzidi mkubwa wake anatafutiwa fitna na kuzimwa. Hii imo hadi maofisini mkuu, siku ukipata ajira Bongo chunga sana maana wakajua unatoka Ulaya watakushtakia kwa Wachawi (wenyewe wanaita waganga) kwa sababu tu wanafikri umekuja chukua nafasi zao. Utapakwa kwa kila jambo hadi ukimbie mwenyewe. Ni Hulka yetu ya asili umaskini huja na WIVU!

Dr.Slaa amewajibika kwa mapenzi ya chama na imani yake baada ya kutoka Hijja. Mbowe kafanikiwa kuaondoa threats. Kwa hiyo sisi tutamuona hafai kwa sababu siku zote Muongo kwetu ni yule anayesema UKWELI mahala na wakati asotakiwa. Huitwa mchonganishi!
 
Nasisimkwa na uzito wa hoja za wachangaiji, ahsanteni sana

Niaanze kupitia hoja ya King Suleiman

Dr Slaa alipokaa kimya alitoa benefit of doubt kwa waliomwaminimisimamo na hekima interview zime clear doubt

Kuna quote inasema hivi ''Sometime it's better to keep silent than to tell others what you feel because it will only hurt you when you know they can hear you but they can't understand''

Nyingine inasema ‘a meaningful silence is always better thana meaning less words'

Tunajua sasa, ni suala la Urais,yote yanayoendelea ni hasira tu zinazotokana na hilo


Serena; Dr Slaa alisema Urais haikuwa hoja. Juzi karudia, kama mwanadamu mwenye nyama ilimuuma.

Alidai kushiriki katika maongezi ya kumleta Lowassa kupitiaMshenga. Juzi karudia tena.
Dr alituambia ni makosa kuhamishia choo ndani yanyumba


Hapa kuna fikra kidogo. Kwanini aslishiriki katika mipangoya kuhamisha choo ndani?

Akiwa ameshaandaliwa, hoja kubwa ilikuwa kupata nguvu ya kuuungwamkono. Ndio msingi wakusema ‘anakuja na watu wangapi'.

Kwa fikra tu, Dr alikuwa tayari kusafisha ‘ufisadi' onlyand only if, ufisadi ungetoa msaada akiwa mbeba bendera

Anachokifanya ni mwaga mboga na mwaga ugali.
Anapewa takwimu, hakuwa nazo kwa muda wote wa kupigana na ufisadi!!!


Hoja ya Richmond anamlenga EL aliyechukua nafasi yake ingawa aliletwa na Dr kwa ushiriki kwasababu asisoweka wazi.

Hiawezekani apigane na ufisadi wa 2008 akiacha mauza uza kama ya Escrow n.k.
Na hii inadhihirishwa na kauli kuwa Magufuli ‘ana afadhali' katika ufisadi'


Lini mwanamke aliwahikudai kuna kimimba kidogo! (Little pregnancy)

Kwa mfano wa kuwa ‘kuna mzinifu mkubwa kwasababu amempachika binti mimba , na mzinifu mdogo hakusababisha mimba, ilikuwa ni ''one night stand'

Dhambi ni dhambi hakuna dhambi ndogo au kubwa, ni dhambi tu. Kwanini Magufuli awe na ndogo?

Dr Slaa aliacha siasa July 28 saa sita usiku. Kwasasa anafanya shughuli zinazohusiana na siasa!

Ni vema akawa naNGO au akatangaza kushiriki siasa. Hiyo ni haki yake, na ndiyo credibilityyenyewe.

Anchofanya sasa hivi ni siasa
. Neno timing linaeleza yote
 
Hii kasi ya kujiadhirisha mbele ya kadamnasi inamfuta kabisa kutoka kuwa mtu mahiri na mwenye busara.

Inaelekea baada ya Serena, kafuata interview ya Tido na sasa Star TV kujitetea mno na kuendelea kutoa hoja ambayo ni kutwanga ngumi kwenye maji.

Lakini pia hii ni mbinu ya kuondoa wanahabari kufuatilia kampeni za Ukawa. Propaganda za CCM ni distortation na mis-information.

Dr. Slaa anajitangaza kana kwamba kaonewa haki ya kuwa mgombea wa Chadema/Ukawa (his tone and choice of words says it in plain english despite his continuous refusal kuwa hautaki Uraisi) hivyo anatafuta sympathy ya wananchi ambao wanahamasishwa kuanza maandamano ya kumuaga na yeye eti anaanza kampeni ya kuaga wananchi kutembelea mikoa.

Go figure mtu anayedai kuwa na roho safi kabisa!
Mkuu Rev
Kumbu kumbu zinaonyesha mwaka 2010 Dr Slaa huktarajia kupewa nafasi ya kugombea.
Uteuzi ulifanyika na aliombwa tu kufuatana ‘na tafiti' zao


Kupewa nafasi ya kupeperusha bendera 2015 si haki ilikuwa privilege.Malalamiko yake hayazingatii alitokea wapi

Pili, hakika mzee anajiondoa katika kundi la watu mahiri. Kuzungumzia matatizo na chama chake ni haki yake.

Kuzungumzia siasa za nchi ni haki yake kama mwananchi mwingine


Tatizo ni pale anapotumia umaarufu wake kutaka kupotosha umma.

Hapa ndipo anatualika na hakika tunamuomba radhi in advance kwasababu hatutakaa kimya.
Hana immunity, ana heshima na si vema kutumia heshima kuudanganya umma. Tutasimama na umma

Kwanini tunasema hivyo!

Moja, Dr Slaa anaposema kastaafu siasa kuanzia July 28 saa sita usiku, ina maana ni raia kama mwingine.
Hapaswi kutumia siasa aliyostaafu kuzua habari za kupotosha


Kwa mfano, kama alichukia choo kuhamishiwa ndani, ilikuwaje aliongea na ‘mafundi' kuhusu kuhamishia choo hicho ndani?

Ni choo kipi anachozungumzia leo tofauti na kile alichotuambia ameshiriki katika kuongea na mafundi kihamishiwe ndani?


Pili, Dr anaposema msimamo wake ni kupigana na ufisadi na aliaminiwa kwa hilo, leo inakuwaje askari huyo huyo anarudi kuomba nondo kutokakwa Mwakyembe?

Ni ufisadi upi aliouona na upi uliojiri sasa? Je, nondo ni za EPA Escrow, nyumba za serikali au!


Tatu, anapoongelea ufisadi wa Richmond lazima pia aueleze ukweli.

Huyu Lowassa anayetuhumiwa alituhumiwa kutumia wapambe kurudisha Richmond bungeni.


Spika wa wakati huo Mh Sitta alikataa hoja,Mwakyembe akitaka irudi afumue na mambo mengine ya serikali

Dr Slaa anawajibu wa , kwanza, kumuuliza Sitta kwanini alikataa suala lisirudi ambalo pengine leo Lowassa angeshahukumiwa tena mahkamani?

Kwanini Dr Mwakyembe alisema‘mambo mengine yatakayoivua nguo serikali?


Dr Slaa anatakiwa asiruke hatua. Rmond ina mlolongo , anawajibu wa kueleza mlolongo huo asimwache Lowassa, Sitta au Mwakyembe bilaupendeleo au uonevu

Kuhusu Dr Slaa kuondoa umma katika hoja na kupotosha, hilondilo linatumiwa na CCM.

Njia nyepesi ya kufunika Escrow na mauza uza mengineni kuleta Richmond.

Na mtu anayeweza kulisema bila aibu ni Dr Slaa. Ndiye tunaona aantumia NGO ya siasa kuelezanusu ya ukweli na si ukweli kama ulivyo, tena akipotosha


Kwa upande mwingine, bado UKAWA hawana strategists , mbona hili la Dr Slaa/CCM na Richmond linazungumzika vizuri?

Tena CCM wangefunga hoja maana ingegusa maeneo mengine yasiyoguswa kutokana na ‘taboo' zetu
 
JokaKuu,

Umenifurahisha. Ila kwenye chagua namba moja mbona Lowasa hujamnasibisha na UKAWA. Umemtaja kama mgombea binafsi bana.

Mimi siko kwenye hizo chaguzi zote mbili. Kwa nini sitachajua hilo chaguo la pili, well its CCM halihitaji maelezo zaidi. Kwanini sitachagua hilo chaguo la kwanza kama ulivyoliweka hapo, well, historia ya nchi imenifundisha nisikipe chama kimoja serikali na bunge.

Atakae pata kura yangu ya uraisi, hatapata kura yangu kwenye ubunge. Nakushauri sana ndugu kama kweli unataka serikali ijayo iwe accountable usifanye uamuzi wa kutoa kura zako zote kwenye chama kimoja. Haijalishi nani ataend up madarakani, kwa maslahi ya taifa hili tunahitaji upinzani imara.

Natamani ningekuwa na uwezo kufanya kampeni inayosema "Ewe mtanzania, usiweke mayai yako yote kwenye kikapu kimoja. Acha kucheza ngoma ya wanasiasa".
Hili la kuweka mayai yote kapu moja linaweza kutokea.

Huko nyuma katika mijadala tuliwahi kuzungumza na JokaKuu . Tulisema hivi


Plan ya UKAWA , Plan A1 kushinda dola na bunge, Plan A2 kushinda kimoja kati ya dola au Bunge.
Hakuna Plan A na B


Kwa hali iliyopo inaonekana linawezekana kwasababu hizi

UKAWA wanaweza kushinda Bunge na Serikali

CCM wanaweza kushinda bunge na Serikali

Kwa bahati mbaya UKAWA wameacha jukumu la kuwa ‘power broker'

Ukitazama kwa jicho pevu attention yao imeondoka katika suala la bunge

Kwahiyo wameamua kucheza karata moja kubwa! Ni hatari isiyoonekana lakini ipo

Kwa maana kuwa meli ikizama izame na mzigo
 
UKAWA

RICHMOND INAZUNGUMZIKA


Hili ni suala lililosumbua taifa kwa muda mrefu. Hadi sasa hatujui ukweli kamili kutokana na kila wakati kuchukua sura mpya.

Tunachojua ni kuwa lilikuwepo tatizo lililomlazimisha Lowassa Kujuzulu. Tatizo lipo


Tatizo kubwa ni suala nyeti kama hili kugeuzwa mchezo wa kisiasa kwa gharama za wananchi.

Yaani kura zitafutwe kwa kuficha ukweli au kupotosha wakati wanaolipia gharama za uozo uliotendeka ni wananchi hao hao


CCM imeligeuza kama tatizo la wapinzani wakimtumia aliyejiuzulu

Hili linazumngumzika vizuri sana katika mukatadha huu

Kwanza, wahusika wote walikuwa CCM wakati likitokea nawalikuwa ndani ya serikali ya CCM

Bunge lililongozwa na CCM na kupitisha hoja kwa misingi ya wingi wao

Swali: Ni kwanini wahusika hawakuchukuliwa hatua , eti leo tunaambiwa ni wahalifu?
Ni kwanini CCM haikuchukulia hatua wakati wakiwa ndani ya CCM
?

Pili, Dr Mwakyembe aliomba lirudishwe bungeni kujadiliwa upya baada ya kuonekana kuna dalili za kusafishana
Swali: Dr Mwakyembe , ni kipi hasa kilikusukuma ukataka lirudi bungeni?

Tatu, Alyekataa lisizungumzwe bungeni ni Samwel Sitta akiwa Spika
Swali: Kwanini Sitta alikataa lizungumzwe bungeni leo linazungumzwa nje tena katika kampeni na yeye akiwemo?

Nne, Dr Mwakyembe alisema ‘ataongea na mengine yatakayoivuanguo serikali'
Swali: Kwavile leo limekuwa agenda ya uchaguzi, Dr Mwakyembe ambaye Dr Slaa amekiri kupokea habari zaidi, ni yapi yaliyolenga kuivua nguo serikali ambayo leo tunaweza kuyasema tu kama tunavyosema kuhusu Lowassa na Richmond?

Tano, Dr Slaa, unaweza kutupa ufahamu kidogo kuhusu hayo manne hapo juu kwavile ulibahatika kupata habari zaidi kutoka chanzo?
 
..fortunately Lowassa ameliacha genge lake CCM.

..hata Dr.Slaa amesema wale wabunge 50 na wenyeviti wa mikoa wa chama 20 waliokuwa wahame na Lowassa kwenda chadema, wamebadilisha mawazo na kubakia CCM.

cc Alinda, King Suleiman

Hivi ni akina nani wanaunda 'Genge' la Lowassa?...

Kuna yeyote anaweza kunisaidia kuwataja kwa majina?...

Pia si vibaya mkuu wangu ukaanza na hao aliowaacha CCM...
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom