CHADEMA/UKAWA: Uwekezaji usiotabirika

CHADEMA/UKAWA: Uwekezaji usiotabirika

Kuna usemi wa Kiingereza unasema desperate times call for desperate measures lakini hapo hapo upo unaosema desperate times require despearte measures. Hizi semi ukizipitia kwa haraka haraka unaweza ukadhani zinafanana lakini naomba niwahakikishie zinatofautiana sana kimaudhui. Zote unaweza kuzitumia katika kuliangalia swala la Lowassa kupokelewa Chadema na swala la Dr. Slaa kuamua kubwagwa manyanga (actually mimi siamini Dr. kweli kabwaga manyanga, anajaribu kuzuia mafuriko kwa mkono)

Kwa bahati mbaya muda wangu ni mdogo lakini nitajaribu kurudi kufafanua ila kabla sijaaga naongezea kwa kusema hivi "extremis malis extrema remedia" au kwa kiingereza, the desperate disease requires a dangerous remedy...

...baadaye wana jamvi.
 
[/COLOR]
Ukishaanza mipasho hapo ninakuwa sina la kukusaidia zaidi ya kukuignore kama nifanyavyo kwa wengine..

Si kwamba mipasho, kejeri au matusi siwezi bali ni kwa vile hayo nimeishayavuka.. Njoo kivingine tujadiliane.. Huu ni mjadala si ugomvi na wala hatutafuti mshindi.. bali tunapanuana mawazo na kujifunza mambo mbali mbali kutoka wa watu mbali mbali...
Alaaa mipasho kwa vipi kukwambia kwamba kuna viongozi wa Chadema waongo na wafitini? Ama ya kwamba uongozi wa kamati kuu CDM wamekuwa na maamuzi mabaya na yametokana na baadhi roho zao mbaya!.

Mimi simkejeri mtu nasema nachokijua na kila mara Alinda nisemalo humu matokeo yake huwa kama nilivyotegemea na huwashtua nyie kuona matokeo hayakuwa kama mlivyodhani ama kupendelea. Kwa hiyo wewe ita mipasho lakini ndio hali halisi yenyewe na huwezi kuigeuza!
 
Last edited by a moderator:
HOJA

Wakuu Mzee Mwanakijiji na Eric Cartman naomba nichangie hoja zenu


Kuhusu viongozi: CCM walitangaza mchakato wa kupata mgombeamwezi wa nne. UKAWA walikuwa navikao visivyoisha kwa hadi July.

Wengine tulihoji (bandiko lipo) iweje UKAWAwasue sue tukijua hawana rasilimali za kutumia za kampeni kwa muda mfupi?''Dilly dallying'' iliendelea kwa muda tu


Ghafla CUF wanachachamaa kumwita mwenyekiti wao.Tukahoji, kama hilo ni tatizo kwanini kisiitishwe kikao cha dharura eti nimpaka wasubiriwe wiki 3?

Prof alikuwa na uwezo wa kutisha kikao ili mamboyaende haraka. Halikufanyika!


Mara ujio wa Lowassa na kuanzia hapo kila jambolilipata msukumo wa haraka sana.
Kuna kila sababu ya kuamini viongozi walikuwana mpango huo kwa muda mrefu.
Kuchelewa chelewa ilikuwa dilly dallying. Hayoyamethibitishwa na Lissu pamoja na Dr Slaa


Lipumba:
Amekiri kushiriki, kinachomsumbua ni nafsiinamsuta, kasema wazi alishiriki.
Pengine ndio maana hatakikuingia katika undani akijua ni sehemu ya mpango huo.


Mbowe:
Katika baraza kuu , alisema ‘hatuwezi kuacha fursahii iliyojitokeza'
Kwamba hatuwezikuongelea ufisadi kila siku, lazima tuongelee maendeleo. Hapa alitaka kuyeyushamsimamo wa Dr Slaa kwa kuiweka hoja ya ufisadi nje ya hoja kuu. Alifanya hivyokuungwa mkono na baraza kuu.


Lissu:
Akasema katika video moja, bado CDM/UKAWA walikuwadhaifu baadhi ya maeneo.
Alimaanisha ujio utaimarisha maeneo dhaifu. Lakini pia amejitokeza mara zote kueleza ushiriki wake katika ujio


Dr Slaa:
Msimo wake kuhusu ufisadi unajulikana. Juzi kwakinywa chake kasema ni kweli alishiriki ingawa aliweka masharti. Hoja ya msingihapa ni kuwa alishiriki, kama alivyoshiriki Lipumba, Mbowe na Lissu


Rafiki wa Mhakama (Inaendelea
 
Naomba niwe ‘amicus curiae' rafiki wa mahakama katika hii ‘criminal proceeding'

Huu ni mfano tu, wala hauna uhusiano na wahusika . Ni katika mjadala

Nikitumia sheria ya New south Wales (crime act 1900) inasema

1 Mtu anayeshiriki tendo la uhalifu ana hatia ikiwa:

  1. Ananjua au ana ufahamu kuhusu ‘genge' la uhalifu
  2. Anaju, au ana ufahamu kwamba ushiriki wakeutatoa matokeo ya uhalifu

Na pia mtu anayejua au kufahamukuhusu ‘kundi la uhalifu'l inaloandaa au kuendeleza uhalaifu


Mfanon wa pili
ACCOMPLICE (Mshiriki)


Ni neno linalomaanisha mtu anayeshiriki ‘uhalifu' hata kama hakutenda uhalifu huo mwenyewe

Kwa mukatadha huo, wote hapo ni washiriki wa kumleta Lowassa ingawa viwango vya ushiriki vinatofautiana.
Nahilo ndilo haswa, limezaa maswali yasiyo na majibu.


KWANINI LINAONEKANA SUALA NI LADAKTARI IKIWA WAPO WASHIRIKI WENGINE?

Kwanza, Dr Slaa ana uhuru wakutoa maoni kadri anavyoweza.
Maoni yake ni haki yake hayawezi kuwa sahihi au yenye makossa.. Alichokifanya Serena Hotel hakina kosa


Endapo hakukuwepo na makosa,kwanini watu wanahoji sana hotuba yake?

1 Hotuba yake imeacha maswali mengi yasiyo na majibu.
Kwa mfano, Slaa anawezaje kutaja Lowassa na Mshenga kuanzia alipokatwa kana kwamba hakuna mawasiliano kabla


2 Kukiri na kisha kujitoa katika ushiriki ili apate nafasi ya kusema mengine

3 Kushambulia watu wasio na uhusiano na suala Zima

4 Mwasiliano duni, mabovu na ya jazba

Inaendelea
 
Kwanini ni Dr.Slaa tu ndio wakuwekwa mtu kati kwanini isiwe Mbowe, Mbatia na Lissu kama bado ni wanasiasa wa kuaminiwa na kama kweli Lowassa wanamtumia kwa sababu ya mabadiliko au wana motives tofauti.

The Alibi so far on what is going on.

Prof.Lipumba
Huyu ndio wa kwanza kujitoa katika uongozi wa UKAWA kwa madai ya kuwa agenda imebadilika na vilevile dhamira inamsuta. Dhamira gani? tunajua wagombea wa uraisi wa UKAWA walikaa na kukubaliana ya kuwa Dr.Slaa ndio atapepea bendera. Hili Lipumba alilisema hadharani na Mbatia amelirudia. Kwa hivyo through series of events Dr.Slaa awezi kupokewa au kujadiliana na UKAWA kuwa mgombea wao kama CDM walikuwa awajampitisha bado.

Kwanini sasa Lipumba aondoke ghafla wakati ndio mtu aliyeandika waraka wa kumpokea Lowassa mara alipoingia kwenye mkutano wao, waraka uliosomwa na Mbatia. Ina maana mpaka dakika hiyo maamuzi ya kuwa Lowassa atakuwa mgombea wa UKAWA yalikuwa bado ayajaamuliwa na pengine maelewano ilikuwa support yake tu ndio wanayo itaka. This is the only reason why Lipumba left baada ya Lowassa kupewa unahodha wa kambi.

Dr.Slaa
Nilikuwa tayari nimeshapitishwa na chama kuwa mgombea wao kwa taratibu za ndani; kilichobaki ina maana ni ilikuwa ni public appearance tu. Jumlisha na facts za kuwa kulikuwa na mgogoro mkubwa sana kupata mgombea wa UKAWA ambao ilibidi watu watoke Dodoma na wakae mpaka saa tisa za usiku ina maana Dr.Slaa nayeye alikuwa tayari keshajiandaa kugombea uraisi pia. Kwa vyovyote vile ujio wa Lowassa kwa Dr.Slaa ni mkakati wa kuivuriga CCM kwenye campaign zake kwakuwa aliahidi kuja na wafuasi na kulikuwa na some elements of that based on his nomination campaign support aliyokuwa nayo CCM ilikuwa ni dhahiri mpaka wanachama kuimba nyimbo za kukosa nidhamu ndani ya kikao chao baada ya kukatwa kwa Lowassa.

Tundu Lissu
Dr.Slaa alishapitishwa na vikao halali vya chama kuwa mgombea wa chama chetu kwa nafasi ya uraisi. Inathibitisha zaidi by now Dr.Slaa alijua ya kuwa yeye ni mgombea tayari na ujio wa Lowassa usingeweza tengua hilo ata kama huku pembeni alikuwa anaongea na Gwajima kuhusu Lowassa sidhani kama lengo ujio wake uwe kwa sababu ya uraisi.


Baada ya hizo events nadhani kilichofuata ni hiki kutoka kwa timu ya Lowassa kwa kuitazama safu ya watu walio CDM
especially kama walianza kumfuata wakati bado yuko kwenye campaign za kuwania uongozi kupitia CCM.
Ukiangalia tu historia yake ya kutoa vibaasha sidhani kama anawapa viongozi kwa sababu ya kura moja zao, bali anajuwa wanamakundi ya wafuasi wenye uwezo wa kumpa kura nyingi tu. Kwenye ethics wanasema uwezi defy nature ya kitu viumbe vinatabia ya kurudia mambo yaleyale given the challenge or circumstances.

Je iliwezekana vipi Lowassa kupitishwa kuwa mgombea wa CDM na UKAWA kitendo kilichopelekea prof Lipumba kuacha uongozi maana hata kama CDM walimptisha surely Lipumba utegemei nayeye akubali kirahisi kwa sababu tunajua kwa Dr.Slaa tu ilichukuwa alot of convincing from his other leaders kukubali. Na kwanini CDM ilivunja kanuni zake za ndani maana Dr.Slaa walishamteua kususa kwa Dr.Slaa sidhani kama ni kwa hoja zake tu bali kutolewa kwenye position aliyokuwa keshapitiwa na chama chake pamoja na viongozi wa vyama vingine.

Tukirudi kwenye nature ya Lowassa kwanini tusiamini hakutumia tena vibaasha vyake kununua viongozi wa UKAWA kupata support ya watu wao ili kuendeleza ndoto yake ya uraisi; je hii ndoto inaendana na vision ya UKAWA.

If you ask me there is no historical evidence to back that claim kwamba Lowassa anamapenzi na upinzani ni ndoto zake tu za uraisi na kwa njia zilezile anazotumia ndio zimemfikisha kileleni upinzani pia, why should anyone believe akiukwaa uraisi atabadilika wakati all the evidence points otherwise.

Sielewi kwanini watu amumuoni huyu mtu for what he is na jinsi gani Mbowe, Mbatia, Lissu jumlisha na Sharif Hamad walivyokuwa si watu wa kuaminiwa. Mimi bado namueshimu sana Dr.Slaa na Prof.Lipumba ndio watu pekee walio na morals ata kama walibariki ujio wa Lowassa sio kwa sababu ya kuuza nguvu zao pia na kuwapa mafisadi platform nyingine. Huyo Mbowe ndio kabisa hana loyalty yaani kejeli za jana kwa Dr.Slaa sikuamini kama anaweza rusha vijembe vya namna hile inawezekana ata Dr.Slaa alikuwa anamtumia pia kuongeza wabunge na ruzuku ya chama.

EC:

To me, this year election is comical at best, or to put it mildly, the mockery of democracy. Watu wanatembeza vibaasha kila kona na sasa wanaitwa wakombozi.
 
MAWASILIANO DUNI (PR KATIKA MEDIA )

Prof Lipumba alieleza maneno mawili tu ‘nafsi inamsuta' kabla ya hapo alikiri kushiriki kila hatua.

Hakwenda mbali kueleza mambo ya kiofisi au migogoro mingine


Dr Slaa, naye alieleza kile asichokubaliana nacho.

Hakuna mtanzania asiyejua misimamo yake hasa suala la ufisadi.

Mkutano wa Serena ulilenga kueleza kwanini ameondoka na hatma yake.

Hakupaswa kuwa jukwaa ‘lisilo' rasmi la siasa ikiwa ameacha siasa


Tunasisitiza, tatizo si kutoa maoni. Tatizo ni approach na maudhui yasiyolingana na muda na haja ya wakati

Hakuna sababu za Dr kuzuiliwa kusema kama mtanzania mwingine.
Hilo angelifanya kwa wakati mwingine, na wala asitumie mtafaruku uliopo kuficha ushiriki wake


Kwa mfano, suala la maji Monduli lina uhusiano gani na UKAWA?
Suala la shule za kata lina uhusiano gani na kujiuzulu kwake?

Mambo ya dini yameingiaje katika kujiuzulu kwake?

Mashambulizi kwa Sumaye na wenzake yalikuwa na sababu gani tukijua kuwa hadi July 25 hakupewa jina la mtu

Je, akina Sumaye, Gununita, Msindai wana ushiriki upi katika kumleta UKAWA ambao Dr hakuusema?


Kuna mambo mawili ya kukumbukwa.

Kwanza, suala la ushiriki na pili ni ‘communique' iliyokosa vionjo vya public relations na hilo ndilo tatizo kubwa linaliozua mjadala


Communique yake si mpya, aliyozungumza mengi yaliwahi kutumiwa na watu kama CCM kwa nyakati mbali mbali.

Hivyo, anayeondoa benefit of doubt ni Slaa mwenyewe, si watu



Tumalize kwa kusema haya
1 Kwamba, viongozi wa UKAWA walikuwa na yao moyoni ! Jibu nikweli, kuchelewa chelewa ilikuwa ni danganya tu.
Kuna walichokuwa wanasubiri


2 Kwamba, UKAWA walishiriki kumleta Lowasa, Jibu" Hakuna shaka kwa kukiri kwao

3. Dr Slaa Alishiriki katika kumleta Lowassa, jibu ni ndiyo na tumonyesha hapo juu na amekiri

4 Dr Slaa ana haki ya kuhutubia na kutoa maoni sasa na baadaye, Jibu: Ni kweli na ndiyo

5 Kwamba, Dr Slaa alishindwa kuandaa mawasiliano, Jibu ni kweli.
Hotuba yake iliacha mambo muhimu, ikaingiza mambo yasiyo na uhusiano,akashambulia bila sababu


6 Kwamba anashambulia watu bila sababu za msingi na mashiko!Jibu ni ndiyo

7 Kwamba anatafuta sababu za kuficha ushiriki wake-Jibu ni ndiyo

Tusemezane
 
Mkuu Nguruvi3

Pamoja na madhaifu ya Lowasa lakini jambo moja lililo wazi ni kwamba ujio wake UKAWA kwa mara ya kwanza umewaunganisha wapinzani hawa bila kujali vyama vyao. Umejenga momentu ambayo mpaka sasa haijatetereka pamoja na misukosuko kadhaa iliyotokea.

Hivi umewahi kujiuliza kwanini rection ya watu baada ya Lipumba kuachia ngazi ilikuwa ni kama vile hakuna alieshtuka na watu wakaendelea kuchapa mwendo kama kawaida? Pamoja na ukimya wa Slaa wakati wa shamra shamra za kumpokea Lowasa lakini hio nayo haijaonekana kuathiri mwamko wa wana UKAWA hata kidogo. Maana yake ni nini?

Pengine Slaa & Lipumba walitaraji kujiengua kwao kungeteteresha mwendo wa jahazi hili la UKAWA kiasi cha kuwafanya wafikirie upya uamuzi wao wa kumkaribisha Lowasa... Lakini matokeo yake yamekuwa ni kinyume! Na hili pengine ndilo linalomuumiza zaidi Slaa kuona kwamba Lowasa ghafla amevaa vyema viatu ambavyo alipaswa kuvivaa yeye. Pengine alitaraji kuona wananchi wakiandamana kupinga ujio wake lakini ghafla anaona hali ni kinyume!

Ndio maana kwenye ile press conference akajikuta anapoteza uelekeo kutoka kueleza kiini cha tofauti kati yake na mwenyekiti na kuanza kushambulia kila mtu. Upande mmoja anakiri kushiriki mchakato mara upande wa pili anamtupia furushi la lawama mwenyekiti wake, mara anatema sumu hata kwa wale ambao hawakuhusika na mchakato wa kumkaribisha Lowasa UKAWA!
 
Last edited by a moderator:
Bado najiuliza Gwajima ana interest gani na urais wa Lowassa? Imekuwaje mpaka Lowassa akamuamini Gwajima kiasi kikubwa hivyo. Dr. Slaa anasema Gwajima amemwambia kuwa Lowassa kawahonga maaskofu 30 ili wamuunge mkono, je iwapo hili ni kweli, siasa za mgombea wa namna hii zina athari gani kwa taifa?

Bado naamini kujadili vitu vyepesivyepesi badala ya mambo makubwa ni kutokulitendea haki taifa...
 
Bado najiuliza Gwajima ana interest gani na urais wa Lowassa? Imekuwaje mpaka Lowassa akamuamini Gwajima kiasi kikubwa hivyo. Dr. Slaa anasema Gwajima amemwambia kuwa Lowassa kawahonga maaskofu 30 ili wamuunge mkono, je iwapo hili ni kweli, siasa za mgombea wa namna hii zina athari gani kwa taifa?

Bado naamini kujadili vitu vyepesivyepesi badala ya mambo makubwa ni kutokulitendea haki taifa...
Siasa za Tanzania zimekuwa kichekesho,yaani kweli huu yashutuma zote alizotoa Slaa mwenyewe , ananon'gonezwa kwamba Lowasa kahonga maaskofu 30 halafu bila kuchunguza ana jiunga kwenye mazungumzo ya kumkaribisha chamani na kumsikiliza na kumuwekea masharti?
Nasema kujiunga na mazungumzo kwa sababu sitaki au nashindwa kumeza ukweli kwamba inawezekana Dr ndie aliye kuwa wa kwanza kuongea na lowasa kuhusu kujiunga
 
Bado najiuliza Gwajima ana interest gani na urais wa Lowassa? Imekuwaje mpaka Lowassa akamuamini Gwajima kiasi kikubwa hivyo. Dr. Slaa anasema Gwajima amemwambia kuwa Lowassa kawahonga maaskofu 30 ili wamuunge mkono, je iwapo hili ni kweli, siasa za mgombea wa namna hii zina athari gani kwa taifa?

Bado naamini kujadili vitu vyepesivyepesi badala ya mambo makubwa ni kutokulitendea haki taifa...

Gwajima ni rafiki wa Lowassa hii Gwajima alishasema kitambo.

Dr. Slaa baada ya kuwekewa pingamizi la kufunga ndoa na Josephina, Josephina alikasirka na kumshauri Dr. Slaa kuhama kanisa, Hivyo walihamia kanisani kwa Gwajima pia Gwajima na Dr. Slaa ni marafiki lakini sijui kama urafiki wao ulianza walipohamia kanisani kwake au kabla..
Kwa hiyo mpaka hapo unaweza kuunganisha nukta na kuona Gwajima anaingiaje kwenye ili sanga..

Inawezekana kabisa baada ya DR. Slaa kufahamu kuwa yeye ni mgombea urais, alikuwa anatafuta mtu ambaye anaweza kumsapport nje ya Chadame hivyo akaongea na Gwajima ili aongee na Lowassa haweze kujiunga nao.. Sote humu ndani tunafahamu nguvu na mikakati ya Lowassa nafikiri hata Lowassa kwenda Chadema ni pigo kubwa sana kwa CCM .

Au inawezekana Lowassa alimuomba Gwajima aongee na Dr, Slaa kama anaweza kujiunga na Chadema endapo CCM watakata jina lake.. (Na nafikiri Lowassa alimwendea Mbowe, Na Mbowe akamwambia aende kwa Dr. Slaa, hivyo akatafutwa mtu wa kumuingia DR. Slaa ambaye si mwanaUkawa au mwana CCM)

Na kwa mjibu wa ex wa Dr. ugomvi kati ya Dr.Slaa na Lowassa si mkubwa vile kama tunavyofikria sisi, hawa wao wanaelewana maana huyu mama alisema baada ya kutangaza ile "list of Shame" alikwenda kwa Lowassa na kupata dinner.

Hivyo ukianza kuunganisha hizo dot unapata picha kamili ilivyochezwa, Nafikiri Dr,Slaa alikuwa hana nia vilee ya kuwa mgombea wa urais na ndio maana alipotaka kutangazwa alikataa na kusema wasubiri ili wafanye shamra shamra.. (nafikiri hapa mambo ya Lowassa yalikuwa bado hayajakaa sawa.
Na kusapport point yangu hapo juu, ni pamoja na kufahamu kuwa nia ya Lowassa ni kugombea urais wa Tanzania iwe kwa kupitia CCM, au Ukawa au ACT ilikuwa inajulikana kwa kila mtanzania na kama Dr. Slaa angetaka kumzuia hasigombee urais kupitia Ukawa basi siku ile angekubali kutangazwa maana walishakubalina wagombe urais wote kuwa Slaa apewe nafasi.. Na pia ukisoma maelelzo ya Tai Ngwilizi ambayo Dr. Slaa anasema "kiongozi ambaye anaenda kuwa raisi wa nchi lazima awe na wafuasi nyuma yake.Hivyo basi unaona kuwa nia ya Lowassa ilijulikana mapema na pia ijulikana hata kwa huyu aliyemleta.

Pia tukumbuke vikao vya kumtambulisha Lowassa viliandaliwa na Dr. Slaa na mpaka hapo kulikuwa hakuna wasi wasi wote.. Kwenye Halmashauri/Kamati kuu alijieleza na walimuelewa. Baada ya hapo Dr. Slaa aligeuka ghafla maana walikuwa wamepanga wakutane wote siku ya kumtambulisha Lowassa lakini Dr. hakujitokeza na alipopigiwa simu alikuwa haipatikani ndipo Pro. Safari alimfuata nyumbani kwake na Dr. kumkabidhi Pro. barua ya kujihudhuru..

Inapofika hapo ndipo ile point ya Lissu inapoleta mantiki kuwa mama Josephina hakufurahishwa Lowassa kupeperusha bendera-- yaliyosemwa mmeyasikia. Hivi ndivyo nionavyo katika sakata ili.

Ila ninaweza kusema kuwa Dr. Slaa analeta siasa za kinafiki maana mtu amemkaribisha yeye, halafu leo analalamika kuwa ni fisadi sasa wakati anamkaribisha hakufahamu kuwa ni fisadi?

Juzi katika Press yake alikuwa na Mwakyembe (kitu ambacho si kibaya) na alipouliza alisema kuhusu kuonekana yeye na Mwakyembe (mwana CCM ambaye anapingana na mgombea urais Ukawa) alisema: "
research’ (utafiti) lazima urudi kwenye ‘source’ (chanzo) ya hilo jambo na ndiyo maana nilikuwa na jeuri ya kuzungumza kwa kujiamini"

Sasa swali la kujiuliza wakati wanazunguka nchi nzima kutangaza kuwa Lowassa ni fisadi alikuwa hajafanya research ya kutosha? Ina maana alikuwa hana uhakika ni kile anachotulisha, Je ndio maana akamkaribisha Lowassa Ukawa?

Na je vipi ile list of shame alifanya reseach ya kutosha isije kuwa nayo hana uhakika nayo.. Yaani katika wanasiasa niliyowapenda na kuamini kila watamkalo alikuwa Dr, Slaa hila huu ulaghai na uongo alionza kwa kweli amenisikitisha sana sikutegemea mzee mzima kama yule ukaa mbele ya camera ya kutulisha uongo..

Anasema Sumaye hawaongei.. Ex wake anasema alimpa No. ya simu Sumaye wiki tatu zilizopita, na waliongea vizuri tu, anasema mshahara wake alikuwa anachangia chama na wao wanakula Mihongo, anaulizwa vipi hii press nani kalipa nabaki kusema kwani nilipokwenda USA mara mbili nani alilipa maana chama kilinipa sh. Laki Tano.. Sasa jamani kama mtu mzima unaongopa kwa vitu vidogo namna hii itakuwaje kwa mambo makumbwa ambayo hatuwezi kuyafatilia na kuwa na uhakika na unachokisema? Nimeumia sana..

Kama ni swala la kutoa na kupokea rushwa, sote humu ndani tukiwa wakweli, baada ya Dr. Slaa naye kupokea mlungula ninaweza kusema tena kwa kujihamini wanasiasa wote wa Tanzania ni watoaji na wapokeaji rushwa, si Kikwete, si Kinana, si Mbowe, si Lipumba, si Zitto, si Dr. Slaa si Lowassa, si Mbatia ila hizi kelele tunazozisika kuwa ooh fulani ni mtoa rushwa, ooh fulani kapokea rushwa wanakuwa wamezidiana madili yao..

Huwezi kuniamba kuwa Dr, Slaa amejitoa Chadema ameachana na mshahara wa mil.11 kwa mwezi kwa vile ana uchungu sana na watanzania na. ndio maana anapingana na Lowassa lakini Magufuli na CCM hatii neno wakati machungu ya CCM anayafahamu vizuri.. Hizi huruma kwa watanzania zimetoka wapi?

Hivyo basi tukianza kuwahukumu watoa rushwa tuwahukumu wote bila kuangalia ni akina nani na wanafanya nini..
 
Sasa swali la kujiuliza wakati wanazunguka nchi nzima kutangaza kuwa Lowassa ni fisadi alikuwa hajafanya research ya kutosha? Ina maana alikuwa hana uhakika ni kile anachotulisha, Je ndio maana akamkaribisha Lowassa Ukawa?

Na je vipi ile list of shame alifanya reseach ya kutosha isije kuwa nayo hana uhakika nayo.. Yaani katika wanasiasa niliyowapenda na kuamini kila watamkalo alikuwa Dr, Slaa hila huu ulaghai na uongo alionza kwa kweli amenisikitisha sana sikutegemea mzee mzima kama yule ukaa mbele ya camera ya kutulisha uongo..

Anasema Sumaye hawaongei.. Ex wake anasema alimpa No. ya simu Sumaye wiki tatu zilizopita, na waliongea vizuri tu, anasema mshahara wake alikuwa anachangia chama na wao wanakula Mihongo, anaulizwa vipi hii press nani kalipa nabaki kusema kwani nilipokwenda USA mara mbili nani alilipa maana chama kilinipa sh. Laki Tano.. Sasa jamani kama mtu mzima unaongopa kwa vitu vidogo namna hii itakuwaje kwa mambo makumbwa ambayo hatuwezi kuyafatilia na kuwa na uhakika na unachokisema? Nimeumia sana..

Kama ni swala la kutoa na kupokea rushwa, sote humu ndani tukiwa wakweli, baada ya Dr. Slaa naye kupokea mlungula ninaweza kusema tena kwa kujihamini wanasiasa wote wa Tanzania ni watoaji na wapokeaji rushwa, si Kikwete, si Kinana, si Mbowe, si Lipumba, si Zitto, si Dr. Slaa si Lowassa, si Mbatia ila hizi kelele tunazozisika kuwa ooh fulani ni mtoa rushwa, ooh fulani kapokea rushwa wanakuwa wamezidiana madili yao..

Huwezi kuniamba kuwa Dr, Slaa amejitoa Chadema ameachana na mshahara wa mil.11 kwa mwezi kwa vile ana uchungu sana na watanzania na. ndio maana anapingana na Lowassa lakini Magufuli na CCM hatii neno wakati machungu ya CCM anayafahamu vizuri.. Hizi huruma kwa watanzania zimetoka wapi?

Kwahiyo Gwajima, kama nimekuelewa, maslahi yake ya urafiki tu? Umefafanua vizuri evolution ya uhusiano wa Slaa na Gwajima, ila urafiki wa Lowassa na Gwajima hujaelezea uko based on nini?


Je, maadili ya kazi ya utabiri yanasemaje pale mtu anapotabiri fulani atakuwa Rais kumbe chinichini anamfanyia mikakati ashinde? Nadhani kuna haja ya kudevelop utamaduni wa watu kufanya declaration of interest ili wanaosikia utabiri wajue kuwa kuna conflict of interest. Ni safi zaidi kiongozi wa dini kutoa public endorsement kwa mgombea kuliko kushiriki kwa siri.

Kuhusu list of shame, hivi ile list ni ya Dr Slaa au ya Chadema? Kama list au agenda ina mapungufu, anayebeba lawama za kutokufanya utafiti ni Slaa au Chadema? Nakumbuka list of shame iko mpaka kwenye ilani ya uchaguzi ya Chadema ya mwaka 2010-2015. Kwa misingi hiyo sidhani kama ni sahihi kumbebesha Dr. Slaa personally mzigo wa lawama kuhusu list of shame. Kwahiyo baada ya kuuliza kama Slaa hakufanya research ya kutosha, swali sahihi ni iwapo Chadema haikufanya research ya kutosha.
 
Kwahiyo Gwajima, kama nimekuelewa, maslahi yake ya urafiki tu? Umefafanua vizuri evolution ya uhusiano wa Slaa na Gwajima, ila urafiki wa Lowassa na Gwajima hujaelezea uko based on nini?


Je, maadili ya kazi ya utabiri yanasemaje pale mtu anapotabiri fulani atakuwa Rais kumbe chinichini anamfanyia mikakati ashinde? Nadhani kuna haja ya kudevelop utamaduni wa watu kufanya declaration of interest ili wanaosikia utabiri wajue kuwa kuna conflict of interest. Ni safi zaidi kiongozi wa dini kutoa public endorsement kwa mgombea kuliko kushiriki kwa siri.

Kuhusu list of shame, hivi ile list ni ya Dr Slaa au ya Chadema? Kama list au agenda ina mapungufu, anayebeba lawama za kutokufanya utafiti ni Slaa au Chadema? Nakumbuka list of shame iko mpaka kwenye ilani ya uchaguzi ya Chadema ya mwaka 2010-2015. Kwa misingi hiyo sidhani kama ni sahihi kumbebesha Dr. Slaa personally mzigo wa lawama kuhusu list of shame. Kwahiyo baada ya kuuliza kama Slaa hakufanya research ya kutosha, swali sahihi ni iwapo Chadema haikufanya research ya kutosha.
Kuhusu viongozi wa dini kuwa watabiri wakiwa sehemu ya utabiri nakubaliana nawe kabisa

Pili, list of shame imetumika miaka nenda rudi. Moja ya sababu za Slaa kujiuzulu ni kuilinda na kuienzi kama alivyoitete

Tatu, hili la kukutana na Mwakyembe ili kufanya research ni njia tu ya kukwepa ukweli kuwa alikuwa na jingine.
Ni njia ya kukwepa ukweli unaoweza kuunganishwa kuwa script iliandaliwa sehemu nyingine

Haiwezekani Dr Slaa ajiuzulu kwasababu za ufisafi wa Richmond, halafu baada ya kujiuzulu ndio afanye research. Jamani lazima watu wawe wakweli. Ina maana asingejiuzulu wala asingehitaji research.

Narudia, haki ya maoni anayo, lakini haki hiyo isiharibu credibility yake aliyosema.

Nadhani unaweza kuona kuhusu yeye kujiuzulu halafu kufanya research baada ya kujiuzulu. Inahia akilini kweli
 
Kwahiyo Gwajima, kama nimekuelewa, maslahi yake ya urafiki tu? Umefafanua vizuri evolution ya uhusiano wa Slaa na Gwajima, ila urafiki wa Lowassa na Gwajima hujaelezea uko based on nini?


Je, maadili ya kazi ya utabiri yanasemaje pale mtu anapotabiri fulani atakuwa Rais kumbe chinichini anamfanyia mikakati ashinde? Nadhani kuna haja ya kudevelop utamaduni wa watu kufanya declaration of interest ili wanaosikia utabiri wajue kuwa kuna conflict of interest. Ni safi zaidi kiongozi wa dini kutoa public endorsement kwa mgombea kuliko kushiriki kwa siri.

Kuhusu list of shame, hivi ile list ni ya Dr Slaa au ya Chadema? Kama list au agenda ina mapungufu, anayebeba lawama za kutokufanya utafiti ni Slaa au Chadema? Nakumbuka list of shame iko mpaka kwenye ilani ya uchaguzi ya Chadema ya mwaka 2010-2015. Kwa misingi hiyo sidhani kama ni sahihi kumbebesha Dr. Slaa personally mzigo wa lawama kuhusu list of shame. Kwahiyo baada ya kuuliza kama Slaa hakufanya research ya kutosha, swali sahihi ni iwapo Chadema haikufanya research ya kutosha.
Kuhusu viongozi wa dini kuwa watabiri wakiwa sehemu ya utabiri nakubaliana nawe kabisa

Pili, list of shame imetumika miaka nenda rudi. Moja ya sababu za Slaa kujiuzulu ni kuilinda na kuienzi kama alivyoitete

Tatu, hili la kukutana na Mwakyembe ili kufanya research ni njia tu ya kukwepa ukweli kuwa alikuwa na jingine.
Ni njia ya kukwepa ukweli unaoweza kuunganishwa kuwa script iliandaliwa sehemu nyingine

Haiwezekani Dr Slaa ajiuzulu kwasababu za ufisafi wa Richmond, halafu baada ya kujiuzulu ndio afanye research. Jamani lazima watu wawe wakweli. Ina maana asingejiuzulu wala asingehitaji research.

Narudia, haki ya maoni anayo, lakini haki hiyo isiharibu credibility yake aliyosema.

Nadhani unaweza kuona kuhusu yeye kujiuzulu halafu kufanya research baada ya kujiuzulu. Inahia akilini kweli
 
Anasema Sumaye hawaongei.. Ex wake anasema alimpa No. ya simu Sumaye wiki tatu zilizopita, na waliongea vizuri tu, anasema mshahara wake alikuwa anachangia chama na wao wanakula Mihongo, anaulizwa vipi hii press nani kalipa nabaki kusema kwani nilipokwenda USA mara mbili nani alilipa maana chama kilinipa sh. Laki Tano.. Sasa jamani kama mtu mzima unaongopa kwa vitu vidogo namna hii itakuwaje kwa mambo makumbwa ambayo hatuwezi kuyafatilia na kuwa na uhakika na unachokisema? Nimeumia sana..

Kama ni swala la kutoa na kupokea rushwa, sote humu ndani tukiwa wakweli, baada ya Dr. Slaa naye kupokea mlungula ninaweza kusema tena kwa kujihamini wanasiasa wote wa Tanzania ni watoaji na wapokeaji rushwa, si Kikwete, si Kinana, si Mbowe, si Lipumba, si Zitto, si Dr. Slaa si Lowassa, si Mbatia ila hizi kelele tunazozisika kuwa ooh fulani ni mtoa rushwa, ooh fulani kapokea rushwa wanakuwa wamezidiana madili yao..

Huwezi kuniamba kuwa Dr, Slaa amejitoa Chadema ameachana na mshahara wa mil.11 kwa mwezi kwa vile ana uchungu sana na watanzania na. ndio maana anapingana na Lowassa lakini Magufuli na CCM hatii neno wakati machungu ya CCM anayafahamu vizuri.. Hizi huruma kwa watanzania zimetoka wapi?

Hivyo basi tukianza kuwahukumu watoa rushwa tuwahukumu wote bila kuangalia ni akina nani na wanafanya nini..

Hapo unaposema Dr. Slaa amepokea mlungula bado sijakuelewa mlungula ameupokea kutoka kwa nani?

Kule mwanzo nilitahadharisha kuwa jukwaa la great thinkers lisichukue sura ya kampeni na propaganda. Kuna vitu unaandika ambavyo haviendani na hili jukwaa.
 
Hapo unaposema Dr. Slaa amepokea mlungula bado sijakuelewa mlungula ameupokea kutoka kwa nani?

Kule mwanzo nilitahadharisha kuwa jukwaa la great thinkers lisichukue sura ya kampeni na propaganda. Kuna vitu unaandika ambavyo haviendani na hili jukwaa.

Jamani maana na great thinkers ni nini? uliposema Lowassa ni mtoa rushwa ulimkamata akitoa rushwa? si unatumia akili zako kujua kile na kile kinatokea hiki au!!Hiyo Richmond nikikuuliza Lowassa alijigawai sh. huna jibu,

Ninachoandika ninaandika mawazo yangu na maono yangu, Sasa wewe ukiona kuwa haviendani na jukwaa hili ni sawa na ni haki yako.. Siwezi kuandika kilichomo kichwani mwako au unachotaka kusikia kwa sababu mimi siko kichwani mwako na sijui unataka kusikia nini..

Umeuliza Gwajima nimekujibu jinsi nilivyoelewa...

Mlungula wa Dr. Slaa nitakuuliza hili swali..

Hivi Dr. Slaa pesa za kuitisha press alizitoa wapi hali alituambia kuwa anashindia mihogo? Sasa kama waliweza kumlipia Press kwa vyombo vyote walishindwa kumpa hela ya kula walau mkate?
 
Kwahiyo Gwajima, kama nimekuelewa, maslahi yake ya urafiki tu? Umefafanua vizuri evolution ya uhusiano wa Slaa na Gwajima, ila urafiki wa Lowassa na Gwajima hujaelezea uko based on nini?


Je, maadili ya kazi ya utabiri yanasemaje pale mtu anapotabiri fulani atakuwa Rais kumbe chinichini anamfanyia mikakati ashinde? Nadhani kuna haja ya kudevelop utamaduni wa watu kufanya declaration of interest ili wanaosikia utabiri wajue kuwa kuna conflict of interest. Ni safi zaidi kiongozi wa dini kutoa public endorsement kwa mgombea kuliko kushiriki kwa siri.

Kuhusu list of shame, hivi ile list ni ya Dr Slaa au ya Chadema? Kama list au agenda ina mapungufu, anayebeba lawama za kutokufanya utafiti ni Slaa au Chadema? Nakumbuka list of shame iko mpaka kwenye ilani ya uchaguzi ya Chadema ya mwaka 2010-2015. Kwa misingi hiyo sidhani kama ni sahihi kumbebesha Dr. Slaa personally mzigo wa lawama kuhusu list of shame. Kwahiyo baada ya kuuliza kama Slaa hakufanya research ya kutosha, swali sahihi ni iwapo Chadema haikufanya research ya kutosha.

Urafiki wa Gwajima na Lowassa sifahamu ila nakumbuka wakati Gwajima anaumwa Lowassa na Dr. Slaa walikwenda kumtembelea kwa nyakati tofauti na yeye Gwajima alisema kuwa Lowassa na Dr. Slaa ni marafiki zake na kati ya Lowassa na Dr. Slaa kuna mmojwapo atakuwa rais hivyo hawezi kuacha kukaa karibu na rais mtarajiwa!

Hii ya Dr. Slaa kusali kwa Gwajima ilisemwa na Ex.wa Dr. Slaa jana.. Mambo mengine ni kuunganisha nukta tu...

Kuhusu list of shame aliyesema anafanya reseach ni Dr. Slaa si Chadema...
 
Hapo unaposema Dr. Slaa amepokea mlungula bado sijakuelewa mlungula ameupokea kutoka kwa nani?

Kule mwanzo nilitahadharisha kuwa jukwaa la great thinkers lisichukue sura ya kampeni na propaganda. Kuna vitu unaandika ambavyo haviendani na hili jukwaa.
Mkuu nadhani kuna wakati tukubaliane kuwa tofauti ya mawazo inajenga. Pia tuangalie mambo kwa upana wake

Kama utamuuliza Alinda hilo swali la mlungula basi pia usiache kumjibu, kwamba, wale wanaosema EL ni fisadi wana evidence yoyote?

Mama Tibaijuka kachukua za mboga, tumeambiwa kimaadili hapaswi. Lakini je, ilikuwa ni jambo pristine?

Tumesikia ya Escrow, kamati zimeundwa. Je, unataka kusema hakuna aliyehusika kwavile tu hakuna ushahidi huo?

Yule mzee aliyegawa kutoka mabenki amefanya hivyo kwa kutumia mikataba. Lakini je, hakukuwa na mziangira ya 'rushwa'?

Point yangu ni kuwa tuangalie mambo kwa mtazamo mpana si kwa kutaka kusikia tunachotaka bali hata tusichokitaka
 
Bado najiuliza Gwajima ana interest gani na urais wa Lowassa? Imekuwaje mpaka Lowassa akamuamini Gwajima kiasi kikubwa hivyo. Dr. Slaa anasema Gwajima amemwambia kuwa Lowassa kawahonga maaskofu 30 ili wamuunge mkono, je iwapo hili ni kweli, siasa za mgombea wa namna hii zina athari gani kwa taifa?

Bado naamini kujadili vitu vyepesivyepesi badala ya mambo makubwa ni kutokulitendea haki taifa...
Mkuu , hapa nadhani hutendi haki. Umechukua kauli zisizo na uthibitisho, na sasa unataka zijadiliwe kama jambo kubwa la kitaifa

Maaskofu wameomba Dr Slaa ataje wahusika. Hili ni jambo zuri kwasababu kila mmoja angependa kujua ni wachungaji wangapi wa kondoo walioamua kuchukua vipande 'vitatu kabla ya majogoo hayajawika'

Dr Slaa alitoa kama tuhuma. Ukweli au uongo wa tuhuma bado haupo wazi hadi pale atakapotoa evidence za kuthibbtisha ikiwa ni pamoja na kutaja wahusika.

Hatuoni tatizo kwasababu kawataja akina Sumaye bila shaka.

Na hakika atalitendea taifa haki akiwataja bila huruma. Hicho ndicho kinaitwa 'boldness' iliyomjengea heshima miaka mingi

Hivyo kabla hujalifanya jambo hili kuwa kubwa la kujadiliwa kitaifa, pengine kama una evidence za maneno ya Slaa ziweke hapa.

Nakuhakishia tutajadili. Tusichokubaliana nawe sisi wengine ni kuchukua madai ya mtu na kuyafanya ukweli

Nadhani unaona tatizo la Richmond ambapo hadi leo anatafuta ukweli kwa Mwaky.

Sasa tunawezaje kuanza kujadili hili la maaskofu bila kuwa na evidence mkuu! Tungependa majina ya wachungi na kondoo yaweke hadharani
 
Back
Top Bottom