CHADEMA/UKAWA: Uwekezaji usiotabirika

CHADEMA/UKAWA: Uwekezaji usiotabirika

Tukubali tu kwamba kwa hali ilivyo sasa lolote linaweza kuzungumzwa kwa lengo la kutuliza/kuondoa athari/hasara itayatokana na kauli za Dk. SLAA jana....Mengi yatazungumzwa lakini ukweli wanaujua Slaa, Mbowe, Gwajima na Tundu Lissu

Two sides to a story right?.. sasa mbona kauli ya Lissu inawekewa mashaka na kujengewa hoja ya kuihoji?
 
Nguruvi, ukisoma vizuri kuna kitu ambacho hakijasemwa vizuri. Mazungumzo na Lowassa hayakuanza baada ya jina lake kukatwa. Gwajima alifanya kile alichotakiw akufanya na mhusika mkuu. Walijua kizuizi kikubwa kwa Lowassa kuja CDM ni Slaa, kwanza sababu ya nafasi yake (alikuwa tayari ni mgombea wao) na pili sababu ya msimamo wake ulio tofauti sana na Lowassa. Si unaona wakati mwingine hata ndani ya familia kuna mambo fulani mzazi anajua ili lifanyike lazima mzazi mwenzie ndio atoe "Ok". Hivyo, mtoto ataambiwa nenda kwa "babaako" au "mamaako" si kwamba yule mzazi mwngine hajaimbishwa bado!

Kuna watu walishaimbishwa kwa muda na ulipofika wakati akatumwa mshenga... "nenda kwa Slaa"... the rest is history.

Mzazi anayeulizwa anaweza kusema "Mamaako anajua" halafu mtoto anasema "ntaenda kumuuomba ila ukikubali najua hatakataa..." kumbe dili lilishachongwa muda!! Angalia simulizi hili kwa karibu utaona mchezo huu...

Kama ingekuwa "Mshenga" Gwajima alikuwa anafanya mawasiliano na Mwenyekiti Mbowe halafu Mwenyekiti ndio ashauriane na Katibu wake japo ningemuelewa Slaa. Lakini kwa mujibu wake yeye mwenyewe ni kwamba "Mshenga" aliwasiliana na yeye kumjulisha kwamba Lowasa "amekatwa" wafanyaje. Na yeye akaenda kumpa feedback mwenyekiti wake ili kushauriana cha kufanya.

Ndio maana niliuliza hapo awali kuwa hii "idea" ya ujio wa EL ilianzishwa na nani in the first place kati ya Mbowe na Slaa? Pili, kwa yeye kutoa "masharti" juu ya ujio wa Lowasa ina maana alikuwa "tayari" kumpokea regardless ya lundo la kashfa zinazomwandama ili mradi tu atimize masharti na pia athibitishe kuwa yeye ni "Asset" na sio "Liability".
 
Hili jukwaa la great thinkers nalo mmeligeuza jukwaa la kampeni na propaganda.

Swala la Slaa kumkaribisha Lowassa Chadema sio big deal.
Tatizo ni kumsimamisha agombee urais.

Hata kule CCM walipomkata Lowassa hawakumfuta uanachama na hata angegombea ubunge wasingemkata kama ilivyo 1995 ambapo alionekana ana upungufu wa kimaadili kwa nafasi ya urais lakini akapitishwa kugombea ubunge.

Kwahiyo sioni tatizo Slaa kumkaribisha Lowassa kama mwanachama wa kawaida kuongeza nguvu kwenye timu ya kampeni.

Kama vyama vimekubali kuungana ingawa vinatofautiana itikadi, hakuna tatizo kumkaribisha mtu mmoja. Tatizo ni mtu huyo mmoja mgeni anapopewa nafasi ya kuamua hatma ya chama.

Sikumbuki quote hasa aliyosema Dr. Slaa, lakini alimuita Lowassa Shetani or something to that nature na akihusisha na Upadiri na Ukristo wake.

Wakristo tuna kauli tunasema (tena kinafiki wakati tunajiandaa kupokea Sakramenti, lakini tuna mambo kibao kichwani na moyoni kutokana na uanadamu wetu) Namkataa Shetani na mambo yake yote na kazi zake zote....

Dr. Slaa kama alikubali kumkaribisha Lowassa hata kwenda kuongea na Mwenyekiti na wenzake, ina maana alikuwa anamkaribisha Shetani (si amemuita shetani?)

Ama kama alimkaribisha kikristo kuwa huyu ni mkosaji na tummtake atubu naye awe katika kundi la bwana, si Kamati Kuu ilimhoji Lowassa na kumweka kiti moto kwa masaa na hata wakaridhika na maelezo yake? au ni yeye Dr. Slaa pekee ambaye hakuridhika na kitubio cha Lowassa kusema mhusika na mwenye uamuzi wa mwisho alikuwa ni Rais?

Je leo Dr. Slaa anapoafikiana na Mwakyembe na Sitta kwenye kauli zao dhidi ya Lowassa, ina maana hata Lowassa angekiri vipi au kusema Richmond (let say ni ya Rostum, Brigaia wa Oman au Kikwete), bado yeye asingeamini wala kusamehe ungamo la Lowassa?

Si masuala ya ushabiki, lakini tunapojaribu kupiga hatua mbele ya jamii yenye kuwajibika, kujikosoa, na kutaka uadilifu, si uadilifu wa nafasi za kisiasa na matendo, bali hata kauli zetu zisilete utata au kuacha confusion na maswali ambayo sasa tunayauliza na kushindwa kuelewa mantiki nzima ya mkutano huu wa habari.

Kilichotokea kimeongeza na kitaongeza hisia kubwa kuwa kuna mchezo mchafu unatendeka, kuna mazingira ya watu kuhongwa na kurubuniwa na CCM, Ikulu na hata Usalama wa taifa.


Kwa maoni yangu binafsi, ni heri kauli ya Dr. Slaa ingesema nimejiuzulu siasa, sikubaliana na wenzangu kwa maamuzi ya kumfanya Lowassa kuwa mgombea pamoja na kuwa nilishiriki kumkaribisha. Ngefuata Lipumba way na kusema nafsi ilimsuta na angemalizia kuwaomba watu waheshimu maisha yake ya nyumbani na kuacha kumsimanaga yeye na mpenzi wake.

Just a thought!
 
Alinda , kumbe ni kuanzia May wapo katika maongezi. Naunganisha na ile kauli ya 'amekatwa Dodoma, tunafanyaje'

Maswali yako yanahitaji majibu kwakweli. Na majibu yapo katika ''maongezi'' kati ya May-July

Tundu Lissu amesema Dr.slaa alikuwa kwenye maongezi ya kumhusu Lowassa tangu May na tena hakuwambia viongozi wake juu ya jambo hilo.
na ukichukua maelezo ya Lissu yanaleta mantiki ya hii kauli "jamaa kakatwe" maana kama ingekuwa gafla kwa vyovyote vile Dr. Slaa angemuuliza Gwajima "ni jamaa gani unayemzungumzia? au na unaniambia ili nifanyeje? (yaani walao tungesikia kauli inayoonshea mshangao au upya wa jambo hili)
 
@Ng’wamapalala kuna hoja hapo, unaweza kutusaidia?

Pili, Alinda aliuliza haya

Je, Dr alimkaribisha Lowassa kama nani? Mgombea,mwanachama, au mtu atakayesaidia kampeni?

Mwalimu akaulizahivi ‘ Gwajima alipompigia simu Dr Slaa na kumwambia, Dodoma wamemkatatufanyeje ? Ina maana gan?

Kuna alihojia kuwa nani hasa alimwalika Lowassa kati ya pande mbili?

Ndugu yangu Nguruvi3
Nadhani ni vyema tukamuomba Dr.W.Slaa (kwasababu yeye ni mwanachama humu) aje kutudadavulia ile hotuba kipengele kwa kipengele humu ndani.
Nia kubwa tupate ile clear message aliokuwa anataka kuileta.
Inawezekana alikuwa na nia ya kufikisha ujumbe ila alikosea jinsi ya kuufikisha kwa kurukia rukia mambo.
 
Last edited by a moderator:
Sidhani kama hili ni swali sahihi; kama nijibu nadhani alilitoa mwenyewe na linaeleweka. Lakini kwamba "alimkaribisha" inadhania mambo mengi sana.

Ni kweli linaweza kuwa lisiwe swali sahihi kwa pande wako ila kwangu ni swali sahihi na ambalo ningependa kupata ufafanuzi wa Dr. Slaa au mtu yeyote anayefahamu ni sababu zipi zilizomfanya Dr. Slaa kukubali mtuhumiwa wa ufisadi hata kujadiliwa tu na chama chake? Na kwa bahati mbaya sikusikia sababu za Dr. slaa kufanya hivyo

Rejea majibu yake jinsi gani Lowassa aliomba kuingia lakini pia usisahau kuwa ushahidi mkubwa uliopo ni kuwa tayari Lowassa alishaanza dili ya kutaka kuingia CDM mapema sana kabla ya kukatwa CCM na mtu mhusika mkubwa hakuwa Slaa katika hili. Kimsingi hata kile kinachoitwa "kupitishwa" kwa Slaa kugombea ilikuwa ni geresha tu kwani kuna waliokuwa wanajua mapema dili wanalotaka kuchezewa lichezwe vipi. Slaa alikuwa ni chaguo lao la pili; chaguo lao la kwanza tunalijua sasa.

Mpaka sasa tuliowasikia ni Tundu Lissu huyu amesema kuwa Dr. Slaa alianza mchakato wa Lowassa tangu May..
Dr. Slaa anakiri yeye mwenyewe kupigiwa simu na Gwajima akimueleza kuwa jamaa kakatwa (kama nilivyoeleza huku nyumba hii sentensi ya Gwajima, ukiunganisha ni maneno ya Tundu Lissu unapta mtiririko kamili)
Na Dr. Slaa anajibu ngoja awasiliane na Mwenyekiti kwanza mpaka hapo unaona kuwa aliyempeleka Lowassa Chadema si Mbowe, si Tundu Lissu si Pro. Safari bali ni yeye Dr. Slaa. Sasa unaposema kuwa mhusika mkubwa hakuwa Slaa je alikuwa nani? Maana hapa Dr. Slaa kakiri mwenyewe kupigiwa simu na Gwajima na baada ya hapo walikutana Mwenyekti, wanasheria wa Chadema na Katibu mkuu kwa ajili ya mjadala.. wazo lilitoka kwa Dr. Slaa.

Laita kama angekuwa hataki basi angemwambia Gwajima kwa aongee na Mwenyekiti na kama Gwajima angeongea na Mwenyekti na kutokea haya yaliyotokea hapo ningemuelewa.

Penye ukweli tuseme ukweli kwa hili Dr. Slaa alisokea.. tena sana tu..
 
Nadhani hapa watu pia wanamiss ukweli mwingine; kama CDM walimpitisha Slaa mapema hivyo awe mgombea wao ni kwanini? Waliamini kuwa anawafaa kweli kweli au walifanya kama hadaa? Siyo kwamba walimpitisha kwa sababu waliamini anaweza kuwakilisha maslahi ya chama na harakati zao kwenye Uchaguzi Mkuu? Sasa watu wale wale ndani ya miezi michache wanabadili 360 halafu walitaka Slaa asimame na kusema ndio tu? Ukweli wangemkubalia pale pale aliporesign on principle.

Dr. Slaa alipigiwa simu na 'mshenga' Gwajima baada ya Lowassa kukatwa. Akamuambia inabidi waongee na Mbowe tuone itakuwaje.
Hapo tayari inaashiria ndani ya nafsi yake alimkubali lowassa.
Dr. Slaa akaitisha kikao cha halmashauri kuu kumjadili lowasa na yeye mwenyewe aje kujieleza kuhusu swala la richmond.
Tundu lissu anasema Lowasa alijieleza na akasema Richmond ni ya JK.
Kwanini hizo concern za dr slaa hazikuwa raised kwenye mkutano wa kamati kuu? Kuwa Lowasa ni fisadi na asikubaliwe Chadema?
Dr. Slaa bado hajatuambia alimkaribisha Lowasa awe mwanachama wa kawaida au agombee urais.
 
Alinda;

Pesa na madaraka yanafanya watu wasalitiane. Nimemsikiliza Dr vizuri. Na kwa maoni yangu binafsi, watu wamezidiana. Hili sio swala la kumleta Lowassa ndani ya CDM. Kuna watu wamefaidika na siku zinavyokwenda tutakuja kuyasikia zaidi.

Hilo ni kweli maana siasa za Tanzania zimekuwa biashara.. piga piga kelele, wadangaye watu kuwa unawatetea hata kama pamoja na utetezi wako maisha yao yanabaki vile vile,baada ya kufanya haya subiri wakati wa uchaguzi .Pesa inakuja yenyewe tu.. Ndivyo wanasiasa wanavyofanya siku hizi kuna wanaruka na mamilion hadi Bil inategemea na ushawishi wako kwenye jamii..Poor Tanzania
 
Nguruvi, ukisoma vizuri kuna kitu ambacho hakijasemwa vizuri. Mazungumzo na Lowassa hayakuanza baada ya jina lake kukatwa. Gwajima alifanya kile alichotakiw akufanya na mhusika mkuu. Walijua kizuizi kikubwa kwa Lowassa kuja CDM ni Slaa, kwanza sababu ya nafasi yake (alikuwa tayari ni mgombea wao) na pili sababu ya msimamo wake ulio tofauti sana na Lowassa. Si unaona wakati mwingine hata ndani ya familia kuna mambo fulani mzazi anajua ili lifanyike lazima mzazi mwenzie ndio atoe "Ok". Hivyo, mtoto ataambiwa nenda kwa "babaako" au "mamaako" si kwamba yule mzazi mwngine hajaimbishwa bado!

Kuna watu walishaimbishwa kwa muda na ulipofika wakati akatumwa mshenga... "nenda kwa Slaa"... the rest is history.

Mzazi anayeulizwa anaweza kusema "Mamaako anajua" halafu mtoto anasema "ntaenda kumuuomba ila ukikubali najua hatakataa..." kumbe dili lilishachongwa muda!! Angalia simulizi hili kwa karibu utaona mchezo huu...


Nitatolea hilo la Mzazi maana mimi ni mzazi kama wengine humu ndani..

Mtoto anapotaka kitu kutoka kwa baba, na baba akamwambia kamuulize mama yako kwanza.

ni kwa vile baba na mtoto wanafahamu kuwa msimamo wa mama utakuwa ni HAPANA..
ndio mama mtoto akakimbilia kwa baba na kwa vile baba hataki kumkasilisha mtoto wake,(kwa kumwabia hapana) na pia hataki kuingilia uratibu wa mama anamwambia huyu mtoto "kamuulize mama"

Sasa basi kuna mawili mtoto hasiende kuuliza maana anafahmu kuwa kwa mama ni hapana hata akiuliza hakuna jipya, au mtoto ajitutumue ajaribu bahati yake kwani kuna siku mama umuonea huruma na kumruhusu.

Ikitokea mama akapomruhusu mtoto kufanya jambo ambalo na likaleta madhara fulani hawezi kutupia lawama baba bali kwake yeye mwenyewe.. Hivyo basi hili zigo ni la Dr. Slaa labda kama kuna kitu ambacho alikifcha katika maongezi yake.
 
'UZA UWAPE MASIKINI UNIFUATE' Ushahidi wa Richmond EL anaujua 100%, angeusema. Ndio u-asset wake kwa CDM, laa ni upuuzi.
 
'UZA UWAPE MASIKINI UNIFUATE' Ushahidi wa Richmond EL anaujua 100%, angeusema. Ndio u-asset wake kwa CDM, laa ni upuuzi.

Autoe ushahidi kivipi kwa hio 100% ndio awe asset? Si amekwishamtaja aliseidhinisha Richmond kuwa ni bosi wake? Mlitaka aseme nini zaidi?

Na vipi hao walio na nyaraka za ushahidi ambazo wamekuwa wakitamba nazo mtaani kwa miaka 8 bila chombo chochote cha dola kuchukua hatua kushitaki wahusika? Nyaraka za ushahidi zipo kigugumizi cha nini?
 
Alomleta Lowassa Chadema siwezi kumjua zaidi ya mhusika mwenyewe isipokuwa nasema hawezi kuwa Dr.Slaa kwa maelezo ya Tundu Lissu kwa sababu katika maelezo yake uongo umejitenga wazi kabisa..

1. Mimi nilipokuwa Bongo mwezi November na December mwaka jana nilipata habari hizo sikutaka kuzizungumza hapa kijiweni kwa sababu zilikuwa tuhuma tu. Miezi ilivyopita nikasikia habari mpya kuwa ataenda ACT sio Chadema na ndiye mfadhili wa safari zao.. Nikayaacha kama yalivyo nikisubiri UKWELI ni upi.

2. Hapa hapa JF ilikuwepo mjadala kuhusu Lowassa kuhamia Chadema toka mwaka 2011 kama hatachaguliwa CCM tukazipuuza kwahiyo haikuwa habari mpya. Lissu anaposema kwamba ni Dr.Slaa aliyemleta Lowassa ni uongo kwa sababu nyingi tu za msingi na nimezisema hapo nyuma. a) Haiwezekani mtu alochaguliwa kugombea Urais na kamati kuu ama baraza kuu ajichukulie maamuzi binafsi ya kumtafuta mtu mwingine nje ya chama aje kugombea badala yake hali yeye kisha pitishwa! - Haiwezekani.. Hata wewe leo hii ukichaguliwa kuwa mbunge wa Ilala na umepitishwa huwezi tena kufanya maajabu aloyasema Tundu Lissu na zaidi ya hapo Dr.Slaa na Lowassa ni Mbwa na Chatu! Ningekubali tu kama Tundu Lissu angesema Dr.Slaa amechukia baada ya Kamati ya Chadema kumchagua, lakini ujio wa Lowassa tulimwambia akae pembeni Lowassa atasimama badala yake..

3. Muda aloutaja Tundu Lissu kwamba Dr.Slaa ndio alituma ujumbe, wakati huo Lowassa alikuwa bado hajatoswa CCM, Lowassa alikuwa tumaini la wajumbe wengi wa CCM kuliko mgombea mwingine yeyote na hata yeye mwenyewe alijua atashinda na hakuna wa kumzuia, leo iweje akubali mazungumzo ya kuhamia Chadema hata kabla ya uchaguzi wa ndani wa CCM? Kisha kwa sisi tunaomjua Lowassa huyu mtu ana guts za ajabu, anajiamini kupita kiasi na kwamba anachokifikiria ni lazima kipatikane kwa nguvu zozote zile. Kutoswa CCM ilikuwa pigo kubwa sana ambalo hakulitegemea kabisa. Lowassa alikataa ushauri wa wapambe wake ndani ya CCM kuweka Plan B ikiwa ataenguliwa. Na ndivyo alivyoingia UKAWA akaweka masharti kaa atajiunga Chadema awe mgombea na pasipo ushindani. hili ndio mimi nadhani lilowaondoa Dr.Slaa na Lipuymba UKAWA..

Ni hayo tu... siwezi kwenda taratibu mahala ambapo mnataka kunibana katika jambo ambalo hata nyie wenyewe hamjui nani alomleta Lowassa isipokuwa kwa kuwasoma waongo, wafitini wenye kuwa na kila sababu kila jambo bana wanapolifanya. Uongozi wa kamati kuu Chadema wamekuwa na maamuzi mabaya sana na haya yote yanatokana roho mbaya za vaadhi ya viongozi wenyewe.



Ukishaanza mipasho hapo ninakuwa sina la kukusaidia zaidi ya kukuignore kama nifanyavyo kwa wengine..

Si kwamba mipasho, kejeri au matusi siwezi bali ni kwa vile hayo nimeishayavuka.. Njoo kivingine tujadiliane.. Huu ni mjadala si ugomvi na wala hatutafuti mshindi.. bali tunapanuana mawazo na kujifunza mambo mbali mbali kutoka wa watu mbali mbali...
 
Mkuu Mwalimu, katika Uongozi kuushuhudia ukweli ni KUUWAJIBIKIA. Katika hlo si wao wala ninyi, Bure! Ole wake mnyonge.
 
Last edited by a moderator:
Michango inayoendelea iko very interesting japo naona kuna maswali kama ya nani hasa alimleta Lowasa hayatakaa yapate majibu ambayo common sense inayakubali. Majibu ya Lissu, kuna mchangiaji mmoja kakumbushia Mchungaji Msigwa nae alisema on live television kuwa anafanya kazi na Slaa kuhusu hili suala. Yote kwa undani wake yananipa mimi picha moja, ukweli na owongo umechanganywa sana katika hili suala. Msingi mzima wa Lowasa kuja UKAWA ulikuwa umejengwa kwenye ULAGHAI. Viongozi kufanya ulaghai kwa viongozi wenzao, na waathirika wakubwa ni wanachama wakawaida kwa sababu inavyooneka viongozi waliolaghai viongozi wenzao na viongozi waliolaghaiwa na viongozi wenzao wote wanakuja kuwalaghai wanachama wao. Ulaghai juu ya ulaghai.

Ila kuna logic moja bado inasumbua akili yangu kuielewa. Lets assume (for the sake of sense) kuwa haya ni kweli;
  • Slaa huyu tayari alikuwa ameshapitishwa na chama chake ila yeye mwenyewe akakataa kutangazwa kwa sababu alitaka mbwembwe kwa mujibu wa Mbatia
  • Slaa huyu ambaye siku zote amemtreat Lowasa kuwa ni mortal enermy kama yanavyotuambia matukio ya kihistoria
  • Slaa huyu huyu alikuwa na mazungumzo na Lowasa ya kumleta CMD tangu mwezi May bila viongozi wake kujua kwa mujibu wa Lissu
  • Slaa huyu huyu alilala kwenye gari kwa sababu mkewe "first lady" alimtupia virago kwa sababu ya hili sakata la Lowasa
  • kuwa Slaa huyu huyu ndio alimkaribisha Lowasa as "suggested" by phone call ya "mshenga" Mch. Gwajima huku akijua wazi Lowasa anachotaka ni Uraisi ambao yeye tayari ameshachaguliwa na chama chake kugombea
  • Na baada ya yote hayo Slaa huyu huyu akajiuzulu ukatibu mkuu wake kwa sababu ya Lowasa wakati wa mazungumzo ya kumjadili lowasa.
  • Hapo kuna report zinazosema kuwa Lowasa alishawaengage CDM toka December mwaka jana kuhusu hatima yake ya uraisi (I wonder who was engaged hapa)

Jamani hivi vitu vinaowana kweli? Je, kwa power struggle inayokuwa inaendelea CCM, huku CDM ni katibu mkuu peke (bila viongozi wake kujua) aliyekuwa anapay attention ya kile kilichokuwa kinaendelea?

Kaazi kweli kweli.
 
Kwanini ni Dr.Slaa tu ndio wakuwekwa mtu kati kwanini isiwe Mbowe, Mbatia na Lissu kama bado ni wanasiasa wa kuaminiwa na kama kweli Lowassa wanamtumia kwa sababu ya mabadiliko au wana motives tofauti.

The Alibi so far on what is going on.

Prof.Lipumba
Huyu ndio wa kwanza kujitoa katika uongozi wa UKAWA kwa madai ya kuwa agenda imebadilika na vilevile dhamira inamsuta. Dhamira gani? tunajua wagombea wa uraisi wa UKAWA walikaa na kukubaliana ya kuwa Dr.Slaa ndio atapepea bendera. Hili Lipumba alilisema hadharani na Mbatia amelirudia. Kwa hivyo through series of events Dr.Slaa awezi kupokewa au kujadiliana na UKAWA kuwa mgombea wao kama CDM walikuwa awajampitisha bado.

Kwanini sasa Lipumba aondoke ghafla wakati ndio mtu aliyeandika waraka wa kumpokea Lowassa mara alipoingia kwenye mkutano wao, waraka uliosomwa na Mbatia. Ina maana mpaka dakika hiyo maamuzi ya kuwa Lowassa atakuwa mgombea wa UKAWA yalikuwa bado ayajaamuliwa na pengine maelewano ilikuwa support yake tu ndio wanayo itaka. This is the only reason why Lipumba left baada ya Lowassa kupewa unahodha wa kambi.

Dr.Slaa
Nilikuwa tayari nimeshapitishwa na chama kuwa mgombea wao kwa taratibu za ndani; kilichobaki ina maana ni ilikuwa ni public appearance tu. Jumlisha na facts za kuwa kulikuwa na mgogoro mkubwa sana kupata mgombea wa UKAWA ambao ilibidi watu watoke Dodoma na wakae mpaka saa tisa za usiku ina maana Dr.Slaa nayeye alikuwa tayari keshajiandaa kugombea uraisi pia. Kwa vyovyote vile ujio wa Lowassa kwa Dr.Slaa ni mkakati wa kuivuriga CCM kwenye campaign zake kwakuwa aliahidi kuja na wafuasi na kulikuwa na some elements of that based on his nomination campaign support aliyokuwa nayo CCM ilikuwa ni dhahiri mpaka wanachama kuimba nyimbo za kukosa nidhamu ndani ya kikao chao baada ya kukatwa kwa Lowassa.

Tundu Lissu
Dr.Slaa alishapitishwa na vikao halali vya chama kuwa mgombea wa chama chetu kwa nafasi ya uraisi. Inathibitisha zaidi by now Dr.Slaa alijua ya kuwa yeye ni mgombea tayari na ujio wa Lowassa usingeweza tengua hilo ata kama huku pembeni alikuwa anaongea na Gwajima kuhusu Lowassa sidhani kama lengo ujio wake uwe kwa sababu ya uraisi.


Baada ya hizo events nadhani kilichofuata ni hiki kutoka kwa timu ya Lowassa kwa kuitazama safu ya watu walio CDM
especially kama walianza kumfuata wakati bado yuko kwenye campaign za kuwania uongozi kupitia CCM.
"Churchill: "Madam, would you sleep with me for five million pounds?" Socialite: "My goodness, Mr. Churchill... Well, I suppose... we would have to discuss terms, of course... "
Churchill: "Would you sleep with me for five pounds?"
Socialite: "Mr. Churchill, what kind of woman do you think I am?!"
Churchill: "Madam, we've already established that. Now we are haggling about the price"
Ukiangalia tu historia yake ya kutoa vibaasha sidhani kama anawapa viongozi kwa sababu ya kura moja zao, bali anajuwa wanamakundi ya wafuasi wenye uwezo wa kumpa kura nyingi tu. Kwenye ethics wanasema uwezi defy nature ya kitu viumbe vinatabia ya kurudia mambo yaleyale given the challenge or circumstances.

Je iliwezekana vipi Lowassa kupitishwa kuwa mgombea wa CDM na UKAWA kitendo kilichopelekea prof Lipumba kuacha uongozi maana hata kama CDM walimptisha surely Lipumba utegemei nayeye akubali kirahisi kwa sababu tunajua kwa Dr.Slaa tu ilichukuwa alot of convincing from his other leaders kukubali. Na kwanini CDM ilivunja kanuni zake za ndani maana Dr.Slaa walishamteua kususa kwa Dr.Slaa sidhani kama ni kwa hoja zake tu bali kutolewa kwenye position aliyokuwa keshapitiwa na chama chake pamoja na viongozi wa vyama vingine.

Tukirudi kwenye nature ya Lowassa kwanini tusiamini hakutumia tena vibaasha vyake kununua viongozi wa UKAWA kupata support ya watu wao ili kuendeleza ndoto yake ya uraisi; je hii ndoto inaendana na vision ya UKAWA.

If you ask me there is no historical evidence to back that claim kwamba Lowassa anamapenzi na upinzani ni ndoto zake tu za uraisi na kwa njia zilezile anazotumia ndio zimemfikisha kileleni upinzani pia, why should anyone believe akiukwaa uraisi atabadilika wakati all the evidence points otherwise.

Sielewi kwanini watu amumuoni huyu mtu for what he is na jinsi gani Mbowe, Mbatia, Lissu jumlisha na Sharif Hamad walivyokuwa si watu wa kuaminiwa. Mimi bado namueshimu sana Dr.Slaa na Prof.Lipumba ndio watu pekee walio na morals ata kama walibariki ujio wa Lowassa sio kwa sababu ya kuuza nguvu zao pia na kuwapa mafisadi platform nyingine. Huyo Mbowe ndio kabisa hana loyalty yaani kejeli za jana kwa Dr.Slaa sikuamini kama anaweza rusha vijembe vya namna hile inawezekana ata Dr.Slaa alikuwa anamtumia pia kuongeza wabunge na ruzuku ya chama.
 
Sikumbuki quote hasa aliyosema Dr. Slaa, lakini alimuita Lowassa Shetani or something to that nature na akihusisha na Upadiri na Ukristo wake.

Wakristo tuna kauli tunasema (tena kinafiki wakati tunajiandaa kupokea Sakramenti, lakini tuna mambo kibao kichwani na moyoni kutokana na uanadamu wetu) Namkataa Shetani na mambo yake yote na kazi zake zote....

Dr. Slaa kama alikubali kumkaribisha Lowassa hata kwenda kuongea na Mwenyekiti na wenzake, ina maana alikuwa anamkaribisha Shetani (si amemuita shetani?)

Mkuu,
Kuna bandika moja nimesema tunapozungumzia demokrasia sijui tunaanisha nini. Japo kuwa naamini zaidi kwenye misingi ya dini, lakini hawa watu hawapiganii dini. Wote wanashindana kwenye demokrasia. Hata Slaa akimuita Lowasa majina gani yanayohusiana na dini yake, hili suala linalozungumziwa hapa si la kidini. Ni suala la kisiasa, na siasa katika hii inafanywa kwa demokrasia. Kumuita mtu shetani sio hoja ya kidemokrasia kumzuia mtu kujiunga na chama. Hakuna hoja hapa. Sijaribu kumtetea Slaa ila nadhani hizi sio hoja za msingi.


Je leo Dr. Slaa anapoafikiana na Mwakyembe na Sitta kwenye kauli zao dhidi ya Lowassa, ina maana hata Lowassa angekiri vipi au kusema Richmond (let say ni ya Rostum, Brigaia wa Oman au Kikwete), bado yeye asingeamini wala kusamehe ungamo la Lowassa?

Mi nimeingalia ile press mara mbili na kusoma zile points za summary. Huku kusema Slaa ameafikiana na Mwakyembe na Sitta sio sahihi kabisa. Katika press yake alichofanya ni kufanya reference ya vile vilivyosema na hao jamaa recently on a topic that he was talking about. Huko ndio kuafikiana jamani?

Kwa maoni yangu binafsi, ni heri kauli ya Dr. Slaa ingesema nimejiuzulu siasa, sikubaliana na wenzangu kwa maamuzi ya kumfanya Lowassa kuwa mgombea pamoja na kuwa nilishiriki kumkaribisha. Ngefuata Lipumba way na kusema nafsi ilimsuta na angemalizia kuwaomba watu waheshimu maisha yake ya nyumbani na kuacha kumsimanaga yeye na mpenzi wake.

Watanzania wako entitled to all the information right now. We need informed voter. Sikupenda kabisa Slaa alivyosema eti ana silaha zingine anaziweka pembeni anasubiri majibu. Kama ambavyo sikupenda Lipumba alivyoondoka uwenyekiti na kisababu kimoja tu nafsi inanisuta. Inakusuta kitu gani?? Hii miwili yote ni mifano ya watu ambao wameficha information. Nashangaa kumsifia Lipumba halafu kumuona Slaa amekosea wakati wote katika KIPENGELE HIKI wamefanya makosa yale yale. Hawakuweka wazi infomation zote walizonazo ili voters watake advantage ya hizo information kufanya maamuzi.

We are so afraid of controversy and yet we want competitive politics zituletee viongozi bora. HOW???
 
@Ng'wamapalala kuna hoja hapo,unaweza kutusaidia?

Pili, Alindaaliuliza haya
Je, Dr alimkaribisha Lowassa kama nani? Mgombea,mwanachama, au mtuatakayesaidia kampeni?

Mwalimuakaulizahivi ' Gwajima alipompigia simu Dr Slaa na kumwambia, Dodomawamemkatatufanyeje ? Ina maana gan?

Kuna alihojia kuwa nani hasa alimwalika Lowassa kati ya pande mbili?
Jibu la swali kamba Dr alimkaribisha Lowassa kama naninadhani linapatikana kutoka kwa maelezo ya Slaa mwenyewe kasema "kiongozi ambaye anaenda kuwa raisi wa nchil azima awe na wafuasi nyuma yake" akaendelea kusema… "anakuja peke yake au anawafuasi wa kutosha nyuma yake? Na wafuasi hao wa aina gani?"

Kwa swali la pili Dr Slaa katumia neno ambalo linanifanya niamini kauli zinazosema kwamba mazungumzo ya Lowassa kwenda UKAWA/Chadema yalianza kabla, Slaa kasema (Gwajima) alimpigia simu akiuliza kwamba "sasa kule Dodoma mambo yameshaiva nini kifuate?" DR Slaaa kamjibu kwamba anaomba wawasiliane na Mbowe. Nilivyoelewa hapa inamaanisha kwamba kulikuwa tayari kuna mazungumzo yanaendelea kuhusu Lowasa kuingia chamani, sina uhakika nani alianzisha mazungumzo hayo ila maelezo ya Slaa yanaonyesha alikuwa anafahamu hayo mazungumzo, walikuwa wanasubiria Lowassa akatwe wasonge mbele, hiii ina shabihiana na maelezo ya Mbowe wakati anamkaribisha Lowassa kamatikuu, na maelezo ya Lissu.


Slaa amesema mwenyewe kwamba hakukatwa, jina lake lilipitishwa lakini hakutangaza, na hakuchukua fomu, ila hajasema kama alikubali hiyo nafasi au aliikataa

Slaa anasema alipouliza kuhusu mitaji anayokuja nayo Lowassa jibu la kwanza walilopewa tangu siku ya kwanza kwenye tarehe 12 July nikwamba Lowassa ataenda na watu wabunge wanaomaliza muda wao wasiopungua 50,wenyeviti wa mkoa 22 na wa wilaya 88 Slaa kasema "na mimi nikakiri kama nihivyo kutakuwa na tetemeko la nchi" then akaeleza jinsi alivyo subiri masharti kutekelezwa hadi tarehe 27 pasipo mafanikio

Ninachojiuliza ni kwamba hawa wenyeviti wa wilaya namikoa walikuwa wapokelewe CDM kama nani? Je wangepewa nafasi za kugombea ubunge? Kama ndio nini kingetokea kama wangeshindwa kwenye kura za maoni? Sidhani kama watu wangeacha nyazifa zao na ajira zao kwenda cdm bila kuwa na uhakika wahatma yao unless chadema ina upungufu mkubwa wa viongozi wa mikoa na wilaya

Kuna swali limekuwa likiulizwa, nani kagharimia pressconference ya Slaa? kama Chama tawala kimeshiriki kwa namna yoyote kugharamiapress conference ya Dr Slaa kusema aliyoongea basi ni kofi la uso kwa umma wotewa watanzania wanao unga mkono upinzani
 
na ukichukua maelezo ya Lissu yanaleta mantiki ya hii kauli "jamaa kakatwe" maana kama ingekuwa gafla kwa vyovyote vile Dr. Slaa angemuuliza Gwajima "ni jamaa gani unayemzungumzia? au na unaniambia ili nifanyeje? (yaani walao tungesikia kauli inayoonshea mshangao au upya wa jambo hili)
''Amekatwa Dodoma tunafanye? Nikambiwa subiri niwasiliane na mwenyekiti''
Alinda tunakwenda?Jibu ,ngoja nifunge mlango. Bila mawasiliano yoyote kabla!!!
 
Back
Top Bottom