CHADEMA/UKAWA: Uwekezaji usiotabirika

CHADEMA/UKAWA: Uwekezaji usiotabirika

^1

Hivi Tanzania ufisadi umefanyika katika swala la Richmond tu?

Halafu kitu ambacho sijapata ufafanuzi wa kutosha ni Richmond (ufisadi wa Lowassa) ilizaa Dowans na Dowans ni mkataba wa kifisadi lakini mpaka sasa serikali inaendelea kulipa Dowans pamoja na kujua kuwa Dowans imetokana na Richmond ambayo ni ufasadi wa Lowassa.. Sasa swali ambalo hata wewe nafikiri utakuwa nalo kichwani Je kwanini serikali iendelee kulipa Dowans hali wanafahamu ni mkataba wa kifisadi na ulitoka kwa fisadi Lowassa? Hiki kigugumizi cha nini?

Swali la pili hivi Tanzania tatizo la ufisadi ni Richmond tu? Kama kuna matatizo mengine ambayo ni makubwa zaidi ya Richmond tena ambayo hata Magufuli anahusishwa, ni kwanini haya hayaongelewi linaloongelewa ni Richmond tu?
Je hatufahamu kuwa katika wizara ya Ujenzi bil.265 zimetoweka bila maelezo yeyote?

Na je tunamaelezo gani kuhusu nyumba za serikali pamoja na kuuzwa kwa bei ya kutupwa lakini nyingine ziligawiwa kwa nyumba ndogo?

Tunapojadili ufisadi wa Lowassa ambaye ni mgombea rais kupita Ukawa, basi tujadili hata ufisadi wa Magufuli ambaye ni mgombea urais kupitia CCM.. hama sivyo tutakuwa tunapendelea upande mmoja na upande wa pili kuufanya kuwa mtakatifu wakati sivyo..

Kweli LOWASA amebadilisha wengi,kwa kisingizio cha mabadiliko.. ETI watu wanauliza eti ufisadi ni RICHMOND tu,kwahiyo ndio nini,ugeugeu ni usaliti
 
Mwalimu,

Nilikuwa sijaona hii reply yako. Sijui kama umenielewa nilivyosema Slippery Slope. Namaanisha haya mambo ya kusema mambo yenye national interest yameongelewa ndani ya kamati kuu wamekubaliana bila kutoa specific details ni mteremko wa kuteleza sana. Hiyo ndio tabia ya CCM inayokataliwa sasa hivi. Wamefanya hivi kwenye mikataba mbali mbali, hawataki kutoa details za content ya mikataba wanaishia tu kusema tumesaini mkataba!

Nikisema majibu hayaridhishi ni kweli kuwa hayaridhishi and that is being fair to both sides kwa sababu hiyo ni FACT. List of Shame haikutangazwa kwenye kamati kuu. Iitangazwa hadharani, kujisafisha toka kwenye list of shame ni lazima kufanyike hadharani. Kama kweli kuna hard evidence Lowasa ametoa to convince kamati kuu kwa nini isiwe wazi tuachane na hizi mambo ya Lowasa na Richmond ibaki CCM na Richmond. Ugumu uko wapi kwani??

Haya mambo yanakuwa repeatative mpaka yanachosha. Point sio kuwa Lowasa anachukiwa sana na wenye maoni kama yangu, HAPANA. Tatizo CCM bado kuna mafisadi wengi sana, hii ya Lowasa bila kuhojiwa inaset a loop hole huko mbeleni watu wezi waachie tu kwa sababu wamejieleza kwenye kamati kuu bila kutoa maelezo ya maana nini hasa kimesemwa huko kamati kuu. Na huko kamati kuu kuna watu sio malaika. Jamani kwa nini hamni lioni hili suala!

Wanasema "The End, justify the Means"! But in politics there are no Ends, there are just Means. Watanzania tuwe makini, we are setting precedence kwenye serikali ijayo on how mafisadi wa EPA, Meremeta, Escrow etc will be dealt with!! Again SLIPPERY SLOPE.

Unafikiri mahali muafaka pa kujisafisha dhidi ya tuhuma za ufisadi ni jukwaani na sio kwenye vyombo vya sheria?

Na hii ndio shida tuliyo nayo watanzania. Kashfa ya Richmond imekuwa ni gumzo kwa miaka 8 kwa sababu tumekuwa ni watu wa kupiga makelele tu majukwaani halafu inaishia hapo! Vyombo vya dola (DPP, Polisi, TAKUKURU, etc..) hawajachukua hatua yoyote kwa miaka 8 huku watu wakiendelea kupiga kelele mtaani kuwa na "nyaraka" za ufisadi za Lowasa! Yeye mwenyewe ameshasema mwenye ushahidi dhidi yake aende mahakamani mbona mpaka sasa hakuna aliyekwenda ikiwamo Dr Slaa mwenyewe?

Leo hii naweza kwenda kwenye press nikakutuhumu wewe Galaxy S3 kwamba ni mwizi na nina nyaraka, halafu nakwambia kama unabisha njoo ukanushe ili niibue madudu zaidi (tishia nyau). Vyombo vya dola vinafanya kazi gani?
Na huu ndio utamaduni wa hovyo tuliojijengea kuwa ni watu wa kupiga kelele majukwaani huku wenye wajibu wa kuchunguza na kushitaki wakiwa likizo ndio tunapaswa kuupiga vita kabisa.
 
Kweli LOWASA amebadilisha wengi,kwa kisingizio cha mabadiliko.. ETI watu wanauliza eti ufisadi ni RICHMOND tu,kwahiyo ndio nini,ugeugeu ni usaliti
Nadhani hujawaelewa hao wanaosema hivyo.

Hoja yao ni kuwa , je, tukizungumzia Richmond hilo ndilo tatizo pekee la ufisadi lililopo nchini?


Hawajasema Richmond si tatizo, wameuliza, je, hilo ndilo tatizo pekee la ufisadi tunalodhani ndilo taifa linapaswa kupigana nalo?

Wengine wameuliza vile viporo vingine vipoje?

Hapa unapaswa kuelewa dhana na maana ya swali bilakuwahukumu hao unaowasema kabla ya kuwaelewa

Nadhani hili tumeshaiongelea hapo juu kwa undani ili listuondoe katika kiini cha mada kama alvyosema GalaxyS3
 
Last edited by a moderator:
Bavaria,

Ukipata bunge jingine ya "Wanaokubali, waseme Ndio" NDIYOOOOOOOO , ukaja kulalamika hapa. Ntakuja kukumbusha uhai ukiwepo mungu akipenda. It begins with you.

GalaxyS3
Nadhani hujanielewa ninacho maanisha.
Mimi binafsi napenda mfumo kama unaosema. Ila kwa Tanzania ninayoiona sidhani kama itatokea kwasababu mtu hawezi kusema anamchagua Lowasa kuwa rais na masabauri kuwa mbunge. Hilo haliwezekani kabisa.
Watanzania wanachagua chama hawachagui mtu, hata huyo mtu ameleta hoja kubwa kiasi gani.
 
Alinda,

I think you are missing the point here. Hakuna mjadala wa kusema eti Lowasa ndio fisadi peke kwenye nchi hii, wala hakuna mjadala wa kuwa Dowans, Meremeta, Escrow, EPA, kuuza nyumba za serikali sio ufisadi. Au kuwa upi ulikuwa ufisadi mkubwa zaidi. Sidhani kuwa kuna anaesema hivyo, atleast i know i am not saying that. Ukiwa katika kundi la kunguru halafu ukajitangaza kuwa wewe ni njiwa lazima utegemee watu watakao uhoji huo u'njiwa wako. Sasa ukiianza kujitetea kwa kuwauliza mbona hamuwaulizi wale kunguru wengine kama vile unaonewa unakuwa unatia mashaka kwenye huo u'njiwa wako unaouhubiri.

Leo hii Magufuli akijidai kuibuka na kusema eti zile nyumba alipata amri toka juu, nae pia atakuwa kikaangoni kama alivyo Lowasa. Nasikitika kuwa kwenye mjadala huu unataka kujadili ufisadi wa Magufuli, labda kama sijaelewa huu mjadala unahusu nini au somehow ume evolve into something else completely. Huu mjadala unasema CHADEMA/UKAWA na uwekezaji usiotabirika. Naelewa ni kwa sababu gani issue ya Dr. Slaa imekuwa valid kuongelewa humu kwa sababu yeye ni matokeo ya mwanzo kabisa ya huo uwekezaji unazungumziwa.

Dada angu labda uniambie unataka tu uwasikie wadau wakimkaanga Magufuli na madudu yake, lakini sidhani kama ndio mada hasa inayozungumziwa hapa. Nimeona sehemu umemshauri Nguruvi aanzishe mada ya kuwalinganisha Lowasa na Magufuli kwenye uchaguzi huu, sasa kwenye huo mjadala wadau wakiendelea tu kuongelea Richmond bila kusema hivyo vingne na mimi ntaungana na wewe kukemea huo ubaguzi wa kihoja.

Nimesema hivi kama Richmond ilizaa Dowans kwa maana hiyo Richmond na Dowans ni mikataba ya kifisadi, na haya maneno yanasemwa na serikali (Serikali nikiwa na maana ya Dr. Mwakyembe na Sitta ambao ni mawaziri tena ni wanasheria)

Sasa swali langu kwako au kwa mtu yeyote yule ni kama Richmond ni Lowassa ambayo ilizaa Dowans, Dowans inalipwa mamilion ya shilingi je ni kwanini serikali isisitishe mkataba wa Dowans na kuwachukulia hatua viongozi wote waliohusika na mikataba hewa hiki kigugumizi ni cha nini?

Ningeomba kupata ufafanuzi kutoka kwako....

Swala la Magufuli na nyumba, halihitaji mpaka Magufuli aibuke na kusema hivi au vile kunahitaji mimi na wewe kuhoji ni kwanini aliuza nyumba kwa bei ya kupwa na ni kwanini walihonga nyumba hizo kwa wake zake na wadogo zake? na si nyumba tu kuna hata bil 265 zimepotea katika wizara ya ujenzi, kuna kivuko kibofu cha bil.8 haya ni mambo ambayo hatuwezi kusubiri mpaka Magufuli kuibuka na sema maaana hawezi kuyasema bali ni wajibu wangu mimi na wewe kuhoji na kupata majibu kutoka kwake.

Na kama ndvyo kwa tusubiri mtu mpaka ibuke ndio tumuweke kikaangoni, Je kama Lowassa angekaa kimya inamaana hili Richmond lingepita tu bila kuhojiwa?
 
Mkuu Bavaria nadhanimuhimu ni kubadili mind set za watu.

Nakubaliana na GalaxyS3 kuwa lazima watu watambue umuhimu wa viongozi wao pale walipo


Kama unadhani haliwezekani labda ungejiuliza lini katika historia ya nchi hii mawaziri wakuu wawili wameondoka chama tawala? Kwanini unadhani ni impossible na lini unadhani utakuwa mwanzo wa kubadilika kama si leo hii?

Labda iwe chaguzi zijazo mkuu.

Mawaziri wakuu kuondolewa madarakani ni sehemu ya kuwajibishwa na bunge.

Je, hao wabunge kwanin hawakumuwajibisha rais wa nchi kwa tuhuma za ufisadi?
 

..msamehe tu.

..kama uliweza kumsamehe Lukuvi, why not Lowassa?

..Magufuli naye ana rekodi ya kuongea kilugha kwenye shughuli za kiserekali. Je, hakuna mushkeli hapo?

..ushauri wangu ni kwamba tujikite kwenye sera na ilani za wagombea.
 
Last edited by a moderator:
..msamehe tu.

..kama uliweza kumsamehe Lukuvi, why not Lowassa?

..Magufuli naye ana rekodi ya kuongea kilugha kwenye shughuli za kiserekali. Je, hakuna mushkeli hapo?

..ushauri wangu ni kwamba tujikite kwenye sera na ilani za wagombea.
Wapi na lini nilimshamehe Lukuvi? najua sasa hivi hamuwezi kuona makosa ya Lowassa kwa mahaba nadhani baada ya uchaguzi tutakumbushana hizi kauli za kuomba kura Kanisani.
 
Wapi na lini nilimshamehe Lukuvi? najua sasa hivi hamuwezi kuona makosa ya Lowassa kwa mahaba nadhani baada ya uchaguzi tutakumbushana hizi kauli za kuomba kura Kanisani.

..mbona Magufuli naye amesema aombewe?

..tangu anachukua fomu Magufuli amekuwa akisema aombewe.

..kwanini hukulalamika wakati huo, unalalamika sasa hivi?
 
Mkuu mnashangaa nyie lakini mimi hainishangazi kabisa. Na najua watu watasema mimi mdini lakini ndio hali halisi (Reality) na ndivyo Edo alivyo. Hakuomba aombewe tu ila kasema ni zamu ya Warutheli na ndio kauli yake!..Wengi wanamsikia tu hawajui ya Nigeria na Ujarumani..

Kama aliweza kurudisha shule na Hospital zilizojengwa na Mkoloni Mjarumani mikononi mwa kanisa lake atashindwa nini? Yeye Mrutheli, Mbowe sijui, Mtei sijui, Wakaskazini wengi sijui...kwa nini anapewa support kubwa hivyo sijui!. Panapofuka moshi kuna moto! Mimi ningependa tu kujua huyu Gwajima Askofu mzima ameingiaje katika uongozi wa Chadema au UKAWA hadi awe mshauri na msemaji wao?

- Unategema nini kitaandaliwa hapo? Nimeandika haya najua yatakuja mashambulizi ya hali ya juu kwa sababu watu hawatazami reality, wanataka kudanganyana na bikra ya ndimu! Udini upo mkuu wangu na hautakwisha kirahisi...
 

Nimesikiliza clip yote sijaona alipoomba kura, nimesikia anaomba aombewe, labda kama nime miss habari kamili
 
..mbona Magufuli naye amesema aombewe?

..tangu anachukua fomu Magufuli amekuwa akisema aombewe.

..kwanini hukulalamika wakati huo, unalalamika sasa hivi?

Jokakuu;

Hayo mambo ya kuombewa ni kitu cha kawaida. Kwenye clip hii hapa anasema toka nchi iundwe nchi haijawai kuwa na rais mrutheri. Anasema Nyerere alikuwa mkatoliki, Mkapa alikuwa mkatoliki. Awe wanahusiana vipi na yeye kuombewa?

https://igcdn-videos-b-5-a.akamaihd...6-16/11936206_512395512258265_863362784_n.mp4




https://igcdn-videos-b-5-a.akamaihd...6-16/11936206_512395512258265_863362784_n.mp4
 
..mbona Magufuli naye amesema aombewe?

..tangu anachukua fomu Magufuli amekuwa akisema aombewe.

..kwanini hukulalamika wakati huo, unalalamika sasa hivi?
Kwa faida ya Wanaukumbi unaweza kutuwekea audio au video clip ya Magufuli akiomba kuombewa Kanisani ili ashinde urais kama Mkatoliki?

Halafu mimi silalamiki naeleza hali halisi na video clip hiyo hapo.

Mkuu naona unafunika kombe.....
 
Nimesikiliza clip yote sijaona alipoomba kura, nimesikia anaomba aombewe, labda kama nime miss habari kamili
Hamna tatizo mtu yeyote kuombewa haya maneno mbona ujayasema.

Anasema toka nchi iundwe nchi haijawai kuwa na rais MRUTHERI, Anasema Nyerere alikuwa mkatoliki, Mkapa alikuwa mkatoliki, mkuu hayo ndiyo maombi?

Kama mgombea urais anakwenda Kanisani na kuomba aombewe awe rais na kusema sasa hivi zamu ya MRUTHERI halafu watu wanakaa kimya daah!! Sijui zamu ya Wasabato lini.
 
Mkuu mnashangaa nyie lakini mimi hainishangazi kabisa. Na najua watu watasema mimi mdini lakini ndio hali halisi (Reality) na ndivyo Edo alivyo. Hakuomba aombewe tu ila kasema ni zamu ya Warutheli na ndio kauli yake!..Wengi wanamsikia tu hawajui ya Nigeria na Ujarumani..

Kama aliweza kurudisha shule na Hospital zilizojengwa na Mkoloni Mjarumani mikononi mwa kanisa lake atashindwa nini? Yeye Mrutheli, Mbowe sijui, Mtei sijui, Wakaskazini wengi sijui...kwa nini anapewa support kubwa hivyo sijui!. Panapofuka moshi kuna moto! Mimi ningependa tu kujua huyu Gwajima Askofu mzima ameingiaje katika uongozi wa Chadema au UKAWA hadi awe mshauri na msemaji wao?

- Unategema nini kitaandaliwa hapo? Nimeandika haya najua yatakuja mashambulizi ya hali ya juu kwa sababu watu hawatazami reality, wanataka kudanganyana na bikra ya ndimu! Udini upo mkuu wangu na hautakwisha kirahisi...

Twende taratibu ni sek. ya ngapi anasema hayo maneno yaani hapo kwenye nyekundu?
 
Back
Top Bottom