CHADEMA waendelea na ajenda yao ya maandamano ya amani. Wapeleka barua Polisi kuomba ulinzi

Kuna haja ya kuhakikisha kuwa tunailewa Katiba, taratibu na Sheria pamoja na Barua ya Chadema. Barua ya Chadema, kama nimeilewa vizuri, siyo ya kuomba ruhusa kwa Polisi ili kufanya maandamano. Inailitaarifu jeshi kuwa inatarajia kufanya maandamano ya amani. Je kuna mahali kwenye Katiba na Sheria za nchi yetu ambapo Jeshi la Polisi linabidi liombwe ruhusa ya kufanya maandamano? Au liombwe kuandaa maandamano?
 
Kama unaandamana porini ambako hakuna makazi na viwanja vya watu au mashamba ya watu na hakuna mali asili nadhani huhitaji kibali sababu kisheria huja trespass eneo la mtu au la mali asili

Lakini kama utatumia barabara kuna sheria za usalama barabarani lazima upate kibali polisi ili usisumbue watumia Barabara wengine wasio na mpango na maandamano kuzuia uhuru wao wa kutumia barabara na wanalipa kodi kwa kila lita ya mafuta wananunua zijenge barabara hizo
 
Uzuri moderators wanafahamu kazi yao wamekuleta kwenye huu uzi angalia ipo huu uzi mwanzoni kabisa wa hii mada

Heko moderators kukulleta huku mjinga wewe ili uione
Wakati mwingine jaribu kuficha utaahira wako.
 
Ona JF ilivyovamiwa na kuigeuza kutoka "home of great thinkers" to "kusanyiko la mbumbumbu". Wewe wapi umeona hii ni barua ya Chadema kuomba kufanya maandamano?
Kunyamaza na kuficha ujinga ni busara zaidi kuliko kukurupuka kwa jambo hujaelewa. Hiyo ni taarifa kwa umma yaani Tangazo.
Nimegundua kwa nini watu kama wewe CCM inawapenda sana.
Empty heads"
 
Vipi kama wote ni Wendawazimu?yaani polisi,chadema,Wananchi,Viongozi.
Ni vile tu Sheria imeelekeza kufanya hivyo,

Ni ngumu sana CDM kuwataarifu polisi kwamba njoni mtulinde tuwaseme jinsi msivyoweza kutulinda.
 
Hata Makongoro Nyerere alikuwa Chadema na huku baba yake ni gwiji wa CCM. Sio lazima watoto wa Mbowe na Lissu nao ni wanaharakati za kisiasa, nao wana maamuzi yao kama binadamu.
Kwa hiyo mbowe na lisu kwa kuwa ni vingunge wa chadema watakuwa frontline kuongoza mapambano?
 
We mbwah hv unajikuaga ni nani kwenye hii nchi...!!
Badala ya kutumia nguvu nyingi kutukana, ingeonyesha una hekima kama na busara kama ungetuhakikishia kuwa mbowe na lisu na familia zao watakuwa frontline. Hilo ndiyo swali la mwanajamii alilouliza kutaka kujua.
 
Hili sio ombi ni taarifa
 
Unavyosema sasa hapo nyuma chadema iliwahi kuvunja amani
 
Hii imeandikwa na Mwanasheria nguri........ polisi hawaombwi wanapewa taarifa
 
ombi kwa uongozi wa Chadema, uwe tayari kupokea majibu yao kesho, wakikataliwa wasiandamane.

P
Mbona hueleweki? Hilo la kukataliwa linatoka wapi? Wametoa taarifa ya kuandamana kwa amani kama Katiba inavyowataka na wameomba ulinzi kama inavyotakiwa.
 
Mkuu wakikataa wasiandamane tena?

Tunahitaji kupeleka The Hague.

Acha watawala wajichanganye
Tulipofika sio kabsaaaa
 
Mkuu Paskal unanifanya niamini kuwa The level of compliance with laws correlates to the level of immorality. Na maisha ya kufata sheria ni kuishi bila hekima na busara ingawa sheria nayo ina hekima yake.
Sheria inasema ukitaka kuandamana toka taarifa polisi.(SAWA). Sheria hiyo hiyo inasema wenye mamlaka ya kuchuguza uhalifu ni hapa Tanzania ni polisi. CHADEMA wanataka Scotland Yard. Halafu unawapa sifa hapa kwamba wanafata sheria?
 
1. Kwanza you are right
Ukitaka kuandamana toa taarifa ya maandishi polisi, sio kuomba ruhusa!.
2. Baada ya kutoa taarifa lazima usubirie kibali cha maandishi kuruhusu, kuandamana.
3. Serikali inaposhindwa kuchunguza tukio, Scotland Yard huwa wanaitwa, hivyo Chadema are right.
P
 
Kwani wanaoandamana hawalipi kodi? Nchi nyingi hapa duniani hutokea maandamano uliwahi kusikia watu wanaenda kuandamana porini? Na kama kuna haja ya kuwashauri waliotoa taarifa ya kuandamana kuhusu muda, siku na njia ya maandamano basi ingekuwa busara kukutana nao wazungumze na kukubaliana jinsi ya kufikisha ujumbe wao. Haya tunayaongea watu ambao wala si wana Chadema lakini tunaona haja ya Taifa kuendeshwa kistarabu. Tulipambania uhuru wa nini kama leo tunapigana, kuumizana na kutendeana unyama wenyewe kwa wenyewe?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…