CHADEMA wakaziwa na Umoja wa Waandishi wa Habari Kanda ya Pwani

Shinikizo kutoka kule kulee.

Kwanini kuweweseka? Kama wananchi wamekosa kusikiliza sera, it's simple, wapeleke kura zao kule waliposikiliza sera. Haina haja kuwapressure wachumia tumbo kugomea habari za watu flani.
 
Hawa TBC na vyombo vingine vya habari uchwara wanachekesha sana, kwani wamekuwa wanarusha habari za CHADEMA? Mwenyewe nilishangaa nilipooana eti TBCCM itarusha mubashara mkutano wa CHADEMA!

Actually nilitegemea wafanye mabaya Zaidi! Hapa wana Lumumba A.K.A MATAGA ndo watatoka povu! CHADEMA walifanya vyema sana kufukuzia mbali wanafiki na wazandiki hawa TBCCM!
 
Umoja wa Waandishi wa Habari wa Kujitegemea kanda ya Pwani ( UWHP) umetoa tamko la kutoandika habari za Chadema hadi pale chama hicho kitakapoomba radhi kwa kituo cha TBC na kusamehewa.

UWHP umewataka waandishi wa habari wa taasisi za habari kote duniani kuisusia Chadema kwa sababu imewadharau.

Maendeleo hayana vyama!
 
Umoja wa Waandishi wa Habari wa Kujitegemea kanda ya Pwani ( UWHP) umetoa tamko la kutoandika habari za Chadema hadi pale chama hicho kitakapoomba radhi kwa kituo cha TBC na kusamehewa...
TBC Ni TV ya ajabu duniani. Tena jiepusheni nayo haina watazamaji na nyie mkijiunga nayo hakuna mtu atasoma habari zenu mtazisoma wenyewe.
 
Hauwezi kuzuia habari za Chadema zisisambae sababu wafuasi wa Chadema ni waandishi tosha, pamoja na mikutano yake kutotangazwa na vyombo vya habari ila habari yake mmeipata huko huko. Hakuna aliebebwa kwenye mkutano watu wanakuja wenyewe.
 
Wameanza lini kuandika? Halafu Ndo vizuri kwanza maana watakuwa na uhakika wa kutofungiwa.
 
Tbc wanafki tu na hao waandishi wa habari kanda ya pwani wanatumika na mwenyekiti wao ni kada wa chama cha mapinduzi!
 
Chadema hatutawaomba radhi hao vibaraka wa CCM
 
Umoja wa Waandishi wa Habari wa Kujitegemea kanda ya Pwani ( UWHP) umetoa tamko la kutoandika habari za Chadema hadi pale chama hicho kitakapoomba radhi kwa kituo cha TBC na kusamehewa...
Msipo andika habari za chadema hizo zingine mnamwandikia nani na nani atazisoma. Ajira yenu ipo mikononi mwa habari za chadema Kama hamna habari.

Magazeti yote usipoandika habari za cdm hayo magazeti yataenda kufungiwa sukari kesho yake. Sasa tunadusia Kununua magazeti yote na kuangalia TBC.
 
Wanapoteza muda tu hao MAMLUKI WA CCM, kuna vyanzo vingi mno vya kupata habari siku hizi.
 
Ni ajabu waandishi wa habari bado wanajiona relevant. In this day and age, information monopoly hakuna tena.
Wamebaki waandishi uchwara wanaoandikia yale magazeti lukuki ambayo vichwa vya mbele vya habari ni Magufuri tu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…