LGE2024 CHADEMA wanazungumza na Waandishi wa Habari kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

LGE2024 CHADEMA wanazungumza na Waandishi wa Habari kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869

13 November 2024 Arusha, Tanzania​


CHADEMA WANAZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI MUDA HUU, tathimini kuelekea uchaguzi 2024


Katibu wa CHADEMA Kanda ya Kaskazini Mhe. Amani Golugwa Leo tarehe 13 November 2024, akiwa na Godbless Lema ambaye ni mwenyekiti wa CHADEMA kanda ya Kaskazini pamoja na kamanda Benson Kigaila Naibu Katibu mkuu wa CHADEMA bara watoa takwimu za ndani juu ya CHADEMA ilivyo jizatiti kwa kusimamisha wagombea nafasi zote kwa asilimia 100 za uongozi katika uchaguzi wa serikali za mitaa, vitongoji na vijiji ..

Ingawa wasimamizi wasaidizi wamewaeunga wagombea wengi wa CHADEMA ila taratibu za kukata rufaa dhidi ya mapingamizi zinaendelea na kuwa CHADEMA haitajitoa ktk uchaguzi wa 2024 ...

Takwimu nzito alizozisoma Katibu wa CHADEMA Kanda ya Kaskazini Mhe. Amani Golugwa, ni kujibu propaganda za CCM na vyama rafiki vya chama dola tawala wanazosambaza kuwa CHADEMA haikuwa imejipanga. Propaganda hizo zimekuwa zikirudiwa na katibu uenezi, itikadi na mafunzo wa Halmashauri kuu ya CCM ndugu CPA Amos Makala hivi karibuni ..

kamanda Benson Kigaila Naibu Katibu mkuu wa CHADEMA bara amepiga kama kwa muda mrefu kanda ya kaskazini kwa kazi za kichama kuangalia tangu mwanzo zoezi la kuandikisha wakazi katika daftari la mkaazi (mtaani), uchukuaji fomu za kugombea uongozi serikali za mitaa, uteuzi wa wagombea uliofanywa na TAMISEMI, kubandika majina ya wagombea hadi kuenguliwa wagombea.

Na sasa kumulika usikilizaji wa rufani za wagombea wa CHADEMA walioenguliwa pia kuona kauli ya rais Samia Suluhu Hassan kupitia Katibu mkuu wa CCM Dr. Emmanuel Nchimbi kuhusu 'makosa madogo katika fomu' zinatekelezwaje kimatendo kuwarudisha wagombea katika kinyanganyiro cha uchaguzi wa TAMISEMI, kutayarisha ripoti itakayopelekwa Kamati Kuu ya CHADEMA kuhusu hali halisi ilivyo...

CHADEMA warejea kauli ya katibu mkuu wa CCM balozi Dr. Emmanuel Nchimbi hapa chini :

12 November 2024

CCM: TAMISEMI IPUUZE MAKOSA MADOGO MADOGO, KUKUZA DEMOKRASIA​

1731509125398.jpeg

Imewekwa tar.: November 12th, 2024

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeiomba Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), kuwaelekeza Wasimamizi Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, kupuuza makosa madogo madogo yaliyotokea, ili kuruhusu wagombea wengi kushiriki uchaguzi huo.

Akizungumza na wahariri na waandishi waandamizi wa vyombo vya habari nchini, Katibu Mkuu wa CCM, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, ametoa mfano wa makosa hayo yanayostahili kupuuzwa ni pamoja na wagombea kukosea herufi.

Kupitia mkutano huo uliofanyika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar es Salaam, leo Novemba 12, 2024, Balozi Nchimbi amesema ni vyema TAMISEMI ikaangalia uwezekano wa kuwarudisha wagombea wote walioenguliwa kutokana na makosa hayo madogo madogo ili kuhamasisha ukuaji wa demokrasia kwenye uchaguzi huo.

Aidha, kuhusu sehemu kubwa ya malalamiko mengi ya kuenguliwa kuonekana ni ya wagombea wa vyama vya upinzani, Balozi Nchimbi amewatoa shaka Watanzania kuwa, si kweli kwamba wagombea walioenguliwa ni wale wa vyama vya upinzani pekee, bali pia hata wagombea wa CCM wapo waliowekewa mapingamizi ya kugombea.

“Waziri wa TAMISEMI tunajua anafuata sheria, lakini ni muhimu kutambua demokrasia yetu hii bado ni changa hivyo tunahitaji muda wa kuendelea kujiífunza tunaziomba mamlaka hasa TAMISEMI katika nyakati za mwisho za rufaa kuyapuuza makosa madogo madogo ili watu wengi wapate nafasi ya kugombea", alisema Dkt. Nchimbi.

PIA SOMA
- LGE2024 - Lema: CCM wanakaa vikao na ACT Wazalendo ili kukifanya kuwa Chama Kikuu cha Upinzani nchini na kuondoa hadhi yetu

Source : OR TAMISEMI
 
Wamepewa fursa ya hisani kwenye rufaa wachangamkie maana wakisusia ACT na vyama vilivyonunuliwa watakula.
 

13 November 2024​

CHADEMA WANAZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI MUDA HUU


View: https://m.youtube.com/watch?v=GStMiPMklKs
Chadema warejea kauli ya katibu mkuu wa CCM balozi Dr. Emmanuel Nchimbi hapa chini :


12 November 2024

CCM: TAMISEMI IPUUZE MAKOSA MADOGO MADOGO, KUKUZA DEMOKRASIA​

View attachment 3151515

Imewekwa tar.: November 12th, 2024

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeiomba Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), kuwaelekeza Wasimamizi Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, kupuuza makosa madogo madogo yaliyotokea, ili kuruhusu wagombea wengi kushiriki uchaguzi huo.

Akizungumza na wahariri na waandishi waandamizi wa vyombo vya habari nchini, Katibu Mkuu wa CCM, Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, ametoa mfano wa makosa hayo yanayostahili kupuuzwa ni pamoja na wagombea kukosea herufi.

Kupitia mkutano huo uliofanyika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar es Salaam, leo Novemba 12, 2024, Balozi Nchimbi amesema ni vyema TAMISEMI ikaangalia uwezekano wa kuwarudisha wagombea wote walioenguliwa kutokana na makosa hayo madogo madogo ili kuhamasisha ukuaji wa demokrasia kwenye uchaguzi huo.

Aidha, kuhusu sehemu kubwa ya malalamiko mengi ya kuenguliwa kuonekana ni ya wagombea wa vyama vya upinzani, Balozi Nchimbi amewatoa shaka Watanzania kuwa, si kweli kwamba wagombea walioenguliwa ni wale wa vyama vya upinzani pekee, bali pia hata wagombea wa CCM wapo waliowekewa mapingamizi ya kugombea.

“Waziri wa TAMISEMI tunajua anafuata sheria, lakini ni muhimu kutambua demokrasia yetu hii bado ni changa hivyo tunahitaji muda wa kuendelea kujiífunza tunaziomba mamlaka hasa TAMISEMI katika nyakati za mwisho za rufaa kuyapuuza makosa madogo madogo ili watu wengi wapate nafasi ya kugombea", alisema Dkt. Nchimbi.

Source : OR TAMISEMI

kama ni kamanda kigaila ndio anaongea ndo basi tena chama kimepoteza uelekeo zaid. huko ni kijaribu kumjibu Lisu :pedroP:
 
CHADEMA bara watoa takwimu za ndani juu ya CHADEMA ilivyo jizatiti kwa kusimamisha wagombea nafasi zote kwa asilimia 100 za uongozi katika uchaguzi wa serikali za mitaa, vitongoji na vijiji .

Hakika CHADEMA wamejitayarisha mapema, hatoki mtu mpaka kieleweke
 
Kwa ajili ya kuombea misaada isisitishwe na wahisani wapenda demokrasia walioamini kauli mbiu za 4R :

12 November 2024

THE RULING PARTY IN TANZANIA -CCM : TELLS OFFICE OF THE PRESIDENT REGIONAL GOVERNMENTS TO IGNORE SMALL MISTAKES, TO PROMOTE DEMOCRACY​


1731515358251.jpeg

Dr. Emmanuel Nchimbi addressing members of the press in Dar es Salaam, Tanzania Photo: courtesy of CCM Secretary General office.

Dated: November 12th, 2024
By Our Writer, Dar es Salaam

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) has asked the ministry under the President's Office for Regional Administrations and Local Governments (TAMISEMI), to instruct the Election Supervisors of Local Governments, to ignore the minor mistakes that occurred during the initial stages of filling forms to vie for political position at the grass root levels , in order to allow more candidates to participate in the election.

Speaking to editors and senior reporters of the media in the country, the Secretary General of CCM, Hon. Ambassador Dr. Emmanuel John Nchimbi, has given an example of those mistakes that deserve to be ignored, including the candidates misspelling the alphabetical letters.

Through the meeting held at the Offices of the CCM Headquarters, located at Lumumba Street, in the city of Dar es Salaam, today November 12, 2024, Ambassador Nchimbi said that it is good for TAMISEMI to look at the possibility of bringing back all the candidates who were disqualified due to those minor mistakes in order to encourage the growth of democracy in the upcoming election schedule to take place on the 27th of November 2024.

In addition, with regard to the majority of complaints about the disqualification of candidates mainly hitting over 100,000 candidates from the opposition parties, Ambassador Nchimbi has said to the Tanzanians that it is not true that the disqualified candidates from the opposition parties, but also that there tens of ruling party CCM candidates who have been barred from running. .

"We know that the Minister of TAMISEMI Hon. Mohamed Mchengerwa is following the strict line of the law, but it is important to realize that our democracy is still young, so we need time to continue learning. We are asking the authorities, especially in TAMISEMI, to ignore minor mistakes so that many people have a chance to run in this coming grassroots level election also known as local government elections ", said Dr. Emmanuel Nchimbi.
 
13 November 2024
Tunduma, Songwe
Tanzania

CHADEMA KANDA YA NYASA YATOA TAMKO ZITO KUENGULIWA WAGOMBEA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA 2024


View: https://m.youtube.com/watch?v=gJMHXd2oSFA
CHADEMA Tunduma watoa tamko zito kuenguli kwa wagombea " Wananchi Wanahitaji Mabadilko " asema makamu mwenyekiti kanda ya Nyasa CHADEMA kamanda Frank Mwakajoka akiwa na viongozi waliopoongea na wanachama wa CHADEMA pia press club ya Tunduma
 
CHADEMA mwaka huu 2024 operesheni zake zimeibua madudu yaanayoipa upendeleo haramu CCM nje ya uchaguzi wa haki na huru.
 

12 November 2024​

CYPRIAN MUSIBA ATOA TAHADHARI KUBWA, "CCM "WATADONDOKA HAWATAAMINI, WATU WATACHOKA CHAMA DOLA KONGWE CCM KAMA KULE BOTSWANA "

1731521724227.jpeg

CCM imeshindwa kukidhi ndoto za watanzania, mafisadi wanapeleka watoto shule kwa kutumia V8, huku umma mkubwa mpana wa watanzania unaishi katika lindi kubwa la umasikini, kule Afrika ya Kusini chupuchupu ANC chama kongwe cha ukombozi bado kidogo king'olewe, FRELIMO mambo mazito ... mwanaharakati huru Musiba aonya ...
 
Vyama dola kongwe Kusini mwa Afrika vinaelekea kungolewa, komredi Bi. Alcinda Abreu mjumbe wa NEC aliye katibu uenezi, itikadi na mafunzo wa FRELIMO asema.

Kauli hiyo ya komredi Alcinda Abreu inashabiana na ya mwanaharakati huru wa nchini Tanzania ndugu Cyprian Majura Musiba aliyotoa jana katika mahojiano na vyombo vya habari kuhusu hatihati ya CCM Tanzania , FRELIMO Mozambique, ZANU PF Zimbabwe, ANC, BDP Botswana, SWAPO Namibia n.k

7 November 2024
Lisbon, Portugal

HALMASHAURI KUU YA CHAMA (NEC) DOLA KONGWE FRELIMO YAONGEA NA WAANDISHI WA HABARI

Msumbiji: Frelimo inaunganisha maandamano ya baada ya uchaguzi na jaribio la mapinduzi na maslahi ya nje - Tazama​

6:17 | 07 Nov 2024

Frelimosp.yt_

Picha : TVM . Mnec Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya chama dola kongwe FRELIMO aliye katibu wa Siasa, mafunzo na Uenezi komredi Bi. Alcinda Abreu

Chama cha Frelimo kinasema kuwa kuna vuguvugu la kuviondoa madarakani vyama vilivyokomboa baadhi ya nchi katika bara la Afrika kupitia mapinduzi ya kijeshi na kwamba huenda ikawa hivyo nchini Msumbiji.

Akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari, chama tawala kongwe FRELIMO kilifahamisha kuwa kinaamini kuwa nchi hiyo ina maliasili ambazo baadhi ya nchi zinatamani
Ilikuwa ni kuwaomba raia wa Msumbiji kuheshimu Katiba ya Jamhuri na kutoa wito kwa wakazi kuwa na utulivu kupitia taarifa kwa umma toka Kamati ya Kisiasa ya Frelimo iliitisha mkutano na waandishi wa habari Jumatano jioni, katika jiji la Maputo.


Bi. Alcinda de Abreu, anayewakilisha Halmashauri Kuu ya chama hicho FRELIMO , aliwasilisha msimamo wa Frelimo kuhusu maandamano na uharibifu katika kupinga uchaguzi mkuu wa tarehe 9 Oktoba 2024.


"Msumbiji, nchi yetu nzuri na tunayopenda, inadhulumiwa kwa njia isiyo ya kawaida, inayoonyeshwa na maandamano ya vurugu ambayo yanaleta maombolezo, maumivu, uharibifu, na kuongezeka kwa njaa na umaskini ndani ya familia kubwa ya Msumbiji," alisema Alcinda de Abreu, anaripoti mwandishi wa shirika la habari la ABNA.

Halmashauri Kuu ya Taifa ya Kisiasa ya chama kongwe dola Frelimo,
"Imechukua miaka ya kazi ngumu kufikia hapa tulipo leo. Tunaelewa kuwa tumepitia nyakati ngumu za mizozo ya kiuchumi na kifedha, iliyosababishwa na sababu za ndani na nje, pamoja na ugaidi huko Cabo Delgado, lakini, kama raia wa Msumbiji, lazima tufanye kazi kwa maendeleo ya nchi, "alisema komredi Bi. Alcinda Abreu MNEC mjumbe wa NEC FRELIMO .

Msemaji wa kikao cha 36 cha kawaida cha halmashauri kuu ya chama cha Frelimo alisisitiza wazo la Waziri wa Ulinzi kwamba kuna watu wanaotaka kufanya mapinduzi.


"Frelimo, kama chama kilichoikomboa Msumbiji kutoka kwa ukoloni mkongwe wa Mreno , ni sehemu ya vuguvugu la ukombozi wa taifa, na leo kuna harakati za kuondoa vyama vilivyokomboa baadhi ya nchi za Kusini mwa Afrika ."


MNEC Alcinda de Abreu pia alisema kuwa nchi hiyo ina utajiri mkubwa wa maliasili ambazo baadhi ya nchi zinatamani na, kwa hivyo, huajiri watu "waliokengeushwa" ili kuchochea ukosefu wa utulivu nchini.


More :
 
Mungu atubariki Tanzania turudi katika ustaarabu wa kuchaguana kwa haki
 
Miaka 35 demokrasia yetu bado changa? Itakua lini!!

Ni njama zinazoongozwa kwa kuratibiwa na komredi SG balozi Dr. Emmanuel Nchimbi kukaribisha makosa ya uenguaji yaendelee kwa muda zaidi. Hii ni hadaa kama ya zile 4R zinazoimbwa sana bila kutekelezwa kwa vitendo.
 
Back
Top Bottom