CHADEMA watashiriki Uchaguzi Mkuu wa 2025 bila katiba mpya

Hao mliokuwa mnaona ni mtaji wenu huko vijijini walimalizika baada ya TV na internet kuingia. Kizazi hiki sio kile cha zamani kilichokuwa kinaona mbolea na zahanati nyingi hisani ya serikali. Kwa taarifa yako hata ikiingia serikali ya kijeshi, itajenga zahanati, shule, kupeleka mbolea nk maana huo ni wajibu wa serikali inayokusanya kodi.

Mngekuwa mnategemea kura za huko vijijini tusingeona chaguzi za kihayawani vile. Danganyeni wajinga sio werevu.
 
Hahahaaaaa! Si nyie ndio mlikuwa mnapiga picha watoto wa shule msingi wakisomea chini ya miti huku mvua ikinyesha. Hivi kodi zilikuwa hazikusanywi? Mtaji huu kama hoja ya kuwaingiza IKULU hautajitokeza tena. Poleni!
Bwawa la umeme la Nyerere si ni mpango uliokuwepo toka enzi za Nyerere- Hivi wakati wote kodi zilikuwa hazipo. Fly over hizo nazo, Daraja la Busisi, SGR, N.K. Hivi huko nyuma kodi hazikuwepo? Jamani anayestahili, mpeni maua yake! Msiwe na choyo.
TV na internet vijijini bado sana. Simu huko vijijini hutumika sana katika sms, m-pesa, tigo/halo-pesa. Bando la Internet kama mjini mnalalamika unafikiri vijijini wanalo la kusikiliza hotuba ya kuboa ya LISSU, Dr Slaa n.k? Mnajidanganya mchana kweupeeeee!
 
Mkuu '1000Digits', nimekusoma kwa uangalifu mkubwa sana hadi mwisho wa andiko lako, na ni nadra sana kwangu kutaka kurudia nilichosoma mara ya kwanza (huwa nasoma kwa spidi kubwa sana), ili niliyoyasoma kwa mara ya kwanza yaniingie vizuri akilini.

Sasa niseme, ninakubaliana nawe kwa ujumla. Kilichonifanya kusita kwa mara ya kwanza ni hayo maswala ya 'Hela'; siyo hela za kuwalipa wanachama huko matawini wanaofanya kazi kubwa sana; ni swala la "HELA" kuifanya kuwa rushwa katika uchaguzi.
Lakini hata hili, kwa wakati huu tuliomo, na hasa baada ya kuona CCM wanavyoitumia njia hiyo kuvuruga chaguzi ndani ya nchi hii, inanilazimu pia nilifumbie macho kama CHADEMA watahitaji kufanya hivyo ili kuwaondoa CCM madarakani.

Ninakubaliana nawe moja kwa moja, kuhusu CHADEMA kutafuta pesa za kuwasaidia katika chaguzi hizi, lakini isiwe ni kwa kuuza hisa za chama kwa wenye uwezo mkubwa wa pesa kwa mategemeo ya kuvuna baada ya CHADEMA kuingia madarakani.

Kwa hiyo, niseme hapa wazi, kwamba ninaungana nawe, na ninawasihi CHADEMA kuanzia sasa watafute vyanzo vya kuingiza pesa ndani ya chama kwa lengo la kufanikisha chaguzi zinazokuja karibuni. Ninakubaliana nawe pia, kwamba, pamoja na kuwahamasisha wanachama wao na viongozi wao huko mashinani, ni muhimu sana kuwapa motisha wafanye kazi zao kwa ufanisi zaidi huko kwenye ngazi za chini, kwa kuwawezesha kulipia mahitaji yao muhimu.

Mawazo haya yote ni sehemu ya mchango kwa chama hiki ili kiweze kufanikiwa zaidi katika shughuli yao kubwa ya kuiondoa madarakani CCM.
 
Nisikilize boss, haya wanayofanya CCM ni wajibu sio hisani, na yoyote atakayeingia madarakani anapaswa kutekeleza, tena kwa speed kubwa katika kuliko hiyo ya CCM. Kizazi limebadilika na CCM sio chama cha kizazi hiki. Hao wajinga wa kuamini kuwa wajibu wa serikali unaweza kutekelezwa na CCM tu walishazeeka. Kizazi hiki kinataka ladha mpya na sio utawala wa shuruti na mazoea.

Huo ujinga kuwa nchi inaweza kujengwa na chama fulani tu, pia KANU ya Kenya waliaminisha watu hivyo, na kuwaburuza watakavyo, leo hii KANU ni marehemu wa muda mrefu, na bado Kenya ina uchumi mzuri kuliko sisi makondoo wa Tanzania. Zama za CCM zilishapita, chama chochote kinaweza kujenga shule, vituo vya afya, barabara nk. Kama CCM ingekuwa na mtaji huo wa wajinga tusingeshuhudia chaguzi za kihayawani vile ili CCM watangazwe washindi kwa shuruti.
 
Binafsi sioni dalili ya kupata katiba mpya au tume huru ya uchaguzi sioni kabisa muamko wa wananchi kujitokeza kupiga kura kama vyama vya upinzani wataingia kwenye uchaguzi huu wategemee kupatiwa wabunge wa hisani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…